Tuesday, 19 January 2016

Juzuu 4 Kutoonekana kwa Allah----Kujenga Uongofu katika nyoyo za Vijana-----




        ﯪﯫ              ﯱﯲ                 ﯺﯻ        ﯿ              ﰃﰄ                ﰇﰈ                 ﭓﭔ          ﭘﭙ          ﭝﭞ                                  ﭪﭫ           الأنعام: ١٠٠ - ١٠٣



“Na (juu ya hivi) wamemfanyia Allah (Subhanahu Wataala) Majini kuwa washirika wake, hali yeye ndiye aliyeumba (si majini). Na wamemsingizia (Allah (Subhanahu Wataala) ) kuwa ana watoto wa kiume na wakike. (wanasema haya) pasipo kujua. Ameepukana (Allah) na upungufu, na yu juu kuliko yale wanayomsifu nayo”.

“Yeye ndiye Muumba wa Mbingu na Ardhi. Inamkinikaje awe na mwana, hali hana mke. Naye ndiye aliyeumba kila kitu. Naye ni mjuzi wa vitu vyote. Huyo ndiye Allah, Mola wenu. Hakuna anayeabudiwa kwa haki ila yeye, Muumba wa kila kitu. Kwa hivyo, muabuduni yeye tu, Naye ni Mlinzi wa kila kitu”.

“Macho hayamfikii (kumuona yaani haonekani) bali yeye anayafikia macho (kuwaona wenye macho na wasiokuwa na macho). Naye ni mwenye kujua yaliyofichikana na yaliyo dhahiri”.




Suala:

Sheikhe wetu mkubwa Mufti Ahmed bin Hamed Al-Khaliliy: Zipi hizo dalili za kiakili na zilizonukuliwa zinazoonesha kutoonekana kwa Allah (Subhanahu Wataala) katika Dunia na Akhera.


Jawabu:

Kwa jina la Allah Mwenye kuneemesha neema kubwa kubwa na Mwenye kuneemesha neema ndogo ndogo. Shukrani zote anastahiki Allah, Mola wa walimwengu wote na Rehema zake na Amani zake zimwendee Mbora wa Mitume Bwana wetu Muhammad na ziwaendee jamaa zake na Sahaba zake wote. Ama baada ya haya. Ni katika mambo yanayojulikana kabisa kuwa Allah (Subhanahu Wataala) yeye ni kinyume na viumbe vyake vyote katika sifa zake zote kwani havifanani nae kwa chochote wala yeye (Allah (Subhanahu Wataala)) Hafanani navyo kwa chochote, basi kwa hivyo Hasifiwi Subhanahu Wataala kuwa Yeye ni dhati yaani kuwa ni kitu kinachochukua nafasi (جوهر ) (k.m. dhahabu, udongo, mbao) wala kuwa ni sifa (عرض) (k.m. rangi, umoto, ubaridi) wala kuwa ni mwili (k.m. kitu hai, gilasi, karatasi). Wala hasifiki Mola Subhanahu Wataala kuwa amekuweko pahala fulani au ametokeya wakati Fulani, kwani pahala na nyakati hazina athari kwa Allah (Subhanahu Wataala) kwasababu Yeye Subhanahu Wataala Yupo kabla ya kuumba wakati na pahala. Yeye yupo kama alivyotangulia kuwepo haonekani kwa jicho wala hatafutwi kwa kuulizwa pale alipo.


Basi sifa zote za viumbe ni muhali kwake Subhanahu Wataala kwa hivyo yabainika kuwa Dhati yake Subhanahu Wataala (ukweli wake) haiwezi kuonekana kwani haiyumkiniki kujulikana Subhanahu Wataala kwa jicho wala kwa hisia yoyote (sense) katika hisia za mwanadamu, kama alivyokuwa muhali kujulikana kwa kumfikiri. Na hakika kikomo cha mwanadamu kuijua Dhati ya Allah (Subhanahu Wataala) ni kukubali kwake kushindwa kuitambua (yaani kukubali kwa binaadamu kuwa ameshindwa kumjua Mola Subhanahu Wataala basi ndio kumjua kwake) kama ilivyotolewa kutokana na Assidiq RA kuwa amesema:

‘Kushindwa kumjua (Allah (Subhanahu Wataala)) ndio kumjua’.

           

Umma wa Kiislamu umekhitilafiana katika kumuona Mola Subhanahu Wataala, na kauli ya haki iliyokuwa haina shaka ndani yake ni kuwa Allah (Subhanahu Wataala) haifai kusemwa kuwa aonekana (au ataonekana) hapa Duniani wala huko Akhera na hayo ndiyo Aliyoyasema Yeye Mwenyewe Subhanahu Wataala juu ya Nafsi yake, basi haifai kupinga cho chote Alichokieleza Subhanahu Wataala juu ya Nafsi yake au juu ya kingine. Bali Anasema Allah (Subhanahu Wataala) katika kujieleza Nafsi yake:


            ﭪﭫ        الأنعام: ١٠٣

“Macho hayamfikilii (kumuona) bali yeye anayafikilia macho (kuyaona na kuwaona hao wenye macho). Naye ni mwenye kujua yaliyofichikana na yaliyo dhahiri."


Na wale wanaotaka kuthibitisha kuonekana kwa Allah (Subhanahu Wataala) katika Akhera au katika Dunia na Akhera wamefasiri neno الإدراك (kufikilia) katika Aya hii kwa maana ya الإحاطة  maana yake “kuzunguka” na hiyo haisihi kabisa kwasababu الإدراك halifasiriwi kwa الإحاطة  kwani huwezi kukuta katika makamusi ya lugha ya kiarabu kuwa “Al-Idrak” limefasiriwa kwa maana ya “Al-Ihaatah” kama ilivyokuja katika “Al-Qamoos” na “Sherehi” yake na katika “Lisaan Al-Arab”. Imekuja vile vile katika “Lisaan Al-Arab” kuwa “Adraktuhu Biayniy” kwa maana nimemuona na hivyo hivyo imekuja katika sherehi yake katika kitabu hiki cha lugha kikubwa kinachotegemewa na waarabu wote vipi basi itasemwa kuwa Al-Idraak katika Aya hii imekuja kwa maana ya Al-Ihaata الإحاطة  .

Inasemwa vile vile “Adraktu hayaat fulaan” na kauli hii inaweza ikatokana na mtu ambaye hakumwahi mwenzake kutoka mwanzo mpaka mwisho basi vipi liletwe neno la “Idraak” hali ya kuwa hakuuwahi uhai wake tokea mwanzo mpaka mwisho. Vile vile husemwa “Adrakahu Assahmu” ikiwa (mtu amelengwa na mkuki) ukamfikia na kumchoma, kwa hiyo halina maana neno hilo kuwa mkuki umemzunguka pande zote. Kisha Waarabu waiita mvua isiyokatika: “Al-Matar Al-Mutadaarik” na maana yake matone yake yameshikana wala haina maana kuwa kila tone limezunguka matone mengine kitu ambacho hakiwezekani kabisa. Na Allah (Subhanahu Wataala) amesema juu ya watu wa Motoni:


         الأعراف: ٣٨

“Mpaka watakapokusanyika wote humo.”


Wala haikusudiwi kwa “Hattaa Idha iddaarakuu” isipokuwa maana ya kufikiana (au kukusanyika).


Na upande mwengine twamuona Mama wa Waumini Aisha RA anakanusha huu mchanganyiko uliopo katika kuifasiri Aya hii tukufu: Ameitoa Imam Al-Rabii na Mashekhe wawili (Bukhari na Muslim) na wengineo kwa njia ya Bibi Aisha RA kuwa amesema:- “Asemaye moja katika mambo matatu amezusha uwongo mkubwa juu ya Allah” Hadithi hii amesema Masrook kutokana na Bibi Aisha: “Anaesema kuwa Muhammad amemuona Mola wake basi amemzulia Allah uwongo mkubwa” Akasema Masrook: Na nilikuwa nimeegemea nikakaa nikasema ewe Mama yangu, nipe wasaa wala usiniharakishe: Je Hakusema Allah (Subhanahu Wataala):


          النجم: ١٣

“Na hakika (Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam)) akamuona (Jibril) mara nyingine (kwa sura ile yake ya ki-Malaika katika usiku wa Miraji)”


Na je Hakusema Mola Subhanahu Wataala:


         التكوير: ٢٣

“Na hakika yeye alimuona (Jibril) kwenye upeo wa macho uliosafi wa mbinguni”


Akasema (bibi Aisha RA):- Mimi ni mtu wa mwanzo katika Umma huu (wa Kiislamu) kumuuliza Mtume Salallahu Alayhi Wasalam jambo hilo akasema: Huyo ni Jibril AS sikumuona katika sura yake aliyemuumba nayo Allah (Subhanahu Wataala) isipokuwa mara  mbili. Kisha akasema (Bibi Aisha RA): Hukusikia kuwa Allah Anasema:-


            ﭪﭫ  الأنعام: ١٠٣

“Macho hayamfikii (kumuona) bali yeye anayafikia macho (kuyaona na kuwaona hao wenye macho)”.


Jee basi itafichika kwa Mama wa Waumini Aisha RA maana ya neno “Al-Idraak” kama ingekuwa maana yake ni “Al-Ihaata”? Naye in mwenye ulimi wa kiarabu na amekulia katika ulezi wa Utume na akanyonya maziwa ya Wahyi na akafahamu maana ya Qur'ani na maana ya maneno ya waarabu.


Je inawezekana kuwa itafichika maana ya neno “Al-Idraak” (kufikia) kutokana na kumbukumbu ya huyu mjuzi mwenye maarifa (Bibi Aisha RA) na waje kujua waliokuja baada yake kuwa maana yake ni Al-Ihaata (kuizunguka).

Basi Aya hii tukufu inakanusha kufikia (“Al-Idraak”). Na kufikia katika kila kitu ni kwa mujibu kilivyo. Kwani kufikia (Idraak) kwa mkono ni kukamata kwake, kufikia (Idraak) kwa jicho ni kuona kwake, kufikia (Idraak) kwa sikio ni kusikia kwake na kufikia (Idraak) kwa silaha ni kupata shabaha, na vivyo hivyo inasemwa kuhusu “Idraak” ya ujumla kuwa maana yake ni kufikia kama vilivyoonesha hivyo vitabu vya lugha ya kiarabu.


Wako waliodai kuwa Aya hii tukufu imekusudiwa kukanusha kumuona Allah (Subhanahu Wataala) katika maisha ya Dunia bila ya maisha ya Akhera. Jawabu la dai hilo ni kama ifuatavyo: Sifa za Allah (Subhanahu Wataala) hazibadiliki kwani Allah (Subhanahu Wataala) amejisifu kwa sifa nyingi na amejikanushia Dhati yake iliyotukuka mambo mengi ambayo hayawafikiani na utukufu wake na ukubwa wake. Mfano wa hayo kauli yake Subhanahu Wataala katika kujikanushia sifa ya kusinzia na kulala:-


        البقرة: ٢٥٥

“Kusinzia hakumshiki wala kulala”


Na kauli yake Subhanahu Wataala katika kujikanushia dhulma:


         الكهف: ٤٩

“Na Mola wako hamdhulumu  yeyote”.


Na kauli yake katika kujikatalia mke na mwana:


                      الجن: ٣

“Na kwa hakika utukufu wa Mola wetu umetukuka kabisa, hakujifanyia mke wala mwana.”


Na kauli yake Subhanahu Wataala katika kujikatalia kuzaa na kuzaliwa:


                        الإخلاص: ٣ - ٤

“Hakuzaa wala Hakuzaliwa, Wala hana anayefanana naye hata mmoja”.

           

Basi je! Inawezekana  kusemwa kuwa mambo aliyojikatalia Allah (Subhanahu Wataala) nafsi yake mwisho wake ni huu uhai wa Dunia bila ya kuendelea katika uhai wa Akhera? Na isemwe kuwa Allah (Subhanahu Wataala) yawezekana kusifika huko Akhera kuwa Anazaa? Anazaliwa? Ana mke? Adhulumu? Ametukuka Subhanahu Wataala na hayo, na kuwa huko Akhera yuko aliyefanana naye? Na mengineyo aliyojikanushia Subhanahu Wataala nafsi yake. Basi hayo yote yatuonesha dalili wazi kuwa Allah (Subhanahu Wataala) Ametaka kwa kauli yake {لا تُدْرِكُهُ الْأَبْصَارُ} (kutufahamisha) kujikatalia Nafsi yake kuonekana katika Dunia na huko Akhera.

           

Wamedai baadhi ya wale wanaothibitisha kuonekana kwa Allah kuwa Yeye Subhanahu Wataala hajisifu kwa kilichokanushwa (لا تدركه الأبصار) bali wathibitisha badala yake (hicho kitu alichojikanushia Subhanahu Wataala) kitu kilichopo. Na ikikanushwa kuonekana kwake Subhanahu Wataala kinakuwa kitu kisichokuwepo na haiwezekani Allah (Subhanahu Wataala) kujisifu kwa kitu kama hicho. Na wamesema ukweli uliopo ni kuwa Allah amejisifu Nafsi Yake kwa ukanusho kwa sababu katika kujisifu huku au katika kujikanushia huku ipo maana nyingine ya kuthibitisha (sifa) wakasema kuwa makusudio ya kauli yake Subhanahu Wataala:

 (لا تأخذه سنة ولا نوم) nikuthibitisha sifa ya Usimamizi wa kila jambo, na kusudio la kujikatalia Allah kuwa na mke na mtoto ni kujithibitishia sifa ya upweke, na kusudio la kujikatalia kudhulumu ni kujithibitishia uadilifu, na kama hivyo katika kukanusha kila kinachokanushwa na Dhati Yake Subhanahu Wataala kunakusudiwa kuthibitisha maana fulani (kama katika maelezo yaliyopita).


Ama kuonekana kwa Allah (Subhanahu Wataala) (imekuja katika Qur'ani kwa njia ya kukanushwa) haina (kama mengineyo) maana ya kuthibitishwa ambayo hujisifu nayo Allah (Subhanahu Wataala) kwa kujithibitishia Nafsi yake. Hivi ndivyo alivyosema Ibn Al-Qayyim kumfuata Shekhe wake Ibn Taiymiya.


Na jawabu lake ni kuwa Allah (Subhanahu Wataala) amejikanushia Dhati Yake yale aliyojikanushia kwa sababu hayawafikiani na ukubwa wa shani yake, Kibriyaai Yake na Utukufu wake. Na kama tungelisema kuwa inafaa kuthibitisha yale Aliyojikanushia Subhanahu Wataala Nafsi yake basi tungelifanya jambo lenye hatari sana na tungeliyakataa maneno ya Allah (Subhanahu Wataala). Na tafsiri kama hii aliyoitaja Ibn Al-Qayyim inapelekea kukimbia kutoka mnamo uwazi kwenda kwenye matatizo na kutoka mnamo uhakika kwenda kwenye njozi.


Na kama tungetaka kumjibu (Ibn Al-Qayyim) kwa njia ile ile aliyoitumia tungesema:-

Katika kukanusha kumuona Allah (Subhanahu Wataala) iko mukabili wake maana ya uthibitisho vile vile nayo ni kusifika Subhanahu Wataala kwa Ukubwa au Utukufu (Kibriyaau) na (Al-Jalaalu) kwani mkanusho (wa kumuona Subhanahu Wataala) uliokuja katika Aya hii umekuja katika maonesho ya kuisifu Dhati ya Allah (Subhanahu Wataala) kwa Ukubwa na Utukufu, vipi tena isemwe kuwa kukanusha kumuona Subhanahu Wataala ni kitu kisicho na maana hakuna ndani yake kitu cha uthibitisho kinyume na zile sifa nyingine alizojikanusha nazo. Na mbali ya yote hayo twaziona hadithi sahihi za Mtume Salallahu Alayhi Wasalam ambazo zinakanusha kuonekana Subhanahu Wataala, na katika hadithi hizo ni ile aliyoitoa Muslim katika Sahihi yake kwa njia ya Abi Dhar RA kuwa amemuuliza Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) Je umemuona Mola wako usiku uliopelekwa “Israa”? Mtume ziwe juu yake bora ya Rehema na Amani akamjibu “Nuru vipi nimuone?”.


Basi huku ni kukanusha kwa Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) kumuona Allah (Subhanahu Wataala) na kama tulivyosema kuwa sifa zake Subhanahu Wataala za Dhati hazibadiliki kama ilivyokuwa Dhati Yake (Yeye Mwenyewe Subhanahu Wataala) haibadiliki, basi kwa hivyo hayumkiniki kuonekana Mola Subhanahu Wataala Duniani wala Akhera.


Vile vile ziko hadithi nyingine nyingi zinazokanusha kuonekana kwa Dhati Yake tukufu Subhanahu Wataala. Na licha ya dalili hizo zipo dalili nyingine za kiakili na miongoni mwa hizo kuwa kitendo cha kuona kunalazimika kuwepo baadhi ya mambo ambayo hayo hayawezekani kwa Allah (Subhanahu Wataala) kama kuwa kile kitu kinachoonekana katika mahali fulani na mahali hapo pawe upande uliokabiliana na muonaji, na kiwe (hicho kinachoonekana) hakikugandana na jicho linalotizama wala kisiwe mbali nalo umbali mkubwa, na kisiwe mwili uliofichika sana ukawa haunekani kwa uwezo wa kuona wa kawaida (macho yetu ya kibinaadamu) kama hewa, na kisiwe kidogo sana, na hiyo inahitilafiana na uwezo wa kuona na mambo mengineyo yanayopingana na Utukufu wa Allah (Subhanahu Wataala) na Nguvu Yake na Ukubwa wake.


Ama zile dalili za kiakili na zilizomo katika Kitabu na Sunna wanazozitumia wanaodai kuonekana kwa Allah (Subhanahu Wataala) hazikubaliki. Katika dalili za kiakili walizozitumia kuwa wamesema: Kuwa Allah (Subhanahu Wataala) Yupo na kila kilichopo kinaweza kuonekana. Maneno haya sio kweli; kwa mfano akili ipo na je akili ya mtu yaonekana? Na Roho ipo katika mwili je inaonekana? Maneno yapo je yaonekana? Basi hivyo hivyo vitu vyote vingine visivyoonekana, bali upepo hauonekani na hali upo. Na wametumia pia dalili za Qur'an na Sunna na katika hizi kauli ya Allah (Subhanahu Wataala) :

                               القيامة: ٢٢ - ٢٣

“Nyuso nyingine siku hiyo zitangara kweli kweli. Zitamsubiri Mola wao (Awape rehema zake)”.


Na sisi tunawaambia kuwa kauli yake Subhanahu Wataala:

Kwanza: وجوه يومئذ ناضرة  chanzo chake ni   النضارة  kwa herufi ya ض   na maana yake ni uzuri wa sura (na kun’gara),  إلى ربها ناظرة  yaani zinangojea rehema yake Allah (Subhanahu Wataala) na kuingizwa katika Pepo yake kwa dalili kuwa Subhanahu Wataala Amesema baada ya hivyo:

ووجوه يومئذ باسرة   maana ya باسرة  zitakunjana ambayo inakabiliana na kauli yake Subhanahu Wataala ناضرة  kwa ض .  Kisha akasema تظن أن يفعل بها فاقرة  yaani zinangojea jambo ambalo litakata tindi za migongo yake, na (kauli) hii ndio inayokabiliana na kauli yake Subhanahu Wataala إلى ربها ناظرة  na kama ingesemwa kuwa kauli yake Subhanahu Wataala  إلى ربها ناظرة  inakusudiwa kuwa hizo nyuso zitamtazama Allah (Subhanahu Wataala) ingesemwa juu ya hizo nyuso nyingine (zinazokabiliana na hizi):

  ووجوه يومئذ باسـرة عـن رؤية ربها قاصرة

“Na nyuso zingine siku hiyo zitakunjika hazitoweza kumuona Mola wake”. Au maneno kama haya yanayoleta kukabiliana kwa maana baina ya watu hawa na wale.


Wale waliosema kuwa Allah (Subhanahu Wataala) aonekana na wakatoa Aya hii kuwa dalili yao wamesema kuwa النظر  kama imeletwa kwa maana ya (الانتظار) ‘kungojea’ basi haiunganishwi na إلى  lakini inaunganishwa na إلى  ikiwa katika maana ya kuona na khasa ikiwa imehusishwa na nyuso. Jawabu kwa maneno hayo kuwa maneno ya waarabu yapinga hoja hiyo. Huyu Hassan bin Thaabit asema:

وجوه يوم بدر ناظرات    إلى الرحمن يأتى بالفلاح

‘Nyuso siku ya Badri (yaani wenye nyuso) zamngojea Rahmani Alete ushindi’

Na je walikuwa wakuu wa Waumini katika siku ya Badr wamtizama (wamuone) Allah (Subhanahu Wataala) wakati mwanashairi aliposema hayo juu yao:

( و إذا نظرت إليك من ملك   و البحر دونك زدتني نعما )

‘Na ninapokutaraji nawe ni mfalme, na bahari haikufikii kwa ukarimu, wewe huniongeza neema’

Na asema mwingine:

( كل الخلائق ينظرون سجاله   نظر الحجيج إلى طلوع هلال )

‘Viumbe wote wanangoja zawadi zake, kama mahujaji wanavyongoja kuandama kwa mwezi’

Kama ingekuwa النظر  haiunganishwi kabla yake na إلى  isipokuwa ikiwa kwa maana ya kuona ingelazimika kuwa Allah (Subhanahu Wataala) hawaoni waovu Siku ya Kiyama kwa sababu amesema Subhanahu Wataala:


                                                        ﯿ                     آل عمران: ٧٧

“Hakika wale wanaouza ahadi ya Allah na viapo vyao kwa ajili ya thamani ndogo ya kilimwengu hao ndio hawatakuwa na sehemu ya kheri katika Akhera wala Allah hatasema nao (maneno mazuri) wala hatawatazama (jicho la rehema) siku hiyo ya Kiyama. Wala hatawatakasa (na madhambi yao) nao watapata adhabu iumizayo”.


Je makusudi ya kauli yake Subhanahu Wataala:

ولا ينظر إليهم يوم القيامة  ni kuwa hawaoni (hao watu waovu Siku ya Kiyama) basi atakuwa anawaona baadhi ya viumbe wake na hawaoni baadhi nyingine? Allah ametukuka na hayo wanayosema juu yake kutukuka kukubwa. Na hakika makusudio ya kauli yake Subhanahu Wataala hiyo ni kuwa hao Allah (Subhanahu Wataala) hatawaenezea Rehema Yake Siku ya Kiyama. Kwa hivyo نظر الله تعالى إلى عبده  ikija kwa njia hii maana yake huwa “Allah kumuenezea Rehema Yake mja wake” na نظرالعبد إلى ربه و  maana yake “Mja kungojea Rehema ya Mola wake”. Juu ya hivyo kitendo cha kuona hufanyika kwa macho sio kwa nyuso, basi vipi hapa kinahusishwa na nyuso na kuhusishwa huko na nyuso ni matumizi ya asli (“Hakika”) au ya kimethali (“Majaaz”)? Na kwa nini zikahusishwa na nyuso bila ya kuhusishwa na viungo vingine vya mwili juu ya kuwa kutazama kitu cha kupendeza kwasababisha moyo ufurahike kabla ya uso, na athari ya kufurahika huku (kwa moyo) inarudisha (furaha hiyo) kwa mwili mzima. Kwa nini basi nyuso ndizo zinazohusishwa na kutazama? Yote haya yatuonesha kuwa النظر  katika Aya hii ni kwa maana ya الانتظار  yaani kungojea (sio kutazama au kuona).

           

Vile vile wametumia hadithi za Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) dalili ya kuonekana kwa Allah (Subhanahu Wataala). Zimetolewa hadithi hizi katika Sahihi Bukhari, Sahihi Muslim na venginevyo zinaonesha kuwa Allah (Subhanahu Wataala) ataonekana Siku ya Kiyama katika hizo:

Kuwa Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) amesema: “Mtamuona Mola wenu kama mnavyouona mwezi usiku wa Badri (mwezi unapokamilika)”.


Nami nataka kujibu juu ya kutumia hadithi hizi kama dalili ya kumuona Subhanahu Wataala kuwa kwanza hadithi hizi ni “hadithi Ahaadiya” (yaani hadithi zilizopokewa kwa njia ya Sahaba mmoja mmoja kutoka kwa Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam). Na hadithi kama hizi zawajibisha vitendo lakini hazithibitishi elimu. Kwa hiyo mambo ya Itikadi hayawezi yakajengwa juu ya msingi wa (hadithi hizo za Ahaadiya) kwa sababu Itikadi inajengwa na hoja zilizo na yakini na hakika wala haijengwi na hoja za dhana, mbali tena ikiwa hadithi hizo zapingana na hoja za hakika kutokana na Qur'an na Sunna zilizo na nguvu na makubaliano ya watu wema waliopita. Na licha ya yote hayo zikichukuliwa hadithi hizi kuthibitisha kuonekana kwa Allah (Subhanahu Wataala) zitasababisha mpingamano wa hatari na mkubwa sana. Kwani hadithi wanayoitumia sana:

 ( وإنكم سترون ربكم يوم القيامة كما ترون القمر ليلة البدر )

“Na hakika mtamuona Mola wenu Siku ya Kiyama kama mnavyouona mwezi usiku wa Badri (mwezi unapokamilika)”


Wameitoa hadithi hii mashekhe wawili (Al-Bukhari na Muslim) kwa njia ya Abi Huraira na Abi Saeed Al-Khudry RA. Na naleta hapa hadithi iliokuwa karibu zaidi na hadithi ya Abi Huraira kimatamko kama ilivyokuja katika Sahihi Muslim: Imekuja katika hadithi hii kuwa Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) aliulizwa: Je tutamuona Mola wetu Siku ya Kiyama? Akasema: Je mnakusanyana kuliona jua (kulitizama) wakati wa mchana bila ya kuwa na kizuizi cho chote (kama mawingu n.k). Wakasema: Hapana Ewe Mtume wa Allah, Akasema: Kama hivyo Mtamuona. Watafufuliwa watu Siku ya Kiyama katika sehemu moja kisha wataambiwa na wafuate kila Umma kile walichokuwa wakikiabudu. Basi kuna katika wao watakaofuata Jua na wengine wao watakaofuata Mwezi na miongoni mwao watakaofuata viongozi wa upotofu, na utabakia Umma huu na ndani yake mna wanafiki wake na atawajia mola wao katika sura sio ile wanayoijua awambie mimi mola wenu, basi hapo watamjibu twajikinga kwa Allah nawe! Hatuondoki mahala petu hapa mpaka atujie mola wetu. Basi hapo atawajia (mola wao) katika sura wanayoijua... mpaka mwisho wa hadithi.


Hapa mimi nataka kuwauliza kabla ya kitu chochote wale wanaosema kuwa watamuona Mola wao Siku ya Kiyama wakiitegemea hadithi hii. Je kumuona Allah (Subhanahu Wataala) kwa namna (mfano) au bila ya namna? Kwa sababu twawasikia wakisema kuwa watamuona bila ya namna yoyote na wakati hadithi inasema: namna hiyo mtamuona (kama hivyo) yaani kama mnavyouona Mwezi na mnavyoliona Jua na kuliona Jua na kuona Mwezi ni kwa namna Fulani, vipi basi wanadai kuwa watamuona bila ya namna.


Pili: Je waamini kuwa Allah (Subhanahu Wataala) anabadilika kutoka sura fulani kwenda sura nyingine na kutoka hali kwenda hali nyingine? Na hali inajulikana kuwa kila kinachobadilika kimeumbwa.


Tatu: Je wamewahi watu kumuona Duniani hata waijue sura yake Subhanahu Wataala na wakati atakapowajia kwa sura tofauti na ile wanayoijua waseme: Twajikinga kwa Allah nawe hatuondoki mahali petu hapa mpaka atakapotujia Mola wetu. Nimeyafanya majadiliano haya na baadhi ya wale wanaodai kuwa Allah (Subhanahu Wataala) ataonekana Siku ya Kiyama, na lilikuwa jawabu lao kwa nukta hii ya mwisho ni kuwa Allah (Subhanahu Wataala) ameeleza juu ya sifa zake na vile vile Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) amewaambia Umma wake juu ya sifa za Allah (Subhanahu Wataala), kwa hiyo wakija kumuona Allah (Subhanahu Wataala) kwa sifa tofauti na zile sifa walizoambiwa anazo itaingia shaka katika nafsi zao na husema: Hatuondoki mahala petu mpaka atujie Mola wetu. Nikawajibu kwa hayo: Ikiwa sifa za Allah zabadilika kutoka hali kwenda hali nyingine na kutoka sifa kwenda sifa nyingine je isingekuwa hiyo dalili kuwa Yeye Allah (Subhanahu Wataala) ni kiumbe (amekuwako baada ya kuwa hayupo) kwa sababu kila chenye kubadilika kimeumbwa. Ametukuka Allah (Subhanahu Wataala) na hayo Utukufu mkubwa. Na upande mwingine je inawezekana Allah (Subhanahu Wataala) kujisifu Nafsi Yake kwa kitu asichokuwa nacho? Au Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) kusema juu ya Allah (Subhanahu Wataala) kitu asichokuwa nacho? Wakajibu juu ya hayo: Hayo yanaweza (Ya kumsifu Allah sifa asiyokuwa nayo) yakafanywa kwa makusudio ya mtihani na majaribio. Nikawajibu kama ingekuwa makusudio ni mtihani na majaribio katika kusema juu ya sifa za Allah tofauti na Alivyo basi ingewezekana kuwa kila Alichotwambia Allah (Subhanahu Wataala) ni kwa makusudio ya mtihani na majaribio na sio ukweli ulivyo, kwa hiyo kusingekuwa na Pepo wala Moto wala malipo kwa mema na maovu.

           

Na vile vile wale wanaodai kuwa watamuona Mola wao Siku ya Kiyama kwa hiyo baada ya kuwa wamekwisha kusoma Kitabu cha Allah na wamekwisha soma Sunna ya Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) na wametizama zile sifa Alizojisifu nazo Allah (Subhanahu Wataala) katika Kitabu (Qur'an) na zile sifa alizozisema Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) juu ya Mola wake Je anaweza mmoja katika hao atusifie sura ambayo anatarajia kumuona Allah (Subhanahu Wataala) nayo Siku ya Kiyama kutokana na aliyeyajua katika Kitabu cha Allah na Sunna ya Mtume wake Salallahu Alayhi Wasalam?


Hapana shaka hakuna mmoja anaeweza kujibu suala hilo yaani atujulishe sura ambayo atamuona nayo Allah Siku ya Kiyama kwa namna alivyoijua kutokana na Qur'an na Sunna na wala hakuna mtu aweza kuzungumzia juu ya Dhati Iliyotukuka kama ilivyo kwa sababu Allah (Subhanahu Wataala) Peke yake ndiye anayeijua ilivyo. Naye husema Subhanahu Wataala:

              طه: ١١٠

“Wala wao hawawezi kumjua (Mungu) vilivyo”


Kwa hiyo hawawezi kuijua Dhati Tukufu (Allah (Subhanahu Wataala)).


Na upande mwingine dai hilo halikubaliki, na hivyo kwa sababu katika Sahihi Muslim kuna hadithi ya Abi Saeed inayohusika na jambo hili:

( سيأتيهم ربهم في غير الصورة التي رأوه فيها أول مرة )

“Atawajia Mola wao katika sura tofauti na ile waliomuona nayo mara ya kwanza”.


Hapa ni pahala pa mwanzo wanaposimama watu katika visimamo vya Siku ya Kiyama, mara ipi hiyo ya mwanzo (waliomuona Mola wao) inayozungumziwa katika hadithi hii? Je alionekana Allah (Subhanahu Wataala) kaburini, au kulikuweko kumuona Allah kabla ya mauti hata isemwe kuwa watamuona Allah kama walivyomuona mara ya kwanza na Akiwajia kwa sura tofauti na ile wanayoijua husema: Twajikinga kwa Allah na wewe hatuondoki mahala petu hapa mpaka atujie Mola wetu.


Vile vile katika hadithi hii kuna kinachoirudi itikadi yao kwani wao wanaamini kuwa kumuona Allah (Subhanahu Wataala) ni neema inayowahusu waja wa Mola Waumini tu siku hiyo, wakati hadithi hii inasema:

فتبقى هـذه الأمة فيها منافـقـوها فيأتيهم ربهم فى غير الصورة التى يعرفونه بها

"Na utabakia Umma huu wakiwemo wanafiki wao na atawajia Mola wao katika sura tofauti na ile wanayoijua."



Kwa hiyo kutokana na hadithi hii ni wazi kuwa Waumini na wanafiki wote watashirikiana katika kumuona Allah (Subhanahu Wataala), na huku wao wanasema kuwa kumuona Allah (Subhanahu Wataala) kutakuwa huko Akhera Peponi, na hapa wameitumia kauli ya Allah (Subhanahu Wataala):


      يونس: ٢٦

“Wale waliofanya wema watapata (jazaa yao) wema wao na zaidi”


Wao wakasema الحسنى kuingia Peponi na الزيادة kuutizama uso wa Allah (Subhanahu Wataala). Na zimekuja hadithi vile vile zinazoonesha hayo (zinazotia nguvu tafsiri yao hiyo), kati yake ni hadithi ya Suheib: Kuwa Allah (Subhanahu Wataala) Atawaambia waja wake Waumini Siku ya Kiyama: Je nisiwazidishie? (nisiwaongezee kitu juu ya haya niliowapa?). Hapo watamwambia: Je hukuzifanya nyuso zetu zikiwa nyeupe na ukatuingiza Peponi? Hapo Atafunua hijabu (Sitara). Ni wazi kabisa kuwa kumuona Allah katika hadithi hii ni baada ya kutulia huko Peponi na hali hadithi ya Abi Huraira ambayo wanaitolea hoja sana juu ya kuonekana kwa Subhanahu Wataala na hadithi ya Abi Saeed hizi mbili zinaonesha kuonekana kwake Subhanahu Wataala ni katika msimamo wa Siku ya Kiyama (sio Peponi), kwa hiyo hapa kuna mpingamano (hadithi ya kwanza inatwambia kuonekana kwa Subhanahu Wataala ni Peponi na hali hadithi mbili za mwisho ni katika msimamo wa Siku ya Kiyama). Kwa hiyo hakuna njia ya kuepukana na mpingamano huu isipokuwa kutambua kuwa makusudio ya الرؤية  ni kuongezewa maarifa ya sifa zake Allah (Subhanahu Wataala) Siku ya Kiyama, ama vinginevyo haiwezekani kabisa.


Dalili nyingine walioitumia ni hadithi ya Ibn Abbas RA kuwa amesema: Hakika Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) amemuona Mola wake usiku aliopelekwa “Israa”.


Na jawabu lake kuwa maneno hayo hayakuthibiti kuwa yamesemwa na mtarajimu wa Qur'an Karim ambaye ni Ibn Abbas Alimu wa Umma huu R.A, bali imethibiti kutoka kwake kinyume cha hayo kama ilivyokuja katika Musnad ya mhifadhifu aliye hoja Al-Rabii Ibn Habiib, bali vile vile ameitoa Imam Muslim katika Sahihi yake kutokana na Ibn Abbas R.A kuhusu kuona kwa Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) usiku aliopelekwa “Israa” Amesema:

Umemuona moyo wake mara mbili رآه فؤاده مرتين   na makusudio ya kuona moyo wake ni kuzidi kupata maarifa ya Sifa zake Subhanahu Wataala na siyo vinginevyo. Na kama imesihi hadithi iliyofunguliwa (مطلق)  na ikiwa ipo hadithi nyingine iliyofungwa (مقيد)  basi hurudishwa ile hadithi iliyofunguliwa kwenye hadithi iliyofungwa. Wanazo vile vile wanatoa dalili kwa Aya nyingi za Qur'an ambazo hazioneshi kabisa kuonekana kwa Allah sio kwa mbali wala karibu kama:


                    المطففين: ١٥

“Hakika watazuiliwa, siku hiyo na (Rehema) za Mola wao”.


Na kuitolea kwao dalili Aya hii ni katika mlango wa kutoa dalili kwa kinyume cha andiko (مفهوم المخالفة) , jambo ambalo wamehitilafiana wanavyuoni juu ya hoja yake katika mambo ya dhana licha mambo ya yakini (Imani). Na vile vile maana ya kuzuiliwa na Allah (Subhanahu Wataala) ni kuzuiliwa na Rehema yake.


Pia wametoa dalili kwa ombi la Nabii Musa A.S. kwa Mola wake Subhanahu Wataala:


        الأعراف: ١٤٣

“Akasema: Mola wangu! Nioneshe (Nafsi yako) ili nikuone”


Lakini Musa AS hakuomba hilo kwa ajili ya nafsi yake, lakini kwa hakika ameomba hilo kwa ajili ya kuwanyamazisha watu wake. Na kama inavyosemwa juu ya suala la Nabii Ibrahim AS; kwani Ibrahim AS sio alikuwa hajui kuwa Allah (Subhanahu Wataala) Ahitilafiana na viumbe vyake na juu ya hivyo alivyoiona Nyota akasema: Huyu mungu wangu, na vile vile alivyoliona Jua akasema: Huyu mungu wangu huyu mkubwa. Lakini hakika amesema hivyo kwa kutaka kuwanyamazisha watu wake (kuwashinda kwa hoja) ambao walikuwa wakiabudu nyota na wakiyatukuza maumbile (Nature) na kutaka kuwasimamisha katika uhakika mmoja kuwa kila kitu kinatoweka isipokuwa Dhati Yake Subhanahu Wataala. Kwa hiyo jawabu ni moja kutokana na maneno ya Musa na maneno ya Ibrahim Salamu na Amani za Allah ziwe juu yao.


Kwa hiyo inabainika kuwa kauli ya haki isiyokuwa na shaka kuwa Dhati ya Allah (Subhanahu Wataala) (Yeye Mwenyewe (Subhanahu Wataala)) haionekani katika Dunia wala Akhera. Allah (Subhanahu Wataala) Ametukuka na hayo Utukufu Mkubwa.

Na jawabu kuhusu لن  katika kauli yake Subhanahu Wataala  لن تراني  ni kwamba hiyo ni dalili ya kuwa muhali kuonekana kwake Subhanahu Wataala yaani hawezekani kuonekana.


Wao (wanaosema kuwa Allah Ataonekana) wasema kuwa لن  haina maana ya milele na jawabu lake kuwa kukanusha kwa لن  kunamaanisha milele mara na mara nyingine kunamaanisha sio milele lakini uhakika ulioko ni kuwa katika kukanusha kwa “Lan” (لن)  linatizamwa lile jambo lililokanushwa na likiwa katika mambo yanayolazimika kukanushwa milele huchukuliwa hivyo na ikiwa sio hivyo huchukuliwa kinyume chake. Na katika mahala iliyotumika “Lan” (لن)  kwa maana ya kukanushwa milele kauli yake Subhanahu Wataala:


                         الحج: ٧٣

 “Hakika ya wale mnaowaabudu badala ya Allah hawawezi kuumba nzi hata wakikusanyika kwa kumuumba”


Hapa kwa hakika ni muhali wao kuumba nzi katika wakati wo wote ule na sio kukanushwa huku kwa wakati fulani bila ya wakati mwingine. Na Allah (Subhanahu Wataala) ni Mjuzi zaidi.


Na mimi niko tayari kufanya mdahalo (debate) kwa yule anayesema juu ya kuonekana kwa Allah (Subhanahu Wataala) aje nijadiliane nae mpaka nimrudishe kwenye haki au yeye anirudishe mimi kwenye rai yake akinishinda kwa hoja, na akitaka tufanye “Mubahala” (1) tutafanya. Allah (Subhanahu Wataala) ndie mwenye kutoa Tawfiiq.

Haya ni maneno ya Sheikh Ahmed bin Hamed Al-Khalily Mufti wa  Oman.

No comments:

Post a Comment

Note: only a member of this blog may post a comment.