Jua
(ewe Muislamu) Allah akuongoze wewe pamoja nasi katika kumtii Subhanahu Wataala
kuwa kitu cha mwanzo kinachomuwajibikia Muislamu kukijua ni kumjua Mola wake
aliyemuumba na kumpa riziki, naye ni “Allah”. Allah ambaye ameumba kila kitu na
hakuna kitu kilicho kama Yeye, wala haonekani
Duniani wala Akhera; kwani angekuwa aonekana basi angefanana na viumbe vyake.
Hana mshirika wala msaidizi, wala waziri wala mshauri. Yuhai siku zote na ni
mwenye uwezo na ujuzi wa kila kitu.
Kasema
Allah katika sura Al-An’aam, aya 59:
ﭽ
ﯬ
ﯭ ﯮ ﯯ
ﯰ ﯱ ﯲﯳ
ﯴ ﯵ ﯶ
ﯷ ﯸﯹ ﯺ
ﯻ ﯼ ﯽ
ﯾ ﯿ ﰀ
ﰁ ﰂ ﰃ
ﰄ ﰅ ﰆ
ﰇ ﰈ ﰉ
ﰊ ﰋ ﰌ
ﭼ
الأنعام: ٥٩
"Na
ziko kwake funguo za siri; hakuna azijuaye ila yeye tu. Na anajua yaliyomo
katika bara na bahari. Na halianguki jani ila anajua; wala (haianguki) punje
katika giza la
ardhi (ila anajua), wala (hakianguki) kilicho kibichi wala kikavu (ila anajua).
(Hapana chochote) ila kimo katika kitabu kinachobainisha (kila kitu)."
Kasema
Allah katika sura Fatir, aya 11:
ﭽ
ﯺ ﯻ
ﯼ ﯽ ﯾ
ﯿ ﰀ ﰁ
ﰂ ﰃﰄ ﰅ
ﰆ ﰇ ﰈ
ﰉ ﰊ ﰋ
ﰌﰍ ﰎ ﰏ
ﰐ ﰑ ﰒ
ﰓ ﰔ ﰕ
ﰖ ﰗ ﰘﰙ
ﰚ ﰛ ﰜ
ﰝ ﰞ ﭼ فاطر: ١١
“Na Allah Amekuumbeni kwa udongo, kisha kwa
tone la manii, kisha akakufanyeni wanaume na wanawake. Na mwanamke ye yote
hapati mimba wala hazai ila kwa kujua Yeye (Mola). Na mwenye kupewa umri hapewi
umri (zaidi) wala hapunguziwi umri ila mambo hayo yamo katika kitabu (cha
Mola). Bila shaka (kuyapitisha) haya ni sahali kwa Allah ”
Hayo
ndiyo mambo ya mwanzo ambayo ni lazima Muislamu ayajue. Kisha inampasa amjue
Mtume wake Muhammad Salallahu Alayhi Wasalam kuwa ndiye aliyeletwa na Allah Subhanahu
Wataala ili awaongoze watu katika njia ya Haki na yeye ni mkweli kwa ayasemayo,
na ni wajibu wa kila Muislamu kufuata ayasemayo Salallahu Alayhi Wasalam na
ayatendayo. Na kuwa yeye Salallahu Alayhi Wasalam amezaliwa Makka na akapewa
Utume na Ujumbe huko huko Makka, kisha akahamia Madina na kuanzia huko
ikatangaa Dini ya Kiislamu. Alifia huko Madina na kaburi lake liko
huko mpaka Siku ya Kiyama.
Baada ya haya ni juu yake kuyajua yafuatayo:-
- Dini yake na mambo yaliyo lazima kuyaamini.
- Mambo yaliyo lazima kuyafanya.
- Mambo yaliyo lazima kujitenga nayo.
La kwanza katika matatu hayo:
Itikadi - Ni
lazima aamini kuwa aliyokuja nayo Mtume Salallahu Alayhi Wasalam ni haki, na
kuwa mauti ni haki, na kufufuliwa Siku ya Kiyama ni haki, na kuhisabiwa ni
haki, na kuwa Siraati ni haki (njia ya Allah anaewatakiya waja wake waifuate),
na kuwa Mizani ni haki (sio mizani tunayo ijua iliyo na mikono miwili na kuwa
mema yatiwa katika mkono mmoja na mabaya yatiwa katika mkono mwingine bali ni
uadilifu na uwezo wa Allah Subhanahu Wataala wa kujua vitendo vya waja wake
(vibaya na vizuri), na kuwa Pepo ni haki na Moto ni haki na kuwa aingiaye
Peponi hatoki tena milele na humo Peponi kuna kila inachotamani nafsi na kila
linachoona raha jicho kukitizama. Na aingiaye Motoni hatoki tena milele
ataadhibiwa na kufungwa pingu humo, atan’gatwa na wadudu wake watambaao
(wanaotisha), ataunguzwa na moto wake na atazamishwa katika Zamharir yake (wadi
katika Jahannamu inayokata viwiliwili kwa ubaridi wake kama ukatavyo moto
viwiliwili kwa joto lake) atatamani mauti yamjie lakini hayatomjia na atatamani
kurudishwa Duniani ili apate kufanya mambo mema hatokubaliwa, atakuwa
akihamishwa kutoka kwenye joto la moto kwenda kwenye baridi ya Zamharir. Allah Subhanahu
Wataala ametayarisha adhabu kali hiyo kwa waliomuasi na hawakukubali kumtii
wala kumtii Mtume wake. Allah atuepushe hayo sisi na nyinyi.
Kasema
Allah Subhanahu Wataala katika sura Annisa’a, aya 13 na 14:
ﭽ
ﯚ ﯛ
ﯜ ﯝ ﯞ
ﯟ ﯠ ﯡ
ﯢ ﯣ ﯤ
ﯥﯦ ﯧ ﯨ
ﯩ ﯪ ﯫ
ﯬ ﯭ ﯮ
ﯯ ﯰ ﯱ
ﯲ ﯳ ﯴ
ﯵ ﯶ ﯷ
ﯸ ﭼ النساء: ١٣
– ١٤
[Na anayemtii Mola na Mtume wake, yeye (Mola) atamuingiza katika
Bustani zipitazo mito
mbele yake; wakae humo milele. Na
huko ndiko kufaulu kukubwa. Na anayemuasi Mola na Mtume wake na kuikiuka mipaka
yake (Mola) atamtia Motoni, humo atakaa milele na atapata adhabu
zifedheheshazo.]
Vile
vile ni wajibu wake aamini kuwa anaemtii Allah Subhanahu Wataala na Mtume wake
Salallahu Alayhi Wasalam na akafanya kwa mujibu wa amri zao na akafa katika
hali hiyo basi Allah atamtia Peponi na anawajibika kupendwa (na Waislamu) na mapenzi hayo huitwa “Al-Walaya” (الولاية) na anaemuasi Mola na Mtume wake na
akafanya kinyume na amri zao na akafa katika hali hiyo (ya uasi) Allah atamtia
Motoni na anawajibika kuchukiwa (na Waislamu) na huko kunaitwa Al-Baraa (البراءة).
Pia
aamini kuwa anaekufa katika maasi hataombewa na Mtume Salallahu Alayhi Wasalam
(kwa Allah Subhanahu Wataala) yaani الشفاعة .
Kasema Allah katika sura Ghafir, aya 18:
ﭽ ﭪ ﭫ
ﭬ ﭭ ﭮ
ﭯ ﭰ ﭼ غافر:
١٨
[Madhalimu
hawatakuwa na rafiki wala muombezi atakayesikilizwa.]
Kasema Allah katika sura Al-Anbiya, 28:
ﭽ ﭹ ﭺ
ﭻ ﭼ ﭽ ﭼ
الأنبياء: ٢٨
[Na (Hao Malaika)
hawamuombei (ye yote) ila yule aliyemridhia (Allah).]
Mwenye kuasi hawezi kuwa mwenye kuridhiwa na Mola
mpaka aombe maghufira na atubu.
Na Muislamu lazima aamini kuwa sifa za Mola ni Dhati yake
Subhanahu Wataala (Yeye Mwenyewe) na wala hapana tafauti baina ya Dhati yake na
sifa zake, na maana yake ni kuwa Allah ni mwenye elimu yaani katika sifa zake Subhanahu
Wataala ni elimu, na elimu yake si elimu ya kupatikana kama ipatikanavyo elimu
ya viumbe; kwani kiumbe huzaliwa mjinga kisha akasoma na kupata elimu wakati
sivyo hivyo hali ya Mola Subhanahu Wataala, maana elimu yake sio ya ya
kupatikana bali ni dhati yake. Na upime katika msingi huo sifa zake zote.
Vitendo - Inamlazimikia Muislamu afanye yale aliyoamrishwa na
Allah kuyafanya kama kusali, kutoa Zaka,
kufunga Ramadhani, kuhiji, kusitiri utupu wake, kuwa na tabia njema, kuwatii na
kuwafanyia wema wazee wake wawili, kuwasiliana na jamaa zake (kwa kuwatembelea
au kuwaandikia au kuwapigia simu au kuwapelekea zawadi au salamu), kuwaliwaza
majirani (katika misiba) na kutowaudhi na kustahamili kero lao, kuwa na
maingiliano mazuri na watu, kutekeleza haki za Mola na za watu, kuwapenda (na
kuwahurumia) wenye kuamini, kuwachukia na kuwaepuka makafiri, kuwatembelea
wagonjwa, kushindikiza (au kufuata) majeneza ya Waislamu, kuwapenda mafakiri na
kuwaliwaza, kutoa nasaha kwa ajili ya Allah Subhanahu Wataala, Mtume wake
Salallahu Alayhi Wasalam na Waislamu kwa ujumla, kupatanisha waliogombana,
kwenda kutekeleza haja za Waislamu, kutubia, kutekeleza ahadi, kusubiri katika
shida, kuyategemesha kwa Allah Subhanahu Wataala mambo yake yote na kutawakali
kwake, kujisafisha na najisi za mwili, nguo na mwahala pa kusalia, kuoga janaba
na kuridhika na aliyogawa Mola katika mali na vyeo.
Kasema Allah katika sura Fussilat aya 46:
ﭽ ﰎ ﰏ
ﰐ ﰑﰒ ﰓ
ﰔ ﰕﰖ ﰗ
ﰘ ﰙ ﰚ ﭼ
فصلت: ٤٦
[Anayefanya mema
anajifanyia mwenyewe nafsi yake, na mwenye kutenda ubaya ni juu ya nafsi yake
(vile vile), na Mola wako si dhalimu (hata kidogo) kwa watumwa wake.]
Kasema
Allah katika sura ya Israa aya 7:
ﭽ ﮭ ﮮ
ﮯ ﮰﮱ ﯓ
ﯔ ﯕ ﭼ الإسراء:
٧
[Basi mkifanya
wema, mnajifanyia wenyewe nafsi zenu; na mkifanya ubaya, mnajifanyia nafsi zenu
wenyewe.]
Kujitenga: - Inamlazimu
Muislamu ajitenge na mambo aliyoyakataza Allah
Subhanahu Wataala na Mtume wake Salallahu Alayhi Wasalam nayo ni kama
yafuatayo:- Kuzini, kula Riba na
maingiliano yoyote yanayohusu Riba (haifai kuchukua mkopo Benki wa Riba hata
ikiwa imebadilishwa jina ikaitwa “interest” yaani faida), kuangalia utupu na
kuuonyesha, kukojoa wima, kufanya liwati , kula nyama ya maiti, kuua nafsi
(iliyokatazwa kuuliwa), kula nyama ya nguruwe, kuvuta sigara, kunywa pombe,
kula mali ya watu bila ya ridha yao, kunyoa ndevu (hata kuzikata), kula nyama
isiyochinjwa kihalali na kwa ajili ya Allah (kama ya muhanga au uganga au
shetani), kuwatupa wazee wawili (kuwaasi au kutowatazama), kusema uwongo,
kusengenya na kufitinisha watu
(kugombanisha), kusema maneno yaliyo batili kama mazungumzo yasiyopendeza,
matusi na kutaja aibu za watu na kutaja tupu zao. Asijiweke Muislamu katika
hali ya kutiliwa shaka na kutuhumiwa kwa mfano kwenda sinema, kusimama na
mwanamke ajnabi (asiye Mahram kwake) au kumtizama, kucheka nae au kumkonyeza
kwa jicho au nyusi, vile vile kukonyezana na mtu kwa kumdharau Muislamu
mwenzao, kuwafanyia watu masikhara na asimsumbulie Allah Subhanahu Wataala kwa
ajili ya vitendo vyake vizuri (Allah Subhanahu Wataala hana haja ya ibada yake,
bali faida ya vitendo vyake inarudi kwake mwenyewe) kwani vitendo vya mja hata
vikafika vinavyofika kwa uwingi na uzuri havifikii neema moja katika neema
nyingi zisizohisabika alizopewa na Allah Subhanahu Wataala. Mja hakuvifanya
hivyo vitendo vizuri isipokuwa kwa Tawfiiq ya Allah Subhanahu Wataala basi tena
uko wapi uhodari wa mja?
Kasema
Allah katika sura Fatir:
ﭽ
ﮥ ﮦ
ﮧ ﮨ ﮩ
ﮪﮫ ﮬ ﮭ
ﮮ ﮯ ﮰ
ﮱ ﯓ ﯔ
ﯕ ﯖ ﯗ
ﯘ ﯙ ﯚ
ﯛ ﯜ ﯝ
ﯞ ﭼ فاطر:
١٥ – ١٧
[Enyi watu! Nyinyi ndio wenye haja kwa
Allah na Allah ndiye Mwenye kujitosheleza na Mwenye kusifiwa (kwa neema zake).
Akitaka atakuondoeni na ataleta viumbe wapya. Na hilo kwa Allah kamwe si gumu.]
Tena ni juu ya Muislamu ajifunze
kujitia tohara – kujitoharisha mkojo na choo kikubwa, ambavyo vinaitwa
“Al-hadathi Al-Asghari” (hadathi ndogo). Na kujitoharisha janaba, ambalo
linaitwa “Al-hadathi Al-Akbari” (hadathi kubwa). Na ajifunze kufanya mambo
haya.
Hadathi Ndogo:
Akitaka
kukojoa ni lazima asitiri utupu wake asionekane wala asifunue nguo yake mpaka
achutame, wala asikojoe pahala pagumu (kama
juu ya saruji au mawe) kwa sababu chembe za mkojo zitamrukia nguoni mwake au
mwilini. Akimaliza kukojoa asifanye haraka ya kuinuka kabla ya kufanya
“istibraa”, nako ni kuikamua dhakari yake kutoka shinani (upande wa duburi)
kuelekea upande wa kutokea mkojo kisha aikun`gute, afanye hivyo mara tatu mpaka
ahakikishapo kuwa hakukubakia kitu ajipanguse pale panapotokea mkojo kwa kitu
kigumu kinachofyonza kama jiwe au karatasi ya “tissue” (badala ya jiwe unaweza
kutumia hizi karatasi “tissue paper”), kisha ajioshe kwa maji pamoja na sehemu
zilizo kando yake. Na kadhalika choo kikubwa ajisafishe hivyo hivyo kwanza kwa
karatasi halafu kwa maji. Na haitoshi kabisa kujisafisha kwa karatasi tu bila
kufuatilia na maji, kwani akifanya hivyo Sala yake atakayoisali itakuwa batili.
Na kikomo cha kujiosha ni kutumaini kuwa hakuna najisi iliyobakia. Na hii
“Istibraa”, iliyokwisha zungumziwa, ni “Sunna” hapana budi kuifanya; ama
kujiosha kwa maji ni faradhi anayeiwacha amekufuru (“Kufr neema”).
Hadathi Kubwa:
Nayo
ni janaba. Janaba hupatikana kwa kutoka
manii katika utupu wa mtu (mwanamme au mwanamke) au kukutana ncha mbili za
utupu hata ikiwa chini ya kizuizi kama nguo. Pia hiyo “Hadathi Kubwa”ni hedhi au nifasi” (ujusi).
Kuoga Janaba:
Inampasa
aogae janaba kwanza akojoe ili yatoke manii yaliyobakia katika utupu wake;
kisha aisafishe hiyo najisi kwenye utupu wake na pembezoni mwake; kisha ajioshe
kutoka magotini mpaka kitovuni; kisha atawadhe udhu kama
wa Sala. Kisha aoshe kichwa chake akitia vidole vyake nyweleni, kisha aoshe
kifuani na tumboni na ahakikishe kuwa maji yafika katika zile sehemu zilizokuwa
tabu maji kufika (kama baina ya vidole, kwapa
na sehemu nyingine zilizo finyu), kisha aoge mgongo na kwapa na pande zote
mbili za mwili, kisha aoshe kutoka magotini mpaka kwenye ncha za vidole na
akishafanya hivyo anaweza akasali (bila ya kutawadha) ikiwa hakugusa utupu
wake. Vile vile “Wadii” na “Madhii” vinatoka katika utupu wa mwanamme lakini
haimuwajibikii mtu kuoga kama yakitoka manii, bali yamtosha tu kuosha zile
sehemu zilizofikiwa na najisi hizi kama vile
anavyojiosha mkojo. Kama tulivyoeleza kuwa
manii ni najisi ioshwe katika kiwiliwili na nguo, na inawapasa wote wawili
kuoga janaba mwanamme na mwanamke. Na kujihifadhi na najisi ni ibada kwa sababu
ibada (kama kusali na Saumu) haitimii ila kwa
kujitoharisha na najisi.
Wakati
wa Sala ukifika anatakiwa Muislamu kwanza atawadhe. Na atawadhe kama ifuatavyo:
Aoshe
viganja vyake huku akisema “Bismillah” na atie niya katika moyo wake kuwa anatawadha
kwa kusali faradhi ya Adhuhuri au Al-Asiri au Al-Maghribi au Al-Isha au
Al-Fajiri na aendelee kuihudhurisha niya hiyo moyoni mwake mpaka amalize
kutawadha, kisha asukutue mara tatu akiyafikisha maji mpaka kooni isipokuwa
akiwa amefunga asifikishe maji kooni, kisha ayatie maji puani huku avuta pumzi
ndani ili maji yaingie vizuri, mara tatu, kisha aoshe uso mara tatu kuanzia
mwanzo wa nywele kipajini mpaka mwisho wa kidevu na mapana kutoka sikio mpaka
sikio, na ajioshe vizuri baina ya masikio na mashavu, kisha aoshe mkono wa
kulia mara tatu kutoka kwenye kibwiko mpaka vidole na apenyeze maji baina ya
vidole, afanye hivyo hivyo kwa mkono wa kushoto, kisha apanguse kichwani aanze
mbele ya kichwa kwenda nyuma, apanguse mara moja, halafu apanguse masikio mara
moja nje na ndani na huku atie vidole vyake ndani ya matundu ya masikio, kisha
aoshe mguu wake wa kulia mara tatu kuanzia juu ya kisigino mpaka ncha za vidole
na apenyeze maji baina ya vidole na ahakikishe kuwa kisigino kimerowa maji na
wayo vile vile na afikishe maji kwenye mvungu wa mguu wake ausugue vizuri,
halafu aoshe mguu wake wa kushoto hivyo hivyo kama wa kulia. Mpaka hapa udhu
wake umetimia basi amuombe Allah Subhanahu Wataala ampe tawfiiq kwa kufanya
faridha yake vizuri na amuombe Allah Subhanahu Wataala ampokelee amali yake.
Kasema
Allah katika sura ya Al-Ankabut aya 69:
ﭽ ﮠ ﮡ
ﮢ ﮣ ﮤﮥ
ﮦ ﮧ ﮨ
ﮩ ﭼ العنكبوت:
٦٩
[Na wale
wanaojitahidi kwa ajili yetu, kwa yakini tutawaongoza katika njia zetu. Na bila
shaka Allah yu pamoja na wafanyao mema.]
Akimaliza
kujitia udhu atakwenda kusali na ataelekea Qibla na kutia niya moyoni kuwa
anasali faradhi fulani, kwa mfano atasema:
( أتقرب إلى الله بأداء فريضة الظهر (أًو العصر
أو المغرب أو العشاء أو الفجر )
Halafu
atakimu kama ifuatavyo:
( الله أكبر
الله أكبر الله أكبر الله أكبر، أشهد أن لا إله إلا الله أشهد أن لا إله إلا الله،
أشهد أن محمداً رسول الله أشهد أن محمداً رسول الله، حي على الصلاة حي على الصلاة،
حي على الفلاح حي على الفلاح، قد قامت الصلاة قد قامت الصلاة، الله أكبر الله
أكبر، لا إله إلا الله )
Adhana huwa
kama hivi isipokuwa قد قامت الصلاة haisemwi. Wala asiseme katika adhana ya Sala ya
Al-Fajir: الصلاة خير من النوم . Na ni sharti kuisema “Ikama” upesi upesi sio kuisema
polepole na kuivuta. Kisha atasoma Tawjih:
( سبحانك
اللهم وبحمدك تبارك اسمك وتعالى جدك ولا إله غيرك إني وجهت وجهي للذي فطر السموات
والأرض حنيفا وما أنا من المشركين )
Kisha atapiga Takbirat Al-Ihram, bila ya kusita baina ya Tawjih na hiyo
Takbirat Al-Ihram, katika hali ya unyenyekevu na kuhudhurisha niya moyoni kuwa
anahirimia Sala ya faradhi fulani (mambo yaliyokuwa halali kabla yanakuwa
haramu baada ya takbirat Al-Ihram kama
kuzungumza, kugeukageuka, kutizama watu, kula, kunywa na kadhalika). Wanavyuoni wanasema ikiwa hakuihudhurisha niya kwenye
Takbirat Al-Ihram basi Sala yake inaharibika. Kisha atasoma: أعوذ بالله من الشيطان
الرجيم kwa siri, halafu atasoma sura ya Al-Fatiha
peke yake katika Sala ya Adhuhuri na Al-Asiri na katika rakaa ya tatu ya
Al-Maghribi na rakaa ya tatu na ya nne ya Al-Ishaa. Na atasoma Al-Fatiha na
sura au aya tatu kwa uchache katika rakaa mbili za mwanzo za Al-Maghrib na Al-Isha
na Al-fajir. Kisha atarukuu na atasema katika rukuu: سبحان ربي العظيم mara tatu kisha
atasimama na atasema katika kunyanyuka kwake: سمع الله لمن حمد na akishakuwa
amesimama wima atasema: ربنا
ولك الحمد . Halafu atasujudu na atasema humo: سبحان ربي الأعلى mara tatu kisha atakaa
mpaka atulie katika kikao chake hicho, kisha atasujudu tena afanye kama mwanzo halafu asimame na kusoma kisha arukuu kisha
asimame halafu asujudu halafu akae na kusujudu tena kisha akae kikao cha
Tahiyatu cha mwanzo aseme:
التحيات المباركات لله والصلوات الطيبات،
السلام عليك أيها النبي ورحمة الله وبركاته، السلام علينا وعلى عباد الله
الصالحين، أشهد أن لا إله إلا الله وحده لا شريك له وأشهد أن محمداً عبده ورسوله
Kisha
asimame, asome, arukuu, asujudu kama mwanzo.
Kisha asimame tena, arukuu, asimame na asujudu kama
hapo mwanzo. Kisha akae kikao cha pili cha Tahiyatu na asome kama
alivyosoma mwanzo na akifika عبده ورسوله aongeze:
( صلى الله
عليه وسلم أرسله بالهدى ودين الحق ليظهره على الدين كله ولو كره المشركون ربنا
آتنا في الدنيا حسنة وفي الآخرة حسنة وقنا عذاب النار )
Na akitaka kuongeza kusoma dua ni vizuri akiwa peke
yake lakini akiwa Imamu asiwacheleweshe jamaa. Akiomba dua bora ziwe dua za
(kuomba) Akhera, katika dua ilizotuelekeza Qurani na Sunna kuzisoma. Na
atahadhari asikae juu ya visigino vyake (katika Tahiyatu) akasimamisha nyayo zake
au kujibweteka chini au kukaa kitako akasimamisha magoti yake kwani mikao hii
yote inabatilisha sala. Kisha atoe salamu ageuke kulia na kusema السلام عليكم kisha kushoto na
kusema:
ورحمة الله .
Wakati
Imamu anapotoa Salamu hutia niya ya kuwatolea wale wanaosali nyuma yake. Ama
akiwa mtu anasali peke yake hutia niya ya kuwatolea Malaika. Na asiseme kitu
baina ya Sijda mbili (kwenye kikao). Baada ya kutoka kwenye Sala aombe dua
yoyote ile atakayojaaliwa na Allah. Na inapendelewa asome aya ya “Al-Kursiy”
baada ya kutoa Salamu. Na aihifadhi Sala yake baina ya Takbirat Al-Ihram na
kutoa Salamu, asigeukegeuke wala kucheka wala asicheze (yaani asisogeze viungo
vyake ovyo ovyo kama kujikuna au kushika ndevu n.k.) asitazame juu, asijikohoze
isipokuwa kwa kutengeneza kisomo chake, wala asinyanyue mikono yake mpaka
masikioni (wakati wa kupiga Takbiratu Al-Ihram) wala asifunge mikono (kwa
kuweka mkono wake wa kulia juu ya mkono wa kushoto hata kinyume chake) wakati
wa kusimama, wala asinyooshe kidole chake au kukizungusha wakati wa Tahiyatu,
wala asiseme “Aamin” baada ya kusoma suratul Al-Fatiha kwani haya yanabatilisha
Sala. Wala asimfanyie mtu ishara kwa mkono au kwa jicho wala asifikirie jambo
lolote katika mambo ya Dunia kwa hiari yake (yaani kwa kutaka mwenyewe. Ama
akiwa amepotezwa akili na Iblis basi na ajaribu kwa uwezo wake kushindana naye
arudi kwenye Sala asikubali kutolewa kwenye Sala moja kwa moja) kwa sababu yeye
yuko katika kisimamo kitukufu mbele ya Mfalme Mkubwa sana ambaye hawezekani na
yeyote katika Mbingu wala Ardhi (na wala hakiwi chochote isipokuwa anachotaka
yeye Subhanahu Wataala) kwa hiyo anawajibika kusimama mbele yake kwa adabu.
Sala ni nguzo ya Dini na mwenye kutengeza Sala yake basi ibada zake nyingine
vile vile zitatengenea. Kasema Allah katika sura ya Israa aya 22 -39
ﭽ
ﮌ ﮍ
ﮎ ﮏ ﮐ
ﮑ ﮒ ﮓ
ﮔ ﮕ ﮖ
ﮗ ﮘ ﮙ
ﮚ ﮛ ﮜ
ﮝ ﮞﮟ ﮠ
ﮡ ﮢ ﮣ
ﮤ ﮥ ﮦ
ﮧ ﮨ ﮩ
ﮪ ﮫ ﮬ
ﮭ ﮮ ﮯ
ﮰ ﮱ ﯓ
ﯔ ﯕ ﯖ
ﯗ ﯘ ﯙ
ﯚ ﯛ ﯜ
ﯝ ﯞ ﯟ
ﯠ ﯡ ﯢ
ﯣ ﯤﯥ ﯦ
ﯧ ﯨ ﯩ
ﯪ ﯫ ﯬ
ﯭ ﯮ ﯯ
ﯰ ﯱ ﯲ
ﯳ ﯴ ﯵ
ﯶ ﯷ ﯸ
ﯹ ﯺ ﯻ
ﯼ ﯽﯾ ﯿ
ﰀ ﰁ ﰂ
ﰃ ﭑ
ﭒ ﭓ ﭔ
ﭕ ﭖ ﭗ
ﭘ ﭙ ﭚ
ﭛ ﭜ ﭝ
ﭞ ﭟ ﭠ
ﭡ ﭢ ﭣ
ﭤ ﭥ ﭦ
ﭧ ﭨ ﭩ
ﭪ ﭫ ﭬ
ﭭ ﭮ ﭯ
ﭰ ﭱ ﭲﭳ
ﭴ ﭵ ﭶ
ﭷ ﭸ ﭹ
ﭺ ﭻ ﭼ
ﭽ ﭾﭿ ﮀ
ﮁ ﮂﮃ ﮄ
ﮅ ﮆ ﮇ
ﮈ ﮉ ﮊ
ﮋ ﮌﮍ ﮎ
ﮏ ﮐ ﮑ
ﮒ ﮓ ﮔ
ﮕ ﮖ ﮗ
ﮘ ﮙ ﮚ
ﮛﮜ ﮝ ﮞ
ﮟ ﮠ ﮡ
ﮢ ﮣ ﮤ
ﮥ ﮦ ﮧﮨ
ﮩ ﮪ ﮫ
ﮬ ﮭ ﮮ
ﮯ ﮰ ﮱ
ﯓ ﯔ ﯕ
ﯖ ﯗ ﯘﯙ
ﯚ ﯛﯜ ﯝ
ﯞ ﯟ ﯠ ﯡ
ﯢ ﯣ ﯤ
ﯥ ﯦ ﯧ
ﯨﯩ ﯪ ﯫ
ﯬ ﯭ ﯮ
ﯯ ﯰ ﯱ
ﯲ ﯳ ﯴ
ﯵﯶ ﯷ ﯸ
ﯹ ﯺ ﯻ
ﯼ ﯽ ﯾ
ﯿ ﰀ ﰁ
ﰂ ﰃ ﰄ
ﰅﰆ ﰇ ﰈ
ﰉ ﰊ ﰋ
ﰌ ﰍ ﰎ
ﰏ ﰐ ﰑ
ﰒ ﰓ ﰔ
ﰕ ﰖ ﰗ ﭑ ﭒ
ﭓ ﭔ ﭕ
ﭖ ﭗﭘ ﭙ
ﭚ ﭛ ﭜ
ﭝ ﭞ ﭟ
ﭠ ﭡ ﭢ
ﭣ ﭤ ﭼ الإسراء: ٢٢ - ٣٩
"Usifanye mungu mwingine pamoja na Allah usije ukawa mwenye
kulaumiwa (na) mwenye kukosa wa kukunusuru (22) Na Mola wako amehukumu kuwa
msimuabudu yeyote ila yeye tu. Na
(ameagiza) kuwafanyia wema (mkubwa) wazazi. Kama
mmoja wao akifikia uzee, (naye yuko) pamoja nawe, au wote wawili basi
usiwaambie hata Ah! Wala usiwakemee na useme nao kwa msemo wa heshima (kabisa)
(23) Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa (njia ya kuwaonea) huruma (kwa
kuwaona wamekuwa wazee) na useme: Mola wangu! Warehemu (wazee wangu) kama
walivyonilea katika utoto (24) Mola wenu anajua sana yaliyo nyoyoni mwenu. Kama mkiwa wema
(kwa wazee wenu daima; lakini mara moja mbili hivi mkapotea, basi Allah Subhanahu
Wataala atakusameheni) kwani yeye ni mwenye kuwaghufiria wenye kurejea (kwake)
(25) Na umpe jamaa (yako) haki yake, na maskini na msafiri aliyeharibikiwa,
wala usitawanye (mali yako) kwa ubadhirifu (26) Hakika watumiao kwa ubadhirifu
ni ndugu wa mashetani (wanamfuata mashetani). Na shetani ni mwenye kumkufuru
Mola wake (27) Na kama unajipurukusha nao (sasa hivi kwa kuwa huna kitu) lakini
unatafuta rehema ya Mola wako (riziki) unayoitumai, basi sema nao maneno laini
(ya kuwapa waadi ya kuwa ukipata utawapa) (28) Wala usifanye mkono wako kama
uliofungwa shingoni mwako, wala usiukunjue wote, utakuwa mwenye kulaumiwa
(ukifanya hivyo) na kufilisika (ukiukunjua ovyo ovyo) (29) Hakika Mola wako
humkunjulia riziki amtakaye na humdhikishia (atakaye). Hakika Yeye kwa waja
wake ni Mwenye kuwajua na kuwaona; (anajua yupi anayestahiki utajiri na yupi
anayestahiki ufakiri) (30) Wala msiwaue watoto wenu kwa kuogopa umaskini. Sisi
ndio tunaowaruzuku wao na nyinyi (pia). Kwa yakini kuwaua ni khatia kubwa (31)
Wala msikaribie zina. Hakika hiyo ni uchafu (mkubwa) na ni njia mbaya (kabisa)
(32) Wala msiue nafsi ambayo Allah amekataza (kuiua) isipokuwa kwa haki
(Akahukumu Hakimu kuwa mtu huyo anastahiki kuuawa na akatoa amri ya kuuawa). Na
mwenye kuuawa kwa kudhulumiwa, basi tumempa nguvu mrithi wake (juu ya muuaji
huyo) akitaka ataomba kwa Hakimu kuwa amuue kama
alivyomuua mtu wake na akitaka atamsamehe na akitaka atamtoza kitu). Basi
(huyo mrithi asifanye fujo katika kuua
kwa ajili ya mtu wake aliyeuliwa). Hakika yeye atasaidiwa (na sharia maadam
anayo haki (33) Wala msiyakaribie (msiyaguse) mali ya yatima, isipokuwa kwa njia
iliyo bora (kwa hao mayatima) mpaka afike baleghe yake (huyo yatima akabidhiwe
mwenyewe). Na timizeni ahadi. Kwa hakika ahadi itaulizwa (Siku ya Kiyama) (34)
Na timizeni kipimo mpimapo, na pimeni kwa mizani zilizo sawa. Hayo ni wema
kwenu na bora mwishoni (kwake) (35) Wala usifuate (ukipita ukiyasema au
kuyafanya) usiyo na elimu (ujuzi) nayo. Hakika masikio na macho na moyo; hivyo
vyote vitaulizwa (36) Wala usitembee (usende) katika ardhi kwa maringo. Hakika
wewe huwezi kuipasua ardhi wala huwezi kufikia urefu wa mlima. (Basi unajivuna
nini) (37) Haya yote ubaya wake ni wenye kuchukiza mbele ya Mola wako. (38)
Haya ni katika yale aliyekufunulia Mola wako katika hekima (zake). Wala
usimueke pamoja na Allah, mungu mwingine, usije kutupwa katika Jahannam hali ya
kuwa mwenye kulaumiwa (na) mwenye kufukuzwa (huku na huku) (39)."
Hii
ndiyo madhehebu ya Mtume Salallahu Alayhi Wasalam ambayo ameteremka nayo Jibril
A.S kutoka kwenye Al-Lawhi Al-Mahfoodh kutoka kwa Allah Mtukufu, Mwenye nguvu
na sifa zote nzuri.
Walioko
kwenye madhehebu hii wao ndio wenye haki pasi na shaka yoyote, na madhehebu
nyingine zimetokana na madhehebu hii (kwani hii ndio asili na nyingine ni
matawi yake). Jina hili (Ibaadhi) wamepewa kwa kunasibishwa na Abdullah bin
Abaadh ambaye alikuwa mwenye heshima na mkali kwa ajili ya kufuata Dini. Na
huku kunasibishwa madhehebu na yeye sio kwa kuwa yeye ndiye Imamu wa madhehebu
hii kama walivyo Maimamu wa madhehebu nyingine, hapana, kwani Imamu wa
Maibaadhi ni Mtume Salallahu Alayhi Wasalam na Masahaba wake watukufu Radhi za
Allah ziwe juu yao. Wao ndio waliochukua sheria ya Dini kutoka kwa Mtume
Salallahu Alayhi Wasalam kisha wakampa Muibaadhi muaminifu mwenye kutegemewa
na Mwanachuoni mkubwa alietoka Oman
naye ni Jabir bin Zayd ambaye hakukosolewa katika uaminifu wake na ukweli wake
sio na wafuasi wake tu bali hata na wapinzani wake.
Lakini
sababu ya kunasibishwa Maibadhi na Abdullah bin Abaadh ni kuwa alikuwa anaihami
na kuitetea Dini na alikuwa muongofu katika tabia yake na kuihami Dini katika
wakati ulipogawanyika Umma ukawa madhehebu mbali mbali wakapata Waislamu
mtihani mkubwa kwa mfarakano huu, jambo ambalo Allah Subhanahu Wataala
hakuliamrisha lifanywe. Walikuwa Waislamu kama mwili mmoja na iwapo kiungo
kimoja kitashtaki (katika mwili huo) basi viungo vyote vilivyobakia vitahisi
maumivu hayo na homa hiyo (iliyosibu hicho kiungo kimoja). Kama alivyosema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam na kutabiri kwa tukio hilo la kufarikiana Umma huu. Na
kilichoandikwa na Allah hakina budi ila kutokea.
Amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam:-
افترقت اليهود على إحدى وسبعين فرقة كلها هالكة إلا واحدة وافترقت النصارى على اثنين وسبعين
فرقة كلها هالكة إلا واحدة وستفترق أمتي على ثلاث وسبعين فرقة كلها هالكة إلا
واحدة قيل فمن الواحدة يا رسول الله قال : من كانت على ما أنا عليه أو كما قال
رسول الله
“Wamefarikiana
mayahudi katika makundi sabini na moja na yote yameangamia isipokuwa kikundi
kimoja na wamefarikiana manasara makundi sabini na mbili yote yameangamia
isipokuwa kikundi kimoja na utafarikiana Umma wangu makundi sabini na tatu yote
yameangamia isipokuwa kikundi kimoja” akaulizwa ewe Mtume wa Allah: Nani hao
wenye kikundi hicho kimoja. Akasema: Kikundi hicho ni wale watakaofuata yale
ninayofanya mimi. Au kama alivyosema Mtume wa Allah Salallahu Alayhi Wasalam”.
(Wakati huo
wa fitina hizo akatokea huyu Abdullah bin Abaadh aliyekuwa na wivu na Dini ya
Allah na mshupavu akaita watu warudi katika njia ya Mtume Salallahu Alayhi
Wasalam na makhalifa wake waliofuata njia ya sawa (khulafaa Arrashidiin) na
kuwapinga vikali sana
viongozi wa Bani Umayya basi hao walioitikia mwito wake wakaitwa “Maibaadhi”).
Maibaadhi
hawakubadilisha kitu katika Dini tokea kuujua kwao Uislamu, wao wanakubaliana
na Umma wa Kiislamu katika mambo yote ya Dini isipokuwa katika baadhi ya mambo
ya itikadi ambayo haiwezekani kuhitilafiana juu yake (kwani haki iko kwa mmoja
tu) na tumeyataja yaliyo muhimu miongoni mwa hayo katika kijitabu hichi kifupi.
Na
watungaji wa vitabu wa Kiibaadhi huchukua haki kwa Mwanachuoni ye yote yule
akiwa katika wao au katika wapinzani wao na hulikataa jambo lolote
linalopingana na haki likiwa limeletwa na mwanachuoni wao au mwingineo. Tena
siyo kila Muibaadhi maridhiya kwao isipokuwa wanavyohukumu kuwa Muislamu yeyote
afaye bila ya kutubu na yungali aendelea kufanya maasi makubwa wanaona kuwa
ataingia Motoni iwapo Ibaadhi au mwengineo, kwani hakuna aliye karibu na Allah
isipokuwa mcha Mungu na hakuna aliye mbali naye isipokuwa muovu.
ﭽ ﯓ ﯔ
ﯕ ﯖ ﯗ
ﯘ ﯙ ﯚ
ﯛ ﯜ ﯝ
ﯞ ﭼ
طه: ١٠٩
“Siku
hiyo hautamfaa uombezi wa yeyote ila wa yule anayemruhusu Mola na kuiridhia
kauli yake”.
Anasema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam katika kuwasemeza baadhi ya watu wake:-
( يا فاطمة بنت محمد ويا صفية عمة
محمد : اشتريا أنفسكما من الله فإني لا أغني عنكما من الله شيئا لا يأتينى الناس
بأعمالهم و تأتوني بأنسابكم )
"Ewe Fatma bint Muhammad na ewe Safiya shangazi yake
Muhammad zinunueni nafsi zenu kwa Allah, kwani mimi siwafai kitu kwa Allah,
wasinijie watu na vitendo vyao nanyi mkanijia na nasabu zenu"
(Uhusiano wenu kwangu wa kidamu mkafikiria kuwa utawasaidia, la siku hiyo
haimsaidii mtu isipokuwa amali yake aliyoifanya, hakuna “wasta” wala
“influence”).
Na
anasema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam:-
من قصر به عمله لم يسرع به نسبه
“Mwenye
kupungukiwa na amali (vitendo vyake) haitamsaidia kitu nasaba yake (uhusiano
wake kwangu)”.
Kwa
hiyo anaetilia shaka madhehebu ya Kiibadhi atakuwa ameitilia shaka Dini yote na
mwenye kuwatia makosani Maibadhi atakuwa amewatia makosani Masahaba wa Mtume wa
Allah Salallahu Alayhi Wasalam na hakika Allah Subhanahu Wataala ni Mjuzi wa
kila alitamkalo mtu basi na aseme alitakalo (atahisabiwa na Allah Subhanahu
Wataala Siku ya Kiyama). Na mwenye kutatizwa na jambo lolote awaulize wenye
elimu kwani elimu ndiyo ya kuulizwa.
Tunamuomba
Allah Subhanahu Wataala atuongoze njia ya haki na atufahamishe Dini yetu kwani
Anaemtakia kheri humpa hiyo (kheri). Na hakuna uwezo wala nguvu isipokuwa kwa
Allah Mtukufu na Rehema zake zimfikie Mtume wake mkarimu Salallahu Alayhi
Wasalam na Masahaba zake wenye fadhila kubwa.
No comments:
Post a Comment
Note: only a member of this blog may post a comment.