ﭽ ﭑ ﭒ
ﭓ ﭔ ﭼ
ﭽ
ﭑ ﭒ
ﭓ ﭔ ﭕ
ﭖﭗ ﭘﭙ ﭚ
ﭛ ﭜ ﭝ
ﭞ ﭟ ﭠ
ﭡ ﭢ ﭣ
ﭤ ﭥ ﭦ
ﭧ ﭨ ﭩ
ﭪ ﭫ ﭬ
ﭭ ﭮ ﭯ
ﭰ ﭱ ﭲ
ﭳ ﭴ ﭵ
ﭶ ﭷﭸ ﭹ
ﭺ ﭻ ﭼ ﭼ
البقرة: ١ - ٥
“Alif Laam
Miym. Hiki ni kitabu, kisichokuwa na shaka ndani yake, ni uongozi kwa wamchao
(Allah). Ambao huyaamini yasioonekana (maadamu yamesemwa na Allah na Mtume
wake) na husimamisha Sala na hutoa katika tuliyowapa. Na ambao wanaamini
yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako na wanaamini (kuwa iko)
Akhera. Hao wako juu ya uwongozi utokao kwa Mola wao, na hao ndio wenye
kuongoka”.
Zaka ni
nguzo katika nguzo tano za Kiislamu nazo: Shahada, Sala, Zaka, Saumu na Hija
kwa mwenye uwezo.
Inasemekana
kuwa Zaka imefaridhishwa katika mwaka wa pili wa Hijra baada ya kufaridhishwa
Zaka ya Fitri. Pia imesemwa imefaridhishwa kwa ujumla huko Makka (yaani kabla
ya mwaka wa pili wa Hijra) na kwa ufafanuzi zaidi katika Madina.
Maana yake
kilugha ni kukuwa na kuzidi. Ama maana yake kisheria ni kile kinachotolewa
katika mali
au wanyama kwa mpango maalumu na kupewa watu mahsusi (mafakiri, maskini na wale
wanaokusanya Zaka n.k.)
Amesema
Sheikh Noor Addin Allah amrehemu:
Anasema
Allah Mtukufu:
ﭽ
ﮚ ﮛ
ﮜ ﮝ ﮞ
ﮟ ﮠ ﮡ
ﮢﮣ ﮤ ﮥ
ﮦ ﮧﮨ ﮩ
ﮪ ﮫ ﭼ التوبة: ١٠٣
“Chukua
Sadaka katika mali
zao, uwasafishe kwa ajili ya hizo (sadaka zao) na kuwataja kwa vizuri (mbele
yangu) na uwaombee Dua. Hakika kuwaombea kwako kutawapa utulivu
(watengenekewe); na Allah ndiye asikiaye na ajuwaye”.
Basi kama
isingekuja katika fadhila ya kutoa Zaka isipokuwa Aya hii tu ingetosha kwa
sababu imekusanya (Aya hii) baina ya faida mbili kubwa kwa mtoaji Zaka:
Ya kwanza: Kuwa
inamsafisha na madhambi.
Ya pili: Kustahiki
kuombewa Dua na Mtume Salallahu Alayhi Wasalam kwa kuitoa hiyo Zaka na hiyo ipo
katika kauli yake Subhanahu Wataala وصل عليهم na uwaombee Dua, na hii ndiyo tafsiri ya Ibn Abbas.
Amesema Asshaafiiy: Na katika sunna kuwa Imam akipokea sadaka kutoka kwa
mwenye kuitoa hiyo sadaka amuombee:
آجرك الله فيما أعطيت وبارك لك فيما أبقيت “Allah akulipe kwa ulichokitoa na akubarikie
kwa ulichokibakisha.
Na imepokewa kutoka kwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam kuwa amesema:
( حصنوا
أموالكم بالزكاة وداووا مرضاكم بالصدقة واستدفعوا أنواع البلايا بالدعاء )
“Hifadhini mali
zenu kwa Zaka na wagangeni wagonjwa wenu kwa sadaka na jiepusheni na kila aina
ya balaa kwa Dua.”
Na amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :
(ما نقص
مال من صدقة ، وما تواضع عبد إلا رفعه الله بها عزا)
“Haipungui mali
kwa (kutoa) sadaka, wala hawi mja mnyenyekevu (kwa Waislamu wenzake) isipokuwa
Allah humpandisha kwa huo (unyenyekevu wake) akawa na heshima (na nguvu mbele
ya watu)”
Na amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :
( من أدى
الزكاة وأقرى الضيف وأدى الأمانة فقد وقي شح نفسه )
“Mwenye kutuo Zaka na
kumkirimu mgeni na kuhifadhi Amana basi ameepushwa na ubakhili wa nafsi yake”.
Na amesema
Salallahu Alayhi Wasalam:
( عليكم بالصدقة فإن فيها ست
خصال ثلاث في الدنيا وثلاث في الآخرة فأما التي في الدنيا فتزيد في الرزق وتكثر
المال وتعمر الديار وأما التي في الآخرة فتستر العورة وتصير ظلا فوق الرؤوس وتكون
ستراً من النار )
“Shikilieni
kutoa sadaka kwani ina faida sita, tatu (hupatikana) Duniani na tatu Akhera. Ama
zilizo Duniani, huzidisha riziki na hukuza mali na huimarisha majumba, na ama
zilizo Akhera, husitiri utupu na hugeuka kivuli juu ya vichwa na huwa sitara ya
Moto”.
Baadhi ya
Wenye Hikima wamesema: Hakika katika sadaka kuna faida chungu nzima katika hizo
Duniani na nyinginezo Akhera.
Ama zilizo katika Dunia:
1. Hifadhi
ya mali
kwa mujibu wa kauli yake Salallahu Alayhi Wasalam:
Hifadhini mali
zenu kwa Zaka حصنوا أموالكم
بالزكاة
2. Kutahirisha kwa mwili kwa mujibu wa kauli ya Allah Subhanahu
Wataala:
ﭽ
ﮚ ﮛ
ﮜ ﮝ ﮞ
ﮟ ﮠ ﮡ
ﮢﮣ ﮤ ﮥ
ﮦ ﮧﮨ ﮩ
ﮪ ﮫ ﭼ التوبة: ١٠٣
“Chukua Sadaka katika Mali zao, uwasafishe kwa ajili ya
hizo (sadaka) na kuwataja kwa vizuri (mbele yangu) na uwaombee Dua. Hakika kuwaombea kwako kutawapa utulivu
(watengenekewe) na Allah ndiye asikiaye na ajuaye”.
3. Inaingiza
furaha kwa masikini miongoni mwa walioamini.
4. Baraka
katika Mali
na huzidisha riziki kwa kauli yake Subhanahu Wataala:
ﭽ ﯼ ﯽ ﯾ
ﯿ ﰀ ﰁﰂ ﰃ ﰄ
ﰅ ﭼ سبأ: ٣٩
“Na cho chote mtakachotoa
basi yeye (Mola) atakilipa, naye ni mbora wa wanaoruzuku.”
5.
Inaepusha balaa na maradhi kwa mujibu wa kauli yake Salallahu Alayhi
Wasalam: داووا مرضاكم بالصدقة wagangeni wagonjwa wenu kwa sadaka.
Na ama zilizo katika Akhera:
Inakuwa kwa mwenye kuitoa, kivuli kinamfunika na shida ya joto na
humfanyia hisabu ikawa nyepesi na humzidishia uzito wa mizani na humpandishia
daraja katika Pepo. Na kama ilivyokuwa fadhila
zake ni kubwa vile vile kuna maonyo makubwa kwa mwenye kuwacha kuitoa. Allah Subhanahu
Wataala ameiweka pamoja na Sala katika sehemu mbali mbali katika Qurani. Na
akatoa maonyo makali kwa mwenye kuiwacha kwa hiyo haifai kuiwacha wala
kuifanyia upuzi kwani kuipuuza kuitoa mwishoe hufikishia katika kuiwacha
kabisa. Kwa kuwa anaekaribia mahala palipohadharishwa huenda akaingia ndani
yake.
Anasema Allah Subhanahu Wataala :
ﭽ
ﮂ ﮃ
ﮄ ﮅ ﮆ
ﮇ ﮈ ﮉ
ﮊ ﮋ ﮌ
ﮍ ﮎ ﮏ
ﮐ ﮑ ﮒ
ﮓ ﮔ ﮕ
ﮖ ﮗ ﮘ
ﮙﮚ ﮛ ﮜ
ﮝ ﮞ ﮟ
ﮠ ﮡ ﮢ ﭼ التوبة: ٣٤ - ٣٥
“Na wale
wakusanyao dhahabu na fedha wala hawazitoi katika njia ya Allah, wape habari za
adhabu inayoumiza (inayowangoja). Siku (mali zao) yatakapotiwa Moto katika Moto
wa Jahannam, na kwa hayo vikachomwa vipaji vya nyuso zao na mbavu zao na
migongo yao, (na huku wanaambiwa): Haya ndiyo (yale mali) mliojilimbikiza
(mliojikusanyia) nafsi zenu, basi onjeni (adhabu ya) yale mliyokuwa
mkikusanya”.
Na anasema Subhanahu
Wataala:
ﭽ ﮉ ﮊ
ﮋ ﮌ ﮍ
ﮎ ﮏ ﭼ فصلت: ٦
- ٧
“Na adhabu itawapata
wanaomshirikisha (Allah) ambao hawatoi Zaka”.
Basi adhabu
imejaaliwa kwao kwa sababu ya kuacha kutoa Zaka kama
ilivyojaaliwa kwao kwa kumshirikisha Allah.
Amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :
( يكون كنز أحدكم يوم القيامة
شجاعاً أقرع يفر منه صاحبه وهو يطلبه حتى يلقمه أصابعه )
“Itakuwa
hazina ya mmoja wenu Siku ya Kiyama jichatu (shujaa) lililokuwa halina nywele
kichwani kwa wingi wa sumu yake na umri wake mrefu basi huyo sahibu wake
atalikimbia na yeye atamkimbiza mpaka amtie vidole vyake kinywani”.
Na amesema Mtume
Salallahu Alayhi Wasalam:
( ما من رجل لا
يؤدي زكاة ماله إلا جعل الله له يوم القيامة في عنقه شجاعا ثم قرأ علينا مصداقه من
كتاب الله : ﭽ ﯲ ﯳ
ﯴ ﯵ ﯶ
ﯷ ﯸ ﯹ
ﯺ ﯻ ﯼ
ﯽﯾ ﯿ ﰀ
ﰁ ﰂﰃ ﰄ
ﰅ ﰆ ﰇ
ﰈ ﰉﰊ ﰋ
ﰌ ﰍ ﰎﰏ
ﰐ ﰑ ﰒ
ﰓ ﭼ آل
عمران: ١٨٠
“Mtu yeyote
asiyetowa Zaka Allah atamwekea shingoni mwake jichatu (shujaa) Siku ya Kiyama.
Kisha akatusomea katika Kitabu cha Allah Aya inayosadikisha hayo:-
“Wala
wasione wale ambao wanafanya ubakhili katika yale aliyowapa Allah katika
fadhila zake kuwa ni bora kwao (kufanya ubakhili huo). La, ni vibaya kwao,
watafungwa kongwa (madude ya kunasa shingoni) za yale waliyoyafanya ubakhili,
siku ya kiama. Na urithi wa Mbingu na Ardhi ni wa Allah. Na Allah ana khabari
za yote mnayoyafanya”.
Na amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :
( ما من صاحب ذهب ولا فضة لا
يؤدي منها حقها إلا إذا كان يوم القيامة صفحت له صفائح من نار فأحمي عليها من نار
جهنم فيكوى بها جنبه وجبينه وظهره كلما بردت أعيدت له في يوم كان مقداره خمسين ألف
سنة حتى يقضي بين العباد فيرى سبيله)
“Mtu ye yote mwenye dhahabu au fedha na hatoi
haki yake (yaani hailipii Zaka) Siku ya
Kiyama atachomwa na sahani za Moto. Zinapashwa Moto (hizo sahani) na Moto wa
Jahannam kisha aunguzwe nazo mbavuni mwake na kipajini mwake na mgongoni mwake.
Na kila zikipata baridi zinachochewa tena katika siku iliyo na kadiri ya miaka
elfu khamsini (atakuwa katika hali hiyo) mpaka Allah Subhanahu Wataala amalize
kuwahukumu waja wake kisha atizame nini la kumfanya. Akaambiwa ewe Mtume wa
Allah: Je Ngamia? Akasema:
( ولا صاحب إبل لا يؤدي منها حقها إلا إذا كان يوم القيامة
بطح لها بقاع قرقر أوفر ما كانت لا يفقد منها فصيلا واحداً تطأه بأخفافها وتعضه بأفواهها
كلما مر عليه أخراها رد عليه أولاها في يوم كان مقداره خمسين ألف سنة حتى يقضي بين
العباد فيرى سبيله )
“Wala mwenye
ngamia asietoa haki yao Siku ya Kiyama ataangushwa katika ardhi tambarare laini
na watamjia hao ngamia wote bila ya kukosekana mmoja (katika hao aliokuwa
hakuwatolea Zaka) na watamkanyaga kwa miguu yao na watamn`gata kwa midomo yao
kila akimpitia wa mwisho wao humrudia wa mwanzo wao katika siku yenye
kukadiriwa miaka elfu khamsini mpaka Allah Subhanahu Wataala amalize kuhukumu
waja wake kisha atizame nini la kumfanya.”
Akaulizwa:
Ewe Mtume wa Allah Je n`gombe na mbuzi akasema:
( ولا صاحب بقر ولا غنم لا يؤدي منها حقها إلا إذا كان يوم القيامة بطح لها
بقاع قرقر لا يفقد منها شيئاً ليس فيها عقصاء ولا جلحاء ولا عضباء تنطحه بقرونها
وتطأه بأظلافها كلما مر عليه أخراها رد عليه أولها في يوم كان مقداره خمسين ألف سنة حتى يقضي بين العباد
فيري سبيله )
“Wala
mwenye n’gombe wala mbuzi hatoi haki yao (hawalipii Zaka) Siku ya Kiyama ataangushwa katika ardhi
tambarare laini na hatampotea mmoja katika hao (n’gombe na mbuzi isipokuwa
watahudhuria katika uwanja huo) hamna kati yao wenye pembe za kusokotana wala wasiokuwa
na pembe wala wenye pembe zilizokatika watampiga kwa mapembe yao na kumkanyaga
kwa kwato zao kila akishamaliza kumpitia wa mwisho wao hurudi wa mwanzo wao
katika siku yenye kukadiriwa miaka elfu khamsini mpaka Allah Subhanahu Wataala
amalize kuhukumu waja wake kisha atizame nini la kumfanya.”
Akaulizwa
Ewe Mtume wa Allah Je farasi? Akasema: “Farasi watatu, yuko farasi alie kwa
sahibu yake (bwana wake) ni mzigo wa madhambi, na farasi ni sitara kwa bwana
wake na farasi anampatia bwana wake malipo mazuri. Ama yule alie mzigo wa
madhambi ni yule ambaye bwana wake amemfunga kwa kujionesha au kwa
kujifaharisha na ni uadui juu ya Waislamu. Na yule mwenye kumsitiri bwana wake
ni yule ambaye bwana wake amemfunga kwa njia ya Allah kisha hakusahau haki ya
Allah Subhanahu Wataala (Zaka) kwa anachombebesha juu ya mgongo wake au shingo
yake (mali
anayoipata huitolea Zaka). Ama yule (farasi) anayempatia bwana wake thawabu ni
yule anayemtoa kwa Waislamu ili kupigana kwa njia ya Allah (Jihadi) na kumfunga
malishoni au katika bustani basi huwa hali hapo malishoni au bustanini au kitu
cho chote isipokuwa huandikiwa (huyo mwenye kumtoa huyo farasi kwa ajili ya
Allah) idadi ya anachokila thawabu na aandikiwa idadi ya vinyesi vyake na
mikojo yake thawabu. Na wala hakati kamba yake akalishia katika mnyanyuko au
minyanyuko miwili isipokuwa huandikiwa idadi ya athari ya alichokula na
alichokunywa thawabu, wala bwana wake hakumpitisha mtoni akanywa ndani yake
wala hakutaka kumnywesha isipokuwa Allah humuandikia (huyo mwenye farasi) idadi
ya alichokunywa thawabu.”
Akaulizwa:
Ewe Mtume wa Allah Je Punda? Akasema: Hakuteremsha Allah kitu kuhusu Punda
isipokuwa Aya hii yenye kukusanya maana kubwa:
ﭽ ﮇ ﮈ ﮉ
ﮊ ﮋ ﮌ ﮍ ﮎ
ﮏ ﮐ ﮑ
ﮒ ﮓ ﮔ ﭼ
الزلزلة: ٧ - ٨
“Basi anayefanya
wema hata kiasi cha uzito wa mdudu chungu ataona jaza yake. Na anayefanya uovu
hata wa kiasi cha uzito wa mdudu chungu ataona jaza yake”.
Nasema:
Siku hizi gari zimechukua mahala pa farasi basi na ifuatwe hiyo migawanyiko
mitatu waliopewa farasi. Na Allah hakifichiki kitu kwake.
Na
iliyotolewa ni sehemu ndogo ya malipo makali atakayopata mwenye kuacha kulipa
Zaka na iwapo atatubu kwa Allah na akarudi kwake basi inamlazimu alipe Zaka
zote alizoacha kulipa kwa mujibu wa kauli sahihi iliyo kwa Sheikhe wetu Noor
Addin Allah amrehemu akisema: Zimejengwa ruhusa juu ya msingi wa kurahisisha
mambo na kutoa habari njema (kuwapa moyo wa kupata malipo mazuri), na Rehema za Allah Subhanahu Wataala zimeenea
na msamaha wake mkubwa.
Inamuwajibikia
Muislamu Zaka katika aina mbali mbali ya mali yake kama dhahabu na fedha ni sawa
sawa iwapo ni pesa au mapambo au mapande ya maadini hayo yahifadhiwayo au deni
amemkopesha mtu (mali ya Muislamu yaliyoko kwa mtu mwingine yahisabiwa katika
kutoa Zaka).
Inawajibika
Zaka katika biashara aina yoyote ya biashara hata ikiwa ya mchanga.
Hakuna budi
kuweka mwezi maalumu wa kuilipa Zaka na bora kuwa mwezi wa Ramadhani kwa sababu
malipo katika mwezi huu huongezwa na unaweza ukachagua mwezi wo wote mwingine.
Iwapo kwa
mfano mwezi aliouchagua mtu wa kulipa Zaka ni mwezi wa Ramadhani, basi ahisabu
mwisho wa Shaabani pesa zote alizoziweka (savings) na zile alizozitia katika
biashara ikiwa zimetimia mwaka au hazikutimia ni juu yake kutizama mali yote
aliyonayo katika mwezi aliouchagua kutoa Zaka azitolee Zaka ikiwa zimefika
“Nisaab” (kiwango maalumu ambacho ni wajibu mali kuitolea Zaka ikiifikilia).
Na “Nisaab”
ni mithqaal ishirini ya dhahabu au mithqaal mia mbili ya fedha ikifika hapo
basi ni wajibu kuitolea Zaka na hutolewa robo ya moja kwa kumi (1/40) yaani
2.5% (asilimia) ya mali hiyo iliyotimia kiwango hicho maalumu kilichotajwa hapo
juu kisha hutolewa kwa wowote katika watu wa namna nane zilizotajwa na Allah Subhanahu
Wataala katika Aya ya Zaka katika sura ya Attawbah:
ﭽ
ﮡ ﮢ
ﮣ ﮤ ﮥ
ﮦ ﮧ ﮨ
ﮩ ﮪ ﮫ
ﮬ ﮭ ﮮ
ﮯ ﮰﮱ ﯓ
ﯔ ﯕﯖ ﯗ
ﯘ ﯙ ﭼ التوبة: ٦٠
“Sadaka
hupewa (watu hawa): Mafakiri na Masikini na wanaozitumikia na wanaotiwa nguvu
nyoyo zao juu ya Uislamu na katika kuwapa Uungwana watumwa na katika kuwasaidia
wenye deni na katika kutengeneza mambo aliyoamrisha Allah na katika kupewa
wasafiri (walioharibikiwa). Ni faradhi inayotoka kwa Allah, na Allah ni mjuzi
na mwenye hikima.”
Na Zaka ya
Riyali (currency) zitumikazo baina ya watu katika nchi hutolewa (Zaka yake)
ifikapo thamani yake sawa na mithqaali 20 ishirini ya dhahabu au sawa na
mithqaali 200 mia mbili ya fedha (hiyo “Nisaab” ifikapo kwa kila 100 mia
hutolewa 2.5 mbili na nusu).
Namna ya 3
na ya 4 za Zaka hazikabidhiwi kwa watu binafsi bali kwa Maimamu (wanaotawala
kwa Sharia ya Kiislamu).
Na akipata mali , ijapokuwa nyingi, baada ya kupita mwezi
aliouchagua kutoa Zaka kwa mfano imemuingilia mali hii katika Shawwaal na mwezi
wake wa kutoa Zaka ni Ramadhani basi hatazitolea Zaka pesa hizi ikiwa zitamtoka
kabla ya mwezi wa Ramadhani ufuatao.
Na pia
haitolewi Zaka milki yoyote aliyonayo mtu kama nyumba, gari n.k (possessions)
isipokuwa kama inatumiwa kibiashara yaani
ikiwa anunua nyumba au gari kisha auza.
Vile vile
ikiwa dhahabu peke yake haitimii “nisabu” (kiwango cha Zaka) isipokuwa
ikichanganywa na fedha hutimia basi na zichanganywe. Kama
mfano ikiwa Muislamu ana mithqaali 10 kumi za dhahabu (nusu ya nisabu) na ana
mithqaal 100 mia za fedha (nusu ya nisabu) basi azichanganye zitimie nisabu
kisha atoe katika hiyo “Nisaab” robo (¼) ya moja katika kumi (1/10) yaani 2.5%
asilimia.
Na katika
biashara inahisabiwa mali
yote (aina yote ya mali )
iliyotiwa ndani yake inachanganywa yote pamoja na itakapojulikana hisabu yake
na itolewe 2½% asilimia Zaka. Na vile vile katika mapambo yanapimwa kila mwaka
na kutolewa Zaka yake robo ya moja kwa kumi yaani asilimia 2.5%.
Vile vile
inabidi kuchaguliwa mwezi maalumu wa kutoa Zaka ya wanyama kama ngamia,
ng’ombe, mbuzi na kondoo, wachanganywe waume kwa wake na wadogo kwa wakubwa,
mbuzi kwa kondoo kwani wao ni aina moja (jinsi moja) na n’gombe kwa nyati vile
vile wao ni katika jinsi moja.
Anatolewa
Zaka kwa kila mbuzi arubaini mbuzi mmoja na katika kila ngamia watano mbuzi
mmoja wasiyetumiwa kwa kazi (waitwao “sawaim”) hivyo ni kwa mujibu wa hadithi
ya Anas: Alikuwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam achukua sadaka (Zaka) katika
ngamia, ng’ombe na mbuzi wakiwa hawatumiwi kwa kazi wanalishia katika nyasi
zilizoruhusiwa kwa watu wote (mali ya jamii) kwa muda wa mwaka mzima.
Na Zaka ya
ngamia na n’gombe kila watano hutolewa mbuzi mmoja, na wakiwa kumi hutolewa
mbuzi wawili, na kumi na tano hutolewa mbuzi watatu, na ishirini hutolewa mbuzi
wane, na watakapofika ishirini na tano hutolewa ngamia mke bint Makhaadh (na
huyo ni mtoto wa kike wa ngamia umri wake mwaka mmoja). Na anaetaka maelezo kwa
kirefu na atizame katika vitabu vya fiqh. Na majina ya ngamia yatafuatiana na
majina ya ngo’mbe.
Na hakuna
Zaka kwa wenye makwato kama farasi, punda na
nyumbu na wala watumwa kwa mujibu wa hadithi:
(عفى عن
أمتي زكاة الخيل والبغال والحمير )
“Umesamehewa Umma wangu Zaka
ya farasi, nyumbu na punda.”
Na hadithi
nyingine:
( ليس على المسلم صدقة في عبده ولا فرسه )
“Muislamu si juu yake kutoa
Sadaka (Zaka) ya Mtumwa wake na farasi wake.”
Na ama
mazao na nafaka (kama ngano, mtama, maharage)
Zaka ya vitu hivi haifungamani na muda wa mwaka bali yatolewa katika (wakati
wa) mavuno kwa mujibu wa kauli yake Subhanahu Wataala:
ﭽ ﯕ ﯖ
ﯗ ﯘ ﭼ الأنعام:
١٤١
“Na toeni haki yake siku ya
kuvunwa kwake.”
Na ni
wajibu kutoa Zaka ya tende ikifika uzito wa mazao ya mitende Manni 160 mia na
sitini (kila manni 1 ni sawa na kilogram 4 nne). Ikifika uzito huu basi itolewe
Zaka sehemu moja kwa kumi yake. Ikiwa ni tende mbivu (inayotiwa katika madebe)
au tende kavu au nyingineyo isipokuwa ikiliwa mbichi (ratab) hiyo haina Zaka.
Lakini ikiwa hiyo tende mbichi (ratab) itaanikwa juani na kushindiliwa na
kuuzwa kwa pesa basi itatolewa Zaka hiyo thamani yake sehemu moja kwa kumi
(1/10), ikiwa hiyo mitende yatiliwa maji kwa mifeleji au haitiliziwi maji
kabisa. Lakini ikiwa hiyo mitende yatiliziwa maji kwa wanyama (ngamia, n’gombe
n.k) basi hutolewa Zaka nusu ya sehemu moja kwa kumi (½ ya 1/10) kwa sababu
njia yake hiyo ina mashaka (yaani namna ya kutilia maji). Vile vile zabibu hufuatia
njia hiyo ya tende katika kutoa Zaka.
Zaka ya
Nafaka ni Kama Ifuatavyo:
Ngano,
shairi, adesi, mahindi, ufuta, mtama, kunde, maharage, mbaazi, mchele na kila
kiliwacho katika nafaka zinazoliwa.
Amesema
Sheikh wetu Noor Addin Assaalmiy:
Wala hakuna
Zaka kwetu (kwa mujibu ya maarifa yetu) isipokuwa kwa hivyo vilivyotajwa kwa
makubaliano ya Umma.
Na hivyo
vilivyotajwa (nafaka) vyote vyawajibika kutolewa sehemu moja kwa kumi (Zaka)
vikitimia kiwango cha “Nisaab”, nayo ni pishi mia tatu, na nadhani pishi moja
ni sawasawa na kilogram mbili kwa mujibu wa elimu yangu, na waulizwe wanavyuoni
kuhakikisha zaidi juu ya hilo.
Kitu cha
kuzingatia na cha msingi kinachobainisha vinavyolazimika kutolewa Zaka ni kuwa
kila kiliwacho na kuweza kuhifadhiwa kama tende, zabibu, ngano n.k. (hivi
hutolewa Zaka) ama tikiti (batikhi) na viazi, hivi kwa sababu haviwezi
kuhifadhiwa havina Zaka na vinginevyo vilivyofanana na hivi na vile vile viko
vyakula ambavyo havitegemewi katika maisha ya watu yaani watosheka bila ya
kuvipata kama matunda yote kwa sababu yanaliwa kwa kujifurahisha wakati
yapatikanapo na kama zaituni na nazi ambazo zinatumiwa kama viungo katika
chakula (vyaongezwa katika chakula kuongeza ladha).
Tizama
Ukarimu wa Allah Subhanahu Wataala juu yako, amekupa vingi na ameridhika kutoka
kwako kwa kidogo ili kukujaribu juu ya utiifu wako kwake na juu ya yote hayo
manufaa yarudi kwako wewe mwenyewe yeye hahitajii utiifu wako:
ﭽ ﮥ ﮦ
ﮧ ﮨ ﮩ
ﮪﮫ ﮬ ﮭ
ﮮ ﮯ ﭼ فاطر: ١٥
“Enyi watu! Nyinyi ndio
wenye haja kwa Allah, na Allah Mkwasi (na nyinyi hakuhitajieni), asifiwaye (kwa
neema zake juu ya viumbe vyake vyote)”
ﭽ
ﯣ ﯤ
ﯥ ﯦ ﯧ
ﯨ ﯩ ﯪ
ﯫ ﯬ ﯭﯮ
ﯯ ﯰ ﯱ
ﯲ ﯳ ﭼ البقرة: ٢٤٥
“Na nani
atakayemkatia Allah sehemu bora ya mali yake (kwa kuwapa masikini na
kwa kutoa katika mambo mengine ye kheri) ili Allah amzidishie mzidisho mwingi,
na Allah ndiye anayezuia na ndiye anayetoa, na kwake (nyote) mtarejea.”
ﭽ
ﭽ ﭾ
ﭿ ﮀ ﮁ
ﮂ ﮃ ﮄ
ﮅ ﮆ ﮇ
ﮈ ﮉ ﮊ
ﮋ ﮌ ﮍﮎ
ﮏ ﮐ ﮑ
ﮒﮓ ﮔ ﮕ
ﮖ ﭼ البقرة:
٢٦١
“Mfano wa
wale wanaotoa mali zao
katika njia ya Allah Subhanahu Wataala ni kama
mfano wa punje moja iliyotoa mashuke saba; ikiwa katika kila shuke pana punje
mia. Na Allah Subhanahu Wataala humzidishia amtakaye, zaidi kuliko hivi; na
Allah Subhanahu Wataala ni mwenye wasaa mkubwa na mwenye kujua.”
ﭽ
ﭑ ﭒ
ﭓ ﭔ ﭕ
ﭖ ﭗ ﭘ
ﭙ ﭚ ﭛ
ﭜ ﭝ ﭞ
ﭟ ﭠ ﭡ
ﭢ ﭣ ﭤ
ﭥ ﭦ ﭧﭨ
ﭩ ﭪ ﭫ
ﭬ ﭼ البقرة:
٢٦٥
“Na mfano
wa wale wanaotoa mali zao kwa kutafuta radhi ya Allah na kujithibitisha nafsi
zao katika Dini yake, ni kama mfano wa bustani iliyo mahali pa juu, ikaifikia
mvua kubwa na ikaleta mazao yake mara mbili na zaidi (kuliko ada yake); na kama
haifikiwi na mvua kubwa basi mvua ndogo (huitosheleza) na Allah anayaona
mnayoyatenda.”
ﭽ
ﭢ ﭣ
ﭤ ﭥ ﭦﭧ
ﭨ ﭩ ﭪ
ﭫ ﭬ ﭭ
ﭮﭯ ﭰ ﭱ
ﭲ ﭳﭴ ﭵ
ﭶ ﭷ ﭸ ﭼ البقرة: ٢٧١
“Kama
mkitoa sadaka kwa dhahiri ni vizuri; na kama mkitoa kwa siri na kuwapa
mafakiri, basi huo ni ubora zaidi kwenu; na atakuondoleeni (sehemu ya) maovu
yenu (mkifanya hivyo); na Allah anazo habari za (yote) mnayoyatenda.”
ﭽ
ﮄ ﮅ
ﮆ ﮇ
ﮈﮉ ﮊ ﮋ
ﮌ ﮍ ﮎ
ﮏﮐ ﮑ ﮒ
ﮓ ﮔ ﮕ
ﮖ ﮗ ﮘ
ﮙ ﭼ البقرة:
٢٧٢
“Na mali yoyote
mtakayoyatoa ni faida kwa nafsi zenu. Wala msitoe ila kwa kutafuta radhi ya
Allah. Na mali
yoyote mtakayoyatoa mtarudishiwa kamili (thawabu zake) wala hamtadhulumiwa.”
ﭽ ﯜ ﯝ ﯞ
ﯟ ﯠ ﯡ ﯢ ﯣ
ﯤ ﯥ ﯦ
ﯧ ﯨ ﯩ
ﯪ ﯫ ﯬ ﭼ
البقرة: ٢٧٤
“Wale
watowao mali zao usiku na
mchana, kwa siri na dhahiri, wana ujira wao kwa Mola wao; wala haitakuwa khofu
juu yao wala
hawatahuzunika”.
Na kuhusu
Zaka ya Fitri tumekwisha izungumzia katika jezuu ya sita ya kitabu hichi.
Sadaka
Amesema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam:
( تصدقوا
ولو بشق تمرة تكنون به وجوهكم عن النار )
“Toweni sadaka ijapokuwa
nusu (ubale) ya tende muzihifadhi nyuso zenu na Moto (wa Jahannam)”
Na imesimuliwa:
( تصدقوا ولو بظلف محرق )
“Toweni sadaka ijapokuwa ukwato
wa mbuzi uliounguzwa”
Na
imesimuliwa:
( تصدقوا ولو بتمرة ، فإنها تسد
من الجائع وتطفئ الخطيئة كما يطفئ الماء )
“Toweni
sadaka ijapokuwa kwa chembe moja ya tende kwa sababu inasaidia kuondoa njaa na inazima
kosa kama maji yanavyozima (Moto)”
Na
imesimuliwa:
)ما من عبد يتصدق بصدقة من كسب طيب ولا يقبل الله عز وجل
إلا طيبا إلا كان على الله عز وجل يأخذها فيربيها كما يربي أحدكم فصيله وفي رواية
مهره ، حتى تبلغ الثمرة مثل أحد)
“Hakuna mja yeyote anayetoa sadaka kwa mali yake halali
na Allah Subhanahu Wataala hapokei isipokuwa kilichokuwa kizuri (halali)
isipokuwa Allah mwenye nguvu mtukufu huipokea kisha akailea kama anavyomlea
mmoja wenu ngamia wake mchanga au katika hadithi nyengine “farasi wake mchanga”
hata tunda moja likafika ukubwa wake kama Mlima wa Uhud.”
Amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam kumwambia Abi Addardaa:
( إذا طبخت مرقة فأكثر ماءها ثم انظر أهل بيت من جيرانك فأصبهم منه بمغروف )
“Ukipika
mchuzi, uongezee maji mengi kisha uangalie waliomo katika nyumba ya jirani
uwapelekee utacho chota katika huo mchuzi.”
Na akasema
Salallahu Alayhi Wasalam:
( ما
أحسن عبد الصدقة إلا أحسن الله عز وجل له الخلافة على تركته )
“Hakuna mja atoa Sadaka
vizuri isipokuwa Allah Subhanahu Wataala anamtizamia vizuri atakavyoviacha
baada yake (watoto na mali
yake).”
Na akasema
Salallahu Alayhi Wasalam:
( الرجل
في ظل صدقته يوم القيامة حتى يقضى بين الناس )
“Mtu atakuwa
katika kivuli cha sadaka yake Siku ya Kiyama mpaka watakapo hukumiwa watu.”
Na akasema
Salallahu Alayhi Wasalam:
( الصدقة
تسد تسعين باباً من الشر )
“Sadaka
inafunga milango tisini ya shari.”
Amesema
Salallahu Alayhi Wasalam:
( ما
المعطي من سعة بأفضل أجراً من الذي يقبل من حاجة )
“Hapati, mwenye kutoa
(sadaka) katika wasaa (neema), malipo bora zaidi kuliko anayepokea (sadaka)
katika haja (shida).”
Amesema
Salallahu Alayhi Wasalam:
( أفضل الصدقة أن تتصدق وأنت
صحيح شحيح تأمل البقاء وتخشى الفاقة ولا تمهل حتى إذا بلغت الحلقوم قلت لفلان كذا
ولفلان كذا ولفلان كذا وقد كان لفلان )
“Sadaka
iliyo bora zaidi ni ile unayoitoa ungali katika hali ya afya na ubakhili
unategemea kuishi na unaogopa umasikini wala usingojee mpaka roho ifike kooni
(wakati wa kukata roho) useme: cha fulani kiasi hichi, cha fulani kiasi hichi,
cha fulani kiasi hichi, na hali kishakuwa cha fulani.”
قال صلى الله عليه وسلم : تصدقوا
Amesema
Salallahu Alayhi Wasalam: “Toweni Sadaka.”
( فقيل : عندي دينار قال : لنفسك
)
Akaambiwa!
Nina Dinari, akasema: hiyo ni yako mwenyewe.
( قيل : وآخر قال : أنفقه على
زوجتك )
Akaambiwa:
Je nyingine (dinari) akasema: Itowe kwa matumizi ya mke wako.
( قيل: وآخر قال : أنت أبصر به
)
Akaambiwa:
Je nyingine akasema: Wewe unajua zaidi wapi pa kuitumia.
Amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :
( ردوا
مذلة السائل ولو بمثل رأس الطائر من الطعام )
“Ondoa
madhila ya muombaji (kwa kumpa) chakula ijapokuwa kama
mfano wa kichwa cha ndege (uwingi wake).”
Amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :
( لا تقطعوا المسألة حتى تفرغ
ثم ردوا بوقار ولين، أو ببذل يسير أو برد جميل فإنه قد يأتيكم ملك ينظر كيف صنعكم فيما خولكم الله )
“Msikatize
muombaji maneno yake mpaka amalize kisha mjibuni kwa upole na hishima au kwa
msaada kidogo au kwa jibu zuri kwani huenda akawajieni Malaika kutizama
mnafanya nini kwa alichowapa Allah Subhanahu Wataala.”
Akasema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam:
( ولو صدق السائل ، ما أفلح من رده )
"Ikiwa muombaji ni mkweli
hatofuzu yule aliyemrudisha (asimpe kitu)."
Amesema Issa AS :
( من رد
سائلاً خايباً لم تغش الملائكة بيته الذي هو فيه سبعة أيام وقيل يوماً )
“Mwenye kumrudisha muombaji
mikono mitupu basi hawataingia Malaika nyumba yake anayoishi muda wa siku saba,
na imesemwa ni siku moja”.
Na alikuwa
Mtume wetu Salallahu Alayhi Wasalam anaweka maji yake ya kutawadhia usiku kwa
mkono wake na kuyafunika na huwapa masikini.
Na Malaika
huja usiku kuomba kama (mfano wa) binaadamu na
wakipanda huulizwa na Malaika wenzao: Je mmeona vipi? Basi hujibu: fulani
karimu na wao husema: Ewe Mola mghufirie, Ewe Mola mruzuku, Ewe Mola mbarikie
na umkinaishe. Na hujibu (vile vile) fulani bakhili, hatoi (kusaidia muhitaji)
ni mkali wa maneno. Basi humuombea: Ewe Mola mfanyie kitu fulani. (jambo lisilo
zuri).
Amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :
( ليس المسكين من ترده التمرة
أو التمرتان واللقمة واللقمتان إنما المسكين المعفف اقرأوا إن شئتم : لا يسئلون
الناس إلحافاً )
“Sio masikini yule inayomrudisha tembe moja ya
tende au tembe mbili na tonge moja (ya chakula) au tonge mbili lakini masikini
ni yule anayejizuia kuomba.”
Someni
mkitaka (kauli ya Allah) :
ﭽ ﮭ ﮮ
ﮯ ﮰ ﭼ البقرة:
٢٧٣
“Hawaombi watu wakafanya
ung’ang’anizi.”
Na amesema
Salallahu Alayhi Wasalam:
(ما من
مسلم يكسو مسلماً إلا كان في حفظ الله تعالى ما دامت منه رقعة )
“Hakuna Muislamu amvikae
(nguo) Muislamu (mwenziwe) isipokuwa huwa katika hifadhi ya Allah madamu
kimebakia japo kiraka cha hiyo nguo katika mwili wake.”
Na amesema
Salallahu Alayhi Wasalam :
( الصدقه
تقي مصارع السوء وترفع ميتة السوء )
“Sadaka
inaepusha maafa yanayohilikisha na inazuiya kifo kibaya.”
Amesema
Salallahu Alayhi Wasalam :
( نفقة
الرجل على أهله صدقة )
“Matumizi ya mtu kwa ajili
ya ahli yake (mkewe na watoto wake nyumbani) ni sadaka.”
Amesema
Salallahu Alayhi Wasalam:
( من
أطعم مسلماً تمرة أطعمه الله من ثمار الجنة ومن سقاه جرعة سقاه الله من الرحيق
المختوم)
“Mwenye
kumlisha Muislamu tembe moja ya tende Allah atamlisha katika matunda ya Peponi
na mwenye kumnywisha chubuo (la maji) Allah atamnywisha katika (hodhi la)
Rahiiq Al-Makhtuum.”
Na amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :
( إنما
المسكين الذي لا يجد غني يغنيه ولا
يفطن له فيتصدق عليه ولا يقوم فيسأل الناس )
“Kwa kweli
maskini ni yule ambaye hapati cha kumtosha haja yake wala hatambulikani hata
akapewa sadaka wala hapiti kuomba watu.”
Na amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :
( من أنفق زوجين نودي في الجنة
: يا عبد الله : هذا خير ، و يدعى المتصدق من باب الصدقة والمصلي من
باب الصلاة ، والصايم من باب الريان ويدعى الواحد منها جميعا، ورجا رسول الله صلى
الله عليه وسلم أن يدعى أبو بكر رضي الله عنه منها جميعاً )
“Anaetoa
(sadaka) vitu viwili (kama viatu au chakula akatoa kwa mfano unga na samli au
mchele na nyama) huitwa katika Pepo: Ewe mja wa Allah : Hii kheri, na aitwa
anaetoa sadaka katika mlango wa sadaka na mwenye kusali kwenye mlango wa Sala
na mwenye kufunga kwenye mlango wa Rayyan, na anaitwa mwingine kwenye milango
yote hiyo na akatarajia Mtume Salallahu Alayhi Wasalam kuwa Abu Bakr RA ataitwa
kwenye milango yote hiyo.”
Na mwenye
kutoa sadaka kisirisiri atakuwa katika kivuli cha Al-Arshi siku ambayo hapatakuwa
na kivuli isipokuwa kivuli chake.
Na
ilipoteremka kauli ya Allah Subhanahu Wataala :
ﭽ
ﭑ ﭒ
ﭓ ﭔ ﭕ
ﭖ ﭗ ﭘ
ﭙ ﭚ ﭛﭜ
ﭝ ﭞ ﭟ ﭼ البقرة: ٢٢٥
“Allah
hatakushikeni kwa sababu ya kuapa kwenu kwa upuzi – upuzi. Bali
atakushikeni kwa sababu (ya vile viapo) vilivyofanyiwa nguvu na nyoyo zenu. Na
Allah ni mwingi wa kusamehe (na) Mpole sana . (Sura ya Al-Baqara Aya 225)
Na kauli
yake Subhanahu Wataala:
ﭽ ﰑ ﰒ
ﰓ ﰔ ﰕ
ﰖ ﰗ ﰘ
ﰙ ﰚ ﰛ
ﰜ ﭼ
الحديد: ١١
“Ni nani atakaye mkopesha
Mwenyezi Mungu mkopo mwema, ili amrudishie mardufu, na apate malipo matukufu.”
Akasema Abu
Addahdaah:
Nawatoa
mhanga kwa ajili yako baba yangu na mama yangu ewe Mtume wa Allah, atukopa sisi
Allah naye hana haja na sisi?
Akasema
Salallahu Alayhi Wasalam: Ndio, (kwa
sababu) ataka kuwaingiza Peponi.
Akasema :
Je! Nikimkopesha Mola wangu atanipa dhamana ya (kuingia) Pepo?
Akajibu
Salallahu Alayhi Wasalam : Ndio anayetoa sadaka basi hupewa huko Peponi mfano
wa hiyo sadaka aliyoitowa.
Akasema :
Na mke wangu Um Addahdaah yu pamoja na mimi (katika Pepo)
Akajibu
Salallahu Alayhi Wasalam : Ndio
Akasema :
Na binti yangu Addahdaah yu pamoja na mimi (katika Pepo)
Akajibu
Salallahu Alayhi Wasalam : Ndio
Akasema :
Mimi ninazo bustani mbili (mashamba mawili) moja katika hizo iko chini katika
mitende ya Madina na nyingine iko juu, na Wallahi sina nyinginezo nizitoe mkopo
kwa Allah Mtukufu.
Akasema
Salallahu Alayhi Wasalam: Ijaalie moja katika hizo ya Allah Subhanahu Wataala
na nyingine kwa maisha yako na ya watoto wako.
Akasema :
Basi shuhudia ewe Mtume wa Allah kuwa nimeijaalia ya Allah iliyo bora katika
hizo mbili ni ukuta kuna ndani yake mitende mia sita.
Akasema
Salallahu Alayhi Wasalam : Basi Allah atakulipa Pepo kwa hiyo bustani kisha
akasema: Makole mangapi mazito ya tende makole mangapi makubwa (ya tende) na
nyumba (ngapi) zenye manukato mazuri za Abi Addahdaah huko Peponi!.
Amesema
Adhahaak : Anaetoa sadaka dirham moja kwa kutaka radhi ya Allah basi atalipwa
dirham mia saba Duniani na dirham milioni moja Siku ya Kiyama.
Amesema Abu
Huraira: Tulikuwa twahisabu wakati Mtume Salallahu Alayhi Wasalam yuko baina
yetu : matumizi ya mtu kwa nafsi yake na kwa wenzake na kwa kipando chake
(farasi n.k) katika Jihadi hupata mara milioni mbili zaidi ya alivyotoa.
Amesema Urwah
bin Azzubair :
Hakika
Aisha RA alitoa sadaka dirham khamsini elfu na hali nguo yake ina kiraka.
Na kutokana
na Mujaahid kuwa kauli ya Allah:
ﭽ ﭡ ﭢ
ﭣ ﭤ ﭥ
ﭦ ﭧ ﭼ الإنسان:
٨
“Na huwalisha chakula
masikini na mayatima na wafungwa (mateka), na hali ya kuwa wenyewe wanakipenda
(chakula hicho).”
Yaani
amesema Mujaahid nao wanakitamani hicho chakula.
Na kutokana
na Omar RA alikuwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam asema : Ewe Mola ijaalie
fadhila (mali
na utajiri) kwa walio bora wetu ili wairejeshe kwa wenye haja katika sisi.
Na amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :
( بعض
الصدقة تبلغك نصف الطريق والصوم يبلغك باب الملك)
"Baadhi ya sadaka inakufikisha nusu ya njia na Saumu
inakufikisha kwenye mlango wa Mfalme (Allah Subhanahu Wataala )."
Na amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :
( بعض الصدقه تفك لحيي سبعين
شيطاناً وفضل سرها علانيتها بسبعين ضعفاً )
"Baadhi ya sadaka inafungua matama ya mashetani sabini
(ikiwa midomo yao wazi kwa jinsi wanavyoudhika mtu akitoa sadaka) na fadhila
(ubora) ya sadaka ya kificho juu ya sadaka ya uwazi ni mara sabini."
Na kutokana
na Ibn Masoud : Kuwa mtu mmoja ameabudu Allah Subhanahu Wataala miaka sabini
kisha akazini basi amali ikaporomoka (ikaharibika) halafu akampitia masikini
akampa sadaka ya kipande cha mkate basi Allah Subhanahu Wataala akamghufuria
dhambi zake na akamrudishia amali zake za miaka sabini.
Na amesema
Luqman kumwambia mtoto wake: -
Ukifanya kosa
basi toa sadaka.
Na mwingine
akasema:
Sijui
chembe iliyo na uzito wa milima ya Dunia isipokuwa chembe ya sadaka.
Na wamesema
:
Kuficha
sadaka ni katika hazina za Pepo na matumizi yako kwa watoto wako ni sadaka.
Na alikuwa
Ibn Omar anatoa sadaka ya shukrani (kumshukur Allah Subhanahu Wataala kwa neema
zake juu yake).
Kwa mujibu
wa kauli yake Subhanahu Wataala:
ﭽ ﭑ ﭒ
ﭓ ﭔ ﭕ
ﭖ ﭗ ﭼ آل
عمران: ٩٢
“Hamtaweza kuufikilia wema
khasa mpaka mtowe katika vile mnavyovipenda.”
Na baadhi
wametoa sadaka ya kisima kwa ajili ya kupata malipo mazuri, yaliyokuja katika
Aya hii.
Na
watafufuliwa watu hali wana njaa bila ya kiasi basi alielisha (watu na masikini
hasa) kwa ajili ya Allah Subhanahu Wataala basi Allah atamshibisha (siku hiyo)
na anaenywisha kwa ajili ya Allah kadhalika Subhanahu Wataala atamnywisha (siku
hiyo). Angetaka Subhanahu Wataala angewafanya watu wote matajiri lakini
amewafanya matajiri na masikini kwa kuwafanyia mtihani.
Na kutokana
na Ashshaabiy: Yule asiyejiona nafsi yake kuwa ana haja zaidi ya thawabu ya
sadaka yake anayoitoa kuliko haja ya fakiri kwa hiyo sadaka yake basi huyo
ameiharibu sadaka yake na hupigwa nayo usoni mwake.
Amesema
Al-Hussein kumwambia mtu aliempitia pamoja na kijakazi wake : Je unaridhika kwa thamani yake dirhamu moja au
mbili. Akasema : Hapana. Akamwambia : nenda kwani Allah Mtukufu ameridhika kwa
thamani ya “Huur Aliin” (wanawake wa Peponi) kwa pesa moja au tonge moja.
No comments:
Post a Comment
Note: only a member of this blog may post a comment.