ﭑ ﭒ
ﭓ ﭔ
ﭽ ﭑ ﭒ
ﭓ ﭔ ﭕ
ﭖ ﭗ ﭘ
ﭙ ﭚ ﭛ
ﭜ ﭝ ﭞ
ﭟ ﭠ ﭡ
ﭢ ﭣ ﭤ
ﭥ ﭦ ﭧ
ﭨ ﭩ ﭪ
ﭫ ﭬ ﭭ
ﭮ ﭯ ﭰ
ﭱ ﭲ ﭳ
ﭼ القدر: ١ - ٥
“Hakika tumeiteremsha (Qur'an) katika usiku wenye heshima kubwa (usiku
wa mwezi wa Ramadhani). Na nini
kitakachokujulisha hata ukajuwa nini huo usiku wa Heshima kubwa? Usiku wa
heshima, huo ni bora kuliko miezi elfu. Huteremka Malaika na Al-Ruuh( Jibril
A.S ) katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao kwa kila jambo. Amani (usiku) huo
mpaka mapambazuko ya Al-Fajiri”.
Saumu ni
nguzo ya nne katika nguzo za Uislamu, nayo ni miongoni mwa ibada za kiwiliwili
zinazomfanya mtu ajisafishe na Riyaa (kuabudu kwa kutaka watu wakuone kuwa
hodari sio kwa ajili ya Allah (Subhanahu Wataala) pekee na kutaka radhi yake). Inamuwajibikia
kila mtu aliye baleghe kufunga mwezi wa Ramadhani kila mwaka, nao ni mwezi
wenye baraka nyingi sana .
Saumu
imehusiwa jambo muhimu ambalo halipo katika ibada nyinginezo, nalo ni kuwa
ukweli wa hiyo Saumu kwa mwenye kufunga hakuna anaoujua isipokuwa Allah (Subhanahu
Wataala), kwa ajili hiyo Amesema Subhanahu Wataala:
( الصوم لي وأنا أجازي به الجنة )
“Saumu ni
yangu mimi na mimi namlipa (huyo anaefunga) kwa hiyo (Saumu) Pepo”.
Na juu ya
kuwa Ibada zote ni zake yeye tu Allah (Subhanahu Wataala) (lakini imesisitiziwa
kwa daraja kubwa iliyopewa kwani mtu aweza kudai amefunga lakini akiwa peke
yake huenda akala au akanywa kwa hivyo ukweli wake anaujua Subhanahu Wataala
pekee). Na katika hekima zake kuwa inaondoa maradhi na inasafisha akili na
hutia nuru katika undani wa mwili (yaani moyo ukipata nuru anaepukana mtu na
riyaa, hasadi, chuki, kibri n.k) na humpa mtu nguvu ya kufanya ibada na
huizowesha nafsi kuhimili njaa ili iweze kusubiria mashaka ya maisha, na
kadhalika. Saumu humfanya mtu aweze kupigana vita na magonjwa ya nafsi na kumtakasa
nayo na kumfanya awe na huruma juu ya mafakiri na wenye shida.
Kuhusishwa
Saumu na Mwezi wa Ramadhani ni kwa ajili ya kuhuisha kumbu kumbu ya kuteremka
kwa Qur'an ili iwe uongozi kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongozi na
upambanuzi (wa baina ya haki na batili) na ni kitu cha tabia kwa watu wa Qur'an
kuisherehekea kumbu kumbu hii na kujikaribisha kwa Allah kwa kuishukuru neema
hii yenye kulinda mabaya.
Saumu maana
yake katika lugha ni kujizuia, na maana yake katika Sheria ni kuzuia yafikayo
ndani ya mwili kutoka nje yake na kujizuia na jimaa na madhambi makubwa kwa
kutia nia kutoka Al-Fajiri mpaka kuzama jua (Magharibi) kwa kauli ya Allah (Subhanahu
Wataala) :
ﭽ
ﭣ ﭤ
ﭥ ﭦ ﭧ
ﭨ ﭩ ﭪ
ﭫ ﭬ ﭭ
ﭮ ﭯ ﭰ
ﭱ ﭲ ﭳﭴ
ﭵ ﭶ ﭷ
ﭸ ﭹ ﭺ
ﭻ ﭼ ﭽ
ﭾ ﭿﮀ ﮁ
ﮂ ﮃ ﮄ ﮅ ﮆﮇ
ﮈ ﮉ ﮊ
ﮋ ﮌ ﮍﮎ
ﮏ ﮐ ﮑ
ﮒﮓ ﮔ ﮕ
ﮖ ﮗ ﮘ
ﮙ ﮚ ﮛ
ﮜ ﮝ ﮞ
ﮟ ﮠ ﮡ
ﮢ ﮣﮤ ﮥ
ﮦ ﮧ ﮨ
ﮩﮪ ﮫ ﮬ
ﮭ ﮮ ﮯ
ﮰ ﮱ ﯓ
ﯔ ﯕﯖ ﯗ
ﯘ ﯙ ﯚ
ﯛ ﯜ ﯝ
ﯞ ﯟ ﯠ
ﯡ ﯢ ﯣ
ﯤ ﯥ ﯦ
ﯧ ﯨ ﯩ
ﯪ ﯫ ﯬ
ﯭ ﯮﯯ ﯰ
ﯱ ﯲ ﯳ
ﯴﯵ ﯶ ﯷ
ﯸ ﯹ ﯺ
ﯻ ﯼ ﭑ ﭒ ﭓ
ﭔ ﭕ ﭖ ﭗﭘ ﭙ
ﭚ ﭛ ﭜ
ﭝ ﭞﭟ ﭠ
ﭡ ﭢ ﭣ
ﭤ ﭥ ﭦ
ﭧ ﭨ ﭩﭪ
ﭫ ﭬ ﭭ
ﭮ ﭯ ﭰ
ﭱﭲ ﭳ ﭴ
ﭵ ﭶ ﭷ
ﭸ ﭹ ﭺ
ﭻ ﭼ ﭽ
ﭾﭿ ﮀ ﮁ
ﮂ ﮃ ﮄﮅ
ﮆ ﮇ ﮈ
ﮉ ﮊ ﮋﮌ
ﮍ ﮎ ﮏ
ﮐ ﮑﮒ ﮓ
ﮔ ﮕ ﮖ
ﮗ ﮘ ﮙ ﮚ ﭼ البقرة: ١٨٣ - ١٨٧
“Enyi
Mlioamini mmelazimishwa kufunga (Saumu) kama
walivyolazimishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu (183) Siku chache
tu (kufunga huko). Na atakayekuwa mgonjwa au katika safari basi atimize hisabu
katika siku nyingine. Na wale wasioweza, watoe fidia kwa kumlisha masikini. Na
atakayefanya wema kwa radhi ya nafsi yake, binafsi ni bora kwake. Na huku
kufunga ni bora kwenu ikiwa mnajua. (Haya sasa basi fuateni) (184) (Mwezi huo
mlioambiwa mfunge) ni Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa katika (mwezi) huo
hii Qur'an ili iwe uongozi kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongozi na
upambanuzi (wa baina ya haki na batili). Atakayekuwepo kwake katika huu mwezi
(wa Ramadhani) afunge. Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi (atimize) hisabu
(ya siku alizowacha kufunga) katika siku nyingine. Allah anakutakieni yaliyo
mepesi wala hakutakieni yaliyo mazito, na pia (anakutakieni) kumtukuza Allah
kwa kuwa amekuongozeni, ili mpate kushukuru (185) Na waja wangu watakapo
kuuliza hakika yangu (waambie kuwa) Mimi niko karibu nao. Naitika maombi ya
mwombaji anaponiomba. Basi na waniitikie na waniamini, ili wapate kuongoka
(186) Mmehalalishiwa usiku wa Saumu kuingiliana na wake zenu. Wao ni (kama)
nguo kwenu (zilizokugandeni mwilini) na nyinyi ni (kama) nguo kwao. Allah
anajua kwamba mlikuwa mkizikhini nafsi zenu. Kwa hivyo amekukubalieni toba yenu
na amekusameheni. Basi sasa changanyikeni nao na takeni aliyokuandikieni Allah.
Na kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa Alfajiri katika weusi wa usiku.
Kisha timizeni Saumu mpaka usiku. Wala msichanganyike nao, na hali mnakaa
Itikafu msikitini. Hiyo ni mipaka ya Allah, basi msiikaribie. Namna hivi Allah
anabainisha hoja zake kwa watu ili wapate kumcha (187).” (Aya ya 183 – 187 ya
sura Al-Baqarah)
Na anasema
Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) :
( من صام
رمضان إيمانا واحتسابا غفر له ما تقدم من ذنبه ومن قام رمضان إيمانا واحتسابا ومن
قام ليلة القدر غفر له ما تقدم من ذنبه)
“Anaefunga Ramadhani hali yakuwa anaamini
(wajibu wa kufunga Mwezi huu na kuwa ni faradhi juu yake) na atarajia malipo
mazuri (kwa Allah) basi hughufiriwa madhambi yake (yote) yaliyopita, na
anaesimama (kusali Sala za usiku katika mwezi wa) Ramadhani hali ya kuwa
anaamini na atarajia malipo mazuri na anaesimama (kufanya ibada) usiku wa
Al-Qadri (Laylatul Qadri) hughufiriwa madhambi yake ( yote ) yaliyopita.”
Maana ya إيمانا
yaani anaamini kuwajibika kwa kitendo hicho alichokifanya (hapa ni
Saumu).
Maana
ya احتسابا yaani atiye niya kuwa anafanya kitendo
hichi kwa ajili ya Allah tu, atarajia kwa kitendo hicho thawabu yake tu bila ya
kuwa na lengo lingine.
Na iwapo
atachanganya niya hiyo pamoja na niya nyingine haitakuwa احتسابا kwa
mujibu ya kauli yake Subhanahu Wataala katika hadithi Qudusiy:
( من عمل عملا أشرك فيه غيري
فهو له، وأنا أغنى الشركاء )
“Mwenye
kufanya jambo akamshirikisha ndani yake mwengine asiye Mimi (Allah (Subhanahu
Wataala)) basi hilo (jambo) ni lake yeye
(huyo aliyeshirikishwa), na mimi sina haja na washirika.”
Hili ni
sharti la kwanza. Sharti la pili la kughufiriwa (anayefunga na anaye simama
usiku mwezi wa Ramadhani madhambi yake yote aliyoyafanya kabla) ni kuwa mwenye
kufunga na mwenye kusali usiku asiwe anaendelea kufanya dhambi kubwa katika
haki za Allah (Subhanahu Wataala) (kama kuacha kusali, kutoa Zaka au kunywa
pombe n.k) au kuwadhulumu waja wake kwani wako wanaofunga na kusali
Qiyamul-Leyl na hali bado wameshikilia kufanya madhambi makubwa na kuwadhulumu
waja wa Allah (binaadamu wenzao). Basi hadithi hiyo ya kughufuriwa madhambi
haimkhusu yeye kwa sababu hadithi hii siyo kwa kila anayefunga na kufanya ibada
usiku, kwani ikiwa hivyo itakuwa kinyume na itikadi ya Kiislamu iliyo sahihi.
Basi hili lizingatiwe.
Na katika
hadithi nyingine inayotoa dalili ya kuwajibika kwa Saumu ya Ramadhani ni ile
hadithi aliyoitoa Salman Al-Faarisiy R.A. amesema: Ametuhutubia Mtume
(Salallahu Alayhi Wasalam) katika siku ya mwisho wa Mwezi wa Shaabani akasema:
(يا أيها
الناس قد أظلكم شهر عظيم شهر مبارك شهر فيه ليلة خير من ألف شهر جعل الله صيامه
فريضة وقيام ليله تطوعا ومن تقرب فيه بخصلة من الخير كان كمن أدى فريضة ومن أدى
فريضة فيه كان كمن أدى سبعين فريضة فيما سواه، وهو شهر الصبر، والصبر ثوابه الجنة،
وشهر المواساة وشهر يزاد فيه رزق المؤمن، من فطر فيه صائما كان له مغفرة لذنوبه
وعتق رقبته من النار، وكان له مثل أجره من غير أن ينتقص من أجره شيء، قلنا يا رسول
الله ليس كلنا يجد ما يفطر به الصائم فقال رسول الله صلى الله عليه وسلم يعطي الله
هذا الثواب من فطر صائماً على مذقة لبن أو تمرة أو شرب من ماء، ومن أشبع صائما
سقاه الله من حوضي شربة لا يظمأ حتى يدخل الجنة وهو شهر أوله رحمة وأوسطه مغفرة
وآخره عتق من النار ومن خفف عن مملوكه فيه غفر الله له وأعتقه من النار )
“Enyi watu
umekukaribieni mwezi mtukufu, mwezi wenye baraka, mwezi ndani yake kuna usiku
ulio bora kuliko miezi elfu (yaani “Laiylatul Qadri”), Allah amejaalia kuufunga
(huo mwezi) ni faradhi na kusali Sala za usiku (Qiyamul-Leyl) jambo la
kujitolea kulifanya (lina malipo mazuri). Na anaejikaribisha kwa jambo la kheri
ni kama aliefanya faradhi. Na aliyefanya
faradhi katika mwezi huu ni kama aliyefanya
faradhi sabiini katika miezi mingine. Nao ni mwezi wa subira, na subira thawabu
yake ni Al-Jannah (Pepo) na ni mwezi wa maliwazo, mwezi inaongezwa ndani yake
riziki ya Muumini. Anaemfuturisha ndani yake mwenye kufunga hughufiriwa
madhambi yake na hukombolewa shingo yake (yaani yeye mwenyewe) kutoka Motoni na
hupata malipo kama malipo yake (huyo
aliyefuturishwa) bila ya kupungua kitu katika malipo yake. Tukasema ewe Mtume
wa Allah sio kila mmoja wetu anacho cha kumfuturishia aliyefunga. Akasema Mtume
(Salallahu Alayhi Wasalam): Allah anampa thawabu hii anaemfuturisha aliyefunga
kwa chubuo moja la maziwa au tembe ya tende au kinywaji cha maji na
anaemshibisha aliyefunga Allah atamnywesha katika Hodhi langu kinywaji ambacho
(kitamfanya) hatapata kiu mpaka aingie Peponi. Na ni mwezi ambao mwanzo wake ni Rehema na kati
kati yake ni Maghufira na mwisho wake ni kukombolewa na Moto na yule
anaempunguzia mtumwa wake (kazi), Allah humghufiria na kumkomboa na Moto”.
Sababu ya
kuileta hadithi kwa kirefu ni kupata faida na huenda Allah (Subhanahu Wataala)
akajaalia (miongoni mwa wasomaji) atakayetekeleza yaliyomo humo na nitapata
mimi sehemu katika hayo malipo kwa sababu anayeionesha kheri ni kama yule aliyeifanya kheri hiyo.
Amesema
Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) :
( إن الله
يباهي ملائكته بالشاب العابد فيقول : أيها الشاب التارك شهوته من أجلي المبذل
شبابه لي أنت عندي كبعض ملائكتي )
“Hakika
Allah huwasifia Malaika wake kijana mwenye kufanya Ibada husema: Ewe kijana,
aliyeacha matamanio yake kwa ajili yangu, anaeutumia ujana wake kwangu mimi,
wewe kwangu mimi ni kama baadhi ya Malaika
wangu”.
Unakutosha
ufahari ewe unaefunga kuwa mstari mmoja na Malaika. Sababu ya kuhusishwa vijana
katika kutajwa bila ya wazee kwa kuwa mzee yuko karibu zaidi na utiifu (hana
matamanio makubwa yanayomzuia kufanya Ibada kama kijana) na inasemekana
anayefika miaka arubaini na yungali hajaacha maasi basi huyo yuko karibu na
ghadhabu ya Allah ndio maana unaona kuhimizwa kwa kijana ni zaidi kuliko mzee
kwani yeye ndio sasa anayakabili maisha ama mzee anayapa mgongo. Allah (Subhanahu
Wataala) asema:
ﭽ ﰓ ﰔ
ﰕ ﰖ ﰗ
ﰘ ﭼ
الزمر: ١٠
“Bila shaka wafanyao subira
(wakajizuilia na maasi na wakaendelea na taa) watapewa ujira wao bila ya
hisabu”.
Yaani
wafanyao subira katika kumtii Allah na kujizuia na kumuasi na kusubiri katika
misukosuko na mitihani anayoipata mja. Na anasema Mtume (Salallahu Alayhi
Wasalam):
(الصبر
نصف الإيمان)
“Subira ni nusu ya
Imani”
Na amesema
Salallahu Alayhi Wasalam:
(لكل شيء باب وباب العبادة الصوم)
“Kila kitu
kina mlango na mlango wa Ibada ni Saumu”
Na katika
hadithi Qudusiy:
(كل حسنة بعشرة أمثالها إلى
سبعمائة ضعف إلا الصيام فإنه لي وأنا أجزي به إنما يذر شهوته وطعامه وشرابه لأجلي
، الصوم لي وأنا أجزي به)
“Kila jambo jema hulipwa (ujira) mara kumi hadi mara mia saba
isipokuwa Saumu kwani hiyo ni yangu na mimi nitailipia. Bila ya shaka yeye huacha matamanio yake na chakula
chake na kinywaji chake kwa ajili yangu Mimi. Saumu ni yangu na mimi
nitailipia.”
Amesema
Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) :
(إذا
دخل رمضان فتحت أبواب الجنة وغلقت أبواب جهنم وسلسلت الشياطين)
“Ikiingia
Ramadhani inafunguliwa milango ya Pepo (Al-Jannah) na yafungwa milango ya Moto
(Jahannam) na mashetani hufungwa kwa minyororo.”
Amesema
Salallahu Alayhi Wasalam:
( للصائم فرحتان فرحة عند فطره
وفرحة عند لقاء ربه ولخلوف في الصائم أطيب
عند الله من ريح المسك والصيام جنة فإذا كان يوم صوم أحدكم فلا يرفث، و لا يصخب،
فإن سابه أحد أو قاتله فليقل إني امرؤ صائم )
“Anaefunga
ana furaha mbili: furaha wakati anapofuturu na furaha wakati anapo kutana na
Mola wake. Na harufu ya mdomo wa mwenye kufunga inanukia zaidi kwa Allah kuliko
harufu ya miski. Na Saumu ni kinga, basi siku akiwa mmoja wenu amefunga asiseme
maneno mabaya wala asipige makelele na akimtukana mtu yeyote au akapigana naye
basi na aseme mimi nimefunga.”
Yamekuja
mahadharisho (maonyo) kwa aharibuye Saumu yake katika Aya chungu nzima na
katika hadithi nyingi. Kati ya hadithi hizo kauli ya Mtume (Salallahu Alayhi
Wasalam) :
(من
لم يدع قول الزور والعمل به فليس لله حاجة في أن يدع طعامه وشرابه)
“Asiewacha
kusema uwongo na kuutumia (uwongo) basi Allah hana haja kwa mtu huyo kuacha
chakula chake na kinywaji chake.”
Unaona kwa
uhakika kuwa Allah hataki mja wake akae na njaa na kiu bila ya sababu bali
analolitaka kwake ni kuzuia matamanio ya viungo vyake.
Saumu
imegawika vifungu vinne:
Saumu iliyo
wajibu (faradhi).
Saumu iliyo
haramu.
Saumu iliyo
himizwa.
Saumu iliyo
makruhu.
Saumu ya
Mwezi wa Ramadhani, Saumu ya nadhiri, Saumu ya kaffara, nazo ni: kaffara ya
kuuwa, kaffara ya “Dhihar” (mume kumwambia mkewe: wewe kwangu ni kama mgongo wa
mama yangu basi anaharimika kwake mpaka atoe kaffara), Kaffara ya “Iilaau”
yaani mwanamme kuapa kuwa hatamwingilia mkewe basi hatoweza kumuingilia mpaka
atoe kaffara, kaffara ya kwenda kinyume na kiapo chake, vile vile Saumu ya
(anayehiji) Attamatuu kwa yule asieweza kumiliki kuchinja. Kirefu cha haya
kitapatikana katika vitabu vya Fiqhi.
Kufunga
katika Idi mbili (Al-Fitri na Al-Adh-haa), kufunga kwa aliye katika hedhi na
ujusi (kwa mwanamke) na kufunga siku ya shaka, nayo ni tarehe 30 thelathini
Shaabani haifungiwi siku hii ili isiongezeke siku katika Ramadhani kutoka mwezi
mwengine. Kama ilivyosemwa kutokana na Ikrima R.A. na Ammar R.A. wamesema:
Aliyefunga siku inayotiliwa shaka basi amemuasi Aba Al-Qasim (Mtume -rehema za
Allah na amani zimshukie-) bali anapendelewa ajizuie na vinavyofunguza siku
hiyo mpaka katikati ya mchana huenda ikaja habari ya kuonekana mwezi aendelee
na funga yake, lakini juu ya hivyo hapana budi kuilipa siku hiyo kwa sababu
hakuiamkia kuwa ana hakika kamili kuwa ni Ramadhani, na katika sharti ya Saumu
kuwa atiye niya ya uhakika tokea usiku.
Saumu ya
Ashuraa (siku ya kumi ya Muharram) na aongeze kufunga siku moja kabla yake au
siku baada yake ili kuwahalifu (kwenda kinyume) mayahudi na manasara kwa sababu
wao waitukuza siku hii kwa kuifunga, vile vile inahimizwa kufunga siku ya Arafa
kwa mujibu wa kauli ya Mtume (Salallahu Alayhi Wasalam) :
(صوم يوم عرفة يكفر سنتين ماضية ومستقبلة وصوم يوم عاشوراء يكفر سنة
ماضية)
“Saumu katika siku ya Arafa
hufuta (madhambi ya) miaka miwili uliopita na unaokuja, na Saumu katika siku ya
Aashuraa hufuta madhambi ya mwaka uliopita.”
Inapendelewa
vile vile kufunga siku tatu, “Ayyaam Beiydh” nazo ni tarehe 13, 14 na 15 katika
kila mwezi wa Hijri (mwezi wa Kiislamu) isipokuwa tarehe 13 katika mwezi Dhul
Al-Hijja kwa sababu ni katika siku za “Attashriq”. Amesema Mtume Salallahu
Alayhi Wasalam:
( من صام
في كل شهر ثلاثة أيام فكأنه صام الدهر كله )
“Anaefunga
katika kila mwezi siku tatu basi kama
aliyefunga zama zote (milele).”
Pia
inapendelewa kufunga siku sita katika Shawwaal kwa mujibu wa kauli yake Mtume
Salallahu Alayhi Wasalam:
( من صام رمضان ثم أتبعه بستة أيام من شوال فكأنه صام الدهر كله )
“Anaefunga Ramadhani kisha
akaifuatiliza kwa (kufunga) siku sita katika Shawwaal basi kama
kwamba amefunga milele”.
Inahimizwa
kufanya Itikaaf mwisho wa Ramadhani. Na ifanywavyo ni kuingia msikiti
unaosaliwa jamaa kabla ya kutuwa jua usiku wa tarehe 21 Ramadhani, afanye hivyo
kwa ajili ya kutaka radhi ya Allah Subhanahu Wataala na kutarajia malipo yake
bila ya kuwa na kusudio lingine na ajifunge nafsi yake msikitini humo kwa
kufanya ibada na asitoke humo isipokuwa kwa kwenda kusali Sala ya Idi. Hivi
ndivyo ilivyokuwa Sunna. Anaetaka kufanya Itikaaf chini ya muda huo na atiye
niya kwa mujibu wa siku anazotaka kukaa
Iitikaaf, na haitakiwi kubadilisha niya hiyo wakati yuko msikitini katika Itikaaf
wala asijishughulishe na mambo ya Dunia isipokuwa yaliyo dharura kama kwenda kukidhi haja au kwenda kula ikiwa hawezi kula
msikitini.
Akifanya
Itikaaf katika wakati usiokuwa Ramadhani basi ni sharti afunge. Na kufanya
Itikaaf katika Ramadhani na hasa katika kumi la mwisho kuna mambo ya kheri
Allah huyaleta katika wakati huu na asaa (huenda) akafanikiwa kuipata Laiylatul
Qadri. Mtume Salallahu Alayhi Wasalam alifanya Itikaaf katika mwanzo wa mwezi
wa Ramadhani na katikati yake na mwisho wake na hii ndio ilikuwa amali yake ya
mwisho Salallahu Alayhi Wasalam. Na Masahaba walikuwa wakichukuwa kwa Mtume
Salallahu Alayhi Wasalam vitendo vyake vya mwisho mwisho (hawachukuwi vya
zamani bali wachukuwa vipya). Na alikuwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam
akifunga zaidi katika mwezi wa Shaabani (mbali na mwezi wa Ramadhani) lakini ni
lazima afungue siku mbili za mwisho wa Shaabani asiziunganishe na Ramadhani
kutokana na kukataza kwake Salallahu Alayhi Wasalam kuiunganisha Ramadhani na
mwezi mwengine.
Saumu
iliyo makruhu:
Ni Saumu ya
siku za “Attashriq” nazo ni siku tatu zinazofuatia Idi Al-adh-ha (Idi kubwa)
kwa sababu hizo ni siku ambazo Allah Subhanahu Wataala anawafanyia “dhiyafa”
(anawakaribisha na kuwakirimu) waja wake kwa hiyo haifai kuikataa dhiyafa yake.
Na zimeitwa ayyam “attashriiq” kwa sababu huanikwa nyama juani siku hizo. Na
vile vile ni makruhu kufunga siku moja au mbili kabla ya Ramadhani ili
zisiungane nayo, na pia kufunga siku ya Ijumaa peke yake isipokuwa kama
ikitanguliwa na siku au ikifuatiliwa na siku kwa sababu wamesema kuwa Ijumaa ni
Idi na haifai kufunga siku ya Idi.
Amesema
Shekhe wetu Noor Diin Allah Amrehemu kuwa tofauti iliopo baina ya Idi na siku
ya Ijumaa kuwa imekubaliwa na wote kwamba ni haramu kufunga siku ya Idi hata
ikatanguliwa kufungwa siku moja au ikafatiliwa na siku moja, ambalo ni kinyume
ya siku ya Ijumaa, kwani imekubaliwa na wote kwamba inaruhusiwa kufunga siku ya
Ijumaa ikiwa itatanguliwa au ikafatiliwa na kufunga siku moja. Vile vile katika
Saumu iliyo makruhu kufunga milele.
Amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam:
(لا صام
من صام الأبد)
“Hajafunga mwenye kufunga milele”
Na kauli yake aliyomwambia Abdullah bin Omar:
(صم صيام
داود : كان يصوم يوما ويفـطر يوماً، ولا يفـر إذا لاقى)
“Funga Saumu ya Dawood alikuwa afunga siku na afungua siku, na hakuwa
akikimbia akutanapo (na adui).”
Aliambiwa hivyo wakati aliposhikilia ombi lake la kutaka kufunga milele
akamnasihi Salallahu Alayhi Wasalam asifanye hivyo na akamwambia:
( صم وأفطر وقم ونم، فإن لعينيك عليك حقا وإن لنفسك وأهلك عليك حقا )
“Funga na ufungue
(siku nyingine funga siku nyingine usifunge), usimame (kwa kufanya Ibada) na
ulale, kwani jicho lako lina haki juu yako na nafsi yako na watu wako (mke na
watoto wako) wana haki juu yako”
Na katika
hadithi nyingine “wana fungu kwako”.
Vile vile katika
Saumu iliyo makruhu ni Saumu ya msafiri akiwa amedhoofika hata akawa hawezi
kufanya yale yaliyomuwajibikia kuyafanya, kama
alivyofanya Mtume Salallahu Alayhi Wasallam katika baadhi ya vita vyake
alipoona uchofu umedhihiri kwa masahaba zake kutokana na kufunga basi
akawaamrisha wafungue kwa kuwaonea huruma. Kwa hiyo msafiri amepewa ruhusa ya
kufungua na hiyo ni Rehema ya Allah Subhanahu Wataala juu ya waja wake.
Saumu kwa
ujumla ni kheri na ina fadhila kubwa isipokuwa kwa zile siku zilizokatazwa
kufunga kwa mujibu wa kauli yake Salallahu Alayhi Wasalam:
(لكل شيء زكاة وزكاة الجسد الصوم)
“Kila kitu kina Zaka na Zaka ya kiwiliwili ni Saumu.”
Na katika
kauli yake Salallahu Alayhi Wasalam:
( من صام يوماً ابتغاء وجه
الله أبعده الله من جهنم كبعد غراب طائر وهو فرخ حتى مات هرما )
“Anaefunga
siku moja kwa kutaka kumridhisha Allah (tu peke yake) basi Mola humuweka mbali
na Jahannam kama umbali wa kunguru anaeanza
kuruka yu hali kinda mpaka anapokufa naye amekonga”.
Hadithi
mbili hizi zimetolewa na Abu Huraira. Na katika hadithi:
(الشتاء
ربيع المؤمن طال ليله فقام وقصر نهاره فصام)
“Msimu wa
baridi ni faida kwa mwenye kuamini: usiku wake ni mrefu na kwa hiyo hupata
kusimama (usiku kufanya ibada) na mchana wake ni mfupi na kwa hiyo hufunga.”
Imefaridhishwa
Saumu ya Ramadhani katika mwaka wa pili wa Al-Hijra na zikafutwa faradhi zote
za Saumu zilizokuwepo kabla ya hapo. Na haisihi Saumu isipokuwa kwa kutia niya
tokea usiku kuamkia ile siku atakayofunga. Kwa hiyo mwenye kumtokea Al-Fajiri
kisha akatia niya ya kufunga asubuhi basi huyo atakuwa hana Saumu. Na mwenye
kumtokea Al-Fajiri na ana janaba tokea usiku naye hakuoga janaba basi huyo hana
Saumu kwa mujibu wa kauli yake Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :
)من أصبح جنبا أصبح مفطرا(
“Anaeamka asubuhi na hali ya kuwa ana janaba ameamka amefungua”
Na hadithi nyingine:
( كان
رسول الله صلى الله عليه وسلم يصبح جنبا من جماع غير احتلام )
“Alikuwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam anaamka asubuhi na hali
yakuwa ana janaba ya jimai wala sio (janaba) ya kuota.”
Hii ni
Sunna ya kitendo na ile hadithi ya kwanza ni sunna ya kauli. Na sunna ya kauli
inatangulizwa kabla ya sunna ya kitendo kwa uwezekano wa kuwa sunna ya kitendo
ni katika mambo yanayomhusu yeye Mtume Salallahu Alayhi Wasalam peke yake.
Na katika
mambo yanayopasa kuyajua kuwa wakati zikutanapo tupu mbili basi imekwisha patikana janaba na inapasa
kujiosha nayo, iwapo imetoka manii au haikutoka wala mtu asilifanyie jambo hilo upuuzi akafikiria
madamu haikumtoka manii basi haimlazimikii kuoga janaba sivyo hivyo imekuja
sunna ya Mtume Salallahu Alayhi Wasalam kuamrisha kuoga:
( إذا
التقى الختانان وجب الغسل أنزل أو لم ينزل )
“Zikiingiana tupu mbili hadi
zikakutana sehemu zao zinazotahiriwa, kuoga kwawajibika iwapo yametoka manii au
hayakutoka”
Na anaepata
janaba usingizini na asijuwe mpaka mchana huyu Saumu yake sahihi ikiwa
ataharakisha kwenda kuoga wakati atakapotanabahi na wala asifanye kitu cho
chote kabla ya kuoga, lakini akijichelewesha na kufanya mambo mengine kuna
wasiwasi ya kuharibika Saumu yake.
Saumu iliyo
sahihi ni ile iliyofanywa kwa mujibu inavyotakiwa katika sheria.
Na
inavyotakiwa ni ifuatavyo:
Ni kuwa na
adabu na kutekeleza amri za Dini tukufu na hivyo ni kuizuia nafsi na matamanio
yaliyo dhahiri na yaliyofichika. Kuuzuiya ulimi usiudhi wengine kama kuwasengenya, kuwafitinisha, kuwatukana na maneno
machafu yanayokera watu bila ya haki. Na vile vile kuzuia macho yake yasitizame
yaliokuwa hayafai kutazama na atie niya ya kufunga tokea usiku kabla ya kutoka
Al-Fajiri. Wala asiseme kama wasemavyo wasiojuwa kuwa Al-Fajiri ni ile
Al-Fajiri iingiayo majumbani; hilo ni kosa kubwa kwani huo ni katika wakati wa
mchana na aendelee kuwa na niya yake ya kufunga mpaka kuzama jua (kutua) kuzama
kwa kweli siyo likizama jua nyuma ya mlima au likifunikwa na wingu au kiza. Na
katika kipindi hichi ajizuie na kula, kunywa na kuingiliana na kufanya maasi na
awe anajishughulisha na kumtaja Allah Subhanahu Wataala huku akifanya
yaliyomuwajibikia katika mambo ya faradhi, asiingize tumboni kitu cho chote
kikiwa chakula au kingine, yote hayo ayafanye kwa kutaka radhi ya Mola Subhanahu
Wataala peke yake sio kwa lengo lingine.
Awe na
Imani kuwa hii ni fardhi amemuamrisha Allah Subhanahu Wataala kuifanya na yeye
huifanya bila ya kuuliza kwa nini ameamrishwa kufunga kwani yeye ni mja
anafuata aliyoamrishwa na Mola wake kwa utiifu mkubwa ikiwa amependa au
hakupenda. Na akipenda (akiridhia) atapewa thawabu na hatahasirika kwa
aliyoyafanya na ataadhibiwa kwa kutoridhia amri ya Allah Subhanahu Wataala :
ﭽ ﭑ ﭒ ﭓ
ﭔ ﭕ ﭖ
ﭗ ﭘ ﭙ
ﭚ ﭛ ﭜ
ﭝ ﭞ ﭟ ﭠﭡ ﭢ ﭣ
ﭤ ﭥ ﭦ
ﭧ ﭨ ﭩ ﭼ
الأحزاب: ٣٦
“Haiwi kwa
mwanamme aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Allah na Mtume wake
wanapokata shauri, wawe na hiari katika shauri yao , na mwenye kumuasi Allah na Mtume wake,
hakika amepotea upotofu ulio wazi (kabisa).”
Na Allah Subhanahu
Wataala hana haja ya kuwakalifisha waja wake na wala hana haja ya vitendo vyao
bali amewakalifisha kufanya vitendo hivyo kwa maslaha yao wenyewe na hakuna ajuaye maslaha hayo
isipokuwa yeye Subhanahu Wataala.
ﭽ ﭳ ﭴ ﭵ
ﭶ ﭷ ﭸ ﭹ ﭺ
ﭻ ﭼ ﭽ
ﭾ ﭿ ﮀ
ﮁ ﮂ ﮃ
ﮄ ﮅ ﮆ
ﮇ ﮈ ﮉ
ﮊ ﮋ ﭼ
الذاريات: ٥٦ - ٥٨
“Si
kuwaumba Majini na Watu ila wapate kuniabudu. Sitaki kwao riziki wala sitaki
wanilishe. Kwa yakini Allah ndiye mtoaji wa riziki, Mwenye nguvu, Madhubuti”.
Na hakutaka
Allah Subhanahu Wataala kwa kuwaamrisha waja wake wafunge ili wapate njaa na
kiu tu bali ametaka waingiwe na adabu na wapate faragha ya kumkumbuka yeye Subhanahu
Wataala wakati wanapokuwa na njaa na kiu na wajue kuwa hawakupata njaa na kiu
isipokuwa kwa kutaka radhi za Allah na malipo mema kutoka kwake. Anaetaka radhi
za Allah basi na aitafute katika kila kitu iwapo katika kutekeleza amri zake au
kuacha kufanya aliyoyakataza.
Na katika
kufunga ni kufuata mfano wa Malaika AS kwani wao hawali wala hawanywi. Na
inavyotakiwa mwenye kufunga usichoke ulimi wake kumtaja Allah Subhanahu Wataala
na kusoma Qur’ani, na Muumini akimdhukuru sana
Allah kwenye neema basi humsaidia akiwa na shida.
ﭽ ﮘ ﮙ ﮚ
ﮛ ﮜ ﮝ ﮞ ﮟ
ﮠ ﮡ ﮢ
ﮣ ﮤ ﭼ
الأنبياء: ٨٧
“Basi
(alipozongwa) aliita katika kiza (akasema): ‘Hakuna aabudiwaye isipokuwa wewe,
mtakatifu, hakika mimi nilikuwa miongoni mwa wenye kudhulumu nafsi zao’.”
Na hicho
kiza ni kiza cha tumbo la nyangumi, kiza cha bahari na kiza cha usiku, basi
wakasikia Malaika AS sauti yake na jinsi walivyokuwa wameizoea
sauti yake waliitambua. Wakasema: Ewe Mola wetu twaisikia sauti ijulikanayo
katika mahala pageni. Akawambia Mola wao Subhanahu Wataala sauti hiyo ni ya mja
wangu Yunus, basi hapo Malaika wakamuombea msamaha na uokozi na Allah Subhanahu
Wataala akamuokoa.
ﭽ
ﮦ ﮧ
ﮨ ﮩ ﮪﮫ
ﮬ ﮭ ﮮ ﭼ
الأنبياء: ٨٨
“Basi tukampokelea na tukamuokoa katika huzuni
ile. Na namna hivyo ndivyo tuwaokoavyo walioamini”.
Inasemekana
kuwa alitoka bila ya ngozi na akaudhiwa na nzi basi Allah Subhanahu Wataala
akamuoteshea mti wa “Al-yaqtiin” ambao una siri fulani, hausogelewi na nzi.
Katika hadithi Al-Qudsiy:
( من
دعاني في الرخاء أجبته في الشدة )
“Anaeniomba katika neema
(raha) basi humpokelea (anaponiomba) katika shida”
Na ibada
zote zamfaa mtu katika shida kama ilivyozungumzwa juu ya watu wa Arraqiim
(wenye habari zile zilizoandikwa vitabuni) ambao Allah amewataja katika sura ya
Al-Kahf kuwa wao watatu waliingia pangoni katika mlima basi likaanguka jiwe na
kuliziba hilo
pango waliokuweko na kwa hivyo hawakuweza kutoka wakajiogopea wasiangamie humo.
Wakazikimbilia amali zao nzuri walizozifanya kabla ya hapo (ziwafae katika
shida hiyo). Wakaambiana wenyewe kwa wenyewe: kila mmoja wenu aitaje amali yake
njema ili ajikaribishe nayo kwa Allah Subhanahu Wataala na huenda akatupa faraja.
Hapo akasema mmoja wao: Ndio nilikuwa na binti ammi yangu na nikamtaka afanye
zina nami na baada ya kumuomba sana na yeye kutoa ahadi nyingi sana mwisho
nikafanikiwa kumpata na wakati nilipomkalia mkao wa mwanamme anapotaka kumjamii
mwanamke nikamuacha (nisizini naye) kwa kumuogopa Allah. Ewe Mola ikiwa unajua
kuwa niliacha kufanya yale machafu kwa ajili yako wewe basi tuokoe (na hilaki
hii) basi hapo lile jiwe likasogea kadiri ya kuwa waliweza kuona muangaza.
Akasema wa
pili: Ndio nilikuwa na wazee wangu wawili wamekonga (umri wao mkubwa) na
nilikuwa nawanywesha maziwa ukifika usiku, lakini usiku mmoja nilichelewa kuja kuwaletea
maziwa nipate kuwanywesha nikawakuta wamekwisha lala nikaona tabu kuwaamsha
basi nikakaa nawangojea kando yao na huku maziwa nimeyashika mkononi, kwa
sababu niliogopa kuwa nikiondoka hapo wakiamka hawataniona, nikiwa katika hali
hiyo mpaka kukapambazuka Ewe Mola ikiwa unajua kuwa sikufanya kitendo hichi
isipokuwa kwa ajili yako wewe tu basi tuokoe na janga hili. Na hapo, lile jiwe
likasogea kidogo lakini bado wakawa hawawezi kutoka kwenye huo upenyu.
Akasema
yule wa tatu: Ndio nilikuwa na vibarua wakinifanyia kazi na mmoja wao aligoma
kuchukua ujira wake akenda zake basi nikaukuza huo ujira mpaka ukawa mali
nyingi halafu baada ya kupita muda mrefu akanijia naye kashikwa na haja
akanitaka nimpe ule ujira wake aliougomea kuuchukua hapo nikampa ile mali
nyingi (nilioikuza) nikamwambia: haya ni maendeleo ya mali yako ichukue basi
hakusadiki mpaka nikamhakikishia ukweli wa hayo. Ewe Mola ikiwa unajua kuwa
amali hii nimeifanya kwa ajili yako tu basi tuokoe na balaa hii, likasogea lile
jiwe kisha wakatoka. Basi hii ndio siri (faida) ya utiifu. Na Kitabu cha Allah
kinahakikisha hayo katika kauli yake:
ﭽ ﮚ
ﮛ ﮜ ﮝ
ﮞ ﮟ ﭼ الطلاق:
٢
“Na anayemwogopa Allah,
(Allah) humtengenezea njia ya kuokoka (katika kila balaa)”
ﭽ ﯱ ﯲ
ﯳ ﯴ ﯵ
ﯶ ﯷ ﯸ ﭼ الطلاق: ٤
“Na
anayemwogopa Allah, (Allah) humfanyia mambo yake kuwa mepesi.”
Na ni katika
sunna kusali “Qiyamul-layl” nayo ni sala ya “taraweeh” na sala ya usiku wa
manane (Sahar) katika mwezi wa Ramadhani. Na juu ya “Qiyamul-layl” na fadhila
yake zimekuja hadithi nyingi na zikatiliwa nguvu na Qurani Tukufu kwa kauli
Yake Taala:
ﭽ ﮌ ﮍ
ﮎ ﮏ ﮐ
ﮑ ﮒ ﮓ
ﮔ ﮕ ﮖ ﭼ الذاريات: ١٧ - ١٨
“Walikuwa
wakilala kidogo tu usiku. Na wakiomba maghufira (msamaha) nyakati za kabla ya
Al-Fajiri”.
Anasema
Al-Baidhaawiy: Kama kwamba wamekesha wajikumbusha makosa yao (na kuomba maghufira). Na kauli yake Subhanahu
Wataala:
ﭽ ﮔ ﮕ
ﮖ ﮗ ﮘ
ﮙ ﮚ ﮛ
ﮜ ﮝ ﮞ
ﮟ ﮠ ﮡ
ﮢ ﮣ ﮤ
ﮥ ﮦ ﮧ
ﮨ ﮩ ﮪ
ﮫ ﮬ ﮭ ﭼ
السجدة: ١٦ - ١٧
“Huinuka mbavu zao kutoka vitandani wakati wa
usiku ili kumuabudu Mola wao kwa kuogopa Moto na kutaraji Pepo; na hutoa (Zaka
na Sadaka) katika yale tuliyowapa. Nafsi yoyote haijuwi waliyofichiwa katika
hayo yanayofurahisha macho huko Peponi ni malipo ya yale waliyokuwa
wakiyafanya”.
Na alikuwa
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam asimama usiku (kusali) mpaka miguu yake yavimba,
akaambiwa: unafanya hayo na Allah amekwisha kughufiria madhambi yako yaliyopita
na yajayo. Akajibu : Je nisiwe mja mwenye kushukuru. Na akahimiza Salallahu
Alayhi Wasalam kusali usiku akasema:
( عليكم
بقيام الليل فإنه دأب الصالحين قبلكم ومقربة إلى ربكم ومكفرة للسيئات ومنهاة عن الإثم
ومطردة للداء من الجسد )
“Shikilieni kusali
Sala za usiku kwani hiyo ni tabia (ada) ya watu wema walio kabla yenu na
kikurubisho kwa Mola wenu na kifutio cha madhambi yenu na kizuio cha makosa na
kinafukuza maradhi mwilini”.
Na amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :
( أقرب ما يكون الرب من العبد
في جوف الليل الأخير فإن استطعت أن تكون ممن يذكر الله في تلك الساعة فكن )
“Wakati
anaokuwa Mola karibu sana
na mja wake ni katika sehemu ya mwisho ya usiku (theluthi ya mwisho ya usiku)
basi ukiweza kuwa miongoni mwa wanaomtaja Allah katika wakati huo basi kuwa
(katika hao).”
Na alikuwa
Salallahu Alayhi Wasalam anasema akiamka usiku (kufanya Ibada):
( اللهم لك الحمد أنت نور السموات
والأرض ولك الحمد أنت قيوم السموات والأرض ولك الحمد أنت رب السموات والأرض ومن
فيهن أنت الحق وقولك الحق ووعدك الحق ولقاؤك الحق والجنة حق والنار حق والساعة حق
والنبيون حق ومحمد صلى الله عليه وسلم حق اللهم لك أسلمت وبك آمنت
وعليك توكلت وفيك خاصمت وإليك حاكمت فاغفر لي ما قدمت وأخرت وما أسررت وأعلنت أنت
المقدم وأنت المؤخر وأنت على كل شيء قدير لا إله إلا أنت ولا حول ولا قوة إلا
بالله )
Na baada ya
kusoma Dua hii hupangusa macho yake na kutizama mbinguni huku akisoma Aya kumi
za mwisho za sura ya Al-Imraan.
Amefuzu
mwenye kumuiga Mtume Salallahu Alayhi Wasalam katika harakati zake na kutulia
kwake na maneno yake na vitendo vyake. Na uongofu wote uko katika kumfuata Muhammad
Salallahu Alayhi Wasalam.
Vile vile huitwa “Fitrat Al-abdaan”
na “Zakaat Al-abdaan” na ni sunna iliyotiliwa mkazo kwa kauli yake Mtume
Salallahu Alayhi Wasalam:
( زكاة الفطر على الغني والفقير
من المسلمين أما الغني فيزكيه الله وأما الفقير فيرد الله عليه أكثر مما أعطى)
“Ni juu ya
tajiri na fakiri katika Waislamu kutoa Zakaa ya Fitri, ama tajiri Allah
humsafisha na ama fakiri Allah humrudishia zaidi kuliko alivyotoa.”
Na mafakiri
miongoni mwa Masahaba RA walikuwa wakiipokea kisha hutoa kwa niaba ya nafsi
zao.
Na alikuwa
Imam Al-Khalily Radhi ya Allah iwe juu yake, alikuwa akiwaamrisha wanafunzi
waipokee kisha waitoe kwa niaba ya nafsi zao na alikuwa mmoja wao aipokea
kutoka kwa ndugu yake kisha humpa mwingine na huenda akapewa mara nyingine na
ikabakia kwake.
Na ulimjia
mwaka Imam Salim bin Rashid Al-Kharusiy, Radhi ya Allah iwe juu yake, akawa
hana kitu cha kutoa Zakaa ya Fitri kwa hiyo akapeleka nguo yake sokoni kuuzwa
na ikanunuliwa thamani yake chakula cha Fitri na akabakia yeye ataabika kwa
baridi (alikuwa hana nguo nyingine ya kuvaa). Kisa hichi kimefanana mno na
jinsi alivofanya Mtume Salallahu Alayhi Wasalam wakati alipotoa nguo yake kumpa
aliekuja kuomba akabakia nyumbani hana nguo nyingine ya kutokea.
Na Zaka
Al-Fitri inamlazimu Muislamu kujitolea nafsi yake na kuwatolea wote walio chini
ya maangalizi yake kama mtoto, mke na mtumwa. Anamtolea
kwa kila mmoja pishi ya chakula alichokuwa akila katika Ramadhani (na pishi
inakadiriwa uzito wa kilo 2.05 [mbili na gramu 50]). Na wakati unaotolewa hiyo
Zakaa ni baina ya Sala ya Al-Fajiri na Sala ya Idi kwa mujibu wa kauli yake
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :
(أغـنوهم
هذا اليوم عن السؤال)
“Watoshelezeni siku hii wasiombe”
Na
imehimizwa kutoa sadaka kwa wingi na hasa katika mwezi wa Ramadhani na bora
kuwapa jamaa zako wa karibu na jirani zako.
Alikuwa
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam ukiingia mwezi wa Ramadhani huzidi kuwa karimu
kuliko upepo uliotumwa. Na kumpa sadaka ndugu yako katika Dini ni bora kuliko
mwingine (kumpa sadaka Muislamu mcha Mungu ni bora kuliko kumpa mwengineo).
(سبحان الله والحمد لله والملك
لله والعظمة لله والكبرياء لله ولا إله إلا الله والله أكبر عدد خلقه وزنة عرشه ومداد
كلماته ورضا نفسه وكما ينبغي له وكما هو له أهل لا ينقطع ولا ينفد من أزل الأزل إلى أبد الأبد وصلى الله على
سيدنا محمد وعلى آله وصحبه وسلم )
Dua ya kwanza:
( اللهم إنا
لك نعبد ولك نركع ونسجد وإياك ندعو ونحمد آمنا بك نرجو رحمتك ونخشى عذابك إن عذابك
كان محذوراً اللهم يا فارق الفرقان ومنزل
القرآن خالق الإنسان عالم السر والإعلان بارك اللهم لنا وللمسلمين في صوم شهر
رمضان وأعنا فيه وفي غيره على الصلاة والصيام والقيام وعلى تلاوة القرآن واقطع عنا
حزب الشيطان وزحزحنا عن النيران وامنن علينا بالتوبة والغفران والقبول والرضوان
وحبب اللهم إلينا الإيمان وزينه في قلوبنا وكره إلينا الكفر والفسوق والعصيان
وأسكنا اللهم الجنان وزوجنا فيها من الحور العين الحسان وآتنا من كل فاكهة زوجين
في دار السلام بمنك وفضلك وجودك وكرمك وإحسانك ولطفك يا ذا الجلال والإكرام )
Dua ya pili:
( اللهم اقسم لنا من خشيتك ما
تحول به بيننا وبين معصيتك ومن طاعتك ما يبلغنا رحمتك ومن اليقين بك ما يهون علينا
مصائب الدنيا ومتعنا بأسماعنا وأبصارنا واجعل ذلك الوارث منا وانصرنا على من ظلمنا
وعادانا ولا تجعل مصيبتنا في ديننا ولا تجعل الدنيا أكثر همنا ولا مبلغ علمنا
اللهم إنا نسألك فعل الخيرات وترك المنكرات وحب الصالحات ورحمة المساكين فإذا أردت
بعبادك فتنة فاقبضنا غير مفتونين )
No comments:
Post a Comment
Note: only a member of this blog may post a comment.