Tuesday, 19 January 2016

Juzuu 12 Jihadi----Kujenga uongofu katika nyoyo za vijana-----





الصف: ١٠ - ١٢

“10. Enyi mlioamini! Je! Nikujuulisheni biashara itakayokuokoeni na adhabu iumizayo?

11. Basi biashara yenyewe ni hii: Muaminini Allah na Mtume wake na piganieni dini ya Allah kwa mali zenu na nafsi zenu haya ni bora kwenu ikiwa mnajua (Kuwa ni bora, basi fanyeni).

12. (Mkifanya hayo) Atakusameheni dhambi zenu na atakuingizeni katika mabustani yapitayo mito mbele yake na (atakupeni) masikani mazuri katika bustani za milele huku ndiko kufuzu kukubwa.”




Jihadi kilugha ni kufanya juhudi na kujikalifisha katika kufanya yaliokuwa na tabu na mashaka. Nayo (جهاد) jihadi ni asili ya neno (جاهد) amejahidi nafsi yake kama katika kauli yake Allah Subhanahu Wataala:


الحج: ٧٨

“Na ipiganieni dini ya Allah kama inavyostahiki kupiganiwa.”


Jihadi katika sharia maana yake ni kupigania na kuihami dini, heshima na mali na imechukuliwa kutokana na maana yake ya kilugha kwa hivyo ilivyokuwa katika kupigania dini uchukivu na uzito wa nafsi. Amesema Allah:

البقرة: ٢١٦

“Mmelazimishwa kupigana vita (kwa ajili ya dini). Nalo ni jambo zito kwenu.”



Aina ya Jihadi


Jihadi ni aina mbili:-

Fardhi inayompasa kila Muislamu.

Fardhi ambayo wakifanya jihadi baadhi basi haiwi lazima kwa baadhi nyingine (haiwalazimu).


Katika hiyo fardhi ya kwanza ipo iliokuwa khaas mtu binafsi na iliokuwa kwa ujumla (wote). Hiyo khaas ni jihadi ya nafsi yaani kuilazimisha nafsi kumtii Allah Subhanahu Wataala na kuwa na tabia njema na kujifundisha mambo ya dini na kuwafundisha wengine vilevile na kuikataza kufanya maasi na shubha yanayopeleka katika hilaki kwani nafsi imeumbwa kupenda raha ya dunia ya haraka na kupenda kujidhulumu na kudhulumu wengine bila ya kujifikiria, imesemwa:-

“Kudhulumu ni katika tabia za nafsi, ukimkuta mwenye kujitakasa basi kuna sababu ya kuwa hadhulumu”

Lakini mujahid anaimiliki nafsi yake na kuiongoza anavyotaka mwenyewe kwa tawfiiq ya Allah kama alivyosema katika kitabu chake Subhanahu Wataala:

         العنكبوت: ٦٩

“Na wale wanaojitahidi kwa ajili yetu kwa yakini tunawaongoza katika njia zetu”.


            Basi yule anayeitakia kheri nafsi yake na afuate njia za kuitengeneza na kuilazimisha (hiyo nafsi) kuchukuwa mafundisho aliyoyapata katika wakati huu wa sasa ili yamsaidie katika mustaqbal (kipindi kijacho) kwa kuogopa asije akafanya makosa waliyoyafanya wenzake na kuizoesha kumdhukuru Allah Subhanahu Wataala wakati wote na kuipa mawaidha. Imesemwa kuwa yule aliyekuwa wakati haukumpa mafundisho basi hafaliwi na mawaidha atakayoyasikia kwa yeyote yule. Yule aliyekuwa siku hazikumpa mafundisho basi upotofu ni karibu kwake kuliko uongofu. Yule anayeyapima yale ambayo bado hajayaona kwa yale anayoyaona basi yale yaliyo karibu naye yamuoneshe yale yaliyokuwa mbali naye.


Nafsi ikiwachiwa kama inavyopenda basi itaona raha kufanya yenye ladha naye hajui kuwa sumu imo ndani ya kilionona, basi juu yake kuizoesha (nafsi), tokea mwanzo mambo mazuri ya dini na dunia ili aondokee katika hali hii tokea ujana wake mfano wa mtoto anayenyonya akifika umri wa kuachishwa maziwa, akiachishwa, huwa rahisi kwake na huzoea, basi kama hivyo nafsi ikiwa itafundishwa kufanya mambo mema, imetolewa shairi katika jambo hili:-

Na nafsi ni kama mtoto (mchanga) akipuuzwa huondokea kupenda kunyonya na akiachishwa huacha (kunyonya).


Katika mambo muhimu yaliyokuwa yawajibika kuwa nayo mtu katika kupigana jihadi ya nafsi yake ni kujifunza elimu iliyo lazima kwa nafsi kuijua na iliyo juu yake kuijua. Aina ya kwanza ni kujuwa haki za Allah Subhanahu Wataala zilizo wajibu na zinazojuzu na zilizo kuwa muhali kusifika nazo Allah Subhanahu Wataala na kuwa yeye ni Mpweke na ndiye pekee anaye kusudiwa kwa haja za waja naye amejipwekesha katika umoja hana mshirika wala aliye sawa naye wala  ampingaye wala hakuna aliye mfano wake. Hakuna chochote kilicho mfano wake. (Wenye) Macho hawamuoni Yeye na hakika yeye ana uwezo wa kila kitu. Na katika yaliyo kuwa wajibu juu ya nafsi kujua yale iliyokalifishwa nafsi kufanya katika mambo ya faridha na ya nafla na kujiepusha yale aliyoyaharimisha Allah Subhanahu Wataala katika maasi yaliyo dhahiri kama uongo na kulewa na kula mali ya watu isipokuwa kwa haki, na maasi yaliyofichika kama riyaa, na kujipenda mtu nafsi yake na kutakabari na mengineyo, na kuizowesha (nafsi) ukweli na uaminifu na kuhifadhi ulimi usiwaseme watu na usiwafitinishe watu na kuacha yaliyokuwa hayamuhusu. Na kumkirimu mgeni na kwa kufanya yote hayo itapata (hiyo nafsi) furaha ya nyumba zote mbili (dunia na akhera). Na faridha (ya jihadi) iliyowahusu watu wote ni ile iliyomlazimu kila iliyomuwajibikia taklifu afanye jihadi kwa nafsi yake na mali yake kwa dalili ya kauli yake Allah Subhanahu Wataala:

التوبة: ٤١

“Nendeni (vitani) mkiwa wepesi na mkiwa wazito (wazima na wagonjwa) na piganieni dini ya Allah kwa mali zenu na nafsi zenu”.


Katika jumla ya jihadi kumzuia adui kwa kupigana nae anapohujumu milki ya binafsi, nchi, jamaa (mjumuiko wa watu) au mali. Ikiwa jeshi halina uwezo wa kuihami nchi basi inawapasa raia wote washirikiane na jeshi hilo kwa kupigana na   adui huyo kwa mali na nafsi zao ili wamzuie na waivunje tamaa yake ya kutaka kuiteka nchi yao.

Kuamrishana mema na kukatazana mabaya ni nguzo mbili za msingi zinampasa kila baleghe kadiri ya daraja ya nguzo mbili hizo. Daraja yake ya juu kabisa ni kupigana kwa ajili ya Allah Subhanahu Wataala ili kulinyanyua na kulitia nguvu Neno (kalima) la Haki nalo ni لا إله إلا اللهLa Ilaaha Illa Allah” na daraja ya chini kabisa kuondoa uchafu njiani.


Aina ya pili ya jihadi ni fardhi kifaya wakisimama baadhi ya raia kuifanya hiyo jihadi basi haiwajibikii waliobaki nayo ni kuilinda nchi kutokana na adui ambaye anatarajiwa ubaya wake (uadui wake) kwa kulinda zile sehemu ambazo ni wepesi adui kupenya ili kuhujumu nchi, basi hata ikiwa huyo atakayejifunga kulinda ni mtu mmoja lakini ikiwa wote wakakataa kujifunga katika hizo sehemu basi wote watahiliki, Allah Subhanahu Wataala atuepushe na kurudi nyuma katika Jihadi.




Imefaridhishwa Jihadi katika mwaka wa pili wa Al-Hijra baada ya kutulia Uislamu na waislamu katika mahala pake pa amani napo ni Madina Al-Munawarrah kwa dalili ya kauli yake Subhanahu Wataala:-


الحجرات: ١٥

“Wenye kuamini kweli kweli ni wale waliomuamini Allah na Mtume wake kisha wakawa si wenye shaka, na wakapigania dini ya Allah kwa mali zao na nafsi zao. Hao ndio wenye kuamini kweli”.


التحريم: ٩

“Ewe Nabii shindana na makafiri na wanafiki”.


Hii ni amri ya ujumla (si kwa watu makhsusi katika wakati makhsusi) imewajibikia umma wa Muhammad -rehema za Allah na amani zimshukie- wote katika wakati wowote na mahali popote pale walipo.

Na kauli yake Al Haq:


الحج: ٣٩ - ٤٠

“Wameruhusiwa (kupigana) wale wanaopigwa, kwa sababu wamedhulumiwa. Na kwa yakini Allah ni Muweza wa kuwasaidia (39). Ambao wametolewa majumbani (mijini) mwao pasipo haki ila kwa sababu wanasema “Mola wetu ni Allah”. Na kama Allah asingaliwakinga watu, baadhi yao kwa wengine, bila shaka yangalivunjwa mahekalu na makanisa na nyumba nyingine za ibada na misikiti ambamo jina la Allah hutajwa kwa wingi."


Na kauli yake:

النساء: ٧٤ - ٧٥

“Basi nawapigane katika njia ya Allah wale wanaouza maisha (yao) ya dunia kwa (kununua) ya Akhera. Na anayepigana katika njia ya Allah kisha akauawa au akashinda, tutampa ujira mkuu (74) Na mna nini hampigani katika njia ya Allah na (katika kuwaokoa) wale walio dhaifu katika wanaume na wanawake na watoto ambao husema: Mola wetu! Tutoe katika mji huu ambao watu wake ni madhalimu, na tujaalie tuwe tuna mlinzi anayetoka kwako, na tujaalie tuwe tuna wa kutunusuru kutoka kwako”.


Na kauli yake:-


الصف: ١٠ - ١١

“Enyi mlioamini! Je! Nikujulisheni biashara itakayokuokoeni na adhabu iumizayo? (Basi biashara yenyewe ni hii) Muaminini Allah na Mtume wake na piganieni dini ya Allah kwa mali zenu na nafsi zenu haya ni bora kwenu ikiwa mnajua (kuwa bora basi fanyeni)”


Na kauli yake:


التوبة: ١١١

“Allah amenunua kwa waislamu nafsi zao na mali zao (watoe nafsi zao na mali zao katika kupigania dini) ili na yeye awape pepo. Wanapigana katika njia ya Allah, wanaua na wanauawa. Hii ndiyo ahadi aliyoilazimisha (Allah) katika Taurati na Injili na Qurani. Na ni nani atekelezaye zaidi ahadi yake kuliko Allah? Basi furahini kwa biashara yenu mliyofanya naye (Allah), na huko ndiko kufuzu kukubwa.”


التوبة: ٢٤

“Sema; kama babu zenu na wana wenu na ndugu zenu na wake zenu na jamaa zenu na mali mlizochuma na biashara mnazoogopa kuharibikiwa, na majumba mnayoyapenda, (ikiwa vitu hivi) ni vipenzi zaidi kwenu kuliko Allah na Mtume wake na kupigania dini yake basi ngojeni mpaka Allah alete amri yake”.


Unaona basi kuwa Allah Subhanahu Wataala ametanguliza mapenzi ya jihadi kabla mapenzi ya mababa na watoto na mali na kila kilichoko katika dunia na akamkaripia yule aliyoacha jihadi na akatishia kwa kauli yake فتربصوا   yaani “basi ngojeni” na akamwita yule anayeacha jihadi kuwa ni “Fasiq” yaani mwenye kufanya maasi makubwa kwa mujibu wa kauli yake katika mwisho wa aya iliyopita:


التوبة: ٢٤

"Na Allah hawaongozi watu maasi (njia iliyonyooka)”.


Basi kama inavyoonekana katika aya hii kuwajibika kwa jihadi kuko wazi kabisa bila ya kufichika na kupendelewa na kuekwa mbele (kiupaumbele) kabla ya kitu cho chote kingine. Na wakati Allah Subhanahu Wataala anapotaja Jihadi katika Qur'ani anawasifu wale waliojisubirisha nafsi zao katika kupigania dini kwa kujidhibiti nafsi zao na subra.


Anasema:


آل عمران: ٢٠٠

  “Enyi Mlioamini! Subirini na muwashinde makafiri (katika kusubiri) na kuweni imara (nyoyo zenu) na mcheni Allah ili mpate kufaulu (kufuzu)".


Na mwendo wake Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- ni ushahidi mkubwa na wa kutosha kabisa wa kuwajibika kwa jihadi. Kwani yeye tokea mwanzo wake -rehema za Allah na amani zimshukie- mpaka alivyomchukua Allah Subhanahu Wataala hakuiwacha wala hakuingiwa na udhaifu katika kupigana jihadi tokea kupewa amri ya kufanya hivyo na Mola wake Subhanahu Wataala. Wakaifata njia yake hiyo iliyo wazi masahaba wenye kuhishimiwa amewaridhia Allah wote kisha wakafata njia hiyo baada yao maimamu wa waislamu ambao Allah Subhanahu Wataala amewapa tawfiiq ya kufuata haki na akawaonyesha njia yake.


Jihadi ni miongoni mwa sunna zake Allah katika viumbe vyake kwani amejaalia njia mbili za kuifanya haki ikubaliwe na watu, njia ya kwanza kwa mafahamiano na njia ya pili kwa nguvu kwani mwenye akili na insafu aikubali haki kwa kufahamiana. Ama aliye mjinga na mbishi haikubali haki isipokuwa kwa njia ya nguvu, kwa hivyo amefaridhisha Subhanahu Wataala jihadi na ingekuwa bila yake asingepwekeshwa Allah katika ardhi. Hapa ndipo lilipo ingia nguvu neno lake na kudhihiri dini yake. Na hii haipingani na rehema uliyokuja nayo Uislamu wala uadilifu aliouamrisha Allah Subhanahu Wataala. Na anaepinga wito wa kiislamu ni mbishani na mpingaji wa haki na muenezaji wa batili ni wajibu kukandamizwa na kudhalilishwa kwa kutumia nguvu kwani hatarajiwi kuikubali haki na kuiwacha batili isipokuwa kwa nguvu (kwa kupigana nae jihadi). Imewekwa sharia ya jihadi kwa ajili ya kuzuia dhulma na fasadi katika ardhi na kuhami mwito wa haki, na kuiwezesha  dini ya Kiislamu ienee katika ardhi na kuzuia shari ya makafiri juu ya Waumini, wanaotaka kuwayumbisha wale waliokuwa imani zao dhaifu kabla ya kutamakani uongofu katika nyoyo zao na kujaribu vilevile kuwapoteza walio na imani thabiti kwa kuwatumilia njia (fitina) mbali mbali kama wafanyavyo leo maadui wa kiislamu kwa njia zao za udanganyifu. Na wote bali wengi katika wanao mpwekesha Allah Subhanahu Wataala wameathirika na njia zao hizi kwa sababu ya ghafla yao kutokana na njia ya Mola Subhanahu Wataala kwa hiyo imewekwa jihadi sio kwa ajili ya mapendekezo ya nafsi ya kutaka kumwaga damu au kuhifadhi vyeo (vya dunia) bali imewekwa kwa ajili ya kuihami dini na kutia nguvu na kujikinga na uadui (wa makafiri) kwa hiyo jihadi ni rehema kwa waja. Anasema Allah Subhanahu Wataala:


البقرة: ١٧٩

“Mtakuwa nao uhai (mzuri) katika kulipiza kisasi enyi wenye akili”.


Na dalili zilizoko katika sunna ya Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- zinazoonesha kuwajibika kwa jihadi ni vile vita ambavyo amepigana na kuviongoza mwenyewe -rehema za Allah na amani zimshukie- kama Badr, Uhud na Al Khandaq na kadhalika vile alivyovitayarisha akawapeleka masahaba zake kuwa viongozi wake Allah Subhanahu Wataala awaridhie wote. Kama vile vilivyoongozwa na ammi yake Sahaba mkubwa Simba wa Allah na bwana wa mashahidi Hamza bin Abdul Muttalib kwenda kwa Seif Al Bahr nayo ni madh-har ya kwanza katika kuonesha nguvu ya Kiislamu. Navyo ni vita vya kwanza ambavyo amevituma Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- baada ya kufika katika mji wa Hijra yake na kunusuriwa kwake (Madina Al-Munawwara) kwa miezi saba. Na kauli yake -rehema za Allah na amani zimshukie: “Nimeamrishwa nipigane na watu mpaka washahadie kuwa hakuna Mungu isipokuwa Allah na kuwa Muhammad Mtume wa Allah basi wakisema neno hilo wamekwisha jikinga na mimi damu zao na mali zao isipokuwa  kwa haki yake na hisabu yao iko kwa Allah Subhanahu Wataala".  Hadithi na kauli yake Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie:- "Kichwa(Asili) cha jambo hili ni Uislamu na aliyesilimu amesalimika, na nguzo yake (hilo jambo) ni Sala na kilele cha nundu yake ni jihadi, haipati (hiyo jihadi) isipokuwa aliye bora wao". Na kauli yake -rehema za Allah na amani zimshukie- kumjibu yule aliyemuuliza vitendo gani vilivyokuwa bora akasema "Imani ya Allah na Mtume wake", akaulizwa kisha nini akasema "Jihadi katika njia ya Allah" akaulizwa kisha nini akasema "Hija mabroor (iliyokubaliwa)" akaulizwa kisha nini akasema "kuwafanyia mema wazee wawili". Na kutokana na Abi Musa kuwa Mbeduwi amemjia Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- akasema “Ewe mjumbe wa Mungu mtu apigana kwa kutaka apate mali ngawira (wanyama) na mtu mwingine apigana ili apate kutajwa na mtu apigana ili apate kuonekana mahala pake nani katika hawa apigana kwa ajili ya Allah? Akasema (kujibu) Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani zimshukie: "Anaepigana ili neno la Allah lipate kuwa juu (kuwa na nguvu) basi huyu ndie anayepigana kwa ajili ya Allah".


Fadhila ya wapiganao jihadi kubwa. Anasema Allah Subhanahu Wataala:

النساء: ٩٥

“Lakini Allah amewafadhilisha wale wapiganao kuliko wakaao kwa ujira mkuu”.


Na katika hadithi iliyotoka kwa Ibni Abbas radhi ya Allah iwe juu yake yeye na baba yake amesema:- Nimemsikia Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani zimshukie- akisema:- "Macho mawili moto (wa jahannam) hauyagusi, jicho limelia kwa khofu ya Allah Subhanahu Wataala na jicho limekesha lalinda kwa ajili ya Allah". Na imetolewa kutokana na Sahal Ibn Saad kuwa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- amesema: "Kujifunga siku moja (kwa kulinda adui) katika njia ya Allah Subhanahu Wataala ni bora kuliko dunia na vilivyo kuwemo ndani yake. Na pahala pa fimbo (pasimamishwapo fimbo ambapo ni padogo sana) pa mmoja wenu huko Peponi ni bora kuliko dunia na vilivyo kuwemo ndani yake. Na mwendo wa mchana anaokwenda mja katika njia ya Allah na mwendo wa asubuhi mapema ni bora kuliko dunia na vilivokuwemo ndani yake".


Kuwacha jihadi kumewekewa kitisho kikubwa cha adhabu ya Allah na mabalaa ya kudhalilishwa Waislamu na maadui zao kwa kuacha Jihadi na vile vile kusababisha katika kupotezwa katika dini yao.

Amesema Allah Subhanahu Wataala :


الأنفال: ٢٥

“Na iogopeni adhabu (Allah ya hapa duniani) ambayo haitawasibu peke yao wale waliodhulumu nafsi zao miongoni mwenu (bali itawasibu hata walio nyamaza wasiwakataze bali na wengineo pia)”.


Katika hadithi inayosema:- "Hawakuacha watu jihadi (kupigania dini) isipokuwa Allah awateremshia  adhabu wote". Kutokana na Abi Huraira radhi za Allah ziwe juu yake anasema:- Amesema Mtume wa Allah: "Aliyekufa bila ya nafsi yake kumsemesha kupigana jihadi (kupigania dini ya Mungu) amekufa juu ya tawi katika matawi ya unafiki".


Na adabu za jihadi (taratibu zake) zina daraja kubwa zimetajwa katika hadithi tukufu iliyotolewa kutoka kwake -rehema za Allah na amani zimshukie- kuwa wakati akituma jeshi husema:- "Kwa jina la Allah na kwa Allah na katika njia ya Allah na katika mila ya Mtume wa Allah msipindukie mipaka wala msivunje ahadi, wala msiwakate kate viungo mnaopigana nao, msiuwe mtoto mdogo wala mwanamke wala mzee". Na katika adabu zake isiwe jihadi itokayo nje ya kufuata (taa) amri za Allah na kufarikiana na jamaa na anayekhalifu kisha akafa basi hufa kifo cha jahiliya. Na anaepigana chini ya bendera ya upofu inayoita kwenye kupendeleana kwa ajili ya Ukabila, Ujamaa, Urafiki (sio kupigana kwa kunyanyua dini ya Allah Subhanahu Wataala) au anayeghadhibika juu ya kasumba hiyo basi akiuliwa basi kifo chake cha jahiliya (yaani hakufa katika Uislamu) Allah Subhanahu Wataala atuepushe na kufa kifo kama hicho. Na vile vile katika adabu zake kutokimbia wakati wa vita vimeshika (yaani vikosi viwili vimepambana), na anayekimbia ni asi wa Allah kafiri kufuru ya neema kwani hiyo ni katika madhambi makubwa kwa kauli yake Subhanahu Wataala:


الأنفال: ١٥ – ١٦

“Enyi Mlioamini! Mkutanapo vitani na wale waliokufuru basi msiwageuzie mgongo (mkakimbia) (15) Na atakaewageuzia mgongo wake siku hiyo isipokuwa amegeuka kwa kushambulia au amegeuka akaungane na sehemu nyengine za jeshi hilo hilo la Waislamu (ikiwa si hivyo) atastahiki ghadhabu ya Allah na mahali pake ni Jahannam. Napo ni mahali pabaya pa kurudia (mtu)(16)”.


Amesema Mtume wa Allah Subhanahu Wataala: “Mambo matatu hayafai pamoja nayo amali (vitendo):- Kumshirikisha Allah na kuwaasi wazazi wawili na kukimbia kutoka vitani”. Na juu yake anaepigana jihadi awe na hadhari na awe macho na kuwa amejitayarisha matayarisho makubwa na afuata kauli ya Allah Subhanahu Wataala:


الأنفال: ٦٠

“Basi waandalieni (wawekeeni tayari) nguvu mziwezao (silaha), na mafarasi yaliyofungwa (kufuga) tayari tayari (mipakani), ili kwazo (nguvu hizi) muogopeshe maadui wa Allah na maadui zenu, (mnaowajua) na pia (maadui zenu) wengineo wasiokuwa wao, msiowajua nyinyi”.


Vile vile huyo anaepigana(mujaahid) achukue hadhari kwa kutegemea khadaa ya adui na kuwa adui apeleleza ghafla yake (mujaahid) hata katika wakati wa ibada na haisihi kwa mujaahid aweke chini silaha yake isipokuwa kama kutakuwa cha kumkinga kama alivyotunabihisha Allah Subhanahu Wataala katika kitabu chake kutukufu pale aliposema:-

النساء: ١٠٢

“Na unapokuwa pamoja nao (Waislamu katika vita) ukawasalisha, basi kundi moja miongoni mwao wasimame pamoja nawe (wanasali) na washike silaha zao. Na watakapomaliza sijida zao (kusali) basi nawende nyuma yenu (kwa kulinda) na lije kundi jingine ambalo halijasali na lisali pamoja nawe nao washike hadhari yao na silaha zao (humo ndani ya sala, maana) wale waliokufuru wanataka mghafilike na silaha zenu na vitu vyenu ili wakuvamieni mvamio wa mara moja. Wala si vibaya kwenu ikiwa mnaona udhia kwa sababu ya mvua au mnao ugonjwa, kuondoa silaha zenu. Na mshike hadhari yenu. Hakika Allah amewaandalia makafiri adhabu itakayo wadhalilisha”.


Na Allah kawausia wapiganao katika njia ya Allah kushikana pamoja.

Amesema Mola:-


الصف: ٤

“Kwa yakini Allah anawapenda wale wanaopigana katika njia yake, safu safu (mkono mmoja), kama kwamba wao ni jengo lililokamatana barabara”.


Na akawahimiza kushikamana na kuunganisha rai yao, amesema Allah Subhanahu Wataala:


الأنفال: ٤٦

“Na mtiini Allah na Mtume wake wala msizozane (msigombane), msije mkaharibikiwa na kupotea nguvu”.


Kukhitalifiana rai ni upungufu (pengo) ambao adui bila shaka autumia ili kuwashinda waislamu, na dalili kubwa ya jambo hili wakati washirikina waliposhindwa katika vita vya Uhud waliweza kutambua mara tu wale waislamu, walioamrishwa wasiondoke kutoka Jabali Uhud, walipoanza kuteremka na kuvunja amri ya Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie.


Na Jihadi ina tunda katika dunia, nalo ni furaha, amani, neema na matumaini na tunda lake katika Akhera ni furaha ya milele watakaotiwa humo ndani (Janna) bila ya kutolewa. Na Mujahid alieuliwa kwa sababu ya kutaka kunyanyua Neno la Allah au kumzuia adui dhalimu asiingie katika nchi (watani) yake au kukinga heshima yake (nafsi yake na watu wake) au kupigania mali yake basi anayeuliwa katika sehemu hizi yeye ni shahidi na daraja yake katika Al-Janna yu pamoja na Manabii na Masaddiqqiin. Amesema Allah Subhanahu Wataala:


النساء: ٦٩

“Na wenye kumtii Allah na Mtume wake, basi hao watakuwa pamoja na aliowaneemesha Allah: Manabii na Masadiki na Mashahidi na Masalih (watu wema). Na uzuri ulioje (kwa mtu) watu hao kuwa rafiki (zake)”.




Wapiganaji Jihadi ni aina mbili. Aina ya kwanza ni wale wanaopigana na Washirikina. Na aina ya pili ni wale wanaopigana na waliokiuka mipaka ya Allah Subhanahu Wataala. Washirikina hapa wamekusudiwa Mayahudi, Manasara, wanaoabudu moto, Wasabai na wanaoabudu masanamu katika waarabu na wengineo waliokuwa hawana dini. Na amewataja Mola katika kitabu chake:-


الحج: ١٧

“Na ambao ni Mayahudi na Wasabai na Wakristo na Majusi na wale washirikishao”.


Basi ndio hivyo inabidi kupigana na Mayahudi, Manasara na waliokuwa mfano wao wapigwe mpaka waingie Uislamu au walipe jizya (kodi) kwa hiari yao hali wametii kwa dalili ya kauli ya Mola Subhanahu Wataala:


التوبة: ٢٩

“Piganeni na wale wasiomuamini Allah wala siku ya mwisho wala hawaharimishi alivyo viharimisha Allah na Mtume wake, wala hawashiki dini ya haki, miongoni mwa wale waliopewa Kitabu (piganeni nao) mpaka watoe kodi kwa hiari yao, hali wametii”.


Amma wanaoabudu masanamu na wale waliortadi (wametoka kwenye Uislamu baada ya kuwa waislamu) hawa wapigwa vita mpaka waingie Uislamu wala hawakubaliwi kutoa kodi na mali zao halali kuchukuliwa na hawana hiari nyingine isipokuwa kuingia kwenye Uislamu na kuurudia Uislamu (kwa wale waliortadi) au sivyo upanga (yaani wapigwe vita).


Na vikundi vyote vilivyotajwa katika kitabu cha Allah kitukufu ambavyo vimekwisha tajwa hapo nyuma vina hukumu katika sharia. Wakijichagulia nafsi zao upanga basi zitekelezwe juu yao hukumu za Allah Subhanahu Wataala na zachukuliwa mali zao na wachukuliwa mateka wanawake wao na vizazi vyao na hao amewaita Mola Subhanahu Wataala kinachomilikiwa na mkono wa kuume (milki al yamiin).

Amesema Allah Subhanahu Wataala:


الأحزاب: ٥٠

“Na (wanawake) uliowatamalaki kwa mkono wako wa kulia katika wale aliokupa Allah”


Kama vile vile amewaita katika aya nyinginezo kwa jina la Arriqab (shingo).

Amesema Allah Subhanahu Wataala naye mkamilifu wa ukweli:-


البقرة: ١٧٧

“Sio wema (tu huo peke yake) kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa mashariki na magharibi katika kusali. (Yako na mema mengine). Bali wema (khasa) ni (wa wale) wanaomuamini Allah, na siku ya mwisho na malaika na kitabu na manabii na wanawapa mali – juu ya kuwa wanayapenda – jamaa na mayatima na masikini na wasafiri (walioharibikiwa) na waombao na katika (kuwakomboa) watumwa”.


Vile vile imekuja katika pahala pengine (katika Qur’ani) kwa lafdhi ya upweke (mufrad):

البلد: ١٣

“(Kuukata mlima huo) ni kumpa mtumwa uhuru”.


Kuchukuwa (kupata) mali yao na kuteka wanawake zao na vizazi vyao haya yote thabiti kwa dalili ya Qur’ani na Sunna. Ama katika Qur’ani amesema Allah :-

الأنفال: ٤١

“Na jueni ya kwamba chochote mnachokiteka (mnachokipata ngawira) basi sehemu yake ya tano (moja katika tano)ni kwa ajili ya Allah na Mtume na jamaa (zake mtume) na mayatima na masikini na wasafiri (walioharibikiwa) ikiwa nyinyi mumemuamini Allah na tuliyoyateremsha kwa mja wetu siku ya kipambanuzi, siku (inayowafikiana na siku) yalipokutana majeshi mawili (siku ya vita Badri, jeshi la waislamu na jeshi la makafiri)”.


Basi ndio hivyo yagaiwa mapato (ya nchi zilizofunguliwa na waislamu na ya vita) kama alivyobainisha Allah Subhanahu Wataala  na akaweka wazi katika aya nyenginezo:-

الحشر: ٧

“Mali aliyoleta Allah kwa mtume wake kutoka kwa watu wa hivi vijiji (vilivyo karibu na Madina) ni kwa ajili ya Allah (basi yatatumika kwa ajili ya dini ya Allah) na kwa ajili ya mtume (wake basi atachukuwa mwenyewe) na jamaa (zake) na mayatima na masikini na msafiri aliyeharibikiwa”.


Na katika rehema zake Allah Subhanahu Wataala na uadilifu baina ya waja wake na kuwaweka wote wawe sawa baina yao ni kutunabahisha tuikandamize nafsi yenye kuamrisha kufanya maovu na kujiona bora kuliko mwenzake, basi tusiiwache kama inavyotaka bali tuiteremshe mbele ya mwenzake.

Anasema Allah Subhanahu Wataala :-


الحجرات: ١٣

“Hakika ahishimiwaye sana miongoni mwenu mbele ya Allah ni yule amchaye Mungu zaidi katika nyinyi”.


Kisha baada ya hivyo akapanga Mola Subhanahu Wataala hukumu za kuitowa ile nafsi iliyofungwa na pingu ya utumwa kwa kuirejeshea uhuru wake na kuibandua(kuipapatua) kutokana na hukumu za kutekwa, akajaaliya ukombozi wa mtumwa katika vitendo vyenye thawabu kubwa sana ambapo akifanya kitendo hichi (kukomboa mtumwa) mwenye madhambi kinakuwa sababu ya kumuokoa na kumuepusha (na adhabu ya Allah) kwa upungufu na makosa aliyoyafanya katika haki ya Allah kama kuacha fardhi au kuua nafsi kwa makosa au wenye kuapa kuwa watajitenga na wake zao au wale wawaitao wake zao mama zao basi hawa wakitaka kutubu na kurejea kwa Allah Subhanahu Wataala basi ni juu yao kukomboa mtumwa anayeashiriwa katika kauli yake Subhanahu Wataala:-


الأحزاب: ٥٠

“Na (wanawake) uliowatamalaki kwa mkono wako wa kulia”.


Hekima kubwa (haina shaka yoyote) ya Aliyetakasika na upungufu wowote, Mwenye Hekima, Mwenye Elimu, Mpole kwa waja wake hawezi kukosa kuifahamu(hiyo hekima) isipokuwa yule aliye mpumbavu na asi wa Muumbaji wake. Ajabu kubwa kusikia wale maadui wa Uislamu wawatia fikra mbaya wale Waislamu wenye imani dhaifu kwa kuwambia vipi inaruhusiwa katika Uislamu mtu kummiliki binaadamu mwenzake (ili hali wanaona wazi kuwa Uislamu ndio unaohimiza kukomboa watumwa kwa kumlipa anaefanya hivyo thawabu kubwa) lakini waleta fikra hizo mbaya ili kuhudumu maslaha yao (ya kuuchukiza Uislamu). Wao wameghafilika na mafundisho ya Muumbaji Mwenye Hekima ambaye katika mikono yake kuna funguo za Mbingu na Ardhi kama kwamba wao wako mbele (ya Allah Subhanahu Wataala) katika kujua maslahi ya binaadamu na kuwashughulikia. Waita mwito uliokuwa si wa kweli kabisa eti twataka haki za binaadamu (na wao ndio wa kwanza wanaowateketeza binaadamu kwa kila njia waiwezayo, khasa Waislamu).


البقرة: ١٥٦

"Hakika sisi ni wa Allah, na kwake Yeye tutarejea(atatupa jaza yake)"


Amesema Allah Subhanahu Wataala:


النساء: ٨٩

“Wanataka (makafiri) lau mngekufuru kama walivyokufuru wao ili muwe sawa sawa”.


Basi tahadhari ewe ndugu yangu wa Imani kutokana na neno hilo:-


الفرقان: ٢٨

“Eee Ole wangu (adhabu yangu)! Laiti nisingalimfanya Fulani kuwa rafiki”.


Allah Subhanahu Wataala atuhidi sote kwenye njia iliyonyooka.


Aina ya pili: Waliopindukia mipaka nao ni katika watu wenye kutamka Tawheed ambao husali na hufunga lakini wametakabari juu ya viumbe na wakatoka nje ya utiifu wa hukumu wafanya hivyo katika msingi wa kupindukia mipaka na kufanya uadui. Hawa wapasa kupigwa vita baada ya kusimamishiwa hoja juu yao kuwa wamepotea njia ili warudi chini ya Utawala wa Uadilifu na wafate hukumu zake na anaekufa miongoni mwao katika vita basi huingizwa motoni, Allah atuepushe nao. Aina hii haichukuliwi mali yao wala kutekwa vizazi vyao bali haihalalishiwi mali yao walau kitu kidogo kwa sababu mali ya watu wa Qibla ni haramu kwa kauli ya Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- amesema:-

(من قال لا إله إلا الله  محمد رسول الله  فقد أحرزوا مني أموالهم ودماءهم إلا بحقها وحسابهم على الله)

 “Wanaotamka ‘Lailaha illa Llah, Muhamadan Rasulullah’ basi wamejikinga na mimi (kuwa siwachukulii) mali zao na damu zao isipokuwa kwa haki yake na hisabu yao iko kwa Allah."



Wao ni aina mbili:-

Aina ya kwanza huwa wanapo mahala pa kukimbilia na wanaye kiongozi wa kumrejelea kwa mambo yao. Na aina hii wakishindwa huuliwa majruhi wao (aliyejurihiwa) na hufatwa anaekimbia kati yao mpaka auliwe na mfano wake vita vya Aliy bin Abi Talib katika Safein alipopigana na Muawiya bin Abi Sufyan kwa sababu Muawiya ni marejeo kwa wanaoshindwa.


Aina ya pili – Hawana kituo wala kiongozi wa kurejea kwake basi hao hauliwi majruhi wao wala hafatwi anaekimbia kati yao na mfano huu ni vita vya Aliy bin Abi Talib vile vile siku ya Al Jamal alivyopigana na Talha, Azzubeir na Aisha, basi alieshindwa kati yao hauliwi wala hafatwi aliekimbia kwa sababu viongozi wawili Talha na Azzubeir waliuliwa katika mapambano hayo na Aisha amerejea kutubu (Allah amridhie na amghufirie makosa yake). Na Aliy bin Abi Talib katika vita vyote viwili hivi yeye ni Imam wa haki kwa makubaliano ya Masahaba na ili kujua urefu wa matukio haya arejee atakae vitabu vya tarehe na haiwezekani kujua ukweli au uhakika isipokuwa yule anaeutafuta na kuufuata kwa insaaf. Amma utelezi au upotevu hausemwi. Asije akasema Muislamu kama walivyosema wengine bila ya kujali ikiwa jambo hilo analolisema ni sawa sawa au kosa. Kwani wengi katika waandishi wa tarehe waliopita wameipotoa tarehe ya vita vya Masahaba wakaiandika sio kama vile ilivyotokea na waliokuja baada yao wakawafuata bila ya kujitaabisha kuutafuta ukweli.

 ولا حول ولا قوة إلا بالله Na hakuna uwezo wala nguvu isipokuwa kwa Allah.


Kutaja sifa za wapiganaji katika njia ya Allah Subhanahu Wataala (Mujahidiin).


Twataja sifa za Maimamu na wanavyuoni katika mujahideen wa Ahli Al-Istiqama na twatosheka kwa aliyoyasema Mwana shairi (Mwana chuoni) wa wakati huo Sheikh Abu Muslim Nassir bin Salim Arrawahiy wakati alipotaka kuwasifu watu wazuri hao akatanguliza kuusifu mji wao (mji wa Nizwa) akasema kumwambia yule anayekusudia huo mji. Katika shairi maana yake kama ifuatavyo:-


Fika, teremka katika eneo lote lina utukufu, hapo ndipo haki ina nuru na matawi. Teremka fika kwenye ardhi yenye nuru ambayo imewaweka Maimamu wa dini ya uongozi juu ya mgongo wake na eneo lake tambarare ambapo Malaika wameingia katika sehemu zao. Kawaida kwa hao malaika kuingia na kuondoka katika hizo sehemu (jinsi zilivyokuwa tahiri kwa hao Maimamu) Ardhi imetoharishwa, imebarikiwa inayo nuru na hayo ni matunda ya elimu na imani kwa sababu ya yakini yake (hiyo ardhi tahiri – Nizwa) na kufata kwake amri ya Allah Subhanahu Wataala ameisaidia kwa kuipa ufunguzi, ushindi na kuayidiwa na Allah Subhanahu Wataala. Umethibiti Uislamu hapo kutoka zama na zama ijapokuwa mara nyingine uadilifu hujificha. Toka zamani sana yatajwa ardhi hii kwa kushika kwake dini toka kuingia Tawhiid na Qur'ani. Basi ikasimama ngome ya Kiislamu mpaka maadui wakanyenyekea na kuwa kituo cha kulinda uadilifu na uongofu. Mara ngapi Allah Subhanahu Wataala amewapa ushindi (watu wa ardhi hii) dhidi ya watawala wa dhulma na shaitani. Ameikhusisha Allah Subhanahu Wataala kuwa ndipo pahala pa ushindi na ufunguzi kwa Waislamu. Akaendelea kusema:-  Wakafuatana makhalifa wa Allah Subhanahu Wataala kuanzia Imam Al-Julanda na kumalizia Imam Azzan. Maimamu hawa ndio waliohifadhi dini iliyotoka kwa Mola Subhanahu Wataala toka siku iliyobadilika dini yake kuwa dini chungu nzima walikuwa wenye tabia njema, makarimu na watu wa ibada, Simba (kwa ushujaa) wakataa dhulma, wao ni kama majahazi ya kuokoa watu (kutokana na upotevu) viongozi wa watu nao ni kuta zinazolinda Uislamu. Wakatenda yote yalioko katika Qur'ani katika siri yao na dhahiri yao, Sunna ya Muhammad -rehema za Allah na amani zimshukie- (dini yake safi aliyekuja nayo) ndiyo sira yao kwa kufanya hivyo wataka kuwa na Imani sahihi na Ihsani. Wamefata sira ya Makhalifa wawili (Abu Bakar R.A na Omar R.A.)


Nafsi zao zafanya mkazo mkubwa katika kuinusuru dini ya Allah Subhanahu Wataala na wajaalia nafsi zao fidaa katika kumnusuru Allah Subhanahu Wataala na kufanya jihadi katika njia yake wakimbilia kufanya mambo ya kheri kwa vile walivyokuwa mahodari na wajanja wamezikaribisha nafsi zao (wameziteremsha) ndipo zilipokuwa na nguvu na kila ulipo uongofu utawakuta wapo hapo. Alama zao ni nuru katika umbo lao na  katika tabia zao nao wanafata Sunna za Mtume Muhammad -rehema za Allah na amani zimshukie- Hekima zao zipamoja na hukumu ya Allah Subhanahu Wataala na hima zao. Wao ni wanaoiyona haki na kuisikia zaidi na katika batili wao ni vipofu na viziwi hawapotezwi na mapambo ya dunia na udanganyifu wake kwani hima yao ni kusimama katika njia ya Allah na radhi yake. Wameuza dunia yao ya kupita kwa kutaka ridha ya Mola wao inayo baki kama kwamba ladha ya dunia hii haina ukweli, hawakuwa mbali na njia ya Mukhtar katika mwendo wao wala azima yao haikupindishwa na nafsi wala shetani basi wakapigana jihadi na kunyooka katika njia yake mpaka ukawa utawala wao ni hukumu na sharia ya Allah Subhanahu Wataala. Watu hao ndio mwangaza wangu nimeongoka kwa kuathirika nao na kufuata mfano wao na malipo yake ni kuwapenda watu hao na kupata msamaha wa Allah na kughufuriwa madhambi. Hao ni Maimamu (viongozi) wangu mabwana zangu, dalili yangu ndio waokozi wangu kutokana na dhiki inayonipata. Allah Subhanahu Wataala hakubali dini yoyote nyingine isipokuwa dini yao na hakuna uongofu mwingine isipokuwa ule waliokuja nao, tokea zama za Badr na Uhud hawakuondoshwa kutoka msimamo wa haki na fitina zilizopita na wala nyakati (wamebakia katika msimamo ule ule).


Ikiwa heshima ya watu duniani kwa mali na utajiri wao heshima ya watu hawa (Maimamu) ni kwa yakini na Ikhlasi, kila wanachokifanya ni kwa ajili ya Allah Subhanahu Wataala tu. Unawaona usiku wa manane wamesimama wasali na kusoma Qur'ani. Hao ni Maibadhi wakarimu wenye daraja juu ya watu wengine kwa uwezo wa Allah Subhanahu Wataala. Haujulikani uadilifu isipokuwa katika msimamo wao wa sawa na haikupewa mezani haki yake na usawa isipokuwa kwao wao, kazi yao ni kujiweka mbali na yaliyo haramishwa na Allah Subhanahu Wataala sio kazi yao kuitaka dunia ni sawa sawa kwao wakiipata au wakinyimwa (hiyo dunia) wameridhika na yale maisha waliyopewa na juu ya hivyo wana wasi wasi kuwa labda wamechukua zaidi katika hayo maisha kuliko wanavyostahiki. Alama za kutosheleka na maisha zaonesha katika sura zao kama kwamba ni matajiri, moyo umeshiba na tumbo lina njaa. Njia ya wafalme(namna yao) na uongofu wa manabii katika tabia zao kama kwamba ufakiri kwao ni ufalme, hao hawakudanganyika, na uhakika wa maisha ya dunia kuwa ni hadaa. Wamevuka daraja (mtihani wa dunia) nao wamebeba mzigo mwepesi wana khofu, subra, wamepuuza dunia na washukuru neema za Mola wao. Wamefuzu wenye mizigo myepesi katika mahali hapa pa udanganyifu (dunia) hawana hofu hao wala hawahuzuniki. Wamekwenda na athari yao na kumbusho lao ni nuru na kuwataja ni rehema na malazi yao ni furaha na rehema. Wamefatilia Dola katika athari ya Dola iliyopita yaani mfano ule ule mzuri kama Manabii aliyekuja kaendeleza risala ya mtume aliyopita. Mpaka akasema (huyu mtoa shairi) mpaka ikapambazuka nyota (Sayari) yenye mwangaza mkali na kumetameta na kwa mwangaza wake ikadhihirika haki. 


Na akasema katika kumsifu Imam Salim bin Rashid Al-Kharusi katika Maimamu waliochaguliwa kuongoza kwa sharia ya Qur'ani na Sunna mmoja kati yao alikuwa amejaa imani katika kifua chake na hima yake ilikuwa kubwa sana na alikuwa mwenye kuihifadhi nchi yake na kuitosheleza na mwenye uwezo wa kubeba dhamana ya utawala. Umekuja uimamu wake na nchi imejaa dhulma na watu wako katika hali ya fujo na madhalimu wafanya watakavyo basi akaweza kwa hekima kutengeza hali hii na kueneza badala yake uadilifu na palipohitajia nguvu (jihadi) aliitumia, kwani ushindi wa Allah Subhanahu Wataala mwenza mwenzake ni jihadi (upanga), kwa sababu katika hali kama hii ukitumia tabia nzuri na ukarimu haufai kitu lazima utumie nguvu. Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani zimshukie- wakati alipokuwa Makka alifanyiwa maudhi na dhiki kubwa sana lakini aliporudi kufungua Makka baada ya Al-Hijra amekuja katika hali ya nguvu basi wale wale waliompa dhiki kabla wakamuangukia kumtaka radhi na msamaha.

Hapa zatajwa aina za ukafiri.


Unagawanyika ukafiri sehemu (aina) mbili:-                                                                                                              

(1) Ukafiri wa shirki nao ni kumshirikisha Allah Subhanahu Wataala kwa kuabudu mwengine pamoja na Yeye nayo inayojulikana kwa jina la Al-Musawaa yaani kumfanya mwengine sawa sawa na Yeye Subhanahu Wataala. Au kukataa kuwa kuna Mungu nayo inaitwa “Juhuud” au kukataa mmoja katika Manabii au Mitume wake au Malaika wake au kukataa kitu katika Qur'ani Tukufu walau harufu moja au kukataa kitu katika mambo ya faridha kama nguzo tano za kiislamu au kuhalalisha madhambi makubwa na kuitaqidi kuwa sio haramu, na hizo ni zile kabair (Madhambi makubwa) zilizotajwa katika Qur'ani au Sunna, au kurtadi kutokana na dini ya Kiislamu na kuingia dini nyingine au kuufanya Uislamu sawa sawa na dini nyingine kama mtu kusema:- Hapana kitu kwangu kufata dini yoyote katika hizi dini za Mbinguni (Adyaan Samawiya) au dini za Allah Subhanahu Wataala.

(2) Ukafiri wa neema (kufr Nneema) nao ni kufanya madhambi makubwa makubwa sawa sawa ikiwa madhambi haya ni ya kuonekana au ya ndani (siri) na ya kuonekana kama zina, riba, kula maiti au damu au nyama ya nguruwe, kuuwa nafsi iliyoharamishwa kuuliwa, kuwakatia watu njia ili kuwaibia, kuwadhulumu waja, kuiba, kuudhi Waislamu na kuwatia khofu, kueneza ufisadi katika ardhi, kunusuru batili (kinyume cha haki), kuikataa haki na kuwapinga watu wake (wa haki) kunywa pombe na vileweshaji vyote, kuvaa dhahabu na mengineyo kama kunyoa ndevu, kusaidia watu wabaya na kueneza maasia katika magazeti, kuipamba batili, kutangaza mambo ya washirikina kama kutangazia mavazi yao n.k. Haya yote ni katika madhambi makubwa makubwa yanayoitwa kufr nneema kwa msingi wa Qur'ani na Sunna na Ijmaa ya Umma, miongoni mwa dalili zilizoko katika Qurani kauli yake Mola:-


آل عمران: ٩٧

“Na Allah Amewawajibishia watu wafanye Hija katika Nyumba hiyo yule awezaye kwenda huko na atakayekanusha basi Allah si mhitaji kuwahitajia walimwengu”.


Na kauli yake:-

الروم: ٤٤

“Anayekufuru (madhara ya) kufuru yake ni juu yake (mwenyewe) na wafanyao wema (hao) wanazitengenezea nafsi zao”.


Na akaijaalia kufuru mukabili wake imani. Na kauli yake akizungumzia juu ya Nabii Suleiman A.S.:-

النمل: ٤٠

"(Basi alipokiona kimewekwa mbele yake) alinena:

'Haya ni kwa fadhila za Mola wangu ili anijaribu nitashukuru au nitakufuru (nitakuwa mwizi wa fadhila)'."


Hapa Allah Subhanahu Wataala ameijaalia kufuru mukaabili wake shukrani na kauli yake Mola Subhanahu Wataala:-


البقرة: ١٥٢

“Basi nikumbukeni (kwa kunishukuru kwa hii neema niliyokuneemesheni ya kukuleteeni Mtume) (Nami) nitakukumbukeni, na nishukuruni wala msinikufuru”.


Na dalili katika Sunna ni kauli yake Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- kama alivyoitowa Ibn Abbas R.A.:

(من قال لأخيه يا كافر, فقال أنت الكافر فقد باء بالكفر أحدهما والبادي أظلم)

 "Anaemwambia ndugu yake (mwenzake) ewe kafiri akamjibu kumwambia wewe ndie kafiri basi amejitia katika ukafiri mmoja wao na aliye dhalimu zaidi alieanza"


(من ترك قتل الحية خوف الثأر فقد كفر)

"Anayewacha kumua nyoka kwa kuogopa kumn’gata basi amekufuru"


Na riwaya iliyotolewa na Ibn Abbas R.A.:

 (من أتى الرجال شهوة دون النساء , أو أتى النساء في أعجازهن فقد كفر)

‘Anaewaingilia wanaume badala ya wanawake au kuwaingilia wanawake kwa nyuma basi amekufuru’.


Na katika riwaya nyingine:

( ليس بين العبد والكفر إلا تركه الصلاة)

‘Hakuna baina ya mja na ukafiri isipokuwa kuacha Sala’.


 Na katika riwaya nyingine:-

(العهد الذي بيننا وبينهم الصلاة فمن تركها فقد كفر)

‘Ahadi iliyo baina yetu (Waislamu) na baina yao (Makafiri) ni Sala basi anayeiwacha (asisali) amekufuru’


Na riwaya nyengine:-

(سباب المسلم فسوق , وقتاله كفر)

‘Kumtukana Muislamu ni ufasiki na kupigana naye ni ukafiri’


Na riwaya nyengine:-

(لا ترجعوا بعدي كفارا يضرب بعضكم رقاب بعض)

‘Msirejee baada yangu kuwa makafiri mnakatana shingo wenyewe kwa wenyewe’.


Na maasi yaliyofichika  (yasiyoonekana) ni kama yafuatayo:- Nayo ni kujiona nafsi yake kuwa hakuna kama yeye, kiburi, hasadi, kufanya riyaa (kujionesha kwa watu unapofanya ibada yako ili wakusifu), ghishi, khiyana na yote yale ambayo  tabia mbaya ndio huwa matokeo yake. Na sifa ya kujiona (ujbu) ni kuikuza mtu ile neema aliokuwa nayo na kupendezewa nayo wakati anawacha kufikiri kuwa amepewa neema hiyo na Allah Subhanahu Wataala na kuwa ameipata kwa nguvu zake na uhodari wake na ajiona kuwa ana hadhi. Inakuwa kujiona katika kila kitu katika sifa au mali au uzuri au ukoo au elimu au ushujaa na mengineyo katika yanayo mpendeza mtu, na anayosifiwa kwayo au apenda asifiwe kwa hayo mambo basi Muislamu akisibiwa na ugonjwa huu basi ajiwahi nafsi yake upesi kuwa ajue kuwa Allah Subhanahu Wataala ndiye mwenye fadhila juu yake kwa yale aliyoneemeshwa nayo na kupewa. Na kuwa yeye mwenyewe hana uwezo wowote katika hayo aliyopewa. Kama alivyosema Qaruni na Allah Subhanahu Wataala amemuelezea katika kitabu chake kitukufu kwa kusema :-


القصص: ٧٨

Akasema: “Hakika nimepewa haya kwa sababu ya elimu niliyonayo”. Je, hakujua ya kwamba Allah amewaangamiza kabla yake watu waliokuwa wenye nguvu zaidi kuliko  yeye na wenye mkusanyiko zaidi (kuliko wake yeye)? Na wabaya hawataulizwa makosa yao. (Allah mwenyewe anayajua yote).


Na kiburi – ni kuwadharau viumbe wenzake na kuirudisha haki (bila ya kuiamini na kuifuata) na sababu yake ni kujiona kuwa ana utukufu na ana kitu na daraja wenzake hawana kama uraisi wa nchi, uwaziri au umudiri au ukubwa juu ya  kikundi fulani cha watu, mambo haya yote yanamfanya mwenye kiburi adanganyike navyo na ajione kuwa ana haki navyo vitu hivyo ndipo anapotakabari juu ya wenziwe. Aliepata balaa hii ajitizame asili  yake aliyoumbiwa nayo na wapi utakuwa mwisho wake kama ilivyozungumzwa kutokana na Aliy bin Abi Talib kuwa amesema: ‘Mwanadamu mwanzo wake ni manii iliyo chafu na mwisho wake mzoga unaonuka naye baina ya mawili haya anabeba uchafu katika tumbo lake (kinyesi)’. Imetolewa kutokana na Ibn Abbas: ‘Anaeikuza nafsi yake mbele ya watu Allah humteremsha na yule anayeiteremsha nafsi kwa ajili ya Allah humpandisha’ na imesemwa katika athari: ‘Hauingizi  Al-Jannah uzito wa, chembe ya adesi, wa kiburi na kiwango cha chini kabisa cha kiburi ni kuchukia mtu kueka mdomo wake katika chombo pale alipoweka mdomo wake mnywaji kabla yake’.


Riyaa – ni kufanya vitendo (amali) kwa ajili ya binaadamu (ili wamsifu) na inaitwa shirki ndogo anaitwa kesho mtu kama huyu: Ewe muonyeshaji ewe Fajir, ewe mvunjaji wa ahdi, ewe ulio khasirika jitihada yako ya bure na amali yako imepotea. Anaepewa mtihani huu basi ni juu yake ajue kuwa viumbe havimiliki kumfaa yeye au kumdhuru cho chote au chochote cha kumfaa au kumdhuru bali anaefanya yote hayo ni Allah mmoja pekee ambae hakimshindi cho chote wala hakimpiti cho chote.


Hasadi – ni kutamani mwenzako aondokewe na neema aliopewa na Allah Subhanahu Wataala kama kusema katika nafsi yake mtu huyu ana mali nyingi sana hastahiki kuwa nayo mali haya bora yangekuwa yangu mimi nina haki zaidi nayo kuliko yeye. Dhambi hili ni katika madhambi makubwa kabisa yaliyofichika nalo ni asli ya shari na kwa sababu yake fitina zaenea na nafsi za watu zafisidika. Na mtu hasidi ni adui wa neema za Allah, haridhiki na kadhaa ya Allah Subhanahu Wataala na kadari yake na juu ya yote hayo anakuwa mtu huyu anaghadhabu moyoni mwake ambayo haimsaidii kitu, na moto ambao hauzimiki kwani yeye hawezi kuiondoa neema aliopewa mwenzake kwani anaetoa na kunyima ni Allah Subhanahu Wataala.

Anasema mtungaji shairi:-

Kiumbe anaechukiwa kabisa na Allah ni yule anaekesha amhusudu mwenzake wakati yuko katika kufurahika na neema zake.


Imethibitika kuwa moyo wa hasidi ni kama chumba kilichokuwa kina ngano imebunguliwa na wadudu. Katika hadithi "Ukihusudu usipindukie mpaka (usifanye uadui)". Inajuzu kutamani upate neema kama ya mwenzako bila ya kutamani imuondokee na aina hii yaitwa “ghibta” na ya juzu kutamani iondoke neema ya anaepiga vita Waislamu na kuwaudhi na kila aliekuwa neema yake ni balaa kwa Waislamu.


Imetolewa kutokana na Ibn Masood msije mkahusudu, mkafanya dhana na kufanya uadui (kupindukia mpaka) kwani hana hadhi ya Uislamu anaefanya hivyo wala hadhi katika Uislamu anaefanya jambo moja katika haya. Na kumdhania mtu vibaya inajuzu kwa yule anaejulikana kwa ubaya kama ilivyopokelewa kutokana na Omar bin Khattab R.A.: ‘Tunaemjua ana kheri twamsema kwa kheri na twamdhania vizuri na tunaemjua ana shari twamsema kwa shari na twamdhania vibaya’. Mambo haya ni mifano ya maradhi yaliyo ndani ya nafsi nayo yako mengi sana katika hayo kuwadhania vibaya Waislamu na vile vile miongoni mwa hayo kukata tamaa na Rehma ya Allah Subhanahu Wataala. Hakuna uwezo wala nguvu isipokuwa kwa kupewa na Allah Subhanahu Wataala. Tunamuomba Allah asituharimishie shahada katika njia yake na atupe tawfiiq ya kupata ridha yake na atujaalie tuwapende mawalii (wapenzi) wake na atujaalie tuwachukie maadui zake. Hakika Yeye tu ndie Mwenye kutoa tawfiiq. Na Sala za Allah (Rehma) ziwe juu ya Mtume wake Bwana wetu Muhammad pamoja na watu wake na Masahaba zake na salamu vile vile ziwe juu yao.


No comments:

Post a Comment

Note: only a member of this blog may post a comment.