{
بسم الله الرحمن الرحيم }
ﭽ
ﮖ ﮗ
ﮘ ﮙ ﮚ
ﮛ ﮜﮝ ﮞ
ﮟ ﮠ ﮡ
ﮢ ﮣ ﮤ
ﮥ ﮦ ﮧ
ﮨ ﮩ ﮪ
ﮫ ﮬ ﮭ
ﮮ ﮯﮰ ﮱ
ﯓ ﯔ ﯕ
ﯖ ﯗ ﯘ
ﯙ ﭼ النساء:
٣٦
"Muabuduni
Allah wala msimshirikishe na chochote, na wafanyieni wema (Ihsani) wazazi
wawili (Baba na Mama), na jamaa na mayatima na masikini majirani walio karibu
na majirani walio mbali, na marafiki walio ubavuni (mwenu) na msafiri
aliyeharibikiwa na wale iliyowamiliki mikono yenu ya kulia (kuume). Bila shaka
Allah hawapendi wenye kiburi wajivunao."
Haki ni
aina mbili:
1- Haki
baina ya mja na Mola wake.
2- Haki
baina ya Mtu na Wenzake (Jamii).
1- Haki
iliyo baina ya mja na Mola wake ni kumuabudu Allah Subhanahu Wataala na
kumpwekesha na kumtii na kutomshirikisha na cho chote.
2- Haki
iliyo baina ya mja na wenzake ni haki zinazo wahusu viumbe baina yao wenyewe kwa wenyewe
ili ihsani ienee baina ya binaadamu katika kila mambo ya maisha.
Na hizi
haki ziko zilizo maalumu, za watu wote, za lazima (wajibu) na za kupendelewa.
- Haki
za jamaa waliohusu:
Yatuwajibikia
kuwasiliana nao kwa kuwazuru na kuwafanyia ihsani, na hii ndio daraja ya juu
kabisa ya mawasiliano, au kuwafanyia ihsani kwa mali
bila ya kuwazuru, au kuwatembelea bila ya kuwafanyia ihsani ya mali .
Na ikiwa hawezi kwenda wala kumsaidia kwa pesa basi kwa kumtumia salamu, na hii
ndio daraja ya chini kabisa ya kuwasiliana. Wala asitie niya ya kuwakata jamaa
zake kwani anaewakata huyo amelaaniwa, kama
ilivyokuja katika hadithi ya Mtume Salallahu Alayhi Wasalam.
Allah Subhanahu
Wataala Amemegua jina la “Rahim” (jamaa waliomhusu mtu) kutokana na jina lake
“Arrahiim” basi mwenye kuwasiliana nao Allah Subhanahu Wataala Atawasiliana nae
na mwenye kuwakata (kuwapiga pande) na Allah Subhanahu Wataala Atamkata.
Hizi vile
vile ni katika haki maalumu. Ni wajibu wa mtoto kuwatii wazazi wake wawili na
awafanyie wema kama iwezekanavyo hata wakiwa
waovu. Mtoto awatii wazazi wake katika mambo yaliyokuwa si ya maasi kwasababu:
( لا طاعة لمخلوق في معصية الخالق )
“Haifai
kumtii kiumbe katika kumuasi Muumba.”
Na anyenyekee
kwao na awatekelezee haja zao kwa kupenda na kutarajia malipo kwa Allah Subhanahu
Wataala na wala asiwatazame mtazamo wa kukereka au kuchoshwa nao au kuwadharau,
na wakimwita asiwaitike na huku amekaa
bali awaitike na huku anawakimbilia.
Hadithi inasema: Mwenye kuamka asubuhi na hali wazazi
wake wawili wako radhi na yeye basi huamka na hali amefunguliwa mlango wa
Peponi, na anayeamka na hali amewakasirisha wazazi wake wawili basi huamka na
hali amefunguliwa mlango wa Motoni.
Inamlazimikia baada ya kufa kwao arudie kutubu na
awatembelee marafiki zao na awafanyie wema kwa heshima ya wazazi wake. Ami na
kaka mkubwa ni kama baba, na mjomba na mama mdogo (ndugu ya mama) ni kama mama
inapokuwa baba na mama wamekufa; ni juu yake kuwahishimu hao na vile vile wazee
wa Waislamu.
Imepokewa
kutoka kwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam:-
(رحم
الله والدا لم يحمل ولده على شاق يعصى بتركه)
“Allah
Amrehemu baba ambaye hakumlazimisha mwanawe jambo gumu ambalo huasi kwa
kuliwacha”.
Vile vile mtoto awaombee wazazi wake wawili rehema
baada ya kufariki kwao kama alivyoamuru Allah Subhanahu
Wataala:
ﭽ ﯙ ﯚ
ﯛ ﯜ ﯝ
ﯞ ﭼ
الإسراء: ٢٤
"Sema:
Ee Mola! Warehemu (wazazi wangu) kama wao
walivyonilea na mimi ni bado mdogo."
Imesemwa kuwa mtoto ni (kama) uwa lenye harufu nzuri
(reyhana) katika miaka saba ya mwanzo ya umri wake, kisha katika miaka saba
ifuatayo huwa mtumishi na halafu katika miaka saba mingine huwa mshirika kisha
atakuwa adui au rafiki.
Katika haki za mtoto juu ya baba yake ni kumtafutia
mama mwenye ukoo mzuri na Dini asije akadharauliwa kwa ajili ya hali ya mama
yake.
Amesema Mshairi:-
Ihsani yangu ya mwanzo kwako (mwanangu) ni
kukuchagulia mama mwenye nzuri asili na njema heshima
Amesema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam:
( تخيروا لنطفكم فإن العرق دساس )
"Chagulieni
vizazi vyenu (mama wazuri) kwani mzizi unaendelea chini kwa chini (asili ya
mama na tabia zitadhihirika kwa mtoto)."
Na baada ya kuzaliwa ni juu ya wazazi wake kumchagulia
jina lililo bora kama majina ya Mitume na watu
wema na wamfanyie akika akitimia umri wa siku saba. Akika ni kumchinjia motto
wa mbuzi au kondoo na kugaiwa nyama yake kwa jamaa na majirani. Vile vile
wamhifadhi na vitendo vibaya, na wamfundishe kumjua Allah Subhanahu Wataala na
Mtume wake na kuwajua watu wema. Na wapandikize katika moyo wake chuki ya maovu
na wenye maovu, na wamfundishe Qur'ani na wamhifadhishe. Wamhifadhi asicheze
mwahala mnamochukiza. Akifika miaka saba wamfundishe Sala na wamzoeshe kusali.
Katika wakati wetu huu wa sasa kuna mashule ya
kinidhamu hapana ubaya akipelekwa mtoto kusoma humo lakini kwa sharti mzazi
asiitegemee hiyo shule moja kwa moja bali amchunguze usiku na mchana. Amuulize
nini amejifundisha, wapi amekwenda, vipi amekwenda hata ajue kuwa kuna masuala
ya kuulizwa katika kila harakati yake na asizoee kutoeka nyumbani. Amfanye
mwanawe tangu udogoni amuogope kwani kama
hakumfanyia hivyo kwa kumuonea huruma basi atampoteza na itakuwa vigumu kwake
kumgombeza akiwa mkubwa na atakulia kuwa
hana adabu. Katika maneno ya waliotangulia: Mwenye kumtia adabu mtoto
wake yu ngali mdogo hufurahika naye akiwa mkubwa.
Nimemsikia mtu miongoni mwa wenye akili akisema:-
Ikiwa unampenda mtoto wako sehemu mia ya mapenzi,
usimuonyeshe isipokuwa sehemu moja tu na umfichie sehemu tisini na tisa,
utatengenekewa wewe na atatengenekewa yeye mwenyewe.
Na ampige kwa kuwacha Sala na kuipuuza baada ya kufika
miaka kumi ili mwili wake uchanganyike na utiifu hata ikimfikia taklifu
(ikamuwajibikia ibada) anakuwa tayari kishaijua
ladha ya kumtii Allah Subhanahu Wataala; kwani mtoto mdogo ni kama ardhi iliyo tupu (haijapandwa), cho chote
utakachokipanda ndani yake kitaota, basi tazama kile cha kupanda (kiwe kizuri).
Na katika usia muhimu ninaokuusia ni kuwa yasikufanye
mapenzi ya mwanao umwachie afanye atakalo kwani hayo si mapenzi ijapokuwa
unayachukulia kuwa ni mapenzi. Na muombe Allah Subhanahu Wataala akuepushe
nayo. Asema Mola Subhanahu Wataala:-
ﭽ ﮌ ﮍ
ﮎ ﮏ ﮐ
ﮑ ﮒ ﭼ التغابن:
١٤
"Kwa
yakini baadhi ya wake zenu na watoto wenu ni maadui zenu; basi jihadharini
nao"
Mohammed bin Jaafar alimwambia mwanawe:- Hakika Allah Subhanahu
Wataala ameniridhia mimi kwa ajili yako ndiyo akanihadharisha na mtihani wako,
na hajakuridhia wewe kwa ajili yangu ndiyo akakuusia kwangu (unitii na
usiniasi). Ewe mwanangu mtoto bora ni yule ambaye hisani (ya wazazi wake kwake)
haimpelekei kudharau haki yao
wala upungufu wa hisani haumpelekei kuwaasi.
Vile vile wawatenge baina ya watoto wa kiume na wa
kike katika malazi.
Azidishe baba mtu kumbusu mtoto wake wa kike mdogo kwa
sababu ya ujira mzuri anaopata kwa kufanya hivyo na vile vile kumuepusha
asimchukie kwa hivyo ailazimishe nafsi yake kumbusu binti yake kwani kuchukia
watoto wa kike ni katika masaliyo ya ujinga wa “zama za kijahili”. Ni juu ya
muumini kukubali kila kitokacho kwa Allah Subhanahu Wataala kwani ndicho chenye
kheri na yeye. Mbedui mmoja alimkasirikia mke wake kwa kumzalia mtoto wa kike
na akamhama. Akamtungia shairi kusema: “Ana nini baba yake Hamza haji kwetu
abakia katika nyumba ya pili ameghadhibika kwa sababu hatuzai watoto wa kiume
kwani jambo hilo
haliko katika uwezo wetu, hakika sisi twachukuwa kile tunachopewa”.
Mimi nilikuwa nikiambiwa umepata mtoto wa kike huenda
upesi kumbusu na kumuombea Allah Subhanahu Wataala amuongoze, nafanya hivyo
kuupinga ujahili wa mwanzo (kabla ya Uislamu) na wala simfanyi bora kuliko
mtoto wa kiume kama ilivyo katika ujahili wa
sasa.
Haki za Mke na Mume
ﭽ ﮘ ﮙ ﮚ ﮛ ﮜﮝ
ﮞ ﮟ ﮠ ﭼ البقرة: ٢٢٨
“Nao
(wanawake) wanayo haki kwa sharia (kufanyiwa na waume zao) kama ile haki iliyo
juu yao
kuwafanyia waume zao. Nao wanaume wana daraja zaidi kuliko wao”
ﭽ ﭑ ﭒ ﭓ
ﭔ ﭕ ﭖ ﭗ ﭘ
ﭙ ﭚ ﭛ
ﭜ ﭝ ﭞﭟ
ﭠ ﭡ ﭢ
ﭣ ﭤ ﭥ ﭦﭧ ﭨ
ﭩ ﭪ ﭫ
ﭬ ﭭ ﭮ
ﭯﭰ ﭱ ﭲ
ﭳ ﭴ ﭵ
ﭶﭷ ﭸ ﭹ
ﭺ ﭻ ﭼ ﭼ
النساء: ٣٤
"Wanaume (wawe) ni walinzi wa wanawake kwa sababu Allah
amewafadhilisha baadhi yao kuliko wengine na kwa
sababu ya mali
zao wanazozitoa. Basi wanawake wema ni
wale wenye kutii, wanaojihifadhi (hata) wasipokuwapo (waume zao) kwa kuwa Allah
amewaamrisha wajihifadhi. Na wanawake ambao mnaona uasi wao kwenu waonyeni na
waacheni peke yao
katika vitanda na wapigeni. Na kama
wanakutiini msiwatafutie njia ya kuwaudhi bure. Hakika Allah ndie aliye juu na
Mkuu".
Katika Aya
hii tukufu wanawake wamegawiwa makundi mawili baada ya kupewa mwanamme umbele
kwa ajili ya akili yake na uhodari wa kufanya mambo na uwezo wake wa kuchuma
maisha na kutumia mali .
Kikundi cha kwanza cha wanawake ni wale wanaokikubali hicho cheo alichopewa
mwanamme na Allah Subhanahu Wataala wakawatii waume zao na kuwahifadhi wao na mali
zao, na hao ndio wale wanawake wema wenye kutii, wanaojihifadhi hata
wasipokuwepo waume zao. Kikundi cha pili ni wale wanawake wasiokikubali hicho
cheo alichopewa mwanamme, waliotoka katika tabia zao, hao ndio waasi
wanaotibiwa kwa kuonywa, kukimbiwa na kuachwa peke yao vitandani na kupigwa.
Kila
awachaye tabia yake (katika wanawake) huwa ameasi hata akiridhiwa na mumewe,
maana radhi ya mtu kama huyu haitiwi maanani kwani waume kama
hawa ndio aliowataja Mtume Salallahu Alayhi
Wasalam katika kauli yake:
(كل ديوث في النار)
"Kila
Dayyuuth (Asiyemuonea wivu mkewe) yuko Motoni (ataingia Motoni)."
Nimesema kuwa hawakuharibika wanawake ila baada ya kuharibika wanaume;
waliposhuka wanaume chini ya daraja zao wakashuka wanawake vile vile chini ya
daraja zao.
Vile vile katika haki za mume za kisheria zilizompasa mke ni kumhifadhi
mumewe katika nafsi yake (asimfanyie khiyana) na mali yake na awe mpole kwake na
amliwaze katika shida na amtumainishe na amfanye asihisi upweke. Ikiwa mke hana
sifa hizi basi hautapatikana ule utulivu ambao yeye ameumbwa kwa ajili yake na
ameolewa kwa ajili yake.
Amesema Allah Subhanahu Wataala:
ﭽ ﭱ ﭲ
ﭳ ﭴ ﭵ
ﭶ ﭷ ﭸ
ﭹ ﭺ ﭻ ﭼ الأعراف:
١٨٩
"Yeye
ndie aliyekuumbeni katika nafsi moja na katika (nafsi) hiyo amewaumba wake wao,
ili (kila mwanamme) apate utulivu kwake (mkewe)."
Na mume
anahaki nyingi (kubwa) zinazompasa mke kuzitekeleza kwake. Sheria ya Kiislamu
imezitanguliza kabla ya haki za wazazi wawili.
Amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam:
( لو أمرت أحدا بالسجود لأحد لأمرت المرأة أن
تسجد لزوجها )
"Kama
ningeliamrisha mtu kumsujudia mtu (mwingine) basi ningeliamrisha mke kumsujudia
mumewe."
Na amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam:
( لو لحسته
من قرن لقدم قيحا، ما أدت حقه )
"Kama
(mwanamke) angemramba (mumewe) usaha kutoka kichwani mpaka mguuni (angekuwa na
majeraha yatoka usaha kutoka kichwani mpaka mguuni) bado angekuwa hakutekeleza
haki yake."
Ikiwa mume
atamkataza mke kufanya kitu lazima amtii hata kwa mfano akamkataza kufunga
sunna au kusali sunna, je vipi akimkataza kufanya kitu kilichokuwa na maasi ya
Allah Subhanahu Wataala, basi ikiwa atampinga, Malaika watamlaani mpaka atakaporejea
na akifa katika hali hiyo ya kumuasi mumewe ataingizwa Motoni.
Na katika
haki za mke zilizo juu ya mumewe awe mpole kwake na amuonee huruma.
Amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam:
( خيركم خيركم لأهله و أنا خيركم لأهلي)
“Mbora wenu
ni yule aliye mbora wenu kwa ahli zake (mkewe, wanawe na watu wa nyumbani kwake)
na mimi ni mbora wenu kwa ahli zangu”.
Ni wajibu
wa mume kumstahmilia mkewe akikosea kwani hakuna binaadamu anaekosa upungufu
isipokuwa mwenye kuletewa ujumbe Mtume muaminifu Salallahu Alayhi Wasalam.
Mwanamme asimdhihirishie mkewe kuwa amchukia hata ikiwa amchukia.
Amesema
Mola Subhanahu Wataala:
ﭽ
ﯢ ﯣﯤ
ﯥ ﯦ ﯧ
ﯨ ﯩ ﯪ
ﯫ ﯬ ﯭ
ﯮ ﯯ ﭼالنساء: ١٩
“Na kaeni
nao kwa wema; na kama mkiwachukia (basi
msiwaache) kwani huenda mkakichukia kitu na Allah ametia kheri nyingi ndani
yake”.
Na anasema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam:
( لا
يفرك مؤمن مؤمنة إن كره منها خلقا رضي منها آخر )
"Muumin
(mume) asimchukie Muumin (mke) kwani akichukia moja katika tabia zake (bila
shaka) huridhika na nyingine (katika tabia zake)."
Na juu ya
mume kutomdhiki mkewe katika matumizi na amtimizie kila lililo wajibu wake
katika haki (za mke).
Amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam:
( استوصوا
بالنساء خيراً فإنكم أخذ تموهن بأمانة الله واستحللتم فروجهن بكلمة الله )
"Usianeni kuwafanyia
wake zenu wema kwani mumewachukua kwa amana ya Allah na mmejihalalishia tupu
zao kwa neno la Allah."
Na cha
mwisho alichousia juu yake Mtume Salallahu Alayhi Wasalam kabla ya kufariki ni
mke na mtumwa.
Vile vile
ni juu ya mume amfundishe mkewe mambo ya Dini yake ikiwa yeye ni mjuzi zaidi
katika Dini khasa kujiosha janaba, hedhi na ujusi na kujihifadhi na najisi na
mengineyo yaliyo lazima kuyajua.
Amesema
Allah Subhanahu Wataala:
ﭽ ﯛ ﯜ
ﯝ ﯞ ﯟ
ﯠ ﯡ ﭼ التحريم: ٦
“Enyi Mlioamini, jiokoeni
nafsi zenu na watu wenu na Moto”.
Mola
amemsifu Mtume wake Ismaeel (A.S) kwa kusema:
ﭽ ﭮ ﭯ
ﭰ ﭱ ﭲ
ﭳ ﭴ ﭵ
ﭶ ﭼ
مريم: ٥٥
“Na alikuwa akiwaamrisha
watu wake Sala na Zaka na alikuwa mridhiwa mbele ya Mola wake”.
Na juu ya
mke na mume, wasitoleane siri zao, wala wasimwambie mtu mambo wayafanyayo
wanapoingiliana, kwa sababu afanyaye hivyo huwa ni kama
aliyemuingilia mkewe mbele ya watu.
Kupiga
ponyeto ni zinaa. Nako ni kujichezea mtu utupu wake mpaka ukatoka manii, na hilo licha ya
kuharimishwa kwake pia linaleta madhara kwa alifanyaye, huleta maradhi na
kuleta machofu, na huenda ikawa hawezi kujimiliki nafsi yake kila inapotikisika
dhakari yake humtoka manii sawa akiwa amejitayarisha kwa hayo au
hakujitayarisha. Watu wengi wamepatwa na magonjwa kama
haya. Basi udhia huu anaoupata mtu kwa kufanya kitendo hichi unamtosha kukiacha
kama kingekuwa halali, vipi nacho ni haramu?
Mtume
Salallahu Alayhi Wasalam amewausia vijana wafunge Saumu na amesema:- “Enyi
vijana! Mwenye uwezo kati yenu wa kuoa basi na aoe, na asiyeweza basi na afunge
kwa sababu Saumu itamzuilia matamanio”.
Wako katika
vijana waliotumia Saumu na wakafanikiwa. Basi vijana watahadhari na wafanye
subira juu ya awali ya ujana hasa katika wakati wetu huu ambao mahari yamekuwa
makubwa na ufisadi umezidi. Na mambo yote ni ya Allah tokea mwanzo mpaka mwisho
na hakuna uwezo wala nguvu isipokuwa Kwake Mola Subhanahu Wataala.
Amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam: Hakuacha ndugu yangu Jibril (A.S) anisisitiza
kuniusia juu ya jirani hata nikadhania kuwa atamrithisha (jirani amrithi jirani
yake).
Majirani ni
wa namna tatu:-
Jirani
mwenye haki moja – huyo ni jirani mushrik anayo haki ya ujirani.
Jirani
mwenye haki mbili – huyo ni Muislamu anayo haki ya ujirani na haki ya Uislamu.
Jirani
mwenye haki tatu – huyu ni Muslamu aliye na uhusiano wa damu – anayo haki ya
ujirani, haki ya Uislamu na haki ya uhusiano wa damu.
Namna zote
tatu za majirani wana haki zao, nazo kuwa wasiudhiwe na kuwastahimilia maudhi
yao, wanasihiwe pindi wakenda mwendo mbaya, wapewe hongera kwa furaha zao
(mkono wa furaha) wapewe rambirambi kwa misiba yao (waaziwe), wagawiwe sehemu
ya vitu tunu waliokuwa hawanavyo pindi wakipata habari ya kuweko (vitu hivi kwa
jirani yake), kutopeleleza aibu zao na kutotowa siri zao, kuwatekelezea haja
zao na kumsaidia muhitaji wao.
Inasemekana
kuwa jirani atamshika jirani yake kesho na kushitaki akisema: “Ameninyima
hisani yake”.
Mtume Salallahu
Alayhi Wasalam amesema:
( من كان
يؤمن بالله و اليوم الآخر فليكرم ضيفه )
"Anayemuamini
Allah Subhanahu Wataala na Siku ya mwisho (Kiyama) basi naamkirimu mgeni wake."
Katika haki
za mgeni ni kumshughulikia, kumtengenezea mambo yake, kuwa mpole nae kumkirimu
kwa chakula na kinywaji na mahali pa zuri pa kulala. Asifanye jambo mbele yake
ambalo litamfanya awe mnyonge kama kumpiga
mtoto wake au mfanyakazi wake au hata kuwagombeza. Amsindikize mpaka mlangoni
wakati anapotoka nyumbani na amkaribishe kwa furaha na bashasha aingiapo
nyumbani
Anasema Tegemeo la Maimamu (Mohammed bin Yusuf
Attfeish) Allah Amrehemu: “Wala hana haki mgeni wa kishetani”. Huyo ni yule
aliyetoka kwake ili kufanya maasi au kuwakatia watu njia (kuwaibia),
anayeitukana Dini ya Kiislamu, aupigae vita Uislamu, mzinifu, na aliepigwa
pande na Waislamu. Basi hao wote hawana haki yoyote katika haki za wageni.
Amaeongezea Sheikh Abu Is-haaq Attfeish juu ya kauli yake (Sheikh Mohammed bin
Yusuf Attfeish) anaeitukana Dini ya Waislamu kwa kauli yake: Na wale
wanaoonyesha aibu za Waislamu (jasusi) kwani hao wawili katika mtazamo wa
Sheria ni sawasawa, bali aliekuwa mbaya zaidi ni huyu wa mwisho na khabithi wao
na ana madhara makubwa zaidi kwa Umma wa Kiislamu na Dini, kwasababu yeye ni
jicho la adui kila akiona kuwa Umma unapata nguvu ya mali au hali huwapa habari
madhalimu ili wapige vita kila nguvu au maendeleo katika taifa dhaifu, na humpa
habari mtawala wa kimabavu anaefanya uwezo wa juhudi yake kuwapiga vita
wananchi duni hali ya kuwa wako katika ghafla ili ateketeze kila walichokuwa
nacho kwa ajili ya maslaha yake na matamanio yake.
Basi khaini
au jasusi ajidhuru zaidi yeye mwenyewe kuliko kitu kingine kwa sababu anapiga
vita kile kinacholeta manufaa na furaha kwa Umma wake ambao yeye hufurahika kwa
furaha yake (huo Umma) na hupata tabu kwa tabu yake (Umma). Anabomoa kila
heshima anayostahiki kuipata yeye, watoto wake na wajukuu zake, basi ni adui wa
nafsi yake na adui wa watu wake kwa hiyo ni wajibu kumnyima kila haki
inayompasa. Kwani huyo hana heshima yoyote na Muislamu humtilia shaka mtu kama
huyo kama anayo Imani yoyote, vinginevyo vipi
aliye na imani hata chembe atakuwa ndio chombo cha kubomoa Dini yake na
kuharibu nchi yake (watani wake). Hakika ni katika kuikhini ile amana
aliyoibeba mja kutoka kwa Allah Subhanahu Wataala na khiyana ya Umma na
kuwadhuru Waislamu kuwa mtu huwa pamoja na watu (Waislamu) kisha akageuka
jasusi juu yao
na kuifanya hiyo ndio kazi yake. Hii ni sifa mbaya iliyoje kuwa nayo mtu mbele
ya watu.
Imedhihiri
shari hii mnamo wengi katika wana wa Kiislamu wanaifanya kwa ladha kubwa na wao
wajidai kuwa ni Waislamu na kumbe Uislamu wajiepusha nao (watabarraa nao).
Inamtosha
mtu hasara anayoipata hapa Duniani ya kukosa tawfiiq ya Allah Subhanahu Wataala
(yaani hamnusuru wala hampi msaada) hata ametokana na Dini na Waislamu kwa
ajili ya kuwahudumia wale wanaoifanyia vitimbi Dini na Waislamu, kisha Akhera
anakuwa katika waliohasirika.
Hakuna
jambo lenye sharafu kubwa kwa (Muislamu) kuwa kama
ngome inayokinga Umma wake na vile vile kuwa na Ikhlasi na Dini yake na watani
wake kwani ameumbiwa kwa ajili ya hivyo viwili. Hakuna Salama kwa jamii ila kwa
ukweli wa watu wake na kufanya kila lenye maslaha kwake. Na ataulizwa kila
mmoja wetu katika siku ambayo kila nafsi italipwa kwa ilichokitenda. Hapa
yamekwisha maneno ya Abu Is-haaq Allah Amrehemu.
Mpita njia
ni mtu aliyeachana na watani wake na mali yake. Huyu ashughulikiwe zaidi
kuliko mgeni kwani yeye anahitajia zaidi. Inamlazimu anayempata huyu
amkaribishe na kumkirimu vizuri na amsaidie anayoyahitaji katika safari yake na
apewe kutokana na mali ya
wakfu, mali
ya msikiti au Zaka ijapokuwa yeye ni tajiri kwake.
Huyu
mwenzio katika safari ana haki ya usuhuba na kumliwaza kwa kumpa chakula
safarini na kumhudumu na kumpa anachokihitajia safarini na kumtanguliza kabla
ya nafsi yako usimuudhi na umkinge na maudhia na wala usimtoe kwa anaetaka
kumfanyia ubaya. Anaependwa zaidi katika wao na Allah Subhanahu Wataala aliye
mpole zaidi kwa mwenziwe. Na wala mtu hana ubora zaidi kuliko mwenzake
isipokuwa kwa kumcha Allah. Hakika mtu ni mkubwa kwa kushikana na mwenzake wala
hana heri rafiki aliekuwa hakupendelei anacho kipendelea nafsi yake. Rafiki
bora ni yule anayemsaidia mwenye kukumbuka na anamsaidia mwenye kusahau.
Amesema haya Qutub Al-Aima.
Haki za Wote (Ujumla)
Kuwafanyia
wema mayatima na masikini na wenye haja kama
ilivyopokelewa kutoka kwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam:
( المسلمون كالبنيان يشد بعضه
بعض ، وكالجسد إذا اشتكى منه عضو تداعى له سائر الجسد بالسهر والحمى )
و (كاليدين تغسل إحداهما الأخرى )
و (لا تجسسوا ولا تحسسوا ولا تقاطعوا ولا تدابروا وكونوا
عباد الله إخواناً )
“Waislamu
ni kama jengo (moja), kila sehemu inatiliya nguvu sehemu nyingine na ni kama
kiwili wili, kikishtaki kiungo kimoja basi mwili mzima hupata maumivu na homa
na kukosa usingizi” na “Kama mikono miwili kila mmoja wao unauosha mwingine” na
“Msichunguzane na msipelelezane na msipigane pande na msifanyiane vitimbi na
kuweni waja wa Allah (mnapendana kama) ndugu.”
Kukidhi
haja ya Muislamu na kwenda kwa ajili ya kuikidhi ni bora zaidi kuliko kufanya
“Itikaaf” muda wa miezi miwili. Na inakupasa umpendelee ndugu yako (wa
Kiislamu) kama unavyojipendelea nafsi yako. Na
anaemuudhi Muislamu amelaaniwa. Na aliyesalimika ni yule aliyewasalimisha watu
na ulimi wake na mkono wake.
Na katika
haki za ujumla kumtolea Salamu umuonae. Amepokea Muslim hadithi ya Mtume
Salallahu Alayhi Wasalam:
( لا تدخلو الجنة حتى تؤمنوا ،
ولا تؤمنوا حتى تحابوا ، أولا أدلكم على شيء إذا فعلتموه تحاببتم .... أفشوا السلام بينكم )
“Hamuingii
Peponi mpaka muamini, na hamuamini mpaka mpendane. Je! Nikujulisheni jambo
ambalo mkilifanya mtapendana? Toleaneni Salamu”.
Na katika
haki vile vile kutaka idhini kabla ya kuingia majumbani. Na msipopewa idhini
basi msiingie. Asema Allah Subhanahu Wataala :
ﭽ
ﯯ ﯰ
ﯱ ﯲ ﯳ
ﯴ ﯵ ﯶ
ﯷ ﯸ ﯹ
ﯺ ﯻﯼ ﯽ
ﯾ ﯿ ﰀ
ﰁ ﰂ ﭑ ﭒ ﭓ
ﭔ ﭕ ﭖ ﭗ ﭘ
ﭙ ﭚﭛ ﭜ
ﭝ ﭞ ﭟ
ﭠﭡ ﭢ ﭣ
ﭤﭥ ﭦ ﭧ
ﭨ ﭩ ﭪ ﭼ النور:
٢٧ - ٢٨
“Enyi
Mlioamini! Msiingie nyumba ambazo si zenu mpaka muombe ruhusa, (mpige hodi) na
muwatolee Salamu waliomo humo. Hayo ni bora kwenu; huenda mtakumbuka (mkaona ni
mazuri haya mnayoambiwa). Na kama hamtamkuta
humo yeyote, basi msiingie mpaka mruhusiwe. Na mkiambiwa “Rudini”, basi rudini;
hili ni takaso kwenu. Na Allah anajua mnayoyatenda”.
Vilevile
kumpa mkono ndugu yako ukikutana nae na kuwakumbatia wazee wawili na kaka
mkubwa na kuwabusu watoto.
Na katika
kumtukuza Allah ni kumtukuza mzee na kumtukuza mwenye elimu, pia katika sunna
kuwa na uso mkunjufu kwa watu, na kuwa na bashasha nao isipokuwa wale wazushi
(wenye “bidaa”) hao haifai kuwakunjulia uso. Mfano wa hao kama mwenye kunyoa
ndevu, au mwenye kuvaa dhahabu katika shingo yake au mkononi kwani kuwafanyia
bashasha kama hao kuwasababisha watopee katika uzushi wao isipokuwa ukikusudia
(kwa bashasha yako hiyo) kitu kingine (kama
kumlainisha moyo wake aongoke kwenye njia ya kheri) basi hapo tena mezani ni
nafsi yako na niya yako.
((Na mola anayajua yaliyo
siri na yaliyofichika))
Na katika
sunna ni kuitumia Dunia kwa kuitia nguvu Dini ya Allah Subhanahu Wataala
(Al-Mudaaraah) na kuna tafauti baina yake na kuitumia Dini kwa ajili ya maslaha
ya Dunia (hii sifa mbaya haitakiwi Muislamu awe nayo inaitwa Mudaahanah).
Vile vile
katika haki za wote ni kupatanisha baina ya Waislamu na kufanya juhudi ili
waliozozana wakubali mapatano. Pia miongoni mwa haki ni kumuombea Dua apigaye chafya,
amwambie يرحمك
الله ikiwa baada ya kupiga chafya atasema الحمد
لله na ikiwa hakusema hatapewa haki hiyo (ya kuombewa
Dua), na mwenye mafua akenda chafya vile vile hana haki hiyo. Katika haki vile
vile kumtembelea mgonjwa, na anaemtembelea mgonjwa huwa ameingia katika
mabustani ya Peponi, na anaekaa nae ni kama
aliekaa katika mabustani ya Pepo. Na inatakiwa afupishe kikao chake kwa
mgonjwa. Vile vile afuate jeneza la Muislamu na anayefanya hivyo hupata malipo
(makubwa) “Qiiraat” na ukubwa wake ni kama mlima
wa “Uhud”.
Inasemekana kuwa kuna mambo kumi Allah humpa
ampendaye.
1. Kusema ukweli.
2. Kumpa aombaye.
3. Kumlipa mwenzako kwa kilicho bora zaidi.
4. Kuwasiliana na jamaa waliokuhusu.
5. Kuhifadhi amana.
6. Kumkirimu mgeni.
7. Kusamehe.
8. Kumhishimu jirani.
9. Kumhishimu mwenzako.
10. Kuwa na
haya na ndio kubwa yao .
Kikao cha
elimu ni bora kuliko kikao chochote kingine. Inasemwa kuwa kikao kimoja kizuri
(cha elimu) kinafuta madhambi ya vikao elfu mbili elfu (milioni mbili) viovu.
Na hawakai kwa kumkumbuka Mola wao isipokuwa wazungukwa na Malaika na wafunikwa
na Rehema (za Allah) na Allah awataja kwa aliokuwa nao (Malaika), kikao cha
elimu ni bora kuliko kusali rakaa elfu (sunna), kufunga siku elfu, kutoa sadaka
dirhamu elfu, Hija elfu, kupigana Vita elfu isipokuwa yaliyo faridha. Kwa
sababu Allah aabudiwa kwa elimu, atiiwa kwa elimu basi nyumba mbili (Dunia na
Akhera) ubora wake huja kwa elimu na ushari wake ni kwa ujinga. Aseme mtu
akihudhuria (majlis) kikao cha elimu:-
أشهد
أن لا إله إلا الله وأن محمدا عبده ورسوله و أشهد أن الدين كما شرع وأن إلاسلام كما وصف، وأن الكتاب كما نزل وأن القول كما حدث وأن الله هو الحق المبين ذكر
الله محمدا بخير وصلى عليه وحياه بالسلام
Haya yote
ameyaleta Qutub Al-Aimma.
Maneno haya
yametokana na Sheikh Ahmed Al-Khaliliy Mufti Mkuu wa Sultanate ya Oman :
Suala – Je
wenye madhambi makubwa watapata uombezi Akhera ikiwa wamekufa katika hali hiyo
ya maasi?
Jawabu:
Nataka kumjulisha huyo muulizaji na wengineo kuwa Qur’ani Tukufu imetuletea katika
Aya nyingi kuwa kila afanyaye mema hulipwa kwa aliyoyafanya na aliyefanya maovu
kadhalika hulipwa kwa aliyoyafanya. Na amehadharisha Allah Subhanahu Wataala
Umma huu (wa Kiislamu) kwa kudanganyika
na matamanio. Amesema Mola Subhanahu Wataala:
ﭽ
ﭩ ﭪ
ﭫ ﭬ ﭭ
ﭮﭯ ﭰ ﭱ
ﭲ ﭳ ﭴ
ﭵ ﭶ ﭷ
ﭸ ﭹ ﭺ
ﭻ ﭼ ﭽ ﭼ
النساء: ١٢٣
“(Kuingia Peponi) si kwa matamanio yenu, wala si kwa
matamanio ya watu waliopewa kitabu (kabla yenu, lakini mambo ni haya):
Atakayefanya ubaya atalipwa, wala hatapata mlinzi wala msaidizi kwa ajili yake
mbele ya Allah.”
Na katika
kutaja matamanio ya watu waliopewa kitabu pamoja na matamanio ya Umma huu kuna
ishara kuwa baadhi ya watu wa Umma huu watadanganyika kama walivyodanganyika
hao waliopewa kitabu na watayan`gan`gania hayo matamanio wakimtarajia Allah Subhanahu
Wataala kuwa atawaghufiria madhambi yao
kwa kuwemo kwao tu katika Dini hii na kumuamini Mtume Salallahu Alayhi Wasalam.
Pia katika
kutaja matamanio ya watu waliopewa kitabu pamoja na matamanio ya Umma huu kuna
mahadhirisho kwa Umma huu kufuata mwendo ule ule wa waliopewa kitabu ili kila
mmoja (katika Umma huu) achukue hadhari na ajitahidi awezavyo kumtii Allah Subhanahu
Wataala. Na kuna Aya nyingi katika
Qurani zinazotilia nguvu yaliyokuja katika Aya hii (iliyo hapo juu) ya kuwa
kila mtu atalipwa kwa mujibu wa vitendo vyake. Katika hizo ni kauli yake Allah Subhanahu
Wataala:
ﭽ ﭑ ﭒ ﭓ
ﭔ ﭕ ﭖ ﭗ ﭘ
ﭙ ﭚ ﭛ
ﭜ ﭝ ﭞ
ﭟ ﭠ ﭡ
ﭢ ﭣ ﭤ
ﭥ ﭦ ﭧ
ﭨ ﭩ ﭪ ﭼ
النمل: ٨٩ - ٩٠
“Watakaoleta mema watapata mema kuliko hayo, nao katika mahangaiko ya
siku hiyo watasalimika nayo. Na
watakaoleta ubaya, basi zitasinukishwa nyuso zao Motoni: Waambiwe kwani
mnalipwa kwa mengine isipokuwa yale mliyokuwa mkiyatenda?”
Na kauli
yake Allah Subhanahu Wataala:
ﭽ
ﯷ ﯸ
ﯹ ﯺ ﯻ
ﯼﯽ ﯾ ﯿ
ﰀ ﰁ ﰂ
ﰃ ﰄ ﰅ
ﰆ ﰇ ﰈ
ﰉ ﭼ القصص: ٨٤
“Atakayefanya wema atapata jaza bora kuliko huo wema aliofanya, na
atakaye fanya ubaya basi hawatalipwa wale wafanyao ubaya ila yale waliyokuwa
wakiyafanya.”
Na hizi Aya
ziko wazi kabisa hazikubali upinzani kuwa Allah Subhanahu Wataala amlipa kila
mtu kwa vitendo vyake vikiwa vizuri au vibaya. Vile vile amebainisha Allah Subhanahu
Wataala kuwa yeye husamehe madhambi ya waliotubu siyo madhambi ya wanaoshikilia
kufanya maasi.
Amesema
Mola Alietukuka:-
ﭽ ﮕ ﮖ
ﮗ ﮘ ﮙ
ﮚ ﮛ ﮜ
ﮝ ﭼ
طه: ٨٢
“Na hakika mimi ni msamehevu
sana kwa
anayetubia na kuamini na kutenda mema, tena akashika uongofu(barabara).”
Amebainisha
Subhanahu Wataalaa kuwa anasamehe mabaya ya wale wanaojiepusha na maasi makubwa
yaani anasamehe madhambi madogo sio madhambi makubwa, na hasamehe dhambi ndogo
isipokuwa kwa kujiepusha na madhambi makubwa, na sharti kutoendelea kuyafanya
hayo madhambi madogo kwa kauli yake Subhanahu Wataala:
ﭽ ﮒ ﮓ ﮔ
ﮕ ﮖ ﮗ ﮘ ﮙ
ﮚ ﮛ ﮜ
ﮝ ﭼ
النساء: ٣١
“Kama mkijiepusha na maovu makubwa mnayokatazwa, tutakufutieni makosa
yenu madogo na tutakuingizeni mahala patukufu kabisa (Napo
ni Peponi).”
Basi
akielewa mtu hayo atakuwa amefahamu maana ya kauli yake Mola Subhanahu Wataala:
ﭽ ﮢ ﮣ
ﮤ ﮥ ﮦ
ﮧ ﮨ ﮩ
ﮪ ﮫ ﮬ
ﮭ ﮮ ﭼ النساء:
٤٨
“Hakika Allah hasamehe kushirikishwa, na husamehe yasiyokuwa
haya kwa amtakaye”.
Allah
husamehe yasiyokuwa shirki kwa amtakaye ama kwa kutubia na kuacha kufanya
madhambi makubwa na kurejea kwa Allah Subhanahu Wataala au kwa kujiepusha
madhambi makubwa pamoja na kufanya madhambi madogo bila ya kukusudia kuendelea
nayo na bila ya kuendelea kuyafanya.
Haya ndiyo
yaliyokusudiwa kwa kauli yake Subhanahu Wataala:
ﭽ ﮩ
ﮪ ﮫ ﮬ
ﮭ ﮮﭼ النساء:
٤٨
“Na husamehe yasiyokuwa haya
kwa amtakaye”.
Kwani
amebainisha Mola Subhanahu Wataala katika Aya nyinginezo wale anaotaka
kuwasamehe, nao ni wale wanaojiepusha na madhambi makubwa na wala hawaendelei
na kufanya madhambi madogo madogo. Imekuja hadithi kutoka kwa Mtume Salallahu
Alayhi Wasalam (kutilia nguvu haya):
(لا صغيرة
مع إصرار ولا كبيرة مع استغفار )
“Hakuna dhambi ndogo ikiwa
itaendelea kufanywa (hugeuka kubwa) na hakuna dhambi kubwa pamoja na kutubia”
Vile vile
Mola Subhanahu Wataala amehadharisha na mategemeo ya kughufiriwa madhambi na
amebainisha kuwa kila mtu atalipwa kwa aliyoyafanya. Amehadhirisha vile vile na
mategemeo ya kupata uombezi, na kuhadhirishwa huku kumeletwa kwa Umma huu.
Amesema kuwaambia Waumini:
ﭽ
ﮌ ﮍ
ﮎ ﮏ ﮐ
ﮑ ﮒ ﮓ
ﮔ ﮕ ﮖ
ﮗ ﮘ ﮙ
ﮚ ﮛ ﮜ
ﮝﮞ ﮟ ﮠ
ﮡ ﭼ البقرة: ٢٥٤
“Enyi Mlioamini!
Toeni katika vile tulivyokupeni kabla haijafika siku ambayo hapatakuwa
kujikomboa wala urafiki (wa kusaidiana) wala uombezi. Na waliokufuru ndio
waliojidhulumu kweli kweli”
Katika haya
pia kuna mahadharisho kwa Umma huu na kwa wengine kuhusu kushikilia matarajio
ya uombezi. Kuwa mtu watamuombea Manabii Siku ya Kiyama na kwa hivyo ataepuka
na adhabu. Basi Allah Subhanahu Wataala amebainisha nani wanaostahiki uombezi
wa Mitume na wengineo katika kauli yake:-
ﭽ ﭹ ﭺ
ﭻ ﭼ ﭽ ﭼ
الأنبياء: ٢٨
“Na hawamuombei (yoyote) ila
yule anayemridhia (mwenyewe Mola).”
(Na ziko Aya nyingi zenye
maana hiyo).
Basi
Uombezi anaustahiki yule aliyeridhiwa (na Mola Subhanahu Wataala) pasipo
mwingine, na ikiwa aliyeridhiwa ndio mwenye haki ya kuingia Peponi basi huenda
akatubia mwenye kutubu kutokana na maasi yake akaujalia Allah (Subhanahu
Wataala) huo Uombezi (atakaopewa) ukachangia katika kukubaliwa toba yake.
Ama wale
wanaoendelea kufanya madhambi makubwa (bila ya kutubu na wakafa katika hali
hiyo) basi hao hawapati Uombezi kutokana na Aya hizi zilizo wazi kabisa.
No comments:
Post a Comment
Note: only a member of this blog may post a comment.