الروم: ٢١
"Na katika Ishara Zake(za
kuonyesha ihsani zake juu yenu) ni kuwa Amekuumbieni wake zenu katika jinsi
yenu ili mupate utulivu kwao, naye Amejaalia baina yenu mapenzi na kuoneana
huruma. Bila shaka katika
haya zimo ishara kwa watu wanaofikiri". Aya ya 21 katika Sura Ar-Rum.
Ndoa ni Sunna iliyomo katika sharia ambayo
imesisitizwa na Qurani Takatifu na Sunna ya Mtume -rehema za Allah na amani
zimshukie- Amesema Allah Subhanahu Wataala katika aya ya 3 Sura An-Nisaa:
النساء: ٣
“Basi oeni mnaowapenda katika
wanawake,(maadamu mtawafanyia insafu) wawili au watatu au wane. Na mkiogopa
kuwa hamwezi kufanya uadilifu basi oeni mmoja tu. Au wekeni masuria wale ambao mikono yenu ya kuume imewamilika”.
Sunna imekuja katika kauli na vitendo vyake Mtume
-rehema za Allah na amani zimshukie. Kitendo ni kuowa kwake -rehema za Allah na
amani zimshukie- tokea alipokuwa umri wake miaka ishirini na tano mpaka kufa
wake. Alioa wake wengi. Amemhalalishia Allah Subhanahu Wataala wake aliotaka
kuoa bila ya kumuwekea kikomo(idadi ya wake)
fulani na amekufa na hali ana wake tisa.
Amehimiza Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- umma wake kuowa
katika kauli yake:
( إذا خطب إليكم
الكفء فلا تردوه فنعوذ بالله من بوار البنات )
"Akija
kuposa kwenu aliokuwa kufuu yake basi msimrudishe. Kwani twajikinga kwa Allah
na kudoda kwa watoto wa kike”.
Katika hadithi hii wahimizwa wazazi kuharakisha
kuwaoza watoto wao wa kike na wale wanaume waliokuwa sawa nao (Akiffaa) wale
aliowabainisha Mtume wetu -rehema za Allah na amani zimshukie- katika kauli
yake-:
(الأحرار من أهل التوحيد كلهم أكفاء إلا أربعة :
المولى والحجام والنساج والبقال )
“Waliokuwa huru katika
watu wa tawheed wote "Akiffaa" isipokuwa wane:- Mtumwa, anaepiga
chuku (al-hajjaam), mfumaji (annassaaj) na ajitwikae kapu kichwani akiuza mboga
au nafaka (al-baqqaal).”
Imepokewa kutoka na Anas bin Malik radhi ya Allah Subhanahu
Wataala iwe juu yake, amesema:-
( كان رسول الله صلى الله عليه وسلم يأمر
بالباءة وينهى عن التبتل نهيا شديدا فيقول تزوجوا الودود الولود فإني مكاثر بكم
الأنبياء يوم القيامة )
"Mtume
-rehema za Allah na amani zimshukie- alikuwa anaamrisha kuoa na anakataza kwa
ukali sana kukaa bila ya kuoa, na akisema :- "Oeni wanaopendeka katika
wanawake, wanaozaa kwani mimi nitajisifu kwa wingi wenu kwa Manabii siku ya
kiyama."
Amesema Abu Saeed: Amesema Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani zimshukie:
( تنكح المرأة لدينها ولمالها ولجمالها ، خذ ذات
الدين والخلق تربت يداك ) وفي رواية : ( فاظفر بذات الدين تربت يداك)
"Aolewa mwanamke kwa dini yake, kwa mali yake na kwa uzuri
wake mchague yule mwenye dini na tabia nzuri kusibu kheri mikono yako."
Maana yake anaeoa mwanamke kwa uzuri wake huwa baada
ya muda huisha hamu nae kwani kawaida kila kinachotumiwa huisha hamu. Kwa hiyo
utaona wale mafasiki huwa na mke mzuri lakini akija akiona mwanamke wa nje
njiani husema: - Leo nimeona mwanamke sivyo alivyokuwa mzuri kama paa (ghazaal)
kwa uzuri au maneno kama haya hata akiwa sura
yake mbaya lakini huwa anampambia shetani akawa hashughuliki kumtizama mkewe
halali yake kwa sababu kishachoka nae.
Kadhalika anaemuoa mwanamke kwa mali yake huenda
akafukarika au kikatokea kitu katika hiyo mali kuizuia isifike kwa huyo
mwanamme, au yeye mwanamke akakataa kumpa mali yake, basi hapo hutoweka ile
sababu iliyomfanya avutike kumuoa huyo mwanamke, hapo ndipo anapomchukia au
kitu cha mwisho huacha kumpenda basi kutakuwa wapi kushikamana?
Na katika hadithi iliyomo katika Musnad Imam Ar-Rabii:
“Anaolewa mwanamke kwa mambo manne …” na hilo la nne ni kwa ukoo na heshima yake. Na
anaeoa kwa sababu hii huenda huyo mwanamke akajifakharisha na akatakabari juu
yake na kumdharau, basi hayatadumu mashikamano baina yao ikiwa mume pia ni mwenye heshima. Amma kama akimuoa kwa dini yake basi dini
ndio inayobakia na kwa kubakia kwake yabaki mazoea na mapenzi baina yao . Kwa sababu kufikiria akhera kwa wote wawili
ni zaidi kuliko dunia na khasa ikiwa mume kama yeye (mkewe) katika kukamata
dini, kwani kikitokea kitu chochote baina yao
upesi watafikiria kauli ya Allah Subhanahu Wataala:
النساء:
١٩
“Na kama mkiwachukia basi (msiwaache) kwani huenda mkakichukia
kitu na Allah ametia kheri nyingi ndani yake.”
Aya 19 sura Al-Nisaa na kauli yake Allah Subhanahu Wataala:
الطلاق: ٦
"Na
shaurianeni kwa wema" Aya 6 Sura At-Talaaq
Na kauli yake:
البقرة:
٢٢٩
"Kisha
ni kumweka kwa vizuri au Kumwacha kwa Ihsani."
Aya 229 Sura
Al-Baqarah
Na nyinginezo katika aya zinazofundisha vipi kushikana
baina ya mume na mke.
Na kauli yake Mtume wa Allah –rehema za Allah na amani
zimshukie:
( لا يفرك مؤمن مؤمنة إن
كره منها خلقا سره منها آخر )
“Asimbughudhi Muumin (mwanamme) Muumin (Mwanamke), akichukia
tabia moja yake atapendezewa na nyingine.”
Hadithi zinazovutia katika ndoa ni nyingi na
inakutosha kuwa mwislamu anahifadhi kwa ndoa heshima na dini yake:
(ومن تزوج فقد أحرز نصف
دينه فليتق الله في النصف الآخر )
(Na
anaeoa amepata nusu moja ya dini yake basi amche Allah katika nusu iliyobakia).
Amesema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie:
(النكاح سنتي فمن رغب عن
سنتي فقد رغب عني )
"Ndoa
ni Sunna yangu basi yule anaekataa sunna yangu hakunitaka mimi".
Na amesema:
(
النكاح سنتي فمن أحب فطرتي فليستن بسنتي )
"Ndoa ni Sunna yangu basi anaependa
fitra yangu (maumbile aliyomuumbia Allah Subhanahu Wataala binaadamu ambayo ni ya
Kiislamu) basi ashikamane na sunna yangu (Ya ndoa)”, ameitoa Ibn Abbas.
Vile vile amesema :
( تناكحوا تكاثروا فإني أباهي بكم الأمم يوم
القيامة حتى بالسقط )
“Oaneni, mjifanye muwe wengi kwani mimi nitajisifu kwa ajili
yenu mbele ya umma nyengine siku ya kiyama hata kwa kilichoharibika (kutokana
na mimba)”
Na amesema:
( إذا أتاكم من ترضون دينه
وخلقه فزوجوه ، إلا تفعلوا تكن فتنة في الأرض وفساد كبير)
"Akiwajia
yule mnayeridhia dini yake na tabia zake basi muozesheni, ikiwa hamkufanya
hivyo itakuwa fitna katika ardhi na uharibifu mkubwa".
Hapa waamrishwa wazee wa watoto wa kike wasighalishe mahari. Mtastaajabu nikiwaambia
kuwa katika wakti huu wako wanaofuata hadithi hii tukufu.
Ameniomba kijana mmoja
nimposee mwanamke kutoka kwa mmoja katika watu wema tunaejuana kabla. Basi
nilipomuendea na nikamzungumzia jambo hili akanijibu bila ya kusita:- Muoze na
kile anachotaka kumpa mkewe (mahari) na ampe. Je anaweza mtu kuamini kuwa haya
yametokea katika wakti wetu huu?!
Na katika kutimia Imani yake kasema: Niwambie kitu nimeogopea
nisije nikawaghishi ambacho ni ila ilikuweko katika mtoto wa kike. Huyu mtoto
wa kike amefanyiwa operasheni wa wengu labda imeacha athari katika mwili
wake. Lakini juu ya yote hayo yeye hivi
sasa mzima. Tizama hii amana, kisha tukawa peke yetu mimi na yeye tu
nikamuuliza kwa nini ukatufanyia uzuri wote huu? Akasema Je! Inawezekana wewe unijie kumposea
mtu wamjua kisha nikurudishe? Basi itakuwa mimi nimeipinga hiyo hadithi
(iliyotajwa hapo nyuma). Hapa tena ndio akauliza juu ya mtoto wa kiume na juu
ya ukoo wake, na tabia zake? Allah Subhanahu Wataala amjaze kheri.
Kinashabihiyana na kisa kama
hichi kisa kilichotolewa juu ya Saeed bin Al-Musayyab katika Mataabiina wakubwa
kuwa mwanafunzi wake alifiwa na mkewe, basi akaacha kwenda kusoma kwake kwa masiku
kisha aliporejea akamuuliza Shekhe sababu ya kuacha kwenda kusoma akajibu mke
wangu amefariki. Akamuuliza bado hujaoa baada yake? Akajibu bado. Akamwambia njoo nikuozeshe mtoto wangu wa
kike, basi akamuozesha na ilipofika usiku akamwambia mama yake mtoto
mtayarishe, akamtayarisha akamuamrisha ende nyuma yake. Akamgongea mwanafunzi
wake mlangoni na hakuwa na khabari yoyote wala hakujitayarisha kumpokea arusi
wake. Akamwambia mchukuwe mkeo usilale
bila ya mke. Basi katika visa viwili
hivi kuna mfano mzuri wa kuchukuliwa.
Na vile vile amesema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie:
( من نكح لله وأنكح لله استحق ولاية الله )
"Anaeoa
kwa ajili ya Allah na kuozesha kwa ajili ya Allah amestahiki mapenzi ya
Allah." Ameitoa Muaadh.
Na amesema:
(كل عمل ابن آدم ينقطع بعد موته إلا من ثلاث ولد صالح يدعو له ..)
"Kila kitendo cha
binadamu kinakatika baada ya mauti yake isipokuwa---" kutokana na mambo
matatu hayo mtoto mwema anamuombea dua”
Na hili halipatikani isipokuwa kwa ndoa.
Asema Ibn Abbas: "Na hayatimii manasik ya
anaekwenda kuhiji isipokuwa kwa ndoa." Alikuwa akiwakusanya vijana wake na
kuwaambia "Mkitaka kuoa basi nitawaozesha kwani mja akizini hutolewa Imani
kutoka moyoni mwake."
Ametoa Al-ghazali katika "Al-Ihyaa":- kuwa
Bishr Ibin Al-Harith ameonekana katika ndoto baada ya kufa kwake, akaulizwa
amekufanya nini Allah akasema: zimepandishwa daraja zangu katika al-Janna, na
sikufikia daraja za watu waliooa.
Tukamuuliza amefanya nini Abu Nasser Attammaar? Akajibu amepandishwa juu
yangu kwa daraja sabiini, tukamwambia kwa nini tulikuwa tunakuona juu yake kwa
amali, akajibu kwa subra yake juu ya watoto wake wa kike na familia yake kwa
ujumla. Na sababu yake na imesemwa kuwa
: Fadhli ya aliyeoa juu ya mjane ni kama fadhli ya mujaahid juu ya yule aliebakia nyuma
hakwenda kupigana vita katika njia ya Allah Subhanahu Wataala, na vile vile
rakaa moja ya mwenye kuoa ni bora kuliko rakaa sabiini za yule mjane.
Juu ya kuhimiza kwetu vijana waoe bila shaka twaelewa
hali zao ngumu za kipesa na ughali wa mahari, lakini Muislamu akikusudia
kufanya kitu kwa kutaka radhi ya Allah basi humrahisishia na kumsaidia. Kwani aliyemiliki vilivyomilikiwa asema:
الطلاق: ٢ - ٣
"Anaemuogopa Allah, humtengenezea njia ya kuokoka
(na kila balaa). Na humpa riziki kwa
namna asiyoitazamia” . Aya ya 2-3 Sura ya At-Talaaq.
الطلاق: ٤
“Na
anayemuogopa Allah humfanyia mambo yake huwa mepesi" Aya ya 4 sura ya
At-Talaaq.
Kama ingekuwa vijana wangetia moyoni haya na
wakaziamini hizi aya za Qurani basi yangekuwa mambo yao mepesi lakini yasikitisha kuwa wao
wasema:-
Twaeka katika usalama uhai
(maisha) wetu na twamaliza masomo yetu nini maana ya maneno haya isipokuwa
kutokuwa na yakini kuwa Allah ndio mwenye kugawa riziki wafikiria kuwa wakipata
kazi basi wamekwisha garantii uhai wao anaweza kiumbe chochote kudhamini riziki
ya mwengineye? Na yeye
mwenyewe riziki yake imedhaminiwa na Allah Subhanahu Wataala:
الذاريات:
٥٨
“Kwa yakini
Allah ndiye Mtoaji wa riziki Mwenye nguvu, Madhubuti.”
Inasemekana kuwa mtu mmoja
mwema alikuwa afikiriya juu ya riziki basi likampasukia jiwe gumu akaona ndani
yake mdudu na ndani ya mdomo wake kuna jani la kijani(bichi). Basi Ametakasika
Aliyeumba na Ametakasika Mtoaji wa riziki.
Amesema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie:
(من ترك التزويج مخافة العيلة فليس منا )
“Anayeacha kuoa kwa kuogopa kufukarika si katika sisi”
Ameitoa Abu Saeed.
Amma aseme maneno haya kijana kisha afanye vitendo
vibaya huyu mwisho wake si mzuri na ajifanyia ubaya nafsi yake na mujitamaa
wake.
Amma juu ya vijana wa wakti wetu wa sasa naizuia
kalamu yangu kuandika juu yao
na nasema: "La hawla wala Quwata Illa Billahi" na namuomba Allah Subhanahu
Wataala anihidi mimi na wao.
Amesema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie:
( الدنيا كلها متاع وخير
متاع المؤمن الزوجة الصالحة )
“Dunia
yote ni manufaiko ya kupita na bora ya manufaiko ya Muumini ni mke mwema
(aliyeshika dini yake).”
Na alishtaki mtu mmoja kwa Mtume wa Allah -rehema za
Allah na amani zimshukie- juu ya ufakiri aliokuwa nao, basi akamuamrisha aowe
kwa hiyo katika sharia ya Allah mke huwa msaada kwa mumewe kutokana na ufakiri.
Amma katika maoni ya vijana wa leo na kwa yale waliyoshawishiwa na mashetani
wao mke huwa ndie anayesababisha ufakiri kwao, nani basi katika wao ana haki ya
kufuatwa. Amesema Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani zimshukie:
( شرار أمتي
عزابها )
"Wabaya
wa umma wangu ni wale walio wajane (waliokuwa hawana wake au hawana waume).”
Alitamani Imamu wetu Jabir Bin Zayd (Radhi za Allah
ziwe juu yake) afe mtoto wake kabla yake na afe yeye kabla ya mkewe. Akaulizwa
juu ya matamanio haya akasema: "Nimetamani afe mtoto wangu wa kike kabla
yangu hata awe katika mizani yangu siku ya kiyama na nife mimi kabla ya mke
wangu ili nisiishi mjane (bila ya mke)”. Na katika haya twaona fadhila ya
kufiwa mtu na mtoto mdogo.
Yasemekana kuwa mmoja katika watu wema alitakiwa aowe
akakataa. Basi siku moja akaamka usingizini asema: Niozesheni, niozesheni akaulizwa
juu ya hayo akasema: nimeota kuwa kiyama kimeshasimama nami nina kiu kali ilio
karibu ya kukata koo langu, basi tulivyokuwa sisi tuko katika hali hii
wakatokea watoto wakiuka huu mkusanyiko wa watu katika mikono yao mabirika ya
fedha nao wawapa maji ya kunywa baadhi ya watu na wawaacha kuwapa maji wengi
wao. Basi nikanyoosha mkono kwa mmoja kati yao
kumwambia nipe maji kwani nina kiu kali sana ,
akanijibu huna mtoto kati yetu kwani sisi twawanywesha baba zetu. Nikamuuliza
nani nyie, akanijibu sisi ni katika waliokufa katika watoto wa waislamu.
Basi anaeruzukiwa mke katika waislamu amshukuru Allah Subhanahu
Wataala kwa fadhli zake, na ajuwe kuwa Allah Subhanahu Wataala ndie Bwana wake
aliemhifadhi kutoka na kila michezo na mitelezo (mianguko), na ni wajibu juu
yake kuchukulia umuhimu haki ya hii neema na asione kuwa ni ndogo kwani kwa
hakika ni kubwa, na kila neema za Allah Subhanahu Wataala ni kubwa.
Na atie nia kwa ndoa hii kufuata sunna na kuhifadhi
sharafu na kutotizama yaliyoharamishwa, basi akiingia kwa mkewe na wakaachwa
peke yao afanye kama
vile sharia inavyoamrisha.
Na wakati unapokuwa peke yako na mkeo na ukatumaini
kuwa hakuna mtu mwengine pamoja na nyie na mkajifungia mlango, msogeleane na
mkamate mkono wake huku ukimuuliza hali yake na hali ya baba yake na mama yake
na kila kinachokuhudhurikia katika maneno ya upole na ulaini.
Mwanamwari ni bora kwa mwenye uwezo kutokana na
mahimizo ya Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- juu yake.
حديث عبد الرحمن بن عوف لما جاء وعليه أثر عرس فسأله النبي
صلى الله عليه وسلم ، قال تزوجت ، قال له : أبكرا أم ثيبا ، قال بل ثيب ، قال له :
هلا بكرا تعضها وتعضك ، وقال عليه الصلاة والسلام ؟ عليكم بالأبكار فإنهن أطيب
أفواها وأنتق أرحاما
Katika hadithi ya Abdurrahman bin Awf wakati alipokuja
na athari ya kuoa imedhihirika juu yake. Akamuuliza Mtume -rehema za Allah na
amani zimshukie- akamjibu nimeoa. Akamuuliza: Ni bikra au aliyekwishaolewa
akamjibu: aliyekwishaolewa. Akamwambia si bora bikra umng’ate naye akung’ate?.
Na akasema sala na salamu ziwe juu yake:
(عليكم بالأبكار فإنهن أطيب أفواها وأنتق أرحاما )
"Shikilieni kuoa wanawari kwa hakika harufu
za midomo yao ni nzuri na rahimu zao ni
safi zaidi".
Na kila ukikithirisha utangulizi(mipapaso) wa jimai ni
bora hata ikikuchukulia muda mrefu, usiharakishe na hata kama ukakhainiwa na
kuteremsha (kwa manii) katika wakti huu basi nenda ukajioshe najasa, sukutua na
jitie maji puani (kama katika kutawadha) na mrudie mkeo uendelee kazi yako hata
ujione kuwa umehisi raha na mkeo amezidi hamu yake juu yako basi hapa ndio ukidhi haja inayotakiwa.
Kisha sema:
"أعوذ بالله من الشيطان الرجيم بسم الله الرحمن الرحيم
"
"Audhu Billahi Mina
Shaytani Rajiim, Bismillahi Rrahmani Rrahiim.”
Basi shetani katika hali hii akisikia jina la Allah hukimbia na amma sivyo
akaa pamoja na nyie na anaingilia katika mambo yenu kama
anavyoweza kuingilia na kuharibu. Na
vile vile katika kutaja Allah ni kufuata sunna na kumshinda shetani na ukisahau
kusema hapo mwanzo sema utapokumbuka.
" بسم الله على أوله وآخره "
Bismillahi Ala Awalihi Wa Akhirihi, kama
ilivyokuja katika sunna .
Baadhi ya Mashekhe (Ulamaa) wasema: Ukiwa peke yako na
arusi wako usali rakaa mbili kabla ya kumfanya chochote kama
shukrani kwa Allah Subhanahu Wataala. Kwa hakika jambo hili sio kila mtu
anaweza kulifanya, na akajikalifisha mtu kulifanya hatajuwa nini la kusema
katika sala yake, kwa sababu moyo wake umeshughulishwa na kitu kingine, basi si
lazima kufanya hivyo walakini hana budi kumtaja Allah kwa hali yeyote ile.
Katika mambo nadra kutokea lile alilolitaja
Al-Ghazaaliy katika kitabu chake "Al-Ihyaa": Ameingia mtu katika watu
wema kwa bibi arusi wake akamwambia nasali rakaa mbili kumshukuru Allah,
alipoingia katika sala akamsahau bi arusi wake akangojea mkewe mpaka asubuhi.
Na katika usiku wa pili, wa tatu na wa kumi hivyo hivyo mpaka ikiwapitia miaka
arubaini bado haja muingilia mkewe.
Tuseme huyu mtu alitokea kweli kufanya haya basi subra ya huyu mwanamke
vile vile ilikuwa ya ajabu.
Tulikuwa twamjua mtu ambaye ameoa mwanamke wangali
bado wadogo na wamekufa wamekwisha pindukia umri wao miaka sabiini na wakti
wote huu hakuwahi huyu mwanamme kufunua nguo ya mkewe. Na hakuna aliyejua
habari hii isipokuwa ilipokuwa karibu ya mauti yao, siku moja ukaanguka ushungi
wake mbele ya mumewe basi akasema: Mungu wangu nakuomba sitara yako imeanguka
hijabu yangu mbele ya Mohammed kukusudia mumewe. Akaulizwa vipi wasema hivyo
naye ni mumeo? Akajibu nimeona haya
kwani ni mara ya kwanza yeye kuona kichwa changu na shingo yangu. Na alikuwa mwanamke mwema wamesalimika watu
na ulimi wake, akisali sala za usiku basi si ajabu kusubiri na kujistiri
(kusitiri).
Basi ukishamaliza haja yako na bi arusi wako bado
hajatosheka usifanye haraka ya kunyanyuka, kwani hiyo katika tabia njema ya
kumfikiria mkeo. Hebu fikiria kama yeye angetosheka na wewe bado hujatosheka
kisha akasimama akakuwacha vipi ungeridhika?
Shika kwa mkono wako wa kushoto kitambaa au tissue (karatasi) na yeye
vile vile akamate tissue yake basi ukinyanyuka kutokana naye ifute hiyo najasa
kwa hicho kitambaa na yeye vile vile
afanye hivyo hivyo ama sivyo itawaingia katika nguo zenu au katika godoro
(mahala mnapolala) ambapo itahitajia kuiosha kwani ni najisi. Wala msijifutie kitambaa kimoja (baina ya mume
na mke) kwani kitendo kama hichi kinasababisha
kuchukiana. Na inapendelewa usipite mchana au usiku wa Ijumaa umjaamii mkeo kwa
fadhila anaeoga usiku wa kuamkia Ijumaa au mchana kua anaghufiriwa dhambi zake.
Na kumuingilia mkeo kwa mkao wowote ule inajuzu.
Aya 223 – Suratul Baqarah.
البقرة:
٢٢٣
"Wake
zenu ni kama konde zenu, basi ziendeeni konde
zenu mpendavyo."
Na ukitaka kurudia tena nenda ukaoshe najasa kisha
usukutue na kustanshiq (kutia maji mdomoni na puani na uyapeleke ndani kama iwezekanavyo kisha uyatoe ) na unywe maji vinywa vitatu halafu umrudie
mkeo. Vivyo hivyo ukitaka kurudia mara ya tatu na ya nne, na haikulazimu kuoga
janaba kwa kila unavyofanya kitendo hicho, bali uoge mara moja mwisho baada ya
kutimiza haja zetu wakti wote unapotaka mwanzo wa usiku au mwisho wake, lakini
usilale nawe una najasa. Imetolewa kuwa Mtume -rehema za Allah na amani
zimshukie- amewapitia wake zake wote usiku mmoja na hakuoga ila baada ya
kuwapitia wote. Na tumebainisha namna ya
kuoga janaba katika juzuu ya kwanza ya kitabu hiki, na ikiwa wewe wajua kuoga
janaba na mkeo hajui basi ni wajibu wako kumfundisha.
التحريم:
٦
"Enyi
Mlioamini! Jiokoeni nafsi zenu na watu wenu na moto"
Tumetaja huko nyuma kuwa inamlazimu mwanamume akitaka
kuoga janaba kwanza akojoe hata yatoke yaliyobakia katika dhakar yaani manii.
Vile vile inamlazimu mwanamke kutia vidole vyake katika faraji yake ili atoe
manii ya mwanamme iliyoganda hapo aitoe nje ya rahim kwa sababu mwanamke
akikojoa havitoki kwa huo mkojo vile vilivyokuwa katika faraji (kama katika hali ya mwanamme) kwani mahala pa kutokea
mkojo sio pale pa jimai na hedhi. Lazima azingatie kitu hichi kwa sababu ikiwa
hakuyatoa hayo masalio ya manii kwa vidole vyake, yatatoka baadaye na kunajisi
nguo zake.
Wako baadhi waliokuwa hawataki mtoto basi humwaga nje
manii (nje ya mkewe). Wanasema
Maulamaa:- Mwanamke aliyekuwa huru hamwagiwi nje (na mumewe) isipokuwa kwa
Idhini yake na kitendo hicho kinakuwa wakati anapokaribia mwanamme kukojoa
(kutoa manii) aitoa dhakar yake akamwaga nje ya faraji ya mwanamke.
Hukumu yake inajuzu wakikubaliana mume na mke na haiwi isipokuwa kwa jambo
lililokuwa dharura sana kama kwa kuogopea siha ya mwanamke isiharibike kwa
sababu ya kushika mimba na kuzaa.
Amma watumwa wanawake (masuria) inajuzu kuwamwagia nje
bila idhini yao na walimshauri masahaba radhi za
Mola Subhanahu Wataala ziwe juu yao
Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- katika jambo hili la kumwaga nje
ulipokuwa ujane umewazidia.
Ametoa al-Rabii Rehema za Allah Subhanahu Wataala ziwe
juu yake katika Musnadi wake kutokana na Jabir bin Zayd kutokana na Abi Saeed
Al-Khudry amesema:
(خرجنا مع رسول الله صلى
الله عليه وسلم في غزوة بني المصطلق فأصبنا سبايا فاشتهينا النساء واشتدت علينا
العزبة فأردنا أن نعزل فقلنا نعزل وفينا رسول الله قبل أن نسأله عن ذلك ، قال
فسألناه فقال : ما عليكم أن لا تفعلوا ، فما من نسمة كائنة إلا وهي كائنة إلى يوم
القيامة )
"Tumetoka
pamoja na Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani zimshukie- katika vita vya
Banii Mustalaq tukapata mateka (ya wanawake) tukatamani wanawake na ukatuzidia
ujane na tukataka kutoa nje tukasema
tutatoa nje na baina yetu Mtume wa Allah kabla hatujamuuliza suala hilo,
akasema basi tukamuuliza akasema: "Si juu yenu ikiwa hamtafanya kwani
hakuna nafsi iliyoandikiwa kuweko ila itakuweko mpaka siku ya kiyama."
Imetolewa na Anas kuwa mtu mmoja amemuuliza Mtume -rehema
za Allah na amani zimshukie:
( لو أن الماء الذي يكون منه الولد أفرغته على
صخرة لأخرج الله منها ولدا أو يخرج الله منها ولدا ، وليخلقن الله نفسا وهو خالقها
)
“Kama ingelikuwa yale maji yaliyoandikiwa kutoka ndani
yake kiumbe (mtoto) ungeyamwaga juu ya jabali basi Allah Subhanahu Wataala
angetoa kutokana nalo (hilo
jabali) mtoto na hakika ataumba Allah Subhanahu Wataala nafsi naye ndiye
Muumbaji wake.”
Na katika "Muslim", imetokana na Jabir
(أن رجلا أتى النبي صلى الله عليه وسلم فقال :
إن لي جارية هي خادمنا وسانيتنا ، وأنا أطوف عليها ، وأنا أكره أن تحمل ، فقال :
اعزل عنها إن شئت فإنه سيأتيها ما قدر لها فلبث الرجل ثم أتاه فقال : إن الجارية
قد حملت ، فقال : " قد أخبرتك أنه سيأتيها ما قدر لها ".
kuwa mtu mmoja alimjia Mtume
-rehema za Allah na amani zimshukie- akasema hakika nina kijakazi (mtumwa
mwanamke) (page 156) naye ni mfanya kazi wetu nampitia (kwa kumwingilia) na
nachukia ashike mimba, akamjibu jitenge naye (yaani mwaga nje) ukitaka kwani
kwa hakika kitamjia kile alichoandikiwa
kumjia. Kisha akakaa yule mtu muda halafu akamjia Mtume -rehema za Allah na
amani zimshukie- akamwambia : yule kijakazi amepata mimba, akamjibu:
“Nimekwambia kuwa kitamjia tu kile alichoandikiwa.”
Kama huwezi kuowa na huwezi kusubiria jimai (kuingilia
mwanamke) basi jisaidie kwa kufunga kama alivyotufundisha mwalimu wetu -rehema
za Allah na amani zimshukie- hayo kwa kauli yake:
(من خاف من شدة الميعة
فليصم فإن الصوم له وجاء )
"Yule anayeogopa
hamu kubwa ya jimai ( na kungilia) basi afunge kwani funga humchokesha kwa
hivyo inavunjika hamu yake ya jimai."
Amesema Allah Subhanahu Wataala katika Aya ya 69 Sura
Al-Ankabut:
العنكبوت: ٦٩
"Na wale wanaojitahidi kwa ajili yetu kwa yakini
tunawaongoza kwenye njia zetu. Na bila
shaka Allah yu pamoja na wafanyao mema."
Allah amewapa mtihani wanawake katika hedhi (vipindi
vya mwezi) na nifasi (ujusi – baada yakuzaa) na katika hali mbili hizi
imeharimishwa kumwingilia mwanamke. Ama kustarehe nae katika sehemu zilizobakia
haikukatazwa isipokuwa ajiepushe na utupu na aweke juu yake kitambaa. Na
ameruhusiwa amruhusu mumewe sehemu yoyote nyengine isipokuwa duburi (nyuma)
kwani hiyo ni haramu wakti wote, napo ni mahala pa uchafu si mahala pa
uzalishaji, basi pakimbie mahala hapo mkimbio wa kondoo kutokana na chui. Na
ajifundishe mwanamke vipi ajioshe na hedhi na nifasi nako kama
kujiosha na janaba vile vile. Isipokuwa inamlazimikia kuzifungua nywele zake
katika hedhi na nifasi lakini haimpasi hivyo katika janaba isipokuwa
anazichovya nyewele zake mpaka ziingie maji. Vile vile inampasa kutia vidole
vyake katika utupu wake ili aisafishe kutokana na damu kama anavyojisafisha na
janaba kwani njia yao
ni moja.
Na wanawake wako makundi mawili katika kujua tohara
kutokana na hedhi na nifasi (ujusi), baadhi yao watoharika kwa kutoka maji
meupe na yaitwa maji ya tohara nayo ni maji meupe, mepesi na yafanana na chokaa
hutoka baada ya kukatika damu, na baadhi yao watoharika kwa ukavu, nayo ni
kukatika kwa damu na huyu si kawaida yake kutoka maji meupe. Basi aliyokuwa
kawaida kutoharika kwa maji meupe asijitoharishe kwa ukavu, na hapana budi
ayaone hayo maji meupe na ikiwa hakuyaona na
hali damu imekwishakatika basi angojee siku mbili kisha aoge. Ikiwa
litarudia jambo hili mara tatu (kutoyaona maji meupe) basi abadilishe kawaida
yake kuwa baada ya kujitoharisha kwa kuona maji ajitoharishe kwa ukavu.
Na muda wa tohara hauwi chini ya siku kumi na pindi
akiona damu kabla ya siku kumi basi asiichukulie kuwa hedhi isipokuwa hiyo ni
istihaadha na hawachi kwa hiyo sala wala saumu mpaka afike ule wakti wa kawaida
kupata hedhi, hapo inakuwa hukmu yake ya hedhi badala ya istihaadha, basi anawacha sala na saumu. Na mambo ya
hedhi na tohara yako mengi sana
hayatoshi kuzungumziwa katika mukhtasari (ufupi wa maelezo) huu, lakini juu
yake mwanamke kuuliza juu ya dini yake wala asipuuze au kuona haya kwani Mtume
-rehema za Allah na amani zimshukie- amewasifu wanawake wa ki-Ansaar wakati
alipouliza mmoja wao basi akasema :
(رحم الله نساء
الأنصار لم يمنعهن الحياء أن يتفقهن في الدين )
"Allah Amewarehemu wanawake wa
ki-Ansaar haikuwakataza haya kujifundisha
mambo ya dini yao"
Na sababu ya hadithi hii ni kuwa mwanamke mmoja
amemuuliza Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- akasema:
(برح الخفاء يا رسول الله ، ترى المرأة في النوم
ما يرى الرجل ، أعليها الغسل ؟ فقال رسول الله صلى الله عليه وسلم : عليها الغسل
إذا أنزلت ) وفي رواية ( أن أم سليم امرأة أبي طلحة الأنصاري جاءت إلى رسول الله
صلى الله عليه وسلم فقالت : يا رسول الله : إن الله لا يستحي من الحق ، هل على
المرأة غسل إذا هي احتلمت ؟ قال نعم : إذا رأت الماء )
"Kimedhihiri kilichostirika ewe Mtume Wa Allah, anaona
mwanamke katika usingizi kile anachokiona mwaname, Je! ni juu yake kuoga ? Basi
akasema Mtume wa Allah ni juu yake kuoga akiteremsha (yaani akikojoa)"
Na katika hadithi moja: kuwa Um Saliim mke wa Abi
Talha Al-Ansaariy alikuwa kwa Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani
zimshukie- akasema: "Ewe Mtume Wa Allah hakika Allah haoni haya kutokana
na haki, Je inampasa mwanamke kuoga ikiwa akiota? Akasema: Ndio kama akiona
maji (akikojoa).”
Amesema Jabir: Imekuja juu ya suala hili kutokana na masahaba wengi kuwa haimlazimu
kuoga kama mwanamume bali inamtosha tu kutia
udhu.
Hapa kuna jambo ambalo linatakiwa kuzingatiwa nalo:
Ikiwa mwanamme ataka kumuingilia mkewe na ukagusa utupu wake utupu wa mwanamke
pamoja na kuingiza mbele ya dhakari kisha akarudi pasi na kuendelea na jimai na
lau kwamba hakukojoa basi inawapasa waoge janaba, na pengine watu wengine
watasema kuwa haipasi kuoga janaba isipokuwa baada ya kutoka manii nalo ni kosa
kwani imekuja kutokana na sunna kinyume na hivyo.
Na imetokana na Rabii rehema za Allah ziwe juu yake –
kutoka kwa Abu Ubaida kutoka kwa Jabir Bin Zayd kasema:
( سألت عائشة هل كان يغتسل رسول الله من جماع
ولم ينزل ، قالت عائشة : كان رسول الله صلى الله عليه وسلم يصنع بنا ذلك ويغتسل
ويأمرنا بالغسل ويقول الغسل واجب إذا التقى الختانان ) وقال جابر قالت عائشة رضي الله عنها (يقول النبي صلى الله
عليه وسلم اذا قعد الرجل من المرأة بين شعبها وأجهدها وجب الغسل )
'Nimemuuliza Aisha Radhi za Allah Subhanahu Wataala ziwe juu yake Je!
Alikuwa akioga Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani zimshukie- kwa jimai
ambayo hakutoka manii, akasema Aisha alikuwa Mtume -rehema za Allah na amani
zimshukie- afanya na sisi kama hivyo kisha huoga na atuamrisha sisi kuoga
(janaba) na anasema: “Kuoga ni wajibu zikiingiana tupu mbili hadi zikakutana
sehemu zao zinazotahiriwa" na akasema Jabir amesema Aisha Radhi za Mola
ziwe juu yake amesema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie: “Pindi
mwanamme atakapomkalia mwanamke juu ya mapaja yake na akatia dhakari katika
utupu wake basi wanawajibika kuoga (wote wawili)”.'
Ni haramu kwa mume na mke kutoa habari juu ya yale
yanayotendeka baina yao katika usiri wao, kwani
anaefanya hivyo ni kama anaemjamii mke wake
sokoni au barabarani na hakuna tofauti yoyote.
Asimwingilie mkewe naye amelala kwani yatokea mambo
yanahusiana na kitu hichi :
1)
Inampita ile ladha ambayo inapatikana kutokana na
kitendo hicho.
2)
Pengine ameingia katika kipindi chake cha mwezi
(hedhi).
3)
Pengine asijue kuwa ana janaba na huenda akasali na janaba yake.
4)
Inalazimika kwa mume kumfundisha mkewe mambo ya dini
ikiwa yeye ni mjuzi zaidi.
المائدة:
٢
"Na
saidianeni katika wema na utawa (Ucha Mungu)"
Allah Subhanahu Wataala amemsifu Nabii wake Ismaeel
(A.S.) kwa kauli yake:
مريم: ٥٥
"Na
alikuwa akiwaamrisha watu wake sala na zaka na alikuwa mridhiwa mbele ya Mola
wake"
Na Mola amemuamrisha Mtume wake -rehema za Allah na
amani zimshukie:
طه: ١٣٢
"Na waamrishe watu wako kusali, na uendelee
mwenyewe kwa hayo, hatukuombi riziki bali sisi ndio tunakuruzuku. Na mwisho mwema utawathubutikia wamchao
Mungu."
Na yaungamana na Sala na Zaka mambo yote ya dini
lakini sababu ya kutajwa makhsusi ni kuwa ndio nguzo mbili za msingi katika
nguzo za Kiislamu kwani ni wajibu wa Muislamu kuzihifadhi hizo nguzo mbili
kutokana na mambo ambayo hayajuzu bali hata kutokana na yale yaliokuwa
hayapendezi.
النساء: ٣٤
"Wanaume (wawe) ni walinzi wa wanawake, kwa
sababu Allah amewafadhilisha baadhi yao kuliko wengine, na kwa sababu ya mali
zao wanazozitoa."
Katika wakati wetu huu imefunguka milango ya shari
ambayo wengi miongoni mwa wanawake wameingia ndani yake, hawakuchunga heshima
zao wala hawakuhifadhi dini zao. Nimetangulia kusema kuwa hakuna aliyemharibu
mwanamke isipokuwa mwanamme: na zilipoanguka haiba zao na ukaondoka wivu wao
juu ya wake zao wakawa kama wanyama bali baadhi ya wanyama bora kuliko wao, kwa
sababu wako katika wao wawaonea wivu majike yao .
Walipofika katika daraja hii ( ya kutokuona wivu) basi wakatoka wanawake
zao kutokana na lile umbo ambalo Allah Subhanahu Wataala amewaumba, ukaharibika
mwelekeo wao na kutawanyika. Wengine wakakamata kazi pamoja na wanaume wageni (sio
maharimu wao), wengine wakatoka mabarabarani bila ya kujihifadhi miili na uchi
wao, baadhi yao
wanahudhuria mikutano na afungua mmoja wao mdomo wake mbele ya jamhuri atoa
mashairi au ahutubia. Sisemi isipokuwa إنا لله وإنا إليه راجعون .
Wamekhitalifiana maulamaa juu ya mwanamke Je! Akataze
mabaya? Wakasema baadhi yao sio asifanye hivyo kwa sababu itabidi anyanyue
sauti yake, na kuwa malaika hakika wanalaani mwanamke ambaye sauti yake inatoka
nje ya ukuta wa nyumba yake, vipi basi wale ambao wanawataabisha malaika wao
kuwalaani kula wakati. Na wako miongoni mwao ambao wamejivua na uhuru (wa
kikweli anayestahiki mwanamke wa Kiislamu) wakatoka kwenda kwa kawafeer (Hair
Saloon or Beauty Saloon) na kitu gani kinachokujuulisha nini kawafeer imetoka
jina lake kutokana na kufr.
Mwanamke anapoingia tu katika mahala hapa anakufuru,
na huyo mtu anaefanya kazi hapo mahali akimgusa nywele zake amekufuru mara ya
pili, akimpunguza nywele zake amekufuru
mara ya tatu. Hatimaye anatoka hapo mahali haikubakia kitu katika dini yake, na
hurma (kukatazwa) ya kukata nywele za mwanammke ni kama
mkatazo wa kukata ndevu za mwanamume sawasawa. Dalili ya nguvu ya hurma ya
nywele za mwanamke kuwa anaempiga mwanamke katika kichwa chake ikaanguka nywele
yake na ikiwa haikuota mahala pake nyingine basi lazima amlipe huyo mwanamke
dia(faini), na kama hivyo kwa ndevu za
mwanamme. Basi inakutosha kuwa sharia ya Kiislamu imeeka kwa mambo mawili haya
diya ya muislamu mwanamme na akavipa daraja. Leo utakuta mwanamme asalimisha
ndevu zake kwa kinyozi azikate au kuzinyoa na kadhalika mwanamke asalimisha
nywele zake kwa kinyozi (yoyote yule akiwa mwanamke au mwanamme) azinyoe bila
ya thamani bali wao walipa ujira wa kunyolewa. Basi inakutosha ile shari ya
kusikia haya mambo bila ya wewe kuyafanya vipi hali ya yule anaepata riziki
yake kwa pesa kama hizi na wala hajali shari
yake. Anasema: Anaewaita watu kumkosoa
(kwa vile alivyojieka katika hali mbaya) basi watamkosoa katika yaliyo haki na
yaliyo si haki na amesema vile vile: "Na haifai asili ya mtu kuwa ni Bani
Hashim ikiwa yeye mwenyewe nafsi yake ya ovyo"
Umeona yale wanayoyafanya watu leo, utaona wanasoma
sunna iliyotoharika lakini wanafanya kinyume ya hiyo sunna (mpango
unaostaajabisha). Imeamrisha sharia kukata kucha na wao utawaona wazifuga, na
kama hizo kucha hazioti kwa kawaida yake utawaona wazinunua madukani kisha
wazipachika vidoleni mwao zikiwa kama kucha za
tai (aina fulani ya ndege). Imeamrisha
sharia kufuga ndevu kubwa (kama ilivyokuja katika hadithi ya Mtume -rehema za
Allah na amani zimshukie- na wao wazinyoa, na imeamrisha kukata sharubu na wao
wazifuga, na Imeamrisha mwanamke kukaa nyumbani kwake naye katoka nje.
Azungumza mmoja katika Maulamaa wa Kiislamu asema:
Kuwa siku moja alikuwa amepanda treni pamoja na binti yake na karibu yake kakaa
mwanamke wa kizungu. Huyu mzungu akamzungumzia yule mtoto wa kike wa kimasri
juu ya Omar Bin Al-Khatab, Radhi ya Allah iwe juu yake, na mwendo wake mzuri wa
kusifika. Basi alipoondoka yule mwanamke, akamwambia baba yake: Nataka kitabu katika
tarehe ya Omar bin Al-Khattab akamuuliza baba yake kwa nini? Akasema kwa sababu
huyu mwanamke wa kizungu kanizungumzia juu ya Omar kwa hiyo kanitia hamu ya
kujua tarehe yake. Akamwambia ewe binti yangu nimekuzungumzia yafika mara kumi
juu ya Omar haikufaa kitu lakini wakati alipokuzungumzia huyu mzungu mara
ukamsikiliza, je! Inataka tusiitie kufanya mazuri ila baada ya kuwaona wageni
(waliokuwa si waislamu) wayafanya ndio sisi tuwaige?
Basi ndio hivi wajidai Waislamu kuwa wamepata uhuru
kutokana na ukoloni, nchi zimepata uhuru lakini sio nyoyo zao, zimebakia chini
ya ukoloni zinafanya kama wanavyoamrisha na
kupenda vitendo vyao.
Tumetembea Ulaya, Umarikani, Mashariki ya Asia, China
na Japan hatukuona mwandiko wa Kiarabu, kila mmoja aandika kwa lugha yake tu.
Lakini tizama katika nchi za Kiarabu vipi wameitukuza lugha ya Kiiengereza na
Kifaransa, hata yule anayeuza vinywaji baridi anaandika juu ya duka lake kwa
Kiingereza ili kupata heshima kwa hiyo lugha. Basi Waarabu bado wameshikamana
na maadui zao, na wao (maadui) wameshikamana na wengine (si waarabu). Kama
ilivyosemwa:
Nimeshikana naye (mwanamke) naye kashikana na mwengine
(mwanamme mwingine pasi yangu) na huyo mwanamme kashikana na mwanamke mwengine.
Basi mpaka lini tutakuwa katika hali kama hii. Wala
usiulize juu ya kukata nyusi za wanawake na mengineo katika mambo ambayo sharia
imekataza wazi wazi, kama ilivyotolewa na Ar-Rabii katika Musnadi wake amesema
Abu Ubaidah kutokana na Jabir bin Zayd kutokana na Ibn Abbas Radhi za Allah
ziwe juu yake kuwa Mtume -rehema za
Allah na amani zimshukie- amesema :
( لعن الله النامصة والمتنمصة ،
والواصلة والمستوصلة ، والواشمة والمستوشمة ، والمتفلجات للحسن )
“Allah amemlaani mwanamke
anaekata nyusi zake na yule anayempunguza huyo mwanamke nyusi na yule
anayeongezea nywele zake ili ziwe ndefu na yule anayefanya kitendo hicho cha
kuongeza nywele na yule anayejichora juu ya uso wake na mkono wake (mchoro ule
maarufu uliokuwa hautoki) na yule anayechorwa. Na yule anayechonga meno yake ili awe na mwanya apate
kuwa mzuri.”
Na ametoa Ar-Rabii kutokana na Abu Obaidah kutokana na
Jabir bin Zayd amesema:
(بلغني عن معاوية بن أبي سفيان قال وهو على
المنبر عام حج : فتناول قصة من يد حرسي فقال : يا أهل المدينة : أين علماؤكم :
سمعت رسول الله صلىالله عليه وسلم يقول : " إنما هلكت بنو إسرائيل حين اتخذت
مثل هذه نساؤهم ")
(Imenifikia kutoka kwa Muawiya bin Abi Sufyan amesema naye yuko katika
membari ya Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- katika musimu wa Hija
akachukua kifurushi cha nywele kilichokuwa katika mkono wa askari wake kisha
akasema enyi watu wa Madina wako wapi Maulamaa wenu nimemsikia Mtume wa Allah
-rehema za Allah na amani zimshukie- asema: “Hakika wamehilikika Bani Israeel
wakati wanawake zao walikuwa wakivaa kama hichi”)
Nimesoma katika jarida kuwa bi arusi mmoja alivaa
"wig" (Baarookah) kisha akapelekwa kwa mumewe siku ya arusi, basi
wakati mumewe alipoingia akamkuta amekwisha kufa. Wakati lilipoondolewa hilo
wig akakutwa nyoka ndani yake naye ndiye aliyekuwa sababu ya kifo chake. Basi
laiti kila anayevaa wig amtokee ndani yake nyoka kama huyo (kwa sababu amekwenda
kinyume na sharia ya kiislamu), isipokuwa Allah Subhanahu Wataala anatoa fursa
ya wakati (kwa yule anaefanya maasi na mwenginewe mpaka wakati maalum), lakini
hapuuzi kitu (kila kitu chaandikwa katika kitabu chake na siku ya kiyama
atayakuta yote aliyoyafanya). Na ikiwa huyo nyoka hatomng'ata duniani
atamng'ata katika moto wa Akhera ikiwa hakutubu, na sifikiri yule anayefanya
makusudi kumuasi Allah Subhanahu Wataala na akaendelea hivyo, huyo hapati
tawfiiq ya kutubu. Na nimemsikia Imam
Al-Khalily, Allah Amrehemu, anasema anaingia motoni yule anayekusudia na hajali
nini anatenda (afanya maovu bila ya kujali).
Tumekwisha jua yale mambo mabaya aliyokuwa akifanyiwa
mwanamke kabla ya Uislamu na ukosefu wa heshima na adabu uliokuwa ukimpata.
Kila msomaji anayajua haya hata wale wanawake wanaojidai kuwa wao ni wasomi na
kuwa wamestaarabika, wanajua kuwa Uislamu umewatukuza (umenyanyua cheo chao) na
umewapa heshima. Kwa hiyo waliwajibikiwa waushukuru Uislamu kwa hayo na wafate
amri zake, na kuwa maasi yanaondoa zile neema tulizopewa, na katika kutomtii
Allah Subhanahu Wataala sio maendeleo ya Dunia wala Akhera.
Nastaajabu uhai gani huu unaomfanya mtu adanganyike
nao na atopee katika kumuasi Allah Subhanahu
Wataala bila ya kujali wapi anaelekea, na sote twajua kuwa uhai huu haudumu.
Hatusikii isipokuwa baina ya kula wakti mchache mtu Fulani kaondokana nao na
kuelekea kule ambako ametanguliza vitendo vyake, basi tizama kitu gani
wakitanguliza mbele yako na wapenda kukiendea.
Mfano uliokuwa karibu na haya ni kuwa wakati
unapojenga nyumba mpya wataka kukaa ndani yake, jee utaikalia nayo ni mbovu?
Je! Utaikalia nayo haijakamilika? Utaihamia bila ya kuwa na samani (fanicha)?
Basi mfano kama huu katika kuelekea kwenda akhera nao ndio uhai wa hakika
(ukweli).
العنكبوت: ٦٤
"Na hayakuwa haya maisha ya dunia ila upuuzi na mchezo, na nyumba ya akhera ndio maisha
hasa laiti wangalijua."
Yaani maisha ya
akhera ndio ya kudumu basi mcheni Allah Subhanahu Wataala enyi waja wa Allah
naye haridhii kwa waja wake kumkufuru (ukafiri), na pindi wakimkufuru basi yeye
hawahitajii wao lakini wao ndio waliokuwa mafakiri kwake.
Amesema Mtume wa Mola -rehema za Allah na amani
zimshukie- katika hadithi Qudsiy:
(يا عبادي لو أن أولكم وآخركم وجنكم وإنسكم كانوا على أتقى قلب رجل منكم ما زاد في ملكي شيئا ، ولو أن
أولكم وآخركم وجنكم وإنسكم كانوا على أفجر قلب رجل واحد ، ما نقص ذلك من ملكي
شيئا)
“Enyi waja wangu lau kama wa kwanza wenu na wa mwisho wenu na
majini wenu na mainsi wenu walikuwa kama mtu
miongoni mwenu mwenye moyo unaemcha Allah kuliko wote isingezidisha katika
mulki yangu kitu cho chote. Na lau kama wa kwanza wenu na wa mwisho wenu na
majini wenu na mainsi wenu walikuwa kama mtu miongoni mwenu mwenye moyo wa uasi kuliko wote isingepunguza
kitu katika mulki yangu.”
Na nawaambia wanawake wa kiislamu, mcheni Allah Subhanahu
Wataala na wala msidanganyike na maneno ya wanaopenda kusema (bila ya ilimu) na
vitendo vya Dajjaliin (wapotezaji) kwani ni raha chache inayopita (na haiko
mbali kutoweka).
النساء:
٨٩
"Wanataka
(makafiri) lau mngekufuru kama walivyokufuru wao ili muwe sawa".
Na Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani zimshukie-
asema:
(أقرب ما تكون المرأة من وجه ربها إذا كانت في
قعر بيتها وإن صلاتها في صحن دارها أفضل من صلاتها في المسجد ،
وصلاتها في بيتها أفضل من صلاتها في صحن دارها وصلاتها في مخدعها أفضل من صلاتها
في بيتها )
“Mahala anapokuwa mwanamke karibu kabisa na Mola wake ni pale
akiwa ndani ya nyumba yake, na hakika sala yake katika ua wa nyumba yake ni
bora kuliko sala yake msikitini, na sala yake nyumbani kwake bora kuliko sala
yake katika ua wa nyumba yake, na sala yake chumbani mwake ni bora kuliko sala
yake nyumbani mwake.”
Na asema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie:
( المرأة عورة فإذا خرجت
استشرفها الشيطان )
“Mwanamke
yapasa ajistiri kwani akitoka, shetani huwa pamoja nae (kumpambia).”
Basi haya ikiwa katika salaa ambayo bila shaka yoyote
ni taa (kumtii Allah Subhanahu Wataala) vipi ikiwa katika mchanganyiko na
wanaume katika vikao vyao, mikutano yao na
michezo yao na
mengineyo? Walikuwa wanawake waliopita akitoka mume wa mmoja wao amwambia:
Usije ukachuma haramu kwani sisi twasubiria njaa na shida lakini hatusubirii
moto (Jahannam).
Na kauli iliyojumuisha adabu za mwanamke :
-
Awe amekaa nyumbani kwake hakithirishi kupanda kwake
na kutoka kwake(hatoki isipokuwa kwa dharura).
-
Mwenye maneno kidogo na jirani zake.
-
Amhifadhi mumewe akiwa hayupo.
-
Amfurahishe katika kuwepo kwake .
-
Ajiepushe kusikika Sauti yake na mtu wa mbali.
-
Hamu yake iwe kutengeneza hali yake na kuipanga nyumba
(kuishughulikia) yake.
-
Mwenye
kumuabudu Mola wake.
-
Akinai kwa kile alichoruzukiwa mumewe na Allah Subhanahu
Wataala.
-
Atangulize haki ya mumewe mbele ya haki yake.
-
Asifanye haraka kwenda mlangoni kwa yule anayegonga
kutaka idhni ya kuingia.
-
Awe tayari katika hali yoyote kumsikiliza mumewe.
-
Awe msafi na ajitie manukato na atahadhari asinuse
mumewe harufu itayomkera kutoka kwake au aone kwake mandhari ambayo
itamkirihisha .
-
Awaonee huruma watoto wake na watoto wa mumewe kwa mke
mwingine.
-
Ahifadhi sitara yao (yaani hawatolei hawa watoto aibu
zao).
-
Ulimi wake uwe mfupi hauna maudhi .
Imetolewa kutokana na Mtume -rehema za Allah na amani
zimshukie :
( حرم الله على كل آدمي الجنة يدخلها قبلي، غير
أني نظرت إلى يميني فإذا امرأة تبادرني إلى باب الجنة فأقول : ما لهذه تبادرني ؟
فيقال لي يا محمد : هذه امرأة كانت حسناء جميلة، وكان عندها يتامى لها فصبرت عليهن
حتى بلغ أمرهن الذي بلغ ، فشكر الله لها ذلك )
“Allah Subhanahu Wataala amemharimisha mtu yeyote kuingia Janna
(Peponi) kabla yangu, isipokuwa nnapotizama
kuliani kwangu kuna mwanamke ambaye ananiwahi kufika katika mlango wa
pepo basi husema : Ana nini huyu aniwahi? Ndipo hujibiwa : Ewe Muhammad: Huyu
mwanamke alikuwa mzuri wa kuvutia na alikuwa ana mayatima (watoto wake wanawake) basi akawasubiria
mpaka likafika jambo lao pale lilipofika, basi Allah Subhanahu Wataala
akashukuru (akamjazi) kwa hayo aliyoyatenda.”
Imetolewa kutoka kwa Asmaa bint Abu Bakar Allah Subhanahu
Wataala amridhie: Amenioa Azzubeir na
hali hana kitu katika ardhi yake kama mali au mtumwa wala chochote
isipokuwa farasi na ngamia. Nilikuwa
nikimlisha huyo farasi na kumsaidia
(mume wangu) kumtosholezea huyo farasi mahitajio yake na nikimtwangia nafaka
(chembe za mimea) ngamia wake na kumlisha na kumnywesha na nikiteka maji
kisimani kwa ndoo na nikiponda unga, na nilikuwa nikibeba mbegu juu ya kichwa
changu kutoka umbali wa theluthi mbili ya farsakh (farsakh = maili tatu) mpaka
aliponiletea Abu Bakar kijakazi (mfanya kazi au mtumwa wa kike) basi
akanitosheleza kumshughulikia huyo farasi basi ikawa kama kanikomboa .
Basi hizi ni katika sifa za wanawake wema ambao ndio
wanaotakiwa kuwa mfano kwa wengine. Wale waitao watu kwenye batili(wapotezaji)
katika wakati huu wanapigia mifano wanawake kama hawa ili wawadanganye watu wa
kawaida wasiokuwa na maarifa katika dini yao wapate kuchanganyikana (baina ya
wanaume na wanawake) na watokane na mipaka ya dini yao, kwani umefanywa Uislamu
na watu wake walioongoka lengo la
kuwavutia watu kufanya mabaya (wanawaita watu kufanya mabaya kisha wasema hivi
ndivyo Uislamu unavyohimiza), na Uislamu uko mbali na yale wanayousingizia. Makusudio
yao ni kupoteza watu kwani hakika Uislamu ni wenye nguvu na kila mmoja ataka
awe mwenye nguvu, basi wakishawapoteza wawakimbia kama
alivyosema Allah Subhanahu Wataala katika kitabu chake juu ya sheitani amesema:
الحشر: ١٦ - ١٧
"Ni kama shetani anapomwambia mtu:
"kufuru" na anapokufuru akamwambia: "Mimi si pamoja nawe, hakika
namuogopa Allah, Mola wa walimwengu". Basi mwisho wa wote wawili hao ukawa
waingie motoni kukaa humo daima na hiyo ndiyo jazaa ya madhalimu".
إبراهيم: ٢٢
"Na shetani atasema itapokatwa hukumu (ya wema
kwenda peponi na wabaya kwenda motoni atawaambia wale maasi wataomng'ang'ania): Allah
alikuahidini ahadi ya kweli (na leo ameitimiza), nami nilikuahidini lakini
sikukutimizieni. Wala sikuwa na mamlaka juu yenu (ya kukulazimisheni
kunifuata), isipokuwa nilikwiteni tu nanyi mkaniitika . Basi msinilaumu bali jilaumuni wenyewe:
siwezi kukusaidieni wala nyinyi hamuwezi kunisaidia. Hakika mimi nilikataa kunishirikisha kwenu
toka zamani." Kwa yakini madhalimu
watakuwa na adhabu iumizayo."
Na madhalimu ni wale wanaoasi amri za Allah Subhanahu
Wataala na Mtume wake -rehema za Allah na amani zimshukie.
Hapa kuna jambo ambalo lazima kujitahadharisha nalo
nakuwa watu wanalichukulia wepesi nalo ni zito sana .
Kama ndugu wanaishi katika nyumba moja na wanao wake zao au mmoja katika
wao ana mke na mwingine hana basi utawaona hao wanawake hawajistiri na ndugu za
waume zao bali wajifungua mbele yao
( wazionyesha zile sehemu ambazo wajibu kustiriwa) na vile vile wanakula nao
pamoja.
Na hawatofautishi baina ya mume na shemegi yake
isipokuwa katika unyumba(wakati wa kulala) na hii ni hatari kubwa kwani hakuna
tofauti baina ya ndugu wa kiume wa mume na mwanamme mwengine (aliekuwa si
mahram) katika makatazo.
Mwanamke yeyote yule ambaye mwanamume anasihi
kumuowa basi ni haramu kwake (huyo
mwanamume) kuona sehemu yoyote katika mwili wake au nywele zake , hapana shaka
kuwa mke wa ndugu akimuacha mumewe basi anaweza yule ndugu kumuoa.
النبي صلى الله عليه وسلم قال لرجل سأله عن الدخول على النساء ، فنهاه عن ذلك فقال ما تقول في
الحمو ؟ قال النبي صلى الله عليه وسلم : ( الحمو الموت )
Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie-
amehadhirisha sana
mambo haya, akamwambia mtu fulani aliyemuuliza juu ya kuingia kwa wanawake kuwa
asifanye hivyo yaani kamkataza kuingia walipo wanawake waliokuwa sio mahrim
wake. Akamuuliza tena jee vipi shemegi (yaani ndugu wa mume) akasema Mtume
-rehema za Allah na amani zimshukie- "Shemegi ni mauti". Kamwita
mauti basi kuna kitu baada ya mauti? Twamuomba Allah Subhanahu Wataala afya na
tawfiiq ya kufuata amri zake na kujizuia na makatazo yake na atujaalie katika
wale wanaosikiliza kauli kisha wakaitekeleza vizuri kabisa.
Ameitoa Mufti Mkuu wa Sultanate ya Oman Sheikh
Ahmed Bin Hamed Al-Khaliliy.
Uislamu ni dini ya fitra (kimaumbile) ameiteremsha
Allah Subhanahu Wataala hii dini kuliongoza hilo
umbile (fitra) katika njia yake iliokuwa ya kweli kwa hivyo zimekuja hukumu
zawafikiana na mahitajio yake (hilo
umbile) na zinatekeleza mahitajio yake.
Na katika mambo yaliyokuwa wazi kabisa kuwa kila mmoja
katika mwanamme na mwanamke anazo sifa makhsusi za kimaumbile zinazolazimisha
kutofautiana kwa hali zao kinafsi, kimwili na kijamii basi ndio hivyo utaona
Uislamu umeharamisha kwa kila mmoja katika wao asijivalishe sifa za kimaumbile
za jinsi nyingine kama tunavyoona katika kauli
yake -rehema za Allah na amani zimshukie:
( لعن الله المتشبهين من الرجال بالنساء والمتشبهات من النساء
بالرجال )
“Allah amewalaani wale wanaojishabihisha na wanawake katika
wanaume na wale wanaojishabihisha na wanaume katika wanawake”.
Kwa sababu katika kufanya
hivyo ni kutokana na fitra (maumbile aliyojaalia Allah Subhanahu Wataala katika viumbe vyake) na
kugongana na sunna za uhai na kuingilia zile sifa za wengine.
Na hapana shaka mwanamme aliekuwa maumbile yake
yamebakia katika usalama inamkataza haiba yake ya kiume kuvaa dhahabu kwa
sababu hiyo inapingamana na alama za kiume na ugumu wa hiyo jinsi ya kiume na
kuwa hiyo inaambatana na ulaini wa kike. Kisha tunaona katika athari za sunna
za Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- makatazo ya nguvu na mahadharisho
ya adhabu ya Allah Subhanahu Wataala kwa wale wanaume wanaovaa dhahabu kitu
ambacho hakimuachii mtu nafasi ya kusita kuikubali hukumu, na nyingi katika
hizi athari zimezungumzia juu ya pete.
Ifuatayo ni mifano itakayokuangazia katika njia ya
maarifa.
1- روى إلامام الربيع رحمه الله
عن الإمام علي بن أبي طالب –كرم الله وجهه – قال : نهاني الرسول صلى الله عليه وسلم عن لبس القسي وعن لبس
المعصفر وعن خاتم الذهب وعن قراءة القرآن في الركوع والسجود .. أخرجه النسائي
وكذلك الترمذي ما عدا ذكر القراءة في الركوع والسجود
1.. Ametoa Imam Al-Rabii Rehema za Allah
ziwe juu yake kutokana na Imam Ali Bin Abii Taalib - Allah aukirimu uso wake
- amesema:- Amenikataza Mtume -rehema za Allah na amani
zimshukie- kuvaa aina ya nguo fulani kutoka Misri ambayo imechanganywa na
hariri (Al-Qasiy) na pia kuvaa nguo yenye rangi ya zaafarani (Al-Ma'safir) na
pete ya dhahabu na kusoma Qurani katika rukuu na sujuudu. Ameitoa vile vile Annasai na Attirmidhi isipokuwa kutajwa kusoma katika
rukuu na sujuud na akasema hadithi hasan na sahiih.
2- أخرج البخاري ومسلم والنسائي
عن أبي هريرة أن رسول الله صلى الله عليه وسلم نهى عن خاتم الذهب وفي رواية
للنسائي أن النبي صلى الله عليه وسلم نهاني عن تختم الذهب
2.. Ametoa Al-Bukhari na Muslim na Annisai kutokana na
Abu Huraira kuwa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- amekataza kuvaa
pete ya dhahabu na katika hadithi ya Annasaai kuwa Mtume -rehema za Allah na
amani zimshukie- kanikataza kuvaa pete ya dhahabu.
3- روى الترمذي عن عمران بن
حصين –رضي الله عنه – قال ( نهى رسول صلى الله عليه وسلم عن التختم بالذهب )
3.. Ametoa Attirmidhi kutokana na Imraan Bin Hussein
amridhie Allah Subhanahu Wataala, amesema – amekataza Mtume -rehema za Allah na
amani zimshukie- kuvaa pete ya dhahabu.
4- روى مسلم عن ابن عباس –رضي
الله عنهما – أن رسول الله صلى الله عليه وسلم رأى خاتما من ذهب في يد رجل فنزعه
وطرحه وقال ( يعمد أحدكم إلى جمرة من نار فيطرحها في يده ) فقيل للرجل بعدما ذهب
رسول الله صلى الله عليه وسلم خذ خاتمك انتفع به فقال لا آخذه أبدا وقد طرحه رسول
الله صلى الله عليه وسلم
4.. Ametoa
Muslim kutokana na Ibn Abbas Allah Subhanahu Wataala amridhie yeye na baba yake
kuwa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- ameona pete ya dhahabu katika
mkono wa mwanamme akaipopotoa kisha akaitupa na akasema:- Anakusudia mmoja wenu
jinga la moto na kulitupa mkononi mwake. Akaambiwa yule mtu baada ya kuondoka
Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- chukua pete yako ujinufaishe nayo
akasema siichukui abadan
(milele) baada ya kuitupa Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani zimshukie.
5- روى النسائي عن أبي سعيد
الخدري – رضي الله عنه – أن رجلا قدم من نجران إلى رسول الله صلى الله عليه وسلم
وفي يده خاتم من ذهب فأعرض عنه رسول الله صلى الله عليه وسلم وقال ( إنك جئتني وفي
يدك جمرة من نار )
5.. Ametoa Annasai kutokana na Abi Saeed Al-Khudriy
amridhie Allah Subhanahu Wataala kuwa mtu mmoja alikuja kwa Mtume -rehema za
Allah na amani zimshukie- kutoka Najraan na katika mkono wake pete ya dhahabu
basi akageuka upande mwingine (kuepukana nae) akasema "Hakika wewe
umenijia na katika mkono wako jinga la moto".
6 – روى النسائي عن البراء بن
عازب –رضي الله عنه – أن رجلا كان جالسا عند النبي صلى الله عليه وسلم وعليه خاتم
من ذهب وفي يد النبي صلى الله عليه وسلم مخصرة فضرب بها أصبع الرجل فقال: مالي يا
رسول الله ؟ قال ( ألا تطرح هذا الذي في أصبعك ) فأخذه الرجل فرمى به فرآه النبي
صلى الله عليه وسلم بعد ذلك فقال ( ما فعلت بالخاتم ) قال رميت به قال (ما بهذا
أمرتك إنما أمرتك أن تبيعه فتستعين بثمنه ) ...
6.. Ametoa Annasai kutokana na Al-Barraa bin Aazib
amridhie Allah Subhanahu Wataala kuwa mtu mmoja alikuwa amekaa kwa Mtume
-rehema za Allah na amani zimshukie- na amevaa pete ya dhahabu na katika mkono
wa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- ana fimbo akampiga kwayo vidole
vya huyo mtu, akasema nimefanya nini Mtume wa Allah? Akasema : "Hukitupi
hicho kilichokuwa katika kidole chako akaichukua yule mtu akaitupa kisha Mtume
-rehema za Allah na amani zimshukie- akamuona baadaye akamwambia umeifanya nini
ile pete akamwambia nimeitupa akamwambia "sikukuamrisha kufanya hivyo
lakini nimekuamrisha uiuze na ufaidike na thamani yake". Na yote yatakayosemwa katika hadithi hii
lakini yatiwa mkazo na hadithi nyinginezo sahihi.
7- روى الثعلبي عن أبي ثعلبة
الخشني – رضي الله عنه – أن النبي صلى الله عليه وسلم أبصر في يده خاتما من ذهب
فجعل يقرعه بقضيب معه فلما غفل النبي صلى الله عليه وسلم ألقاه قال ( ما أرانا إلا
قد أوجعناك وأغرمناك )
7.. Imetolewa na Thaalabiy kutokana na baba wa
Thaalaba Al-Khasheniy – Allah Subhanahu Wataala awe radhi naye kuwa Mtume
-rehema za Allah na amani zimshukie- ameona katika kiganja chake pete ya
dhahabu akawa anaipiga ile pete (anaigonga) kwa kigongo alichokuwa nacho na
wakati alipoghafilika Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- akaitupa akasema
"Sioni isipokuwa tumekuumiza na kukutia gharama.”
Zinatosha hadithi hizi kwa yule mwenye moyo au akatega
masikio yake naye ni shahidi. Zinatosha kumzuia asivae pete ya dhahabu wala
kuitumia na hakuwa muumini wa kiume au wa kike baada ya kupitisha Allah na
Mtume wake amri wakawa na khiari ya jambo hilo (isipokuwa kufuata amri
iliyopitishwa na Allah Subhanahu Wataala na Mtume wake) na yule anayemuasi
Allah na Mtume wake basi amepotea
upotevu wa uwazi.
Na ilivyothibiti kuwa pete ya dhahabu haramu kwa mwanamume
kwa dalili hizo zilizokuwa wazi kabisa katika sunna ya Mtume -rehema za Allah
na amani zimshukie, basi pete ile wanayovalishana bwana na bi arusi umezidi ule
uharimisho wake kwa kuwaiga washirikina na kuwafanya mfano wetu, na hayo
hayatokani isipokuwa kwa wale zilizougua nyonyo zao na kutikisika nafsi zao na
kupungua imani yao. Kwani kujishabihisha nao ni kudhihirisha yale yaliyo ndani
ya nyoyo zao (kuwapenda washirikina na Muislamu wa kweli hawi hivyo) ya kuwatukuza na kupenda adaati zao na kufuata
njia zao na haya yote yamehadhirishwa na Allah Subhanahu Wataala kwa waja wake
waumini kuwafanya makafiri marafiki zao.
Je! Niwaambie nini asili ya Dabla ( pete
wanayovalishana mume na mke katika arusi)?.
Hakika asili yake ni upotevu wa Kirumi wa hali ya
chini kabisa. Walikuwa Warumi wanaamini
kuwa mwanamume akimvalisha mwanamke pete ya chuma katika kidole cha kati cha
mkono wa kushoto na kinyume chake pia yaani mwanamume akimvalisha mwanamke katika munasaba wa posa kufanya hivyo kuna
athari katika kuhifadhi mapenzi kwa imani yao kuwa kuna mawasiliano baina ya
hicho kidole na moyo kama kwamba kwa hivyo kila mmoja katika wao anauteka moyo
wa mwenziwe. Kisha ikaendelea mila hiyo kupiga hatuwa zaidi huko ulaya wakawa
wavalishana pete ya dhahabu badala ya chuma.
Basi mila hii ikawavutia wengi wenye maradhi katika
nyoyo zao katika nchi za Kiislamu, ikachukuliwa kuwa katika alama za maendeleo
na ustaarabu na ukweli sio isipokuwa katika dalili za kuchelewa na kushuka
chini.
Watakia nini waislamu kuiga mambo yaliyokuwa hayana
msingi wowote yaliyoletwa na ujahiliya wa kirumi na ukarithiwa na ujahiliya wa
kiuropa. Na haya yameonekana na kuwa
hayana msingi wowote kutokana na majaribio ya kimaisha. Ndoa ngapi zilizofanywa katika msingi huu (wa
kuvalishana pete) zikapindukia kuingia katika taabu na joto la moyo na
kugombana kusikokwisha wala kuwezekana.
Na raha gani waliyopata wengi waliokuwa hawakuifata hii hii mila ya
kijahiliya. Laiti ningejua mpaka lini hawa wanaohisabika katika idadi ya
Waislamu watakuwa ni mikia ya wengine wanaiga kila mila zao za kipuuzi na kila
mambo yao ya ovyo.
Na watu leo wengi katika kuvaa pete wanafuata njia
tofauti na muongozo wa Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani zimshukie-,
kwani wao wanavaa pete kidole cha kati kufuata mila za wengine na ilihali
hadithi za Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- zaonesha kuwa yeye
alikuwa akivaa pete kidole cha mwisho.
روى مسلم عن علي – كرم الله وجهه – قال : نهاني رسول
الله صلى الله عليه وسلم أن أجعل خاتمي في هذه أو التي تليها ، وأشار إلى الوسطى
والتي تليها ونحوه عند أبي داود والنسائي والترمذي
Ametoa Muslim Kutokana na Ali – Allah Subhanahu
Wataala aukirimu uso wake – Kasema amenikataza Mtume wa Allah -rehema za Allah
na amani zimshukie- kuijaalia (kuivaa) pete yangu katika hichi au kinachofuatia
na akaonyesha kidole cha kati na kinachofuatia na imetolewa kama hivyo kwa Abi
Dawood na Annassai na Attirmidhi. Basi na agutuke Muislamu na mambo kama haya
madogo madogo na atahadhari na mtelezo wa miguu na wa fahamu (akili) na Allah
SUBHANAHU WATAALA ndio mwenye kutoa tawfiiq.
Na Rehema za Allah na Amani yake ziwe juu ya bwana wetu Muhammad na juu
ya watu wake na Masahaba zake wote!
No comments:
Post a Comment
Note: only a member of this blog may post a comment.