ﭽ
ﭑ ﭒ
ﭓ ﭔ ﭕ
ﭖﭗ ﭘﭙ ﭚ
ﭛ ﭜ ﭝ
ﭞ ﭟ ﭠ
ﭡ ﭢ ﭣ
ﭤ ﭥ ﭦ
ﭧ ﭨ ﭩ
ﭪ ﭫ ﭬ
ﭭ ﭮ ﭯ
ﭰ ﭱ ﭲ
ﭳ ﭴ ﭵ
ﭶ ﭷﭸ ﭹ
ﭺ ﭻ ﭼ ﭼ
البقرة: ١ - ٥
"Alif
Lam Mym (1) Hiki ni Kitabu, kisichokuwa na shaka ndani yake, ni uongozi kwa
wamchao (Allah) (2) Ambao huyaamini
yasiyoonekana (maadam yamesemwa na Allah na Mtume wake) na kusimamisha Sala na
hutoa katika yale tuliyowapa (3) Na ambao wanaamini yaliyoteremshwa kwako, na
yaliyoteremshwa kabla yako na waamini (kuwa iko) Akhera (4) Hao wako juu ya uongozi utokao kwa Mola
wao na hao ndio wenye kuongoka (5)."
Uislamu ni
kufuata kwa ukamilifu na kunyenyekea amri za Allah (Subhanahu Wataala) na
sharia zake, kuamini Allah na Malaika wake na Vitabu vyake na Mitume wake na
Siku ya Mwisho na Kadari, shari yake na heri yake, kuwa inatokana na Allah (Subhanahu
Wataala).
Nao umejengwa
kwa nguzo tano:
Shahada,
Sala, Saumu, Zaka na Hija. Vile vile umekusanya utendaji, baina ya mja na Mola
wake na haya yako chini ya kifungu cha Ibada mbali mbali kama
mfano wa Sala, Zaka, Saumu n.k na utendaji baina ya mja na mwenzake (binaadamu
mwenzake) na haya yako chini ya kifungu cha dharura za maisha.
Basi Allah
(Subhanahu Wataala) ataka Waislamu maisha yao
yote yawe kama ilivyokuja katika Dini ya Allah katika yanayohusu mambo ya ibada
na mipango (nidhamu) inayomhusu mtu binafsi na inayowahusu jamii (watu baina yao wenyewe kwa wenyewe).
Anasema Allah (Subhanahu Wataala):
ﭽ
ﮭ ﮮ
ﮯ ﮰ ﮱ
ﯓ ﯔ ﯕ
ﯖ ﯗ ﯘﯙ
ﯚ ﯛ ﯜ
ﯝ ﭼ البقرة:
٢٠٨
“Enyi
Mlioamini! Ingieni katika hukumu za Uislamu zote, wala msifuate nyayo za
Shetani; yeye kwenu ni adui dhahiri”.
Na Aya za
kitabu cha Allah (Subhanahu Wataala) na Sunna ya Mtume (Salallahu Alayhi
Wasalam) zimeweka wazi kabisa njia inayowapasa Waislamu kufuata katika maisha
haya ya Dunia.
Na nguzo za
Dini zimesimama juu ya mambo matano wala hakuna cho chote (katika Dini)
kinachoepukana na hayo (matano). Nayo:
1.Wajibu : Nao ni
kila aliloamrisha Allah (Subhanahu Wataala) lifanywe katika yafuatayo:
Kumjua
Allah na kumpwekesha
Kuamini
Mitume yake yote na kwa namna mahsusi baina yao Mtume wetu Muhammad (Salallahu Alayhi
Wasalam).
Kuamini
Vitabu vyake vyote na kwa namna mahsusi baina yake kitabu chetu kitukufu
ambacho ni Qur’an.
Kuamini
Malaika wake wote na kwa namna mahsusi baina yao Malaika wanne nao: Jibril, Mikaaiil,
Israfiil na Malaika wa mauti.
Kuamini
Siku ya mwisho nayo ni siku ambayo watafufuliwa waliokufa kutoka makaburini na
watapelekwa kukusanywa pale alipowataka Mola Subhanahu Wataala.
Basi mtiifu
miongoni mwao ni yule aliyekuja hali ametekeleza ahadi ya Allah; huyo
ataingizwa Peponi kama alivyoahidi Allah (Subhanahu
Wataala).
Na aliekufa
katika hali ya kumshirikisha Mola Subhanahu Wataala au hali ya kufanya madhambi
makubwa na hajatubu kwa Mola Subhanahu Wataala (huyu ni Muislamu lakini
ameendelea kufanya ‘Kabira’ kwa mfano: zina, kuiba, kunywa pombe na kula riba
mpaka kufa kwake bila ya kutubu) huyu Allah (Subhanahu Wataala) Atamuingiza
Motoni - Mola Subhanahu Wataala atukinge na hali kama hiyo - kama Alivyoahidi Subhanahu
Wataala, kwani Yeye Hahalifu ahadi yake ya malipo mazuri (Al-Jannah) wala
Hahalifu ahadi yake ya malipo mabaya (Jahannam). Haiwezekani kabisa kauli yake
kubadilishwa. Na wala Hadhulumu Subhanahu Wataala waja wake.
Pia ni
wajibu kusali, kutoa Zaka, kufunga Ramadhani, kuhiji na kuamrishana mazuri
(mema) na kukatazana maovu na kufanya mengineyo yalokuwa wajibu.
Na vitu
hivi anapata thawabu mtu akivifanya na anapata madhambi kwa kuviwacha.
2.“Al-Mahdhoor”
yaani kilichokatazwa (Haraam).
Kila
alichokikataza Allah (Subhanahu Wataala) kufanywa ikiwa ni kuacha kufanya
wajibu (kama Sala, Zaka, Saumu nk) au kufanya yaliyoharamishwa kama kwa mfano
kuzini, kula mali ya watu bila ya haki, kunywa aina zote za vileweshaji
(pombe), kumsengenya Muislamu na kuchonganyisha (watu ili wagombane) na
mengineyo yaliyokatazwa na sharia.
Mambo haya
Muislamu hupewa thawabu kwa kuyawacha na huadhibiwa kwa kuyafanya. Amesema
Allah (Subhanahu Wataala):
ﭽ ﮕ ﮖ
ﮗ ﮘ ﮙ
ﮚ ﮛ ﮜ
ﮝ ﭼ
طه: ٨٢
“Na hakika mimi ni msamehevu
sana kwa
anayetubia na kuamini na kutenda wema, tena akashika Uongozi bara bara.”
3.Yaliyohimizwa
kufanywa (Sunna)
Nayo ni
kila jambo sheria imehimiza kulifanya katika vitendo vya kheri, tabia njema,
kusaidia Waislamu, kuwaondolea kila kinachowaudhi njiani (kinachowadhuru kwa
mfano miba, vigae, mawe nk) na kutoa sadaka, mbali na Zaka ambayo ni faridha,
na mengineyo. Na mwenye kuyafanya haya hupewa thawabu na haadhibiwi mwenye
kuyaacha na hakuna mtu aliyekuwa hahitajii thawabu za Allah (Subhanahu Wataala).
Kwa hiyo Muislamu ajitahidi awezavyo asiyawache haya. Na kufanya haya
yaliyohimizwa ni kukamilisha yaliyopungua katika mambo ya wajibu (faridha) na
wameutolea mfano kama ujani katika mimea,
amesema Mtume wa Allah (Salallahu Alayhi Wasalam):
Hakika
Allah (Subhanahu Wataala) Amesema:
( من عادى لي ولياً فقد آذنته
بالحرب ، وما تقرب إلي عبدي بشيء أحب إلي مما افترضته عليه ، ولا يزال عبدي يتقرب
إلي بالنوافل حتى أحبه ، فإذا أحببته كنت
سمعه الذي يسمع به وبصره الذي يبصر به ويده التي يبطش بها ورجله التي يمشي عليها ،
ولئن سألني لأعطينه ، ولئن استعاذني لأعيذنه )
“Anayemfanyia
uadui mpenzi wangu basi huyo nimekwisha mtangazia vita. Na hakujikaribisha mja
wangu kwangu kwa kitu ninachokipenda zaidi kuliko yale niliyomuamirisha
kuyafanya (fardhi kwa mfano Sala, Zaka, Saumu na Hija n.k). Na bado mja wangu
azidi kujikaribisha kwangu kwa “Nawafil” (Nawafil ni yale yaliyohimizwa
kufanywa) mpaka nampenda, na nikishampenda huwa Mimi ndio masikio yake anayosikilia
na macho yake anayoonea na mkono wake anaokamatia na mguu wake anaoendea
(anaotembelea), na kwa yakini akiniomba nitampa na akijikinga kwangu
nitamkinga.”
4.Makruhu
– Ni kila kinachochukiza katika sheria:
Na mambo
haya mwenye kuyawacha hupewa thawabu na haadhibiwi anapoyafanya ikiwa hakusudii
kwenda kinyume na “Sunna”; akikusudia kwenda kinyume na “Sunna” basi ameangamia
(amehiliki). Allah atuepushie hayo. Amin.
5.“Al-Mubaah” – Ni kufanya mambo yaliyoruhusiwa, kama
kula chakula kizuri, kupanda kipando kizuri, kuvaa vazi la fahari au kwenda
kujipumzisha (mahala pa zuri na watoto) vitu hivi vyote vimeruhusiwa kwa
anayevifanya kwa nia nzuri lakini hali hiyo yabadilika ikiwa makusudio yake ni
mabaya. Anayekusudia kufanya ufahari akipanda gari nzuri basi kwa nia yake hii
mbaya amekifanya kitendo hicho kuwa haramu na akusudiae anapokula chakula
kizuri kumshukuru Allah (Subhanahu Wataala) kwa neema yake au kupata nguvu ili
amtii Mola Subhanahu Wataala anairudisha mubaah kwa nia yake nzuri hii kuwa
kama aliyefanya wajibu, yaani aliyoamrishwa kuyafanya kwa mfano Sala, Zaka nk.
Aina zote
hizi zimekuja wazi katika hadithi ya “Arrabii” kutoka kwa Abu Ubaidah kutokana
na Jabir bin Zayd kutoka kwa Abi Huraira amesema: “Amesema Mtume (Salallahu
Alayhi Wasalam): Farasi huwa thawabu kwa mtu, na huwa sitara kwa mtu, na huwa
madhambi juu ya mtu”.
Thawabu,
sitara na madhambi yote haya yamepatikana kwenye kitu kimoja, farasi, na kila
mmoja apata tofauti na mwenzake kwa kutofautiana nia. Na nia ni msingi wa kila
kitendo na bila ya nia kitendo hicho kinapotea bure wala hakihisabiki.
Tazama
ukarimu wa Allah (Subhanahu Wataala) kwa mja wake pamoja na kuwa hamhitajii
kitu, na tizama upande mwingine kutokujali kwa mja mbele ya Mola wake pamoja na
kuwa humhitajia kwa kila kitu na kila wakati. Akitia nia mja kufanya jambo jema
Allah amuandikia jema moja hata ikiwa hakulifanya na akilifanya huandikiwa mara
kumi, na akitia nia ya kufanya ubaya haandikiwi kitu juu yake ikiwa hakulifanya
na akilifanya haundikiwa baya moja. Imetolewa hadithi kutoka kwa Mtume
(Salallahu Alayhi Wasalam) kuwa amesema:
( يؤتى بالعبد يوم القيامة ومعه
الحسنات أمثال الجبال فينادي مناد من كان له على فلان مظلمة فليجئ فليأخذ ، فيجيء
أناس فيأخذون حسناته حتى لا يبقى له من الحسنات شيء فيبقى الرجل حيراناً، فيقول له
ربه إن لك عندي كنزاً لم أطلع عليه أحدا من ملائكتي ولا أحدا من خلقي ، فيقول يا
رب ما هو ؟ فيقول نيتك التي كنت نويتها من الخير كتبتها لك سبعين ضعفا)
“Analetwa mja Siku ya Kiyama
ana mema (aliyoyafanya) mfano wa milima (kwa wingi) basi ataita hapo muitaji
nani ambaye kadhulumiwa na fulani na aje ili achukue. Basi waja watu wachukua mema yake mpaka hakimbakilii
kitu katika mema yake (aliyoyafanya) kisha hubakia mtu huyo hajui nini la
kufanya, hapo ndipo Mola wake atamwambia hakika wewe una hazina kwangu
sikumuonyesha (hazina hiyo) yeyote katika Malaika wangu wala yeyote kati ya
viumbe vyangu, atamwambia: Ewe Mola, kitu gani hicho? Atamwambia: Nia yako
ambayo ulinuia kufanya mambo ya kheri nimekuandikia mara sabini nyongeza” (ya
aliyotia nia kuyafanya).
Na hadithi
nyengine:
( يؤتى بالعبد يوم القيامة
فيعطى كتابه بيمينه فيقرأ فيه الحج والجهاد
والزكاة والصدقة وغير ذلك نواه ولم يعمله فيقول العبد في نفسه ما عملت من
هذا شيئا وليس هذا كتابي فيقول الله تبارك وتعالى : اقرأ فإنه كتابك عشت دهرا وأنت
تقول : لو كان لي مال لحججت ولو كان لي
مال لجاهدت وغزوت وفعلت وعرفت ذلك من نيتك أنك صادق فأعطيتك ثواب ذلك كله )
“Analetwa
mja Siku ya Kiyama na hupewa Kitabu chake kwa mkono wake wa kulia kisha husoma
ndani yake: Hija, Jihadi, Zaka, Sadaka na mengineyo ambayo ameyatilia nia
lakini hakuyafanya basi atasema huyo mja katika nafsi yake: Sikufanya kitu
katika haya na wala hichi sio kitabu
changu. Hapo Allah (Subhanahu Wataala) atasema: Soma kwani hiki ni kitabu chako
umeishi muda mrefu na wewe unasema: Kama ningekuwa na mali ningehiji na kama ningekuwa
na mali ningefanya jihadi na ningekwenda kupigana (katika njia ya Allah) na
ningefanya. Na nimejua hayo kutokana na nia yako kuwa ulikuwa mkweli basi kwa
hiyo nikakupa thawabu ya hayo yote.”
Inavyotakiwa
mtu akitaka kufanya cho chote cha kumtii Allah aseme:
أتـقـرب إلى الله بعمل كذا
Yaani:
Najikaribisha kwa Allah kwa kitendo changu kadha. Basi huandikiwa thawabu ya
hicho kitendo na thawabu ya nia ya kujikaribisha.
Na hapa
tutazungumzia kwa kirefu yaliyokuja kuhusu kumpwekesha Allah (Subhanahu Wataala)
na kuamini kile kilichowajibika kukiamini kama
ilivyokuja katika Aya tukufu Kasema Mola Subhanahu Wataala:
ﭽ
ﭤ ﭥ
ﭦ ﭧ ﭨ
ﭩ ﭪ ﭫ
ﭬ ﭭ ﭮ
ﭯ ﭰ ﭱ
ﭲ ﭳ ﭴ
ﭵ ﭶ ﭷ
ﭸﭹ ﭺ ﭻ
ﭼ ﭽ ﭾ
ﭿﮀ ﮁ ﮂ
ﮃﮄ ﮅ ﮆ
ﮇ ﭼ البقرة: ١٧٧
“Na wanawapa
mali juu yakuwa wanayapenda, jamaa na mayatima na maskini na wasafiri
(walioharibikiwa) na waombao na katika
(kuwakomboa) watumwa, na wakawa wanasimamisha Sala na kutoa Zaka na watekelezao
ahadi zao wanapoahidi na wavumiliao katika shida na dhara na katika wakati wa
vita, hao ndio waliosadikisha (Uislamu wao), na hao ndio wamchao Mungu”.
Na kwa
mujibu ilivyokuja katika hadithi sharifu ya Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam)
katika maneno ya Jibril marefu ambayo yamekuja kama
ifuatavyo:
( أخبرني عن الإيمان قال : أن
تؤمن بالله وملائكته وكتبه ورسله واليوم الآخر وتؤمن بالقدر خيره وشره أنه من الله
تعالى)
“Niambie juu ya Imani akasema:
Umuamini Allah na Malaika wake na Vitabu vyake na Mitume yake na Siku ya Mwisho
na Uamini Kadari kheri yake na shari yake kuwa imetoka kwa Allah (Subhanahu
Wataala).”
Kwa hivyo
Imani ya Allah ndio msingi wa “Itikadi ya Dini” ambayo imekusanya mambo saba:-
1. Kumjua
Allah na Majina Yake Mazuri na Sifa zake Tukufu na dalili za kuweko kwake na
yanayodhihirisha Ukubwa wake katika Ulimwengu (Universe) na katika Tabia
(Nature).
2. Kutumia
dalili za viumbe vyake vikubwa kama mbingu na ardhi na upepo na bahari na mito
na hewa na mawingu na miti na miji na vinginevyo katika viumbe vyake ambavyo
havina budi kuwa na Muumbaji alieviumba naye Yuhai Mwenye uwezo ndie Mwangalizi
wa vitu vyote Hahitajii msaidizi wala muokozi. Ni Mmoja katika Dhati yake, ni
Mmoja katika Sifa zake na ni Mmoja katika vitendo vyake.
ﭽ
ﭑ ﭒ
ﭓ ﭔ ﭕ
ﭖ ﭗ ﭘ
ﭙ ﭚ ﭛ
ﭜ ﭝ ﭞ
ﭟ ﭠ ﭡ
ﭢ ﭣ ﭤ ﭥ ﭦ
ﭧ ﭨ ﭩ
ﭪ ﭫ ﭬ
ﭭ ﭮ ﭯ
ﭰ ﭱ ﭲ
ﭳ ﭴ ﭵ
ﭶ ﭷ ﭸ
ﭹ ﭺ ﭻ ﭼ البقرة:
١٦٤
“Hakika katika kuumbwa kwa mbingu na ardhi, na (katika)
kuandamizana usiku na mchana, na (katika mwendo wa) vyombo ambavyo hupita
katika bahari kwa (kuchukua vitu) viwafaavyo watu, na (katika kumiminika) maji
aliyoyateremsha Allah kutoka mawinguni, na kwa (maji) hayo akaihuisha ardhi
baada ya kufa kwake, na akaeneza humo (ulimwenguni kwa ajili ya maji hayo) kila
aina ya wanyama; na katika mabadiliko ya pepo, na mawingu yanayoamrishwa kupita
baina ya mbingu na ardhi, bila shaka (katika haya) zimo ishara kwa watu wenye
akili (kuwa yuko Allah na ni Mmoja tu)”.
Na inampasa
mwenye kumpwekesha Allah awe na itikadi (imani) kuwa kumpwekesha kwake (Allah)
ni neema ya Allah juu yake na kama Angetaka Subhanahu
Wataala angemfanya mnyama au katika wanaomshirikisha Allah au wanaoamini hakuna
maisha ila ya duniani na hawafishwi ila na wakati.
ﭽ
ﯳ ﯴ
ﯵ ﯶﯷ ﯸ
ﯹ ﯺ ﯻ
ﯼﯽ ﯾ ﯿ
ﰀ ﰁ ﰂ
ﰃ ﰄ ﰅ
ﰆ ﰇ ﭼ الحجرات: ١٧
“Wamekusumbulia
kwa kuingia kwao Uislamuni. Sema ‘Msifanye kuwa ni ihsani kwangu kusilimu
kwenu, bali Allah ndiye aliyekufanyieni ihsani kwa kukuongozeni kwenye Uislamu,
ikiwa nyinyi ni wakweli’.”
Ni wazi
kuwa Imani sio tu kusema kauli: لا
إله إلا الله kwani haitomfaa (kauli hiyo) mtu kitu ikiwa
hatofuatilia kwa kufanya vitendo vilivyo wajibu juu yake.
ﭽ
ﭠ ﭡ
ﭢ ﭣ ﭤ
ﭥ ﭦ ﭧ
ﭨ ﭩ ﭪ
ﭫ ﭬ ﭭ
ﭮ ﭯ ﭰ
ﭱ ﭲﭳ ﭴ
ﭵ ﭶ ﭷ ﭼ الأنعام:
١٥٨
“Siku
zitakapofika baadhi ya Ishara za Mola wako, basi mtu (kafiri) haitamfaa imani
yake ambaye alikuwa hakuamini zamani, au (Muislamu) hakuchuma kheri katika
Uislamu wake. Sema: Ngojeni, sisi pia tunangojea”.
Na hakika
kitu kinachotakiwa (mtu afanye) ni kunena kwa Ulimi, na kutenda kwa mujibu wa
nguzo (za Kiislamu) na kuamini kwa moyo Imani iliyojaa moyoni mpaka ikatoka
humo athari yake na athari yake ni vitendo (vyema) kama miangaza inavyotokana
na Jua.
3. Kuamini
Malaika wa Allah: Na huko ni kuamini kuwa Allah anao waja wenye kukirimiwa
Kasema
Allah katika Sura Attahrim aya ya 6:
ﭽ
ﯩ ﯪ
ﯫ ﯬ ﯭ
ﯮ ﯯ ﯰ ﭼ التحريم:
٦
“Hawamuasi Allah kwa amri
zake na wanatenda wanayoamrishwa (yote)”.
Wametakaswa
na upungufu na maasi, wameumbwa na tabia ya aliekuwa hafanyi maasi, chakula
chao ni kufanya “tasbiih” na “tahmiid” (kumsabih na kumshukuru Mola Subhanahu
Wataala). Kila mmoja katika wao amekalifishwa kufanya kazi fulani hachoki
kuifanya wala haghafiliki nayo wala haipuuzi (kuifanya hiyo kazi). Wala
hawasifiki kwa sifa za kula wala kunywa wala kukojoa wala kutema mate na
mengineyo katika uchafu unaotoka mwilini.
Na faida
kubwa ya Imani hii (ya Malaika) ni kuisafisha ‘Itikadi’ ya kumpwekesha Allah (Subhanahu
Wataala) na masalio ya ushirikina, kitu ambacho kilikithiri kwa Waarabu katika
ujahiliya wao kwani walikuwa wakiwafanya Malaika ni Miungu bila ya Allah au
wakiwafanya vizazi vyake Subhanahu Wataala.
Malaika
amewaumba Allah (Subhanahu Wataala) kwa nuru kama alivyomuumba Adam kwa udongo,
na kama alivyowaumba majini kwa Moto usiokuwa
na moshi.
Amesimulia
Assidiqa (Aisha) binti Assidiq (Abu Bakar) RA kutokana na Mtume (Salallahu
Alayhi Wasalam) amesema:
( خلقت الملائكة من نور وخلق
الجان من مارج من نار وخلق آدم مما وصف لكم )
( رواه مسلم )
“Wameumbwa
Malaika kwa nuru, na wameumbwa Majini kwa Moto usiokuwa na moshi (safi ) na ameumbwa Adam kwa
kile mulichosimuliwa (mlichoambiwa).” Ameitoa Muslim.
Na Allah (Subhanahu
Wataala) Amemchagua miongoni mwao Malaika wa kuhishimika (mbora) naye ni Jibril AS ,
naye ndiye Mjumbe wake kwa Mitume. Ama hakika yao
na vipi wameumbwa haya mambo hatukuambiwa cho chote juu yake, lakini
tulichoamrishwa ni kuamini kuwepo kwao na tuilinde haki ya kusuhubiana nao na
vile vile tuimarishe uhusiano wetu nao kama
alivyotuelekeza Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) katika kauli yake:
(إن معكم من لا يفارقكم إلا
عند الخلاء وعند الجماع فاستحيوا منهم وأكرموهم )
“Hakika
wako pamoja na nyinyi wasiowabandukeni isipokuwa wakati wa haja na wakati wa
“jimaa” (anapomuingilia mtu mkewe) basi waoneeni haya na wahishimuni” (hao ni
Malaika).
4. Kuamini
Vitabu vya Allah ambavyo kaviteremsha kwa Manabii wake na Mitume wake, kwani
ameteremsha vitabu kwa Ibrahim, Shiith na kwa Nooh lakini havikujulikana majina
yake na havikujulikana isipokuwa Vitabu vinne:
Azzabuur
kimeletwa kwa Dawood AS
Attawraah
kimeletwa kwa Moosa AS
Al-Injil
kimeletwa kwa Issa AS
Al-Qur'an
kimeletwa kwa Muhammad Salallahu Alayhi Wasalam
Na hii
“Qur'an” imefuta vitabu vyote vilivyotangulia isipokuwa “Tawhiid” kwa sababu
mwito uliokuja kwa “Tawhiid” umelingana katika vitabu vyote vya Allah basi kwa
hivyo haijuzu kuvifuata vitabu hivyo vilivyotangulia.
Kasema Mola
Subhanahu Wataala katika Sura Al-Umran aya ya 85:
ﭽ ﭯ ﭰ ﭱ
ﭲ ﭳ ﭴ ﭵ ﭶ
ﭷ ﭸ ﭹ
ﭺ ﭻ ﭼ
آل عمران: ٨٥
“Na
anayetaka Dini isiyokuwa ya Kiislamu basi haitakubaliwa kwake. Naye Akhera
atakuwa katika wenye khasara (kubwa kabisa)”.
ﭽ ﭓ ﭔ ﭕ
ﭖ ﭗ ﭘ
ﭙ ﭚ ﭛ
ﭜ ﭝ ﭞ
ﭟ ﭠ ﭡ
ﭢ ﭣ ﭤ ﭥ ﭦ
ﭧ ﭨ ﭩ
ﭪ ﭫ ﭬ ﭼ آل
عمران: ٢ - ٤
“Allah,
hakuna aabudiwaye kwa haki isipokuwa yeye mwenye uhai wa milele, na muendeshaji
wa mambo yote (2) Amekuteremshia Kitabu kwa haki, kinachosadiki yaliokuwa kabla
yake. Na aliteremsha Taurat na Injil (3) Zamani ziwe uwongozi kwa watu. Na
akateremsha vitabu vyengine vya kupambanua”.
Na Qur'an
imekusanya yote yaliyomo katika vitabu vilivyotangulia katika mambo ambayo
Allah kayafanya wajibu kwa waja wake.
Kasema
Allah katika Sura Al-Shura aya ya 13:
ﭽ
ﭺ ﭻ
ﭼ ﭽ ﭾ
ﭿ ﮀ ﮁ
ﮂ ﮃ ﮄ
ﮅ ﮆ ﮇ
ﮈ ﮉ ﮊﮋ
ﮌ ﮍ ﮎ
ﮏ ﮐ ﮑ ﭼ الشورى:
١٣
“Amekupeni
Sharia ya Dini ile ile aliyomwusia Nuhu na tuliyokufunulia wewe na tuliyowausia
Ibrahim na Musa na Isa kwamba simamisheni Dini wala msifarikiane kwayo”.
Na Allah (Subhanahu
Wataala) Ameihifadhi Qur'an na hawakuweza (wala hawawezi) mmoja katika maadui
zake kubadilisha ndani yake kitu walau herufi moja kama
vilivyobadilishwa vitabu vilivyotangulia.
ﭽ
ﮏ ﮐ
ﮑ ﮒ ﮓ
ﮔ ﮕ ﮖ
ﮗ ﮘ ﮙ
ﮚ ﮛﮜ ﮝ
ﮞ ﮟ ﮠ ﭼ
فصلت: ٤١ – ٤٢
“Bila shaka hicho ni kitabu kihishimiwacho (41)
Haitakifikia batili mbele yake wala nyuma yake; kimeteremshwa na mwenye hikima
ahimidiwaye (42).”
Na Mola
ameitakia Qur'an ibakie milele mpaka kitakapokuja Kiyama. Na ameifanya iwe
nyepesi kukumbukwa, kuhifadhiwa na kufahamika haiwataabishi watu kufahamu wala
kuifuata (kutekeleza maamrisho yake na kuacha makatazo yake)
ﭽ ﮞ ﮟ
ﮠ ﮡ ﮢ
ﮣ ﮤ ﭼ القمر:
١٧
“Na kwa yakini tumeifanya Qur'an iwe nyepesi kufahamika ili iwe
kikumbusho. Lakini (jee) yuko
anayekumbuka?”
Na hakika
katika Qur'an kuna habari za kila kilichopo kama
alivyotuambia Mtume wa Allah (Subhanahu Wataala) katika kauli yake:
(ستكون من بعدي فتن كقطع الليل
المظلم قيل له : وما المخلص منها يا رسول الله قال : كتاب الله فيه نبأ من قبلكم
وخبر ما بعدكم وحكم ما بينكم وهو الفصل ليس بالهزل ، من تركه من جبار قصمه
الله، ومن ابتغى الهدى في غيره أضله الله
وهو حبل الله المتين ونوره المبين والذكر الحكيم والصراط المستقيم وهو الذي لا
تزيغ به الأهواء ولا تتشعب معه الآراء ولا يمله الأتقياء ولا يخلق على كثرة الرد، وهو الذي لم تنته الجن إذ سمعته أن قالوا : إنا سمعنا قرآنا عجبا ، من قال قوله
صدق ومن حكم به عدل ، ومن عمل به أجر
، ومن اعتصم به فقد هدي إلى صراط مستقيم)
“Kutakuwa baada yangu mitihani kama vipande vya usiku wa giza,
akaambiwa (akaulizwa): Nini kitakachotutoa na hiyo (mitihani) (au
kitachotuokoa) akasema: Kitabu cha Allah, humo ndani yake mna habari ya
waliokuwa kabla yenu na habari itakayokuwa baada yenu na hukumu baina yenu,
nacho ni mpambanuo (baina ya haki na batili) siyo mzaha, anaekiwacha (hicho
kitabu) miongoni mwa waonevu wa watu (wanaoua watu katika ghadhabu “Jabbar”)
basi Allah humvunja, na anaetaka uongofu kwengine pasi na Qur'an Allah
humpoteza, nayo ni Kamba ya Allah iliyo na nguvu, na Nuru yake iliyo wazi, na
kumbusho lililo na hekima, na njia iliyonyooka, kwa hiyo (Qur'an) mapendekezo
hayapotei, wala rai hazikhitilafiani pamoja nayo, wala wachamungu hawachoki
nayo, wala haichakai (katika nafsi za watu) juu ya kurudia kuisoma mara kwa
mara, na ndio hiyo ambayo hawakumaliza majini baada ya kuisikia (inasomwa)
isipokuwa wakasema: Hakika tumesikia kisomo cha ajabu. Anaesema kauli yake (Qur'an) amesema ukweli, na
anayehukumu kwayo amefanya uadilifu, na anaetenda kwa mujibu wake anaongozwa
kwenye njia iliyonyooka.”
5.
Kuamini Mitume wa Allah Rehema zake ziwe
juu yao , kwa
kauli yake Mola Subhanahu Wataala :
ﭽ
ﮗ ﮘ
ﮙ ﮚ ﮛ
ﮜ ﮝ ﮞﮟ
ﮠ ﮡ ﮢ
ﮣ ﮤ ﮥ
ﮦ ﮧ ﮨ
ﮩ ﮪ ﮫﮬ
ﮭ ﮮ ﮯ ﭼ البقرة:
٢٨٥
“Mtume
ameamini yaliyoteremshwa kwake kutoka kwa Mola wake, na Waislamu (pia wameamini
hayo): Wote wamemwamini Allah, na Malaika wake, na Vitabu vyake, na Mitume
yake; (nao hao Waislamu na Mitume wao husema): ‘Hatutafautishi baina ya yoyote
katika Mitume wake (wote tunawaamini)’.”
Na ikiwa
Muislamu ameamini baadhi tu ya Mitume na hakuamini baadhi nyingine basi huyo ni
kafiri kwa mujibu wa kauli yake Mola Subhanahu Wataala :
ﭽ
ﭱ ﭲ
ﭳ ﭴ ﭵ
ﭶ ﭷ ﭸ
ﭹ ﭺ ﭻ
ﭼ ﭽ ﭾ
ﭿ ﮀ ﮁ
ﮂ ﮃ ﮄ
ﮅ ﮆ ﮇ
ﮈ ﮉ ﮊ
ﮋﮌ ﮍ ﮎ
ﮏ ﮐ ﮑ ﭼ
النساء: ١٥٠ – ١٥١
“Hakika wale wanaomkataa Allah na Mitume yake, na
wanataka kutenga baina ya Allah na Mitume yake, kwa kusema: ‘Wengine
tunawaamini na wengine tunawakataa’, na wanataka kushika njia iliyo kati kati
ya haya (si ya Kiislamu khasa wala ya kikafiri). Hao ndio makafiri kweli, na tumewaandalia makafiri adhabu
ifedheheshayo”.
Na lengo la
kuletwa Mitume ni kuwaita watu kwenye Ibada ya Allah na kusimamisha Dini yake.
Amesema Mola Subhanahu Wataala :
ﭽ ﭑ ﭒ ﭓ
ﭔ ﭕ ﭖ ﭗ ﭘ
ﭙ ﭚ ﭛ
ﭜ ﭝ ﭞ
ﭟ ﭼ
الأنبياء: ٢٥
“Na hatukutuma kabla yako mtume ila tulimfunulia ya kwamba
hapana anayestahiki kuabudiwa ila Mimi basi niabuduni.”
Na Amesema Subhanahu
Wataala:
ﭽ ﭴ ﭵ ﭶ
ﭷ ﭸ ﭹ ﭺ ﭻ
ﭼ ﭽ ﭾ ﭼ النحل: ٣٦
“Na bila
shaka tulimpeleka Mtume katika kila umati ya kwamba Muabuduni Allah na
mwepukeni (Iblis) mwovu”.
Na katika
hao Mitume ambao Qur'an imewasimulia na kuwataja majina yao
basi hao ni wajibu kuwaamini kwa kirefu kila mmoja wao peke yake kama Nuuh na Ibrahim na wengineo. Na wale waliokuwa
hawakutajwa kwa jina ni wajibu kuwaamini kwa ujumla.
Anasema
Allah (Subhanahu Wataala) :
ﭽ ﭮ ﭯ ﭰ
ﭱ ﭲ ﭳ ﭴ ﭵ
ﭶ ﭷ ﭼ النساء:
١٦٤
“Na wako
Mitume (tuliwapelekea wahyi) tuliokuhadithia (habari zao) zamani na Mitume
ambao hatuku kuhadithia (habari zao).”
Na Mitume
wote hao wamekuja kuwaongoza na kuwaokoa watu kutokana na upofu (upotofu) na
yametoweka mafundisho yao hao Mitume na zimefutwa Sharia zao isipokuwa Tawhiid
(kumpwekesha Allah (Subhanahu Wataala)), kwani wameafikiana Mitume wote juu
yake (Tawhiid), na imebakia sharia ya Mtume wetu Muhammad (Salallahu Alayhi
Wasalam) ambayo imekuja kufuta sharia zote zilizopita na wala haijuzu kabisa
kufuata sharia yoyote nyingine (ya Vitabu vilivyotangulia) mpaka Siku ya
Kiyama. Kwa hivyo inawabidi watu wote kumuamini Mtume Muhammad (Salallahu
Alayhi Wasalam) na kuamini aliokuja nayo. Na wala mtu asiwasikilize wale
wanaosema kuwa zote hizo ni sharia zilizokuja kutoka Mbinguni kwa hiyo
anayefuata yoyote katika hizo ni sawa. Ni wajibu kumuamini Muhammad kuwa ni
Mtume Mkweli kutoka kwa Allah (Subhanahu Wataala) na kuwa uongozi wake ni
kamili hauna upungufu wala kosa na kuwa yeye ni Mtume wa mwisho aliekuja kwa
Umma huu Salallahu Alayhi Wasalam. Na amepewa na Allah (Subhanahu Wataala)
“Al-Wasila” na Al-Fadhila”.
Na katika
wajumbe (Mitume) wale wanaoitwa “Ulu Al-Azmi “yaani wenye azimio la nguvu na
subira kubwa, na Allah (Subhanahu Wataala) amewataja katika kauli yake:
ﭽ
ﭑ ﭒ
ﭓ ﭔ ﭕ
ﭖ ﭗ ﭘ
ﭙ ﭚ ﭛ
ﭜ ﭝﭞ ﭟ
ﭠ ﭡ ﭢ ﭼ
الأحزاب: ٧
“Na wakumbushe tulipochukuwa ahadi kwa Manabii (wote)
na kwako wewe na Nuhu na Ibrahim na Musa na Issa mwana wa Mariamu na
tulichukuwa kwao ahadi ngumu”.
Na dalili
inayoonesha kuwa Mtume Muhammad (Salallahu Alayhi Wasalam) ni Mtume wa Mwisho
na hakuna Mtume mwengine baada yake kwa mujibu ya kauli ya Allah (Subhanahu
Wataala):
ﭽ ﯧ ﯨ ﯩ
ﯪ ﯫ ﯬ ﯭ ﯮ
ﯯ ﯰ ﯱ ﯲ
ﭼ الأحزاب: ٤٠
“Muhammad
si baba wa yoyote katika wanaume wenu, bali ni Mtume wa Mungu na mwisho wa
Mitume”.
Na mitume
wote wengine kila mmoja kati yao
amepelekwa kwa watu maalumu isipokuwa Mtume Muhammad yeye ameletwa rahma kwa
viumbe wote na watu wote. Na wakati atakapokuja Issa AS
basi atashuka kwa sharia ya Mtume
Muhammad (Salallahu Alayhi Wasalam) na sio kuwa atakuja na sharia mpya.
6. Kuamini
Siku ya Mwisho: Nayo ni Siku ya Kiyama. Na kuamini siku hii ni sehemu katika
fungamano (ahadi baina ya Allah na mja wake) ambalo haitimii Imani isipokuwa
kwa hilo
(fungamano). Na atambue Binaadamu kuwa hakuumbwa bure bila ya kusudio lolote
bali ameumbwa kwa ajili ya kumuabudu Allah.
Kasema
Allah katika Sura Adhaariyat aya ya 56 na 57
ﭽ ﭳ ﭴ ﭵ
ﭶ ﭷ ﭸ ﭹ ﭺ
ﭻ ﭼ ﭽ
ﭾ ﭿ ﮀ
ﮁ ﮂ ﮃ ﭼ
الذاريات: ٥٦ – ٥٧
“Sikuwaumba Majini na Watu ila kwa ajili ya kuniabudu.
Sitaki kwao riziki wala sitaki wanilishe”.
Na kwa
akili inafahamika kuwa anaetaka kwako jambo fulani hapana budi akutake
ulitekeleze hilo
jambo. Amesema Allah (Subhanahu Wataala):
ﭽ ﮮ ﮯ
ﮰ ﮱ ﯓ
ﯔ ﯕ ﯖ ﭼ
المؤمنون: ١١٥
“Je!
Mlidhani ya kwamba tumekuumbeni bure (kwa upuuzi) na ya kwamba ninyi kwetu
hamtarudishwa?”
Na Amesema
Mola Subhanahu Wataala :
ﭽ ﮚ ﮛ ﮜ
ﮝ ﮞ ﮟ
ﮠ ﮡ ﮢ
ﮣ ﮤ ﮥ
ﮦ ﮧ ﮨ
ﮩ ﮪ ﮫ
ﮬ ﮭ ﮮ
ﮯ ﮰ ﮱ
ﯓ ﯔ ﯕ
ﯖ ﯗ ﯘ
ﯙ ﯚ ﭼ القيامة:
٣٦ - ٤٠
“Je! Anafikiri (anadhani)
binaadamu kuwa
ataachwa bure (ovyo tu), asipewe amri za Allah wala makatazo yake? Hakuwa tone la manii lililotonwa? Kisha akawa kidonge
cha damu, kisha akamuumba na akamsawazisha (mwanadamu kamili)? Kisha akamfanya
namna mbili, mwanamume na mwanamke. Je! Hakuwa huyo ni muweza wa kuhuisha
wafu?”
Na Amesema Subhanahu
Wataala:
ﭽ
ﮔ ﮕ
ﮖ ﮗ ﮘﮙ
ﮚ ﮛ ﮜ
ﮝ ﮞ ﮟ
ﮠ ﮡ ﮢ
ﮣ ﮤ ﮥ
ﮦﮧ ﮨ ﮩ
ﮪ ﮫ ﮬ ﭼ
يس: ٧٨ - ٧٩
“Na
katupigia mfano, na kasahau kuumbwa kwake (kwa manii) akasema: “Nani
atakayehuisha mifupa na hali imesagika?” Sema: “Ataihuisha yule aliyeiumba mara
ya kwanza, naye ni mjuzi wa kila (namna ya) kuumba”.
Na Allah
amewajibu washirikina (wanaoabudu wakati) juu ya kauli yao :
ﭽ ﭫ ﭬ
ﭭ ﭮ ﭯ
ﭰ ﭱ ﭲ
ﭳ ﭴ ﭵ
ﭶ ﭼ الجاثية: ٢٤
“Haukuwa uhai ila ni uhai
wetu huu wa Dunia, (hakuna mwengine); tunakufa na tunaishi, wala hakuna
kinachotuangamiza isipokuwa huu huu ulimwengu (kwani ndio ada yake kufisha na
kuhuisha).”
Vile vile
Mola Subhanahu Wataala amewajibu manasara (wakristo) ambao wanaamini Siku ya
Mwisho isipokuwa wao wanaamini kuwa Nabii Isa
AS atajitolea mhanga (fidia) ili
awaokoe na adhabu ya Siku ya Kiyama. Na atawaepusha na malipo mabaya
wanayostahiki kwa maovu waliyoyatenda.
Na pia
amewajibu Subhanahu Wataala mayahudi ambao wanaamini kuwa katika Siku ya Kiyama
lipo lengo kuu kwa ajili yao na wao wamesema:
ﭽ ﭔ ﭕ
ﭖ ﭗ ﭼ المائدة:
١٨
“Sisi ni
wana wa Allah na wapenzi wake.”
Na wote hao
wamesema uongo, na Qur'an imewajibu wao jawabu kali kabisa. Na Siku ya Mwisho
inaanza kwa kubadilika huu Ulimwengu wakati inapopasuka mbingu na nyota
zinapopukutika na majabali (milima) yanapokwenda (yanamung'unyika na kuruka
angani) na wakati inapobadilishwa hii Ardhi yetu (Dunia) ikaletwa ardhi
nyengine na mbingu vile vile zikabadilishwa na kuletwa nyengine na kila kitu
kilichokuweko sasa hivi kitavunjwa vunjwa:
ﭽ
ﯱ ﯲ
ﯳ ﯴ ﯵ
ﯶ ﯷ ﯸ
ﯹ ﯺ ﯻ
ﯼﯽ ﯾ ﯿ
ﰀ ﰁ ﰂ
ﰃ ﰄ ﰅ
ﰆﰇ ﰈ ﰉ
ﰊ ﰋ ﰌ
ﰍ ﰎ ﰏ
ﭼ
الأنعام: ٩٤
“Bila shaka nyinyi mmetujia mmoja mmoja tu, (kila mtu
peke yake na hana mtoto wa kumsaidia wala watumwa wala.....) kama
tulivyokuumbeni mara ya kwanza, na mmeyaacha nyuma yenu tuliyokupeni, na
hatuwaoni waombezi wenu pamoja nanyi ambao mlidai kuwa ni washirika (wa Allah)
kwenu, yamekatika (mahusiano) yalivokuwa kwenu na yamekupoteeni mliyokuwa
mkidai.”
7. Kuamini
kadari kheri yake na shari yake kuwa inatoka kwa Allah (Subhanahu Wataala) kwa
kauli yake Allah Taala:
ﭽ ﭼ ﭽ
ﭾ ﭿ ﮀ
ﮁ ﮂ ﮃ
ﮄ ﮅ ﮆ
ﭼ الحجر: ٢١
“Na hakuna
cho chote ila asili yake inatokana na sisi, wala hatukiteremshi ila kwa kipimo
maalum (si ovyo ovyo tu).”
Na kwa
kauli yake:
ﭽ ﰌ ﰍ
ﰎ ﰏ ﰐ
ﭼ القمر: ٤٩
“Kwa hakika Sisi Tumekiumba
kila kitu kwa kiasi (chake makhsusi).”
Na kwa
kauli yake:
ﭽ
ﮯ ﮰ
ﮱ ﯓ ﯔ
ﯕ ﯖ ﯗ
ﯘ ﯙ ﯚ
ﯛ ﯜ ﯝ
ﯞ ﯟﯠ ﯡ
ﯢ ﯣ ﯤ
ﯥ ﭼ الحديد: ٢٢
“Hautokei msiba katika ardhi wala katika nafsi zenu ila umekwisha
andikwa katika kitabu cha (Allah) kabla hatujauumba. Kwa yakini hayo ni rahisi kwa Allah.”
Na kauli
yake Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) katika hadithi aliyoitowa Arrabii Ibn
Habiib :
( يا عبدي إنك لن تؤمن ولن تبلغ
حقيقة الإيمان حتى تؤمن بالقدر خيره وشره أنه من الله، قال كيف لي أن أؤمن بالقدر خيره وشره ؟ قال : تعلم أن ما أصابك لم يكن ليخطئك وما
أخطأك لم يكن ليصيبك فان مت على غير هذا دخلت النار )
“Ewe mja
wangu kwa yakini wewe hutoamini na wala hutoufikia ukweli wa Imani mpaka uamini
kuwa Kadari kheri yake na shari yake ni kutoka kwa Allah, Akasema: Vipi hata
niweze kuiamini Kadari kheri yake na shari yake? Akamjibu: Ujue kuwa
yaliyokusibu (au yaliyokupata) haiwezekani kuwa yangeweza kukukosa kukusibu na
(vile vile) yaliyokosa kukusibu haiwezekani kuwa yangekusibu, na ukifa nawe
unaamini vinginevyo basi utaingia
Motoni”.
Alipokwenda
Omar bin Al-Khattab RA huko Amwaas kwa ajili ya kupigana vita akasikia kuwa
kuna “Taawuun” (maradhi yaambukizayo kwa haraka, na yanayoua watu) katika mji
huo basi hakuuingia. Na alikuwa Abu Ubaidah bin Al-Jarrah RA amemuwahi kwa
kuingia huo mji akamuambia: Je (hukuingia) kwa kukimbia kadhaa ya Allah ewe
Amiri wa Waumini (kukimbia yaliyokwisha amuliwa na Allah kuwa yatatokea).
Akasema: Lau kama angeyasema maneno haya mwengine (sio wewe) ewe Aba Ubaidah.
Ndio twaikimbia kadhaa ya Allah kuindea Qadari yake (Allah (Subhanahu Wataala).
Na Omar RA alikuwa kisha washauri Masahaba katika jambo hilo akasema Abdul Rahman bin Auf:
Nimehifadhi katika jambo hili hadithi ya Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) asema:
( إذا
سمعتم به بأرض فلا تقدموا عليه ، و إذا
وقع بأرض وأنتم بها فلا تخرجوا فراراً منه )
“Mkiusikia
umo katika ardhi (huo ugonjwa wa “Taawuun”) basi msiende huko, na kama ukitokea katika ardhi nyie mmo ndani yake basi
msitoke kuukimbia”
Basi Omar
akamshukuru Allah (Subhanahu Wataala) na kumsifu kisha akaondoka.
Ametoa Abu
Ubaidah kutokana na Jabir bin Zayd kuwa amesema: imenifikia habari kutoka kwa
Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) kuwa amesema:
(كل شيء
بقـضاء وقـدر حتى العجز والكيس )
“Kila kitu
(kinatokea) kwa kadhaa na kadari hata udhaifu wa kufanya mambo na uhodari.”
Na
aliporudi Ali bin Abi Talib kutoka Safiin, mzee mmoja alimuuliza: Ewe Amiri wa
Waumini tuambie kuhusu kwenda kwetu “Shaam” je kulikuwa kwa “Kadhaa” na “Kadari”. Akasema: Naapa kwa yule aliyeipasua
punje (ya mbegu ikatoa mmea) na akaumba binaadamu hatukukanyaga mahala wala
hatukushuka bonde wala hatukupanda mlima isipokuwa kwa Kadhaa na Kadari.
Akasema yule mtu mzima: Naifikiria ile taabu yangu (niliyoipata katika huo
msafara wa vita) sidhani Wallahi kama nitapata
malipo yoyote mazuri. Akasema Ali: Bali ewe
mzee Allah amewapa malipo makubwa nanyi mnakwenda katika mwendo wenu na katika
kurejea kwenu na hamkuwa mmelazimishwa katika yote mliyoyafanya wala haikuwa
dharura ikiwafanya mtende hayo. Akasema yule mzee: Vipi hatukulazimika kutenda
tuliyoyatenda na Kadhaa na Kadari ndio iliyotupeleka huko na ndio
iliyoturejesha kutoka huko. Basi hapo akasema Ali: Ole wako ewe mzee, unadhania
kuwa kadhaa hiyo ni ya kulazimishwa na kadari hiyo haina budi iwe; basi kama
ingekuwa hivyo kusingekuwa na thawabu wala adhabu (malipo mabaya) na
kusingekuwa na kuahidiwa malipo mazuri (kwa afanyae vitendo vizuri) na
kuahidiwa malipo mabaya nayo ni Moto (kwa afanyae vitendo viovu), na vile vile
kusingekuwa na kuamrishana kufanya mema na kukatazana mabaya, vile vile
kusingekuwa na lawama kwa afanyae madhambi wala kusifiwa kwa afanyae mazuri,
pia asingekuwa mtu mwema ndio wa kusifiwa badala ya mtu muovu, wala mtu muovu
ndio wa kulaumiwa badala ya mtu mwema, kauli kama hizo ni za wale wanaoabudu
masanamu na askari wa shetani na wenye ugomvi na “Arrahman” na wanaotoa
ushahidi wa batili (dhulma) na waliopotoka katika njia ya sawa na hao ndio
“Kadariya” wa Umma huu na ndio Majusi wake (wanaoabudu Moto). Kwa hakika Allah
ameamrisha kwa hiyari yake mtu na amekataza kwa kumhadharisha mtu na mabaya
(adhabu) na amekalifisha kwa wepesi na wala hakuasiwa kwa kushindwa na wala
hakutiiwa kwa kuwalazimisha watu (wamtii) na wala hakupeleka Mitume bure na
hakuumba mbingu na Ardhi bila ya kusudio.
ﭽ ﭙ ﭚ
ﭛ ﭜﭝ ﭞ
ﭟ ﭠ ﭡ
ﭢ ﭼ ص: ٢٧
“Hii ni dhana ya wale
waliokufuru basi adhabu kali ya Moto itawathibitikia wale waliokufuru”.
Hapo yule
mzee akasimama naye amefurahi na sio maana ya Kadari kutegemea na aseme mtu:-
Nikiandikiwa kitu hicho kitanipata na huu ni udhaifu kwani mja ameumbwa ili
afanye (vitendo vizuri na ajikataze na maovu) na Allah (Subhanahu Wataala)
afanya ayatakayo na bora ya afanyayo mtu ili ajikaribishe kwa Mola wake ni
kufanya zile faridha (Sala tano, Zaka, kufunga Ramadhani na Hija) ambazo
amemlazimisha kuzifanya.
Na vile
vile tabia njema zinakuwa pamoja na hizo faridha. Na Mtume (Salallahu Alayhi
Wasalam) amehimiza haya katika kauli yake:
( بعثت
متمما لمكارم الأخلاق )
“Nimetumwa
ili nitimize tabia njema”
Na akasema:
( لو كان حسن الخلق رجلا لدخل الجنة )
“Kama ingelikuwa tabia njema ni mtu angeingia Peponi.”
Imetolewa
kuwa Ali bin Abi Talib amesema: Ewe Allah ulietakasika, kitu gani kilichowafanya
watu wengi wakatae kufanya kheri, amenistaajabisha mtu anaejiwa na ndugu yake
kumtaka haja kisha asijione katika nafsi yake mwenye kumiliki kufanya kheri,
kwani kama tungekuwa hatungojei thawabu (malipo mazuri) au hatuogopi malipo
mabaya basi juu ya hivyo tungelazimika kuwa na tabia njema kwa sababu
zinatuonesha njia ya kuokoka. Akasimama mtu akasema: Nakutolea mhanga baba
yangu na mama yangu ewe Amiri wa Waumini, je umesikia hayo kwa Mtume (Salallahu
Alayhi Wasalam)? Akasema: Ndio na kilichokuwa bora kuliko hayo: Tulipojiwa na
mateka wa “Teyyii” akasema mtoto wa kike (katika hao mateka): Ewe Muhammad, ameangamia baba yangu na
amepotea msaidizi wangu, na ni bora uniwachie wala usiwafanye waarabu
wanifurahikie (kwa kuchukuliwa mateka na kushindwa) kwani mimi ni binti wa
kiongozi wa watu wangu, alikuwa baba yangu akimsaidia mwenye matatizo, na
akimshibisha mwenye njaa na amuhami aliedhulumiwa na humfariji alie na uzito na
alisha chakula na atoa Salamu (kuwaamkia watu) wala hamrudishi mtu haja yake
hata kidogo: mimi ni mtoto wa Haatim Taaiy. Basi hapo akasema Mtume (Salallahu
Alayhi Wasalam):
(يا جارية هذه صفة المؤمن لو
كان أبوك إسلاميا لترحمنا له خلوا عنها فإن أباها كان يحب مكارم الأخلاق والله يحب
مكارم الأخلاق)
“Ewe
mwana mwari (mtoto wa kike bado hajaolewa) hizi ni sifa za muumini, kama angekuwa baba yako Muislamu basi tungelimuombea
rehema (arehemewe na Allah), muachieni kwani baba yake alikuwa apenda tabia
njema, na Allah azipenda tabia njema.”
Na katika
mambo aliyokuwa akiyahimiza Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) na aliyoyausia ni
mwendo mzuri katika kuingiliana na watu na katika biashara na kujikataza
kufanya khiyana na kughishi na mwendo
mbaya wo wote ule na kwa vyovyote vile.
Kwa hakika
mwendo mzuri (maingiliano mzuri na watu) ni katika ibada ambazo
zinamkaribirisha mtu na Allah (Subhanahu Wataala) na hupenda Mola Subhanahu
Wataala waja wake wawe na mwendo mzuri kwa kuwahurumia na kuwapenda. Imetolewa
hadithi kuwa Ali bin Abi Talib alisema: “Kwa yakini Allah (Subhanahu Wataala)
ameweka thawabu kwa wanaomtii na adhabu kwa wanaomuasi kwa ajili ya kuwakimbiza
waja wake kutokana na adhabu yake na kuwapeleka katika Pepo yake”. Vile vile
amesema: Tahadhari asikuone Allah (Subhanahu Wataala) katika kumuasi na
asikukose kwenye kumtii ili usiwe katika waliohasirika. Na ukiwa na nguvu tumia
nguvu hizo katika kumtii Allah, na ukidhoofika basi uwe dhaifu wa kushindwa kuyafanya
maasi ya Allah. Pia amesema: Chochote unachokiona wewe ni kheri lakini
chasababisha kuingia Motoni hicho si kheri, na unachokiona ni shari lakini
chasababisha kuingia Peponi hicho sio shari, na kila raha (ya Duniani)
isiyokuwa raha ya Pepo (“Al-Jannah”) ni upuuzi tu, na kila balaa isiyokuwa
adhabu ya “Jahannam” ni kheri.
Na wamesema
wafasiri wa Qur'an katika kauli yake Subhanahu Wataala:
ﭽ ﯦ ﯧ
ﯨ ﭼ
البقرة: ٨٣
“Na
semeni na watu kwa wema”
Yaani kauli
nzuri isiyokuwa na ukali ndani yake, na kauli nzuri (au njema iliyohimizwa
katika Aya hii) imechukua kila aina ya wema anaoufanya binaadamu kwa binaadamu
mwenzake au hata wanyama kwani imesemwa: kama
ungefanya wema kwa kila kitu lakini ukamfanyia ubaya kuku basi ungekuwa mbaya
(si mwema).
Vile vile
imepokewa katika hadithi:
( المسلم
من سلم المسلمون من لسانه ويده )
“Muislamu ni
yule ambaye Waislamu wanasalimika na (shari) ya ulimi wake na mkono wake.”
Na Allah (Subhanahu
Wataala) asema katika kitabu chake kitukufu:
ﭽ ﭒ ﭓ ﭔ
ﭕ ﭖ ﭗ ﭘ ﭙ
ﭚ ﭛ ﭜ
ﭝ ﭞ ﭟ
ﭠ ﭡ ﭼ النساء:
١١٤
“Hakuna
kheri katika mengi wanayoshauriana kwa siri, isipokuwa (mashauri yao ) wale wanaoamrisha
kutoa Sadaka au kufanya mema au kupatanisha bina ya watu.”
Basi katika
kutekeleza maamrisho ya Aya hii na zilizo mfano wake ni matengeneo ya jamii na
hubakia imeshikamana katika mambo yanayohusu haki za watu baadhi yao kwa baadhi kwani
huwafanya kuoneana huruma, kupenda kutizamana, kupendelea wenziwao juu ya nafsi
zao. Na kujitolea mhanga kwa maslaha ya jamii. Na jamii (mujtamaa) kuchukua
dhamana ya kusuluhisha baina ya wanaogombana ni katika mambo ambayo sharia ya
Kiislamu imeshughulika nayo sana
na imeyahimiza.
Kasema
Allah katika Sura Annisa aya ya 114:
ﭽ ﭣ ﭤ
ﭥ ﭦ ﭧ
ﭨ ﭩ ﭪ
ﭫ ﭬ ﭼ النساء:
١١٤
“Na atakaefanya hivi kwa
kutaka radhi ya Allah, basi tutampa ujira mkubwa.”
Na
kupatanisha watu ni miongoni mwa mambo bora yanayomkaribisha mja kwa Mola wake.
Na nani
aliekuwa nafsi yake haitaki kupata kila kilicho bora katika Dunia na Akhera,
hakuna isipokuwa aliye dhaifu.
Inasemekana
kuwa Omar bin Abdul-Aziz rehema za Allah ziwe juu yake- amesema: Sikupata
daraja katika Dunia isipokuwa nafsi yangu ikatamani kupata daraja ya juu zaidi
(kuliko ile ya kwanza) mpaka nikafikia kupata Khilafa Tukufu (Utawala wa
uadilifu wa hukumu ya Allah), hapo nikaikataa Dunia na nafsi yangu ikatamani
Pepo (“Al-Janna”).
Na Mtume
(Salallahu Alayhi Wasalam) ameisifu daraja hii mpaka akasema:
(ألا أخبركم بأفضل من درجة الصيام والصلاة والصدقة؟ قالوا : بلى يا
رسول الله، قال صلاح ذات البين، فإن فساد ذات البين هي الحالقة)
“Je
niwaambie iliyo bora kuliko daraja ya Saumu na Sala na Sadaka? Wakasema: Ndio
ewe Mtume wa Allah, akasema: Kusuluhisha waliogombana kwani kuwaachia
wanaogombana bila ya kuwapatanisha huzidi uhusiano kuharibika hatimaye huutia
udhofu Uislamu.”
Qur'an
imeusia kupatanisha wanaogombana katika kauli yake Subhanahu Wataala:
ﭽ
ﯜ ﯝ
ﯞ ﯟ ﯠ
ﯡﯢ ﯣ ﯤ
ﯥ ﯦ ﭼ الحجرات: ١٠
“Kwa hakika Waislamu ni ndugu; basi patanisheni baina ya ndugu zenu, na
mcheni Allah, (msipuuze jambo la kupatanisha) ili mrehemewe”.
Basi ni
lazima familiya zishikane, na mshikano wenye nguvu zaidi baina yao ni mshikano
wa Tawhiid (Kumpwekesha Allah (Subhanahu Wataala) yaani mshikano wa Uislamu),
kisha mshikano wa mapenzi na kuwasiliana baina ya “Arhaam” (jamaa wanaohusiana
kwa damu) na kutambua haki zao, na kuwatembelea mafakiri kwa kuwapa Zaka kutoka
kwa matajiri na mengineyo yasiokuwa Zaka kama sadaka zilizozidi katika mali.
Imetolewa
hadithi isemayo:
( جبلت
النفوس على حب من أحسن إليها وبغض من أساء إليها )
“Nafsi
zimeumbwa na tabia ya kumpenda yule anayezifanyia wema na kumchukia yule
anayezifanyia uovu”.
Kwa haya na
mfano wake kunatokea kupendana na kushikana baina ya watu na yatekelezwa kauli
ya Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam):
( المؤمنون بعضهم أولياء بعض
يسعى بذمتهم أدناهم ، و يرد عليهم أقصاهم ،
وهم يد على من سواهم )
“Waumini ni
marafiki wao wenyewe kwa wenyewe, ahadi yao inachungwa na wote hata anapoitoa
mnyonge wao, na anawakatalia ahadi hata aliye mbali kati yao, na wao ni mkono
mmoja (hushirikiana) dhidi ya maadui zao.”
Na kauli
yake Salallahu Alayhi Wasalam:
( مثل المؤمنون في توادهم وتراحمهم وتعاطفهم مثل الجسد الواحد
إذا اشتكى منه عضو تداعى له سائر الجسد بالسهر والحمى )
“Mfano wa Waumini katika kupendana kwao na kuhurumiana kwao na
kufikiriana kwao ni kama mwili mmoja kikishtakia kiungo kimoja ndani yake basi
mwili mzima huyahisi yale maumivu ukakesha na kupata homa.”
Inabainika
kuwa mambo haya ndio msingi wa uhusiano baina ya watu katika mujtamaa (jamii)
ya Kiislamu bali ni juu ya Waislamu mkubwa wao na mdogo wao, tajiri wao na
maskini wao, kiongozi wao na raia wao wawe katika msingi huu wa uhusiano baina yao . Mtume (Salallahu
Alayhi Wasalam) amekanusha Imani ya mtu aliyekuwa hampendelei mwenzake kama anavyojipendelea nafsi yake, akasema (Salallahu
Alayhi Wasalam):
( لا
يؤمن أحدكم حتى يحب لأخيه ما يحب لنفسه )
“Haamini
mmoja wenu mpaka ampendelee ndugu yake (katika Uislamu) kile anachojipendelea
nafsi yake.”
Na Amesema
Salallahu Alayhi Wasalam:
(والله
في عون العبد ما دام العبد في عون أخيه )
“Na Allah
yuko katika kumsaidia mja wake madamu huyo mja yuko katika kumsaidia ndugu
yake(katika Uislamu).”
8. Na
akaitoa mali (kuwasaidia
watu) juu ya kuwa anaipenda (hiyo mali ). Akawapa jamaa zake,
mayatima, maskini, na wapita njia (waliokatikiwa na watani wao), wanaoomba, na
katika kuwakomboa (kuwapa uhuru) watumwa.
Inadhihirika
hapa kuwa mahimizo haya Allah ameyaleta katika sadaka sio Zaka ya mali , kwa
sababu Amesema katika mwisho wa Aya hii (Sura Al-Baqarah Aya ya 177) baada ya
mahimizo haya:
وآتى الزكاة “na kutowa Zaka”.
Na kusudio
la kuamrishwa mtu atoe mali
yake kwa mujibu wanavyosema wataalamu ni kujikomboa na pingu za kun`gan`gania mali , na
kujipendelea kheri nafsi yake tu. Vile vile kusudio lake
ni kuikomboa nafsi na pingu za kupenda
mali kwa hiyo anakuwa mtu
huyu huru kutokana na utumwa wa mali
na kuin’gan’gania Dunia. Kuin’gan’gania Dunia (kushughulika nayo sana ) inawafanya watu
kuwa dhalili. Na wale wenye nafsi zilizo huru na matamanio ndio walio huru
katika jamii (mujtamaa).
Na kupeana
kunaifanya jamii ikamatane baina ya wadogo na wakubwa, kuwasiliana kwa mali ndiko
kunakotia nguvu uhusiano baina ya Waislamu hasa wanaohusiana kwa damu. Kama
ilivyokuja katika hadithi ya Arrabii katika kitabu chake cha kutegemeka, na
vile vile ameitoa Al-Bukhari kutoka kwa Anas bin Malik RA: Alikuwa Abu Talhah
katika Maansari waliokuwa na mitende mingi zaidi huko Madinah, na ilikuwa
katika mali yake anayoyapenda zaidi (shamba liitwalo) “Baiyrahaa” na ilikuwa
mbele ya Msikiti (wa Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam)), na alikuwa Mtume
(Salallahu Alayhi Wasalam) anaingia ndani yake na kunywa maji yake mazuri. Basi
ilipoteremka Aya:
ﭽ ﭑ ﭒ
ﭓ ﭔ ﭕ
ﭖ ﭗ ﭼ آل
عمران: ٩٢
“Hamtaweza
kuufikia wema khasa mpaka mtowe katika vile mnavyovipenda”.
Akasimama
Abu Talhah akasema: Ewe Mtume wa Allah, asema Mola Subhanahu Wataala :
“Hamtaweza kuufikia wema khasa mpaka mtowe katika vile mnavyovipenda” na kwa
hakika katika mali
yangu niyapendayo zaidi ni Baiyrahaa nayo ni sadaka nimeitoa kwa Allah.
Nataraji kupata malipo yake mazuri kwake Mola Subhanahu Wataala, basi yaweke
ewe Mtume wa Allah pale anapokuonesha Allah. Akasema Mtume (Salallahu Alayhi
Wasalam): “Bakhin” “Bakhin” (neno hili lasemwa katika kuridhika na kusifu kitu)
mali hiyo imepata faida, mali hiyo
imepata faida. Na katika hadithi nyingine “mali
hiyo inakwenda, mali
hiyo inakwenda Peponi”. Na nimesikia uliyoyasema na mimi naona uwape mali hayo jamaa
zako, akasema Abu Talhah: Nafanya hivyo Ewe Mtume wa Allah akayagawa Abu Talhah
baina ya jamaa zake na watoto wa Ami yake. Na huu mfano ni wa juu kabisa katika
kutoa mali .
Na kama
alivyofanya katika wafuasi wa hao (Masahaba) Imamu wetu Muhammad bin Abdullah
Al-Khaliliy -Allah (Subhanahu Wataala) Amrehemu- naye alikuwa miongoni mwa
matajiri katika zama zake na akafa naye haoni kuwa Dunia hii ina thamani
yoyote. Mali yake yote
ameitoa kwa kuitia nguvu Dola ya Kiislamu (yeye ndiye Imamu au Khalifa wa Dola
hiyo hapa Oman )
akafa naye apendwa na raia zake na apendwa na Mola wake na wala hakudhurika kwa
kutokuacha kitu.
Inasemekana
kuwa anaependa kuiendea Akhera basi na atangulize mali yake huko kwa kuitoa katika
njia ya kheri.
Na hapana
budi katika kutoa mali kuwe na mambo mawili, kwanza niya nzuri (kuwa unafanya
hivyo kufuata amri ya Allah na kujikaribisha kwake sio kutaka kusifiwa na watu)
na pili kuamini kuwa utalipwa malipo mazuri na Allah (Subhanahu Wataala) na
bila ya hayo mawili anakhasiri mtu mali yake na Akhera yake.
Na
kuamrishana mema na kukatazana mabaya ni katika mshikamano ulio na nguvu zaidi
baina ya Waislamu. Na anayeamrishwa au kukatazwa kitu ijapokuwa atachukiwa
wakati huo anapokatazwa na kuona uzito, lakini hatimaye atashukuru wakati
atakapoona faida yake katika nafsi yake na jamii yake. Na methali inasema:
Kwenye kupambazuka kwa Asubuhi ndio watu waushukuru mwendo wa usiku. Na subira
haina budi kwa anayeamrisha na anayeamrishwa na anayekataza na anayekatazwa.
Ndiyo maana Allah (Subhanahu Wataala) amemalizia wasiya wa Luqman kwa mtoto
wake:
ﭽ ﯤ ﯥ ﯦ ﯧ
ﯨ ﯩ ﯪ
ﯫ ﯬ ﯭ
ﯮ ﯯ ﭼ لقمان:
١٧
“Ewe
mwanangu! Simamisha Sala, na uamrishe mema, na ukataze mabaya, na usubiri juu
ya yale yatakayokusibu.” (Sura Luqman Aya 17).
Na Allah (Subhanahu
Wataala) asema:
ﭽ ﭑ ﭒ ﭓ
ﭔ ﭕ ﭖ ﭗ ﭘ
ﭙ ﭚ ﭛ
ﭜ ﭝ ﭞ
ﭟ ﭠ ﭡ ﭼ
العصر: ١ - ٣
“Naapa kwa zama (zako ewe Nabii Muhammad au zama zote tokea
mwanzo mpaka mwisho) kuwa Binaadamu yuko khasarani isipokuwa wale walioamini na
wakafanya vitendo vizuri, na wakausiana (kufuata) haki na wakausiana
(kushikamana) na Subira, (kustahamiliana)”.
Kwa hiyo
unaona kuwa hapana budi kuwa na subira katika hali yoyote ile.
Zitatengenea
jamii na koo iwapo kutakuwepo na kuamrishana mema na kukatazana mabaya, na
huendelea kuwa katika hali hiyo ya kheri madamu wanakutanika juu ya msingi huu
(wa kuamrishana mema na kukatazana mabaya). Ama akiachwa anaetaka kufanya
mabaya bila kukamatwa mkono wake na kuzuiwa kufanya hivyo hapo ndipo inapo enea
balaa kwa wote kwa wale wanaofanya hayo mabaya na vile vile wale wanaonyamaza.
Na mfano wao hawa ni mfano wa wale waliopanda jahazi na kisa chao maarufu
kilicho tajwa katika Al-Bukhari: “Mfano wa aliesimama kwenye mipaka ya Allah na
alietoka nje yake ni kama watu walioingia jahazini kwa kura wengine wakapata
kuingia juu na wengine wakaingia chini. Na wakawa wale walio chini wakitoka
kuchota maji lazima wawapitie walio juu yao basi
wakasema lau kama tungelitoboa hili jahazi
tukapata mahitajio yetu bila ya kuwaudhi walio juu yetu. Basi kama wangewaacha,
wale walio juu, wafanye watakavyo wangeangamia wote, na kama
wangewazuia wasifanye hivyo wangeokoka wao na wakaokoka wote (walio jahazini).”
Na hii ndio
shani ya watu ambao hawakatazani mabaya, hakika wataangamizwa wote pamoja kwa
haraka au wapewe muda mpaka baadaye.
ﭽ
ﭼ ﭽ
ﭾ ﭿ ﮀ
ﮁﮂ ﮃ ﮄ
ﮅ ﮆ ﭼ المائدة: ٧٩
“Hawakuwa wenye kuzuiana (kukatazana) mambo mabaya
waliyokuwa wakiyafanya, uovu ulioje wa jambo hili walilokuwa wakilifanya”.
Na miongoni mwa mambo yanayoleta uadui baina ya jamaa na
jirani ni kushindaniana juu ya Dunia na kupenda mali kiasi cha kuingia katika
maasi na kutojali njia ya kuipata hiyo mali ijapokuwa njia hiyo inawaudhi jamaa
zake au jirani zake na huu ndio umasikini hasa. Amesema Abu Attayyib:
“Anaetumia masaa chungu nzima katika kukusanya mali kwa
kuuogopa umasikini basi hivyo alivyofanya ndio umaskini wenyewe”.
Pia amesema:
“Kutajikana kwa mtu ni umri wake wa pili, na anachohitaji
ni kiasi anachokula, kutafuta zaidi ni mashughulisho.”
Anasema
Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam):
(من جمع
مالا من تهاوش أذهبه الله في نهابر )
“Anaekusanya
mali
kwa kuchanganya halali na haramu, Allah ataiondoa kwa njia za maangamizo”.
Namuomba
Allah Mwenye uwezo wa kila kitu aihami nchi hii (Oman ) na kila uharibifu na
mharibifu na kila anayeiingia kwa kuitakia ubaya kwa husda na chuki.
Ewe Mola
anaeitakia nchi hii au watu wake huo ubaya basi mrudishie ubaya huo mwenyewe na
vijaalie vile vitimbi vyake ndio kuangamia kwake. Na hakuna uwezo wala nguvu
isipokuwa kwa Allah.
Vile vile kama inavyompasa Muislamu kuamini kufufuliwa inampasa
kuamini mauti pia.
Na mauti ni
kutoka roho kwenye mwili (kufarikiana
roho na mwili), na kitu hicho chajulikana na Muislamu na kafiri na kila mtu
atambua kitu hichi kwa sababu kinampitia kila mtu anapoona watu wanakufa kila siku.
Na juu ya haya inabidi kuamini mauti kwa kauli yake Subhanahu Wataala:
ﭽ ﮞ ﮟ
ﮠ ﮡ ﭼ آل
عمران: ١٨٥
“Kila nafsi
itaonja Mauti”
Kila kitu hakina budi kuwa na mwisho hata visivyo na roho
kwa kauli yake Subhanahu Wataala:
ﭽ ﮖ ﮗ
ﮘ ﮙ ﮚ ﭼ القصص:
٨٨
“Kila kitu kitaangamia isipokuwa yeye Allah”
Na sifa yake mauti ni kuonekana Malaika wa Mauti na roho
(ya binaadamu) basi mara tu roho inapomuona huyo Malaika wa mauti inavutika
kwenda kwake kama namna ya smaku (magnet) inavyovuta chuma. Hivi ndivyo isemwavyo.
Na Allah ndiye Mjuzi zaidi (wa kila kitu).
Na katika kaburi, nalo ndio mlango wa mwanzo kuingia
Akhera, anajua maiti nini mwisho wake kwani kaburi ima ni bustani katika
mabustani ya Pepo kwa Muumini au shimo katika mashimo ya Moto kwa kafiri. Basi
anabakia humo kaburini ima katika raha ikiwa ni Muumini au anaadhibiwa ikiwa ni
kafiri. Bali kabla ya hivyo kila mmoja katika Muumini na kafiri anajua nini
mwisho wake kabla ya kutoka roho yake wakati anapowaona Malaika wamehudhuria
kukamata roho yake, kwani wanaikamata roho ya Muumini Malaika wapole wenye
huruma, ile kuwaona hao Malaika inamsahilishia Muumini tabu ya Mauti kwa sababu
atajua kuwa hataadhibiwa baada ya wakati huu.
Kasema
Allah (Subhanahu Wataala):
ﭽ
ﭡ ﭢ
ﭣ ﭤ ﭥ
ﭦ ﭧﭨ ﭩ
ﭪ ﭫ ﭬﭭ
ﭮ ﭯ ﭰ
ﭱ ﭼ يونس: ٦٤
“Wao wana
bishara njema katika maisha ya dunia na katika Akhera. Hapana mabadiliko katika
maneno ya Mwenyezi Mungu. Huko ndiko kufuzu kukubwa.”
Na
wanakamata roho ya kafiri Malaika wakali wenye nguvu wasiokuwa na huruma, na
wanain’goa roho yake kwa nguvu na fujo kitu kinachomzidishia maumivu na
kukereka na dhiki kwa sababu hapo anajua kuwa yatakayo kuja baada ya mauti
yatakuwa ya taabu zaidi kuliko mauti yenyewe.
ﭽ ﭧ ﭨ ﭩ
ﭪ ﭫ ﭬ ﭭ ﭮ ﭯ ﭰ
ﭱ ﭲ ﭳ
ﭴ ﭵ ﭶ
ﭷ ﭸ ﭹ
ﭺ ﭻ ﭼ الفرقان:
٢٢ - ٢٣
“Siku
watakayowaona Malaika haitokuwa furaha siku hiyo kwa waasi, (itakuwa ndio siku
ya kutolewa roho zao); na watasema siku hiyo): Mungu atuepushie mbali!. (Lakini
haitafaa kitu Dua hiyo). Na tutayaendea yale waliyoyatenda katika amali zao
tuzifanye kama mavumbi yaliyotapanywa
(yaliyotawanyika)"
Unaona kuwa
Allah (Subhanahu Wataala) Amesema juu ya Waumini kuwa watakuwa na furaha
(Bushra) na amesema juu ya waasi watakuwa hawana furaha siku hiyo na vitendo
vyao vizuri walivyovifanya havitawafaa kitu (vitakuwa bure kwa sababu hawakuwa
Waumini). Kasema Allah:
ﭽ ﭠ ﭡ ﭢ
ﭣ ﭤ ﭥ ﭦ ﭧ
ﭨ ﭩ ﭪ
ﭫ ﭬ ﭭ
ﭮ ﭯ ﭰ
ﭱ ﭲ ﭼ الأنعام:
١٥٨
“Siku
zitakapo fika baadhi ya Ishara za Mola wako, kuamini hapo hakutomfaa mtu kitu,
ikiwa hakuwa ameamini kabla yake, au amefanya kheri katika Imani yake”.
Na wasema
wafasiri wa Qur'an katika Aya iliyotangulia maana ya حجرا
محجورا ni kuomba kinga ya kuepushwa na Malaika wa
mauti.
Wakati
yalipomjia mauti Amru bin Al-Aas mtoto wake Abdullah bin Amru akamwambia: Ewe
baba angu ulikuwa wasema: Laiti nimpate mtu mwenye akili anielezee mauti yakoje
na sasa wewe ndie yule mwenye akili tuelezee yakoje, akasema: “Naona kama
mbingu imebatana na ardhi na najiona kama navuta pumzi kutokana na tundu ya
sindano na kama roho yangu inavutwa kutoka mwilini mwangu kama mfano wa sufi inayovutwa
kwa nguvu katika miba” au hivyo ni maana ya hadithi hiyo ijapokuwa haikuja kwa
lafdhi hiyo. Basi hebu angalia ikiwa roho ya anayempwekesha Allah (Subhanahu
Wataala) (Muwahhid) inatolewa hivyo vipi itakuwa roho ya kafiri!!
Twamuomba
Allah (Subhanahu Wataala) salama!
Wakati
Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) alipokuwa akitokwa na roho yalikuwa maumivu
yake yanamzidi akasema: “Hakika mauti yana maumivu makubwa (yana shida)” na
akaomba Umma wake upunguziwe maumivu. Allah amjazi kheri kwa kuwaonea huruma
Umma wake.
Na hakuna
mtu anaejua wapi roho inakwenda baada ya mauti kwani mfano wake ni kama mwangaza wa taa ikizimika haujulikani wapi
umekwenda, isipokuwa kwa habari iliyokuja kuhusu roho za Mashahidi (waliokufa
vitani) kuwa zitakuwa katika vifua vya ndege wa kijani zilizotundikwa chini ya
Arshi na kitu hichi chawahusu Mashahidi tu. Na ni mdhaifu na ni mkosefu wa hima
yule anayeiwacha shahada (kufa kwa ajili ya kunyanyua jina la Allah (Subhanahu
Wataala)) wakati inapomjia na akayataka maisha ya Dunia.
Na baada ya
mauti hakuna budi kufufuliwa na siku hiyo ndio Siku ya Kiyama ambayo imekwisha
zungumziwa habari yake. Ama wanyama, wao vile vile watafufuliwa na Allah (Subhanahu
Wataala) akishapitisha anachokitaka kwao atawaamrisha wawe udongo:
ﭽ ﮒ ﮓ ﮔ
ﮕ ﮖ ﮗ ﮘ ﮙ
ﮚ ﮛ ﮜ
ﮝ ﮞ ﮟ
ﮠ ﭼ
النبأ: ٤٠
“Hakika tunakuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika, siku ambayo mtu
atakapoona yaliyotangulizwa na mikono yake miwili, na kafiri atasema: Laiti
ningelikuwa udongo (nisipate adhabu hii inayoningoja sasa). (sura An-Nabaa Aya 40.)
Yaani
wakati huo atatamani kafiri awe mnyama kisha ageuke udongo kwa ile shida
anayoiona ya siku hiyo na adhabu yake. Lakini atayapata wapi hayo anayoyataka
wakati atakuwa amekamatwa vizuri kabisa wala hawezi kuponyoka, haiwezekani
kabisa hivyo hakuna kitachomuokoa au kumsaidia siku hiyo. Basi hapo husema:
ﭽ ﭣ ﭤ ﭥ
ﭦ ﭧ ﭨ ﭩ ﭪ
ﭫ ﭬ ﭭ
ﭮ ﭯ ﭰ ﭼ
المؤمنون: ١٠٧ - ١٠٨
“Mola wetu!
Tutowe humu (Motoni, uturejeshe tena ulimwenguni, tukafanye amali nzuri) na
tufanyapo tena (mabaya) bila shaka tutakuwa madhalimu (wa nafsi zetu kweli
kweli). Atasema Allah: Hizikeni humo wala msinisemeshe”.
Twamuomba
Allah atuepushe na kila balaa.
Wala hawezi
kufa mtu kabla ya kufika muda wake na hawezi kuchelewa hata kidogo
ukishamalizika muda wake.
ﭽ ﮰ ﮱ
ﯓ ﯔ ﯕ
ﯖﯗ ﯘ ﯙ ﭼ النحل: ٦١
“Na unapofika muda wao
hawawezi kukawilia saa moja wala hawawezi kuutangulia.”
Hapana budi
mtu kuimaliza riziki yake aliyoandikiwa na Allah, kwani riziki inamfuata kiumbe
kama yanavyomfuata mauti. Kama ingekuwa Allah
(Subhanahu Wataala) angeijalia riziki ya kiumbe chake katika jiwe gumu lililothibiti
katikati ya bahari basi lingepasuka hilo
jiwe ili achukue huyo kiumbe alichojaaliwa katika riziki yake.
Nataja hapa
kisa kinachohusu riziki ya mtu kuwa haiwezi kumkosa. Tulikuwa tuko njiani
tunakwenda Makka na gari yetu inakwenda kama
upepo, kutahamaki ghafla ikatusimamikia tukateremka na baadhi yetu wakenda
kukidhi haja zao. Kulikuwa na wadi sehemu hiyo nikalikuta battikhi (tikiti)
limeiva nikalichuma na nikarudi nalo garini tukalikata kisha tukalila na hapo
gari ikawashwa na ikafanya kazi. Hakuna kilichoifanya isimame wenyewe isipokuwa
ile riziki tuliyoandikiwa mahala hapo.
Masikini
wakati alipokhadaika Al-Hajjaj bin Yusuf Athaqafiy na utawala wake akasema:
‘Hakika Allah ametutosheleza riziki yetu
na akatukalifisha vitendo (tufanye amali), laiti angetutosheleza amali na
akatukalifisha riziki.’ Sababu ya kusema hivi alipoona mali nyingi ilioko chini ya milki yake katika
Beit Al-Maal akadhania kuwa mali
hiyo ameipata kwa nguvu yake na ujanja wake. Na hakuna ajabu, amemtangulia kwa
msimamo huo kabla yake Qaaruun aliposema:
ﭽ ﭒ ﭓ
ﭔ ﭕ ﭖ ﭼ القصص:
٧٨
“Hakika nimepewa haya kwa
sababu ya elimu niliyonayo”.
Na Allah
Akamjibu:
ﭽ ﭘ ﭙ ﭚ
ﭛ ﭜ ﭝ ﭞ ﭟ
ﭠ ﭡ ﭢ
ﭣ ﭤ ﭥ
ﭦ ﭧ ﭨﭼ القصص:
٧٨
“Je hakujua
ya kwamba Allah amewaangamiza kabla yake watu waliokuwa wenye nguvu zaidi
kuliko yeye na wenye mkusanyo mwingi zaidi (kuliko wake yeye)?.”
Wanasema
Muutazila kuwa alieuliwa amekufa kabla ya kumalizika muda wake, nayo ni rai
potofu iliyo wazi upotofu wake.
Na ni
wajibu kuiamini Hisabu nayo ni kufananua vitendo (amali) vya waja kuvijua viovu
na vilivyo vyema. Na hisabu sio kama hisabu wanayoijuwa watu bali kama anavyoitaka Allah (Subhanahu Wataala):
ﭽ ﭒ ﭓ
ﭔ ﭕ ﭖ
ﭗ ﭘ ﭼ النحل:
١١١
“Wakumbushe siku ambayo kila
nafsi itakuja kujitetea”.
Inafahamika
kutokana na Aya hii kuwa wataachiwa kuzungumza lakini bila ya faida yoyote
(bila ya mazungumzo hayo kusaidia kitu). Na Attirmidhiy ametoa:
( لا تزول قدما عبد يوم القيامة
حتى يسأل عن أربع: عن عمره فيم أفناه؟ وعن علمه ما عمل به؟ وعن ماله من أين اكتسبه؟ وفيم أنفقه ؟ وعن جسمه
فيم أبلاه؟ )
“Haunyanyuki mguu wa mja Siku ya Kiyama mpaka
aulizwe juu ya mambo manne: juu ya umri wake ameutumia katika nini? Na juu ya
elimu yake ameifanyia nini? Na juu ya mali yake ameipata wapi na vipi
ameitumia? Na juu ya mwili wake ameuchakaza wapi?”
Inasemekana
kuwa binaadamu Siku ya Kiyama atatolewa vitabu vitatu:
Kitabu
ndani yake vimeandikwa vitendo vizuri.
Kitabu
zimeandikwa ndani yake dhambi zake.
Kitabu
zimeandikwa ndani yake neema za Allah juu yake.
Hapo Allah
(Subhanahu Wataala) huiambia ile neema ndogo kabisa katika kitabu cha neema:
chukua thamani yako katika vitendo vyake vizuri. Na inachukua na kuvimaliza
vitendo vyote vizuri. Kisha inasema (hiyo neema): Naapa kwa Nguvu zako bado
sijatosheka (yaani nimevimaliza vitendo vyote vizuri na bado thamani yangu
imebakia) basi hapo zitabakia dhambi na neema. Vitendo vizuri vyote vimekwisha
chukuliwa na ile neema moja tu. Basi Allah akitaka kumrehemu mja wake husema:
Ewe mja wangu nimekuzidishia mema yako na nimekusamehe maovu na nimekugaiya au
nimekutunukia neema zangu.
Na hisabu
watahusika nayo wale waliokasoro kufanya mema na hatimaye wakatubia na pia wale
mafasiki waliofanya madhambi makubwa. Na hekima katika kuvihisabu vifungu
viwili hivi ni kumfanya yule Muumini aliekasoro katika amali (vitendo vizuri)
aijue neema ya Allah juu yake katika kumghufuria madhambi yake na kumstiri aibu
zake. Na hekima ya kumfanyia hisabu fasiki ni kumfanya azidi majuto kwa kuacha
kufanya vitendo vizuri kwani wakati anapoona vitendo vyake alivyovifanya
ambavyo vingeweza kuwa sababu ya kumghufuria madhambi vimefutwa na vitendo
vingine viovu alivyovifanya basi huzidi huzuni na majuto.
Vile vile hekima
katika kuwafanyia hisabu viumbe vyake ni kuonesha uadilifu wake kwa viumbe
vyake, kwa kuwa yeye hawadhulumu watu kitu lakini watu wenyewe ndio
wanaojidhulumu nafsi zao (kwa kufanya maasi). Na wasiokuwa katika vikundi
viwili hivi wao ama wataingizwa Peponi bila ya hisabu na hao ndio waumini
waliotekeleza wajibu wao, au wataingizwa Motoni bila ya hisabu na hao ni
washirikina. (Haya yamo katika kitabu cha “Bahjat Al-Anwaar”)
Na ni
wajibu kuamini kuweko kwa Pepo na Moto na kuwa ndio makazi ya viumbe vyake Subhanahu
Wataala katika majini na binaadamu. Nayo ni malipo yao kwa waliyofanya Duniani watakaa humo
milele bila ya kuwa na mwisho (atakayefanya mema ataingizwa Peponi na
atakaemuasi Allah ataingizwa Motoni). Amezieleza Mola Subhanahu Wataala sehemu
mbili hizi maelezo ambayo hayawezi kuzidishwa tena juu ya hayo katika kauli
yake mnamo sura ya Assafat alipo wataja waja wake wema:
ﭽ
ﯜ ﯝ
ﯞ ﯟ ﯠ
ﯡﯢ ﯣ ﯤ
ﯥ ﯦ ﯧ
ﯨ ﯩ ﯪ
ﯫ ﯬ ﯭ
ﯮ ﯯ ﯰ
ﯱ ﯲ ﯳ
ﯴ ﯵ ﯶ
ﯷ ﯸ ﯹ
ﯺ ﯻ ﯼ
ﯽ ﯾ ﯿ
ﰀ ﰁ ﰂ
ﰃ ﰄ ﰅ
ﰆ ﰇ ﰈ ﭼ
الصافات: ٤١ – ٤٩
“Hao ndio
watakaopata riziki maalumu, Matunda ya kila namna, na watahishimiwa, katika
bustani za neema wako juu ya vitanda, (viti vya enzi) vya fahari, wamekabiliana
(wanazungumza) wanazungushiwa gilasi zenye (vinywaji) safi, vyeupe vyenye ladha
kwa hao wavinywao, kwa vinywaji hautakuwa udhia wala kuondokwa na akili, na
pamoja nao watakuwa wanawake wenye heshima hawatizami isipokuwa waume zao tu na
wenye macho mazuri makubwa (safi) wanawake hao kama mayai yaliyohifadhika.”
Mpaka
Akasema:
ﭽ
ﮌ ﮍ
ﮎ ﮏ ﮐ
ﮑ ﮒ ﮓ
ﮔ ﮕ ﮖ
ﮗ ﮘ ﮙ
ﮚ ﮛ ﮜ
ﮝ ﮞ ﮟ
ﮠ ﮡ ﮢ
ﮣ ﮤ ﮥ
ﮦ ﮧ ﮨ
ﮩ ﮪ ﮫ
ﮬ ﮭ ﮮ
ﮯ ﮰ ﮱ
ﯓ ﯔ ﯕ
ﯖ ﯗ ﯘ
ﯙ ﭼ الصافات: ٦٢ - ٦٨
“Je,
karibisho la namna hii silo bora au kupata mti wa Zakkum (mti mchungu kabisa
watakaolishwa watu wa Motoni). Kwa yakini sisi tumeufanya ni adhabu ya hao
madhalimu wa nafsi zao. Hakika huo ni mti unaotoka (unaota) katikati ya
Jahannam. Panda za matunda yake (zinatisha) kama
kwamba ni vichwa vya mashetani. Bila shaka wao watakula katika mti huo, na kwa
huo wajaze matumbo yao ,
kisha bila shaka utawathibitikia (juu ya uchungu wa mti huo) mchanganyiko wa
maji ya Moto. Halafu, kwa yakini, marudio yatakuwa huko huko kwenye Jahannam,
(hawana mahala pengine).”
Na vile vile Allah amesema katika sura ya Al-Waqia:
ﭽ ﯖ ﯗ
ﯘ ﯙ ﯚ
ﯛ ﯜ ﯝ
ﯞ ﯟ ﯠ
ﯡ ﯢ ﯣ
ﯤ ﯥ ﯦ
ﯧ ﯨ ﯩ
ﯪ ﯫ ﯬ
ﯭ ﯮ ﯯ ﭑ ﭒ
ﭓ ﭔ ﭕ
ﭖ ﭗ ﭘ
ﭙ ﭚ ﭛ
ﭜ ﭝ ﭞ
ﭟ ﭠ ﭡ
ﭢ ﭣ ﭤ
ﭥ ﭦ ﭧ
ﭨ ﭩ ﭪ
ﭫ ﭬ ﭭ
ﭮ ﭯ ﭰ
ﭱ ﭲ ﭳ
ﭴ ﭵ ﭶ
ﭷ ﭸ ﭹ
ﭺ ﭻ ﭼ
ﭽ ﭾ ﭿ
ﮀ ﮁ ﮂ
ﮃ ﮄ ﮅ
ﮆ ﮇ ﮈ
ﮉ ﮊ ﮋ
ﮌ ﮍ ﮎ
ﮏ ﮐ ﮑ
ﮒ ﮓ ﮔ
ﮕ ﮖ ﮗ
ﮘ ﮙ ﮚ
ﮛ ﮜ ﮝ
ﮞ ﮟ ﮠ
ﮡ ﮢ ﮣ
ﮤ ﮥ ﮦ
ﮧ ﮨ ﮩ
ﮪ ﮫ ﮬ
ﮭ ﮮ ﮯ
ﮰ ﮱ ﯓ
ﯔ ﯕ ﯖ
ﯗ ﯘ ﯙ
ﯚ ﯛ ﯜ
ﯝ ﯞ ﯟ
ﯠ ﯡ ﯢ
ﯣ ﯤ ﯥ
ﯦ ﯧ ﯨ
ﯩ ﯪ ﯫ
ﯬ ﯭ ﯮ
ﯯ ﯰ ﯱ
ﯲ ﯳ ﯴ
ﯵ ﯶ ﯷ
ﯸ ﯹ ﯺ
ﯻ ﯼ ﯽ
ﯾ ﯿ ﰀ
ﰁ ﰂ ﰃ
ﰄ ﰅ ﰆ
ﰇ ﰈ ﰉ
ﰊ ﰋ ﰌ
ﰍ ﭑ
ﭒ ﭓ ﭔ
ﭕ ﭖ ﭗ
ﭘ ﭙ ﭚ
ﭛ ﭜ ﭝ
ﭞ ﭟ ﭠ
ﭡ ﭢ ﭣ
ﭤ ﭥ ﭦ
ﭧ ﭨ ﭩ
ﭪ ﭫ ﭬ
ﭭ ﭮ ﭼ الواقعة: ١٠ - ٥٦
“Na walioko
mbele kabisa (katika kheri), nao ndio walioko mbele; hao ndio watakaokaribishwa
(kwa Allah) katika bustani zenye neema. Sehemu kubwa (katika hawa) ni miongoni
mwa (watu) wa mwanzo (huko). Na sehemu ndogo ni miongoni mwa (watu) wa mwisho.
Watakuwa juu ya viti vya fahari vilivyotonewa (vilivyotiwa mapambo).
Wataviegemea waelekeane (wanazungumza). Wawe wanawazungukia wavulana,
(watumishi watoto wanaume) walio daima na sura za ujana za kupendeza kwa
vikombe na mabirika, na gilasi za vinywaji vinavyotoka katika mito inayoonekana kwa mapitio yake. Hawaumwi
na vichwa kwa (kuvinywa vinywaji) hivyo wala hawatatokwa na akili. Na matunda
(namna kwa namna) kama watakayopenda. Na nyama
za ndege kama watakavyotamani (wenyewe). Na
wanawake wenye macho mazuri na makubwa (ya vikombe), (wanapendeza na safi ) kama kwamba ni lulu
zilizofichwa (kwenye chaza yake, ndio kwanza zinapasuliwa). Ni jaza ya hayo
waliyokuwa wakiyatenda, hawatasikia humo maneno ya upuuzi wala maneno ya dhambi,
isipokuwa maneno ya usalama na amani. Na wale watu wa kheri nao; watakuwa namna
gani watu hao wa kheri! (watakuwa) katika vivuli vya mikunazi isiyo na miba, na
migomba iliyopangiliwa uzuri. Na (katika) vivuli vyengine vilivyonyooka kila
upande, na maji yanayomiminika kwa vizuri. Na matunda mengi (ya kila aina).
Hayatindiki, (hayakatiki) wala hayakatazwi (kwa kuwa si yake tu huyu au
yanamdhuru). Na wanawake watukufu; (hawa waliokuwa nao Duniani). Tutawaumba kwa
umbo (bora zaidi). Na tutawafanya bikra (vijana kama
kwamba ndio kwanza wanaolewa). Wanapendana na waume zao (walio) hirimu moja
nao, (yote haya yatafanywa) kwa ajili ya watu wa kheri. Sehemu kubwa katika
hawa watu wa kheri ni miongoni mwa (watu) wa Umma za mwanzo na sehemu kubwa pia
ni miongoni mwa (watu) wa mwisho (wa huu Umma wa Nabii Muhammad). Na watu wa
shari (waovu); watakuwa namna gani hao watu wa shari! (Watakuwa) katika upepo
wa Moto na maji yachemkayo, na kivuli cha moshi mweusi sana , si cha kuleta baridi wala si cha
starehe. Bila shaka wao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa, na
walikuwa wakishikilia, (wakiendelea) kufanya madhambi makubwa, na walikuwa
wakisema; ‘Tutakapokufa na tukawa udongo na mifupa, ndio tutafufuliwa? (uongo
huo). ‘Au wazee wetu wa zamani (ndio watafufuliwa pia?).’ Sema: ‘Bila shaka wa
kwanza na wa mwisho, watakusanywa kwa wakati uliowekwa katika siku maalum.
Kisha nyinyi, mliopotea (na) kukadhibisha kwa yakini mtakula mti wa Zakkum. Na
kwa huo mtajaza matumbo yenu, na juu yake mtakunywa maji Moto yanayochemka.
Tena mtakunywa kama wanywavyo ngamia wenye kiu sana , (na kila wakinywa kiu haiweshi).’ Hiyo
ni karamu yao
siku ya malipo.” (sura Al-Waaqia Aya 10-56)
Na ni
wajibu kuamini kuweko kwa Hodhi nalo ni Hodhi la Mtume Muhammad (Salallahu
Alayhi Wasalam) lilioko katika msimamo wa Siku ya Kiyama ambalo wataliendea
Waumini na katika hadithi :
( حوضى مسيرة شهر وزواياه سواء
وماؤه أبيض من اللبن وأحلى من العسل وريحه أطيب من المسك وكيزانه كنجوم السماء ومن
شرب منه لا يظمأ أبداً ولا يسود وجهه أبداً )
“Hodhi
langu (lina umbali wa) mwendo wa mwezi na pande zake (vile vile mwendo wa
mwezi) sawa na hivyo. Na maji yake ni meupe kuliko maziwa na matamu kuliko
asali na harufu yake nzuri kuliko miski na makopo yake kama nyota mbinguni na anaekunywa ndani yake hapati kiu milele na
wala uso wake hauwi mweusi milele”.
Na
watafukuzwa baadhi ya watu watakaokuja kunywa ndani yake basi atawaona Mtume
(Salallahu Alayhi Wasalam) na hatapendezewa kufukuzwa kwao na atasema: Masahaba
zangu, Masahaba zangu na ataambiwa: Hakika wao wamebadilisha (mambo ya Dini)
baada yako (kuondoka kwako) basi hapo akasema: Potoleeni mbali poteleeni mbali.
Na kwa hayo inatudhihirikia kuwa haiwezekani kunywa katika hodhi hilo isipokuwa yule
alietekeleza Dini ya Allah na akafa yungali katika hali hiyo.
Vile vile inapasa kuamini kuweko kwa mizani nayo ni kwa
maana ya Uadilifu (haki) na usawa na sivyo kama wanavyosema wengine kuwa maana
yake ni hii mizani ya kawaida tunayoijua, yaani nguzo na mikono yake miwili, na
kuwa Allah anaisimamisha Siku ya Kiyama na juu yake vitapimwa vitendo vya waja,
na yule ambaye vitendo vyake vyema vitakuwa vizito zaidi kuliko vitendo vyake
viovu basi ataingia Peponi ama yule ambaye mkono wa vitendo vyake viovu utakuwa
mzito zaidi kuliko mkono wa vitendo vyake vyema ataingia Motoni; haya
hayakuthibiti katika dalili yoyote, na uzito au wepesi wa mizani ulioelezwa
hapa maana yake ni kuokoka na adhabu ya Motoni (na kuingia Peponi) au kuangamia
yaani kuingia Motoni. Na utumiaji wa neno “mizani” kimethali ni maarufu kwa
Warabu; mmoja wao asema:
“Lau wangewaweka baba zangu katika mizani yao
wangeinamisha mizani kwa uzito na baba yako akanyanyuka nayo kwa wepesi”
Na Allah (Subhanahu
Wataala) Asema:
ﭽ ﭪ ﭫ
ﭬ ﭭ ﭮ ﭼ
الأنبياء: ٤٧
“Nasi
tutaweka mizani za uadilifu Siku ya Kiyama”
Unaona hapa
kuwa Uadilifu umewekwa badala ya (mahala pa) Mizani siyo kutowa wasifu wake
(Mizani). Na vitendo vya waja ni “Aaraadh” yaani unavifikiria akilini lakini
huwezi ukavishika au ukaviona kwa hiyo ni muhali kuvipima katika mizani (Kitabu
“Bahjat Al-Anwaar”).
Na vile
vile inatuwajibikia kuamini kuweko kwa الصراط kwa
mujibu wa kauli ya Mola Subhanahu Wataala:
ﭽ ﯩ ﯪ
ﯫ ﯬ ﯭ
ﯮ ﯯ ﯰ
ﯱ ﯲ ﯳ
ﯴ ﭼ
الملك: ٢٢
“Je! Anayekwenda akisinukia
kwa uso wake ni muongofu au anayekwenda katika njia iliyonyooka?”.
Na ni Yeye
Mola aliyemuamrisha mja wake aseme:
ﭽ ﭧ ﭨ
ﭩ ﭼ
الفاتحة: ٦
“Niongoze njia iliyonyooka”.
Nayo (hiyo الصراط ) ina maana ya haki na huwakilisha hali
mbili za mtiifu na anayeasi na pia huwakilisha hali za wale wanaokwenda na
kufuata njia zilizo baina ya aliyepewa tawfiiq na aliyekosa hiyo tawfiiq, na
wala sivyo wanavyodai baadhi ya watu kuwa الصراط ni
daraja limewekwa juu ya mapana ya Jahannam. Na masuala mawili haya (“Sirat”
“Mizan”) sio katika masuala yenye dalili zisizo shaka (za wazi na uhakika)
ambayo hayafai kuhitilafiana juu yake; bali kila mtu aweza kufasiri namna yake.
Sio kama masuala ya kumuona Allah (Subhanahu Wataala) na kutoka Motoni kwa
waliokufa katika maasi (bila ya kutubu) na kupata Uombezi kwa aliyekufa naye
yungali afanya madhambi makubwa (Al-Kabair), kwani masuala haya matatu
haiwezekani kuhitilafiana juu yake kwa sababu haki iko kwa mmoja tu, naye ni
yule anayesema: Allah (Subhanahu Wataala) haonekani, na anayeingia Motoni
hatoki humo (hukaa humo milele) na kuwa Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam)
hamuombei isipokuwa anayemcha Allah. Na dalili za masuala haya matatu
zimekwisha zungumzwa kwa kirefu katika kitabu hiki kutoka kwa Sheikh Ahmed bin
Hamed Al-Khalily – Allah ampe afya. Amin.
Na nimeona katika kitabu: “Bahjat Al-Anwaar” cha Sheikh
wetu Noor Din, Allah amrehemu, ametowa hadithi ndefu asema: Na katika athari
kuwa Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) alikaa juu ya membari yake Salallahu
Alayhi Wasalam kisha akasema:
(الصلاة جامعة –رحمكم الله – ثم قال يا عباس عم رسول الله ويا
فاطمة بنت محمد ويا آل محمد جميعا إني والذي نفسي بيده عند ربي لمطاع مكين فلا
تغرن امرءا نفسه يقول أنا عم رسول الله صلى الله عليه وسلم أو تقول بنت محمد أو من
آل محمد اشتروا أنفسكم من الله فإنكم إن لم تفعلوا هلكتم مع من عرفتم هلاكه ، إني
على الحوض يوم القيامة فارط (اي متقدم ) فيرد علي أناس من أصحابي ليحتلقن نقرة
رأسه ثم لآخذن بحجزته فأقول: أرسلوه إنه من أصحابي فيؤخذ بيدي فكاكا، أرسل، أرسل،
فإنه والله ما مشى من بعدك قدما ولكنه مشى القهقهري، ليدخل جهنم، فلا أستطيع شيئا،
فالحذر الحذر يا آل محمد إني والله لا أغني عنكم من الله شيئا)
“Njooni
kusanyikeni katika Sala, Allah awarehemu. Kisha akasema: Ewe Abbas Ammi wa
Mtume wa Allah, na ewe Fatima binti Muhammad na enyi watu (jamaa) wa Muhammad
nyote, kwa yakini mimi, naapa kwa yule ambaye nafsi yangu iko katika mikono
yake, mbele ya Mola wangu ni mwenye kutiiwa na mwenye kuwezeshwa, basi isije
ikamdanganya mtu nafsi yake, akasema: Mimi Ami wa Mtume wa Allah Salallahu
Alayhi Wasalam au aseme mimi binti Muhammad au katika watu (jamaa) wa Muhammad.
Zinunuweni nafsi zenu kutoka kwa Allah (kwa kufanya mema na kumtii) kwani
hakika nyie ikiwa hamtafanya hivyo mtaangamia pamoja na wale mnaowajua
kuangamia kwao (katika mushrikiin na wanafiki). Mimi nitakuwa katika hodhi Siku
ya Kiyama nimetangulia (huko hodhini) watanijia watu katika masahaba zangu
kisha atanijia mtu namjua naye ni miongoni mwa masahaba zangu na kisha
atachukuliwa mikononi mwangu kwa nguvu (kwa kubabaduliwa) huku ikisemwa:
mwache, mwache kwani yeye wallahi hakwenda baada yako kimbele mbele lakini
amekwenda (baada ya kufa kwa Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam)) kinyume nyume
(ameacha kufuata Dini ya Allah) basi na aingie Jahannam, basi siwezi
(kuwasaidia) kitu kwa hiyo tahadharini, tahadharini enyi jamaa wa Muhammad kwa
sababu hakika mimi Wallahi siwezi kuwafaa kitu mbele ya Allah (Subhanahu
Wataala).”
Na uombezi
aliopewa peke yake Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) sio wa kuwaombea watu
waingizwe Peponi bali ni wa kuwaokoa watu na shida (hali ngumu sana) ya msimamo
wa Siku ya Kiyama na Uombezi huo ndio unaojulikana kwa jina la الشفاعة
العظمى yaani Uombezi Mkuu, na
kwa jina la المقام المحمود yaani Kisimamo
Kisifiwacho, wakati wanaposhindwa Mitume kuufanya huo Uombezi hapo atasimama
Bwana wao Muhammad Salallahu Alayhi Wasalam akisema: Huo ni wangu mimi, huo ni
wangu mimi (yaani mimi nitaufanya Uombezi huo).
Na haya
yaliyotajwa katika mlango huu ndio yanayompasa Muislamu kuyaamini kwani huo
ndio ukweli wa Imani na nguzo zake.
Twamuomba
Allah (Subhanahu Wataala) atuwafikishe kufanya kila anachokipenda na
anachokiridhia. Amin
No comments:
Post a Comment
Note: only a member of this blog may post a comment.