Katika maradhi yanayomganda
Muislamu ni maradhi ya jicho.
Jicho ndio kiongozi wa viungo katika heri na shari. Na maradhi ya
kutazama ni maradhi makubwa, inataka Muislamu ajihifadhi na ubaya wake (fitina
yake) juu ya uzito wa kujihifadhi nayo, lakini inawezekana kuwa mwepesi wa
kujihifadhi nayo kwa kutanabahi na hayo. Maradhi yote (ya nafsi) asili yake ni
kutazama. Kuna methali inayosema:-
“Kutazamana (kwanza) kisha kuchekeana halafu kuamkiana kisha kuzungumza
kisha kupeana miadi na kukutana”. Kwa
hiyo kitu cha kwanza ni kutazama. Lakini mja hahisabiwi kwa mtazamo wa mwanzo
kwa mujibu wa kauli yake Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
( لك الأولى وعليك الثانية )
“Mtazamo wa kwanza ni wako
(huhisabiwi nao kuwa ni kosa) na wa pili ni juu yako (wahisabiwa nao)”.
Ukifuatilia mtazamo mtazamo mwengine unazidi katika jicho lake uzuri
wa huyo anaetazamwa hata ikiwa si mzuri kwani sheitani anampambia aliye mbaya
na pengine asifanikiwe kupata kile alichokitaka kutokana na huyo aliyemtaka. Na
juu ya hivyo amekuwa kisha pambiwa (na shaitani) na kila akikaa humfikiria basi
hiyo ndiyo khasara kubwa Siku ya Kiyama. Na Allah Subhanahu Wataala peke yake ndiye
anayejua ukubwa wa khasara hiyo. Basi inatakiwa wakati anapotazama
kilichoharamishwa na ikaifatilia nafsi yake hicho kitu hapo anavutika kurudia
kutazama (mtazamo wa pili) basi na aizuie nafsi yake asifanye hivyo kwani
mtazamo wa pili ndio ujinga wenyewe unaosababisha maradhi mengi katika moyo
wake. Na akilihifadhi jicho lake
kutazama basi ni njia ya
kuponesha hayo maradhi yaliyo katika moyo wake. Ikiwa halihifadhi jicho lake basi
hataweza kuvihifadhi viungo vyake vingine na huenda akaingia katika balaa kubwa
haiwezi. Amesema Nabii wa Allah Issa
AS :-
( إياكم والنظرة فإنها تزرع في القلب شهوة وكفى بها من فتنة )
“Jiepushe na kutazama
(vilivyoharimishwa) kwani hupanda katika moyo matamanio yatosha peke yake hayo
kuwa ni fitina (upotofu).”
Amesema Nabii wa Allah Dawood AS kumwambia
mtoto wake Suleiman AS :-
( يا بني امش
خلف الأسد والأسود ولا تمش خلف المرأة )
“Ewe mwanangu tembea nyuma
ya simba na simba wengi wala usitembee nyuma ya mwanamke.”
Aliulizwa Nabii Yahya AS:- Kitu gani
kinachotangulia zinaa? Akajibu:-
Kutazama na kutamani.
Amesema Ibliis: Kutazama ni upinde wangu wa
zamani na mshare wangu ambavyo sikosei nikipiga kwavyo.
Imetolewa kutokana na Mtume Salallahu Alayhi
Wasalam amesema:-
( النظرة سهم
مسموم من سهام إبليس فمن تركها خوفاً من الله تعالى أعطاه الله تعالى إيماناً يجد
حلاوته في قلبه )
“Kutazama ni mshare wa sumu miongoni mwa
mishare ya Ibliis mwenye kuacha kwa kumuogopa Allah Subhanahu Wataala anampa
Allah Subhanahu Wataala Imani anaupata utamu wake katika moyo wake”.
Na anasema Salallahu Alayhi Wasalam:-
( ما تركت بعدي فتنة أضر على
الرجال من النساء )
“Sikuacha baada yangu fitina
iliyo na madhara kwa wanaume zaidi kuliko (fitina ya) wanawake.”
Na amesema Salallahu Alayhi Wasalam:-
( اتقوا فتنة
الدنيا وفتنة النساء فإن أول فتنة بني إسرائيل كانت من قبل النساء )
“Ogopeni fitina ya Dunia na fitina ya
wanawake kwani fitina ya kwanza ya Bani Israeel ilikuwa kutokana na wanawake.”
Ameitoa Abu Saeed. Amesema Mtume Salallahu
Alayhi Wasalam :-
( لكل ابن آدم
حظ من الزنا فالعينان تزنيان وزناهما النظر واليدان تزنيان وزناهما البطش والرجلان
تزنيان وزناهما المشي والفم يزني وزناه القبلة والقلب يهم أو يتمنى ويصدق ذلك
الفرج أو يكذبه )
“Kila binadamu ana sehemu
yake katika zinaa kwani macho yazini na zinaa yake ni kutazama na mikono yazini
na zinaa yake ni kushika na miguu yazini na zinaa yake ni kwenda na mdomo
wazini na zina yake ni kubusu na moyo wawa na hamu au watamani na utupu
unakubali hayo (kwa kufuata amri na matamanio ya moyo) au wakadhibisha (yaani
wakataa).” Ameitoa hadithi hii Abu Huraira.
Amesema Ummu Salamah ametaka idhini Ibn Ummu
Maktoum ‘kipofu’ kwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam kuingia nyumbani na mimi na
Maimuna tumekaa akasema AS: Jifunikeni! Tukasema kwani yeye si kipofu, haoni? Akasema AS :
Je nyinyi hamuoni? Na katika hadithi ya Arrabii Allah Subhanahu Wataala
Amrehemu: Je nyinyi vipofu?
Kwa hiyo hadithi hii ni dalili ya kuwakataza
wanawake wasiwatizame wanaume hata vipofu.
Yasemekana kulikuwa na mtu mwema anaadhini
katika msikiti fulani miaka mingi alikuwa hafarikiani na adhana na watu
walikuwa wakimuona katika miongoni mwa watu bora zaidi wa zama zake. Siku moja
akapanda katika mnara wa msikiti akatazama chini yake akamuona binti wa
kinasara yuko nyumbani mwake akarudisha mtazamo(wa pili), akawa hawezi kuondoka hapo mnarani, yule binti wa
kinasara akamuona wakawa watupiana macho yule binti akamuashiria apindukie
ukuta ili amfikie basi katika kupindukia ukuta akaanguka na akafa nyumbani
mwake (yule binti) kabla ya kupata haja yake, twamuomba Allah Subhanahu Wataala
atuepushie vitangulizi vya maangamivu.
Yasemekana kuwa mtu mmoja miongoni mwa taabiina
alikuwa amehifadhi Qur’ani kamili na amehifadhi hadithi nyingi katika hadithi
za Mtume Salallahu Alayhi Wasalam basi akatokea kumuona mwanamke wa kinasara
akauchukua moyo wake (kampenda sana )
akamfuata na huyo mwanamke akamridhia kwa mapendekezo yake lakini kwa sharti
atoke katika Uislamu akakubali kutoka. Allah Subhanahu
Wataala atuepushie hayo; akaishi naye muda katika mji wa Antakiya. Na siku hiyo
baadhi ya marafiki zake walipita Antakiya wakauliza juu yake wakaambiwa yuko
mahali fulani wakamuendea wakamkuta achunga nguruwe wakamuuliza juu ya hali
yake akawajibu muombeni Allah awaepushe na kila maovu. Wakamwambia ulikuwa
umehifadhi Qur’ani na umehifadhi nyingi miongoni mwa hadithi za Mtume Salallahu
Alayhi Wasalam akawajibu haikubakia Qur’ani kwangu isipokuwa Aya mbili:-
ﭽ ﭯ ﭰ ﭱ
ﭲ ﭳ ﭴ ﭵ ﭶ
ﭷ ﭸ ﭹ
ﭺ ﭻ ﭼ
آل عمران: ٨٥
“Na anayetaka Dini isiyokuwa ya Kiislamu basi haitakubaliwa
kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenye khasara (kubwa kabisa).”
ﭽ
ﮘ ﮙ
ﮚ ﮛ ﮜ
ﮝ ﮞ ﮟ
ﮠ ﮡ ﮢ
ﮣ ﮤ ﮥﮦ
ﮧ ﮨ ﮩﮪ
ﮫ ﮬ ﮭ ﭼ البقرة: ٢١٧
“Na watakaotoka katika Dini yao
katika nyinyi kisha wakafa hali ya kuwa makafiri, basi hao ndio ambao amali zao
zimeharibika katika Dunia na Akhera. Nao ndio watu wa Motoni, humo watakaa
milele”.
Na katika hadithi imebakia kwangu hadithi moja nayo: من بدل دينه فاقتلوه Anaebadili Dini yake
basi muuweni (Anayetoka katika Dini ya Uislamu auliwe). Hakuna uwezo wala nguvu
isipokuwa kwa Allah Subhanahu Wataala.
Na miongoni mwa mitizamo inayosababisha kuhiliki ni kuitizama Muislamu
Dunia kwa kuishughulikia sana na kuitukuza na kutoishughulikia Akhera yenye
kubakia na ndio mwisho wa kila mtu huko kwani anaependelea kinachopita
(kisichodumu) juu ya kinachobakia huyo hana akili na inataka mtu aijalie Dunia
kama kipando (anachokipanda mtu kama gari, ndege, meli au mnyama kusafiri)
kinachomchukua kumpeleka katika nchi anayoikusudia kwenda. Kwa hiyo Dunia
haistahiki kupewa heshima ila kwa kadiri ya kukufikisha huko kwenye haja yako
(Al-Janna) na kwa sababu kipando chahifadhiwa na kutunzwa ili kipate
kukufikisha mahala unapopataka kadhalika Dunia yahifadhiwa na kuheshimiwa kwa
ajili ya kukufikisha Akhera kwani Dunia ni sababu na Akhera ndio lengo la mja.
Amesema Allah Subhanahu Wataala :-
ﭽ
ﮝ ﮞ
ﮟ ﮠ ﮡ
ﮢ ﮣ ﮤ
ﮥ ﮦ ﮧﮨ
ﮩ ﮪ ﮫ
ﮬ ﮭ ﮮ ﭼ المنافقون: ٩
“Enyi Mlioamini! Yasikusahaulisheni mali yenu wala watoto wenu
kumkumbuka Allah; Na wafanyao hayo, hao ndio wenye kukhasirika.”
Na amesema Allah Subhanahu Wataala :-
ﭽ
ﮝ ﮞ
ﮟ ﮠﮡ ﮢ
ﮣ ﮤ ﮥ
ﭼ التغابن: ١٥
“Bila shaka mali zenu
na watoto wenu ni jaribio (kwenu, mtihani kutazamwa mtakhalifu amri za Allah
kwa ajili yao
au mtafuata amri zake). Na kwa Allah kuna ujira mkubwa kabisa.”
Na amesema Allah Subhanahu Wataala :-
ﭽ ﭷ ﭸ
ﭹ ﭺ ﭻ ﭼ ﭼ
هود: ١٥
“Wanaotaka
maisha ya Dunia na mapambo yake.”
Na amesema Subhanahu Wataala:-
ﭽ ﮔ ﮕ ﮖ
ﮗ ﮘ ﮙ ﮚ ﮛ
ﮜ ﭼ
العلق: ٦ - ٧
“Sivyo hivi (we binaadamu)! Kwa hakika binaadamu hutakabari (6) Akijiona
amepata utajiri(7).
Na amesema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
)حب المال والشرف ينبتان النفاق في القلب كما ينبت الماء البقل(
“Kupenda mali na utukufu
kwaotesha unafiki katika moyo kama maji yanavyootesha mimea”.
Na amesema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
)ما ذئبان ضاريان أرسلا في زريبة غنم بأكثر إفسادا فيها من
حب الشرف والمال والجاه في دين الرجل المسلم(
“Mbwa mwitu wawili wanaopelekwa katika
kikundi cha mbuzi hawawi waharibifu kwao zaidi kuliko (uharibifu unaofanywa) na
kupenda utukufu na mali na cheo katika Dini ya mtu Muislamu.”
Amesema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
( يهلك
المكثرون إلا من قال به في عباد الله هكذا هكذا وقليل ما هم )
“Wanahiliki wanaopenda mali
nyingi isipokuwa wale wanaozitoa pesa zao katika waja wa Allah kwa njia hii na
njia hii (kwa njia mbali mbali kama kuwapa watoto wao, kuwapa masikini) na hao
ni kidogo”.
Na amesema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
(سيأتي بعدكم
قوم يأكلون أطايب اللذائذ وألوانها
ويركبون فره الخيل وألوانها وينكحون أجمل
النساء وألوانها ويلبسون أجمل الثياب وألوانها لهم بطون من القليل لا تشبع وأنفس بالكثير لا تقنع عاكفون على الدنيا يغدون ويروحون إليها
اتخذوها آلهة من دون إلههم وربا دون ربهم إلى أمرها ينتهون ولهواهم يتبعون فعزيمة
من محمد بن عبد الله لمن أدركه ذلك الزمان من عقب عقبكم وخلف خلفكم أن لا يسلم
عليهم ولا يعود مرضاهم ولا يتبع جنائزهم ولا يوقر كبيرهم فمن فعل ذلك فقد أعان على
هدم الإسلام)
“Watakuja
watu baada yenu wanakula vyakula vyenye ladha na rangi mbali mbali (aina
tofauti) na wapanda farasi wazuri wa starehe na wenye rangi tofauti na wanaoa
wanawake wenye wingi wa uzuri na rangi mbali mbali na wavaa mavazi mazuri
yalioje na yenye rangi mbali mbali hao wana matumbo hayashibi na kidogo na
nafsi hazikinai wamejishughulisha na Dunia wenda na warudi kwa ajili yake
(Dunia) wameifanya kuwa ni Mungu hali ya kuwa wamemuacha Allah wao na wameifanya
kuwa ni mola pasi ya Mola wao Subhanahu Wataala wafuata amri yake na wafuata
matamanio yao basi Muhammad bin Abdullah anamlazimisha yeyote utakaemfikia
wakati huo miongoni mwa watoto wenu na watoto wa watoto wenu watakaokuja baada
yenu na vizazi vyenu vitakavyofuatia baada yenu asiwaamkie hao (sifa zao
zilizotajwa hapo juu) wala asiwatizame wagonjwa wao wala asishindikize majeneza
yao (asiwazike) wala asimheshimu mkubwa wao na atakaefanya hivyo basi amesaidia
katika kuuvunja Uislamu. Ameitoa Abu Amamah.
Na Amesema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
( يقول ابن آدم
مالي مالي وهل لك من مالك إلا ما أكلت فأفنيت أو لبست فأبليت أو تصدقت فأمضيت )
“Binaadamu asema mali yangu mali
yangu, Je unayo mali
wewe ila kile ulichokula ukakiondoa au ulichokivaa ukakichakaza au umekitoa
sadaka ukakipeleka (mbele yako kikiwa katika ujira wako Siku ya Kiyama).”
Na amesema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
( أخلاء ابن آدم
ثلاثة واحد يتبعه إلى قبض روحه والثاني إلى قبره والثالث إلى محشره فالأول ماله
والثاني أهله والثالث عمله )
“Marafiki wa binadamu watatu
mmoja anakuwa pamoja nae mpaka anapochukuliwa roho yake na wa pili (amfata)
mpaka kaburini na watatu mpaka Siku ya Kiyama wa kwanza ni mali yake, wa pili
ahli wake na watatu vitendo vyake.”
Inasemekana kuwa zilivyotengezwa dinari na
darhamu Ibliis akazinyanyua juu ya kichwa chake kisha akazieka juu ya kipaji
chake kisha akazibusu akasema anaekupendeni basi huyo mtumwa wangu wa kweli, na
watu kidogo wanaomiliki nafsi zao mbele ya dinari au dirham kuna methali
inasema:- “Muoneshe dirhamu ujue vipi kujiepusha kwake na mambo ya haramu”.
Vile vile inasema methali nyingine:- Usidanganyike na mtu kwa kuitia kiraka
kanzu yake au kwa kunyanyua nguo yake juu ya vifundo vyake viwili au kwa
mn’garo wa kipaji chake cha uso muoneshe dirhamu utajua utiifu wake au
kujitenga kwake na maharimisho ya Allah Subhanahu Wataala .
Inasemekana kuwa Musallamah bin Abdul Malik
aliingia kwa Omar bin Abdul Aziz, Allah Amrehemu, wakati wa mauti yake akasema:
Ewe Amir Almuminiin umefanya jambo hakufanya mtu kabla yako, umewaacha watoto
wako hawana dirham wala dinari. Na alikuwa na watoto kumi na tatu, basi akasema
Omar nikalisheni wakamkalisha hapo akasema:- Ama kauli yako kuwa sikuwaachia
dinari wala dirhamu kwani sikuwazuia mimi kwenda mashambani wala sikuwapa wao
haki ya watu wengine ama ukweli ni kuwa watoto wangu ni moja katika watu
wawili: Awe mtiifu kwa Allah Subhanahu Wataala basi Yeye atamtosheleza haja
zake kwani Allah Subhanahu Wataala awatizamia watu wema mambo yao au awe (mtoto
wangu) asi kwa Allah na sijali hayo yatakayompata.
Na kwa ujumla utajiri ni bora kuliko umasikini
kwa sababu Mtume Salallahu Alayhi Wasalam amemuomba Allah Subhanahu Wataala
amkinge na ufakiri na akauwita ukosefu ulioje, amma utajiri watumiliwa katika
kumtii Allah Subhanahu Wataala zaidi kuliko ufakiri, na vile vile utajiri
unafaida nyingi za Kidunia na Kidini amma za Kidunia zajulikana na amma faida
za Kidini na za Akhera ni kufanya ibada zinazoambatana na kutoa pesa kama kutoa
matumizi ya nyumbani (chakula, nguo na mengineyo), kuwapa mafakiri, kutoa
sadaka katika mambo ya hija na jihadi, kutoa pesa za kujengea maskani, kuoa, na
kipando (mnyama, pikipiki au gari) ambayo hakuna budi kuyafanya na matumizi
mengineyo ambayo hawezi mtu akafikia kumwabudu Allah Subhanahu Wataala
isipokuwa kwayo. Hizo ni katika ibada ambazo apata thawabu ikiwa atatia niya
nzuri ya kujikaribisha na Allah Subhanahu Wataala. Vile vile kama kuhifadhi
sharafu yake na ya watoto wake, kuwapa ujira wafanya kazi au kujenga misikiti,
madaraja na nyumba za kufikia wageni na mengineyo kama kueka mali wakfu ili
kufanya mambo ya kheri na mambo haya yote ni kheri yanayofikisha katika radhi
ya Allah Subhanahu Wataala. Upande mwingine mali hiyo hiyo inayotolewa kufanya
mambo yote hayo mazuri inaweza ikamletea shari na ubaya mkubwa huyo mwenyewe
ikiwa niya yake ya kutumia mali hiyo ni matamanio ya uasi, ufahari, kujiona
nafsi yake kuwa ni bora na kuwa ana mali nyingi kuliko watu wengine na kufanya
uroho mkubwa kunakomfanya mtu achume mali kihalali halafu aitumie palipokuwa si
halali au yamshughulishe mali na njia ya kuyachuma kwake hata asifanye wajibu
wa Dini yake na kuwa akija msikitini kwa mfano kusali basi huwa kama yuko juu
ya jinga la Moto mpaka atakapotoka humo, mwili wake upo ndani msikitini na roho
yake na moyo wake inafuwata kazi zake nje ya msikiti, wakati ikichelewa adhana
kwa mfano au ikama wamuona atizama saa yake na kumpigia kelele muadhini
umekwisha pita wakati, umekwisha pita wakati haya kimu Sala, kazi zetu
zitaharibika na kama hivyo. Basi wafikiri itakuwa vipi Sala ya mtu kama huyu
isipokuwa usumbufu tu wa hofu na huzuni na kukesha usiku na kutopata usingizi
bila ya kula vidonge vya usingizi na hapati faragha hata ya kula basi nini faida ya mali kama hii?
Basi yeyote yule aliyekuwa haikumstarehesha mali yake, yeye na masikini ni sawa.
Kitu muhimu cha kuzingatia kuwa mwanadamu amezungukwa na mitihani kutoka upande
wa ufakiri na utajiri na anahitajia subira na jihadi ili kupasi mitihani hii.
ﭽ ﯿ ﰀ
ﰁ ﰂ ﭼ الأنبياء:
٣٥
“Na
tutakufanyieni mitihani kwa (mambo ya) shari na ya kheri.”
Twamuomba Allah Mtukufu Atusalimishe na Atusaidie kwa tawfiiqi yake na
ulinzi wake na ukarimu wake kwani Yeye ni Muweza wa hayo. Amin.
Zimekuja hadithi za Mtume Salallahu Alayhi Wasalam katika kusifu kukinai
na kuikosoa tamaa ya vilivyo katika mikono ya watu.
Amesema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
( لو كان
لابن آدم واديان من ذهب لابتغى لهما ثالثا ولا يملأ جوف ابن آدم
إلا التراب ويتوب الله على من تاب)
“Kama
angelikuwa binaadamu ana mabonde mawili ya dhahabu basi angelitaka la tatu na
wala tumbo la binaadamu halijai(hatosheki) isipokuwa na udongo na Allah Apokea
toba ya aliyetubu.”
Na Asema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
( منهومان لا يشبعان منهوم
العلم ومنهوم المال )
“Waroho wawili hawashibi, mroho wa elimu na
mroho wa mali.”
Na asema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
( يهرم بن آدم ويشب معه اثنتان الأمل وحب المال )
“Anazeeka binaadamu na viwili vyabakia nae
katika ujana matumaini na kupenda mali” au kama alivyosema Mtume Salallahu
Alayhi Wasalam.
Na anasema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :
(طوبى لمن هدي للإسلام وكان عيشه كفافاً وقنع به )
“Ana malipo makubwa (mazuri) alieongozwa katika
Uislamu na yakawa maisha yake kiasi ya kumtosheleza bila ya kuhitajia watu na
kuwaomba akakinaika nayo.”
Na anasema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
( ما من أحد
فقير ولا غني إلا ويوم القيامة يتمني أنه
كان أوتي قوتا في الدنيا )
“Hakuna mtu yoyote Siku ya
Kiyama akiwa tajiri au fakiri isipokuwa atamani kuwa Duniani alipewa chakula kiasi
ya kutosheleza siku moja.”
Na anasema Salallahu Alayhi Wasalam:-
( ليس الغنى عن كثرة العرض إنما الغنى غنى النفس )
“Sio utajiri kuwa na mali
nyingi lakini utajiri (wa kweli) ni utajiri wa nafsi”.
Na anasema Salallahu Alayhi Wasalam:-
( أيها الناس أجملوا في الطلب
فإنه ليس لعبد إلا ما كتب له ولن يذهب عبد من الدنيا حتى يأتيه ما كتب له من
الدنيا وهي راغمة )
“Enyi watu ufanyeni uchumi
wenu uwe mzuri (bila ya kutaka haramu au kufanya tamaa na ghishi na kupoteza
ibada kwa kushughulika na maisha) kwani hapati mja isipokuwa kile
alichoandikiwa (kukipata) na haondoki mja Duniani isipokuwa kitamjia alichoandikiwa
chataka au hakitaki.”
Na amesema Ibn Masood amesema Mtume Salallahu
Alayhi Wasalam :-
( إن روح القدس نفث في روعي أن
نفسا لن تموت حتى تستكمل رزقها فاتقوا الله وأجملو في الطلب)
“Hakika Roho mtakatifu (Jibriil)
amepuliza katika moyo wangu kuwa nafsi haifi mpaka imalize riziki yake
(iliyoandikiwa) basi mcheni Allah na ufanyeni uchumi wenu uwe mzuri.”
Amesema Abu Ayoub RA kuwa alikuja mbedui kwa
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam akasema ewe Mtume wa Allah nipe mauidha na
uyafupishe akasema Salallahu Alayhi Wasalam:-
(إذا صليت فصل صلاة مودع ولا
تحدث بحديث تعتذر منه غدا واجمع اليأس مما في يد الناس )
“Ukisali sali Sala ya mwenye
kuaga (kama ni Sala yako ya mwisho na huwahi kusali Sala ijayo) na usizungumze
mazungumzo ambayo kesho itabidi uyatolee udhuru (yaani uyapime yawe mazuri sio
kuteta watu au kufitinisha n.k) na ukate tamaa kwa kilichoko katika mikono ya
watu (usitamani kilichokuwa kwa mwenzako).”
Aliulizwa mwenye hekima nini mali yako akajibu
kujipamba katika umadhihari wangu (nje) kwa makusudio ya kujitengeza undani
wangu (amali ya mtu anayoifanya ina athari kubwa katika nafsi yake, kama kusema
ukweli, kutokughishi, kutoteta watu. Tabia nzuri kwa ujumla yatengeza undani wa
mtu kama kuondoa hasadi, chuki, kujiona bora, kiburi) na kukata tamaa na
kilicho katika mikono ya watu.
Inasemekana kuwa kuna mtu alikamata ndege
(mdogo) akamuambia wanitakia nini? Nataka nikuchinje halafu nikule, akamjibu
wallahi haitamtosheleza (nyama yangu) mtu kwa kuwa haina ladha, wala kama ana
njaa haitamshibisha lakini nitakufundisha mambo matatu ni bora kwako kuliko
kunila mimi. Ama la kwanza nitakufundisha ningali niko katika mkono wako na la
pili nikiwa juu ya mti ama la tatu nikiwa juu ya jabali. Akamwambia haya lete
la kwanza. Akamwambia usisikitike juu ya kitu kilichokupita. Halafu akamwachia,
alipokwenda mtini akamwambia lete la pili. Akamwambia usisadiki kitu
kilichokuwa hakiwezekani, kuwa kitakuwa. Kisha akapuruka kwenda juu ya jabali
akasema:- Ewe mtu wa tabu (mwenye bahati mbaya) kama ungenichinja ungetoa
katika tumbo langu lulu mbili uzito wa kila moja katika hizo ni mithkala
ishirini akajin’gata kwa kusikitika (juu ya kuzikosa hizo lulu) akamwambia haya
lete hilo la tatu akamwambia wewe umeyasahau hayo mawili (ya mwanzo) vipi
nikwambie la tatu. Sikukwambia usilisikitikie lililokupita na usisadiki kitu
kisichowezekana kuwa kitakuwa. Mimi nyama yangu, damu yangu na magoya yangu
vyote havifiki mithkala ishirini vipi basi zitatoka katika tumbo langu lulu
mbili kila moja uzito wake mithkala ishirini
kisha akapuruka akenda zake.
Amesema Abu Attayib:- Anaetumia saa nyingi kwa
kukusanya mali kuogopa usimpate ufakiri basi huo ndio ufakiri wenyewe.
Nami nimesema yenye maana hii:-
“Kila kilichokuwa katika ardhi kimeumbwa kwa
ajili yetu hiyo ni heshima na neema kwetu. Amegawanya (Allah Subhanahu Wataala)
riziki baina ya viumbe vyake na wala haumzidishii mtu uhodari wake isipokuwa
kile alichoandikiwa na tabu yake ya kutafuta riziki iliokuwa haikuandikwa
katika lawhi Al Mahfudhi ni bure. Na kinyume ya hivyo anaipata (riziki
alioandikiwa) ijapokuwa hakuitafuta lakini kuacha kutafuta riziki iliyo halali
ni ajizi kwani riziki haina mabawa bali hiyo ni kama wajibu inayotakiwa
kufanywa na usiwe mzigo (juu ya wenzako) lakini tafuta riziki bila ya
kunyan’ganya na kutumia nguvu na uitafute polepole na kwa uzuri. Kwani kila
kilichokujia kwa unyan’ganyifu (na kugombana) kinakwenda katika kupotea na
kuhiliki. Na kukusanya kwako mali
umri wako wote kwa kuchelea ufakiri basi huo ndio ufakiri wenyewe, Ewe Mola
nakuomba maghufira na maisha ya kunitosheleza, ewe Mola nijalie riziki yangu
iwe ya kutosheleza haja yangu na iniepushe kuomba watu”.
Imesemwa kuwa baadhi ya watu wazuri wamesema:-
“Ajabu kwa anaenunua watumwa kwa mali yake na hanunui watu huru kwa wema
wake”. Kaulizwa mmoja wao juu ya ukarimu akasema:- “Utoe mali yako kwa
ajili ya Allah Subhanahu Wataala”. Akaulizwa nini udhibitifu wa jambo akasema:-
“Uizuie mali
yako kwa ajili Yake(Allah)”. Akaulizwa nini israfu akasema:- “Kutumia mali kwa kutaka
cheo”. Amesema katika wao:- Wewe ni wa
mali (imekumiliki) ukiizuia (kwa ubakhili usiitumie katika kheri) na ukiitumia basi mali ni yako
(umeimiliki) Amesema mwingine:- “Bora ya mali ni ile iliyotumiwa kwa kuhifadhi
heshima na sharafu”.
Amesema mwingine:- “Kufanya jitihada katika kutumia ulichonacho ni
ukarimu wa juu kabisa (wa mwisho)”.
Amesema mwingine:- Sijapata kunyoosha mguu wangu mbele ya niliekaa naye.
Na katika visa vya mabakhili: Alikuwa katika mji wa Basra mtu mmoja
tajiri lakini bakhili. Basi mmoja katika majirani zake akamwalika chakula
akamletea chakula kizuri kinaitwa “tabahijah bibeidh” chapikwa na mayai akawa
anakula yule mgeni (tajiri bakhili). Akala sana na huku anywa maji mpaka
akavimbiwa na akayaona mauti mbele ya macho yake na akawa ajipindua kwa maumivu
mwisho akenda kwa daktari kumuelezea hali yake akamwambia si tatizo kubwa
lakini fanya utapike hicho ulichokula na utakuwa mzima akajibu:- Hah nitapike
“tabahijah bibeidh”!! Bora kufa kuliko kufanya hivyo.
Kuna kisa kingine kinasema: Amekuja mbedui kwa mtu fulani ambaye mbele
yake kuna tini (matunda fulani) basi alivyomuona yule mbedui akazifunika na
nguo yake akakaa yule mbedui, yule mtu akamwambia Je unajua kusoma sura yoyote
ya Qur’ani? Akajibu naam basi akasoma .........والزيتون وطور سينين yule
mtu akamsahihisha(kama kumuuliza) والتين yule mmbedui akasema tini iko chini ya nguo yako.
Mmoja akamwita (kamkaribisha) mwenzake nyumbani kwake bila ya kumpa
chakula akamfunga katika hali hiyo mpaka Al asiri na ikamshika njaa sana mpaka
akawa kama kichaa na yule mwenye nyumba akachukua uudi (gitar- chombo maarufu
cha kupiga muziki) akamuuliza mgeni wake sauti gani unayoitamani nikupigie
akamjibu sauti ya karai (likikaanga nyama au samaki).
Kimetolewa kisa juu ya mtu bakhili. Umepindukia mpaka ubakhili wake.
Akaulizwa mkwewe juu yake:- hebu tusifie meza yake ya chakula inakuwa vipi?
Akajibu:- (jawabu lenye maana kama hii) Chakula kidogo sana na si kizuri (hakiliki). Na akaulizwa
nani ahudhuria chakula hicho? Akajibu:- Malaika karimu wanaoandika amali za
waja. Akaulizwa basi hapana anaekula nae? Akajibu:- Bali
kuna nzi wala pamoja nae. Akaambiwa (huyu mkwe) twaona utupu wako waonekana na
nguo yako imetoboka si bora ungelimuomba kitu akusaidie? Akasema mimi Wallahi
nashindwa kumiliki sindano kushona hii nguo. Na kama mkwe wangu huyu angekuwa
ana nyumba kutoka Baghdad mpaka Nuba (nchi
katika Africa) imejaa sindano kisha akamjia Jibriil na Mikaiil na pamoja nao
Yaaqoub Nabii wa Allah Subhanahu Wataala Salamu ya Allah iwe juu yao wakamuomba sindano
moja awaazime ili waishonee kanzu ya Nabii Yusuf AS ambayo ilipasuliwa kwa
nyuma basi asingewaazima hiyo sindano.
Na mmoja wao (katika mabakhili) alikuwa hali nyama kwa kuona ubakhili
mpaka umjie uchu (kupenda sana )
hapo ndipo humtuma kijana wake ili amnunulie kichwa cha mnyama, akaulizwa,
twaona huli isipokuwa vichwa katika kaskazi (siku za joto) na kipupwe (siku za
baridi) kwa nini wafanya hivyo? Akasema:- Ndio kwa sababu kichwa naijua bei
yake kwa hiyo nasalimika na hiyana ya huyo kijana, na yeye vile vile kichwa sio
nyama yake anayoipika (anayo nyama yake nyingine anayoipika) kwa hiyo hawezi
akanilia nyama yangu akitaka kula jicho, sikio au funda humsimamisha na
kuichukua mimi nikaila kwa hiyo huninunulia na kunipikia bila ya kuweza kula
kitu cho chote kilichokuwa haki yangu. Siku moja alikuwa atoka nyumbani kwake
enda zake kwa khalifa (kiongozi wa nchi) mkewe akamwambia Je utanipa nini
ukirudi umepewa zawadi? Akamwambia nikipewa dirham 100,000 elfu mia nitakupa
dirham moja na akapewa dirham 60,000 elfu sitini akampa dawnaq 4 nne (kasoro ya
dirham moja).
Wako wapi hawa (mabakhili vilivyotajwa visa vyao hapo juu)
ukiwafananisha na yule ansari alieingia kwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam
akamkuta ana mgeni hana chakula cha kumpa (cha usiku) basi akamchukua yule
ansari nyumbani kwake kisha kikaletwa chakula kikaekwa mbele yao akamuamrisha
mkewe azime taa na akanyoosha mkono wake kama kwamba ataka kula kile chakula
lakini hali, akala yule mgeni na alipoamka asubuhi Mtume Salallahu Alayhi Wasalam
akamwambia Allah Subhanahu Wataala kafurahika na kitendo chenu mlichokifanya
usiku kwa mgeni wenu na Allah Subhanahu Wataala Akateremsha Aya:-
ﭽ ﯷ ﯸ
ﯹ ﯺ ﯻ
ﯼ ﯽ ﭼ الحشر:
٩
“Na
wanawapendelea kuliko nafsi zao ingawa wenyewe wana hali ndogo”.
Inasemekana kuwa Abdullah bin Jaafar alitoka kwenda shambani kwake
akapitia shamba la mitende la watu fulani akamkuta kijana mweusi anafanya kazi
humo naye alikuwa (huyo kijana) ameleta chakula chake akaingia humo shambani
mbwa akaja karibu yake yule kijana akamtupia kipande cha mkate kisha akamtupia
cha pili na cha tatu akavila yule mbwa na Abdullah amtizama akamwambia: ewe
kijana kiasi gani chakula chako (unachokula) kwa siku akamjibu hicho
ulichokiona akamwambia kwa nini umempendelea mbwa? Akamjibu hii ardhi hakuna
mbwa kwa hiyo huyu amekuja kutoka umbali mkubwa ana njaa basi nimeona vibaya
nishibe mimi na yeye akae na njaa. Akamwambia wewe utafanya nini leo (utapata
wapi chakula?) akamjibu mimi nimekwisha ifunga siku yangu hii (sili tena wala
sina pa kupata chakula) akasema Abdullah bin Jaafar:- Kijana huyu ni karimu
zaidi kuliko mimi basi akalinunua hilo shamba na kila kilicho ndani yake pamoja
na huyo kijana na kisha akamkomboa huyo kijana na akampa sehemu ya hilo shamba.
Tunatoa hapa kisa cha Thaalaba bin Haatib kwa ajili ya kuhadhirisha na
fitina ya mali. Amesema Thaalaba: Ewe Mtume wa Allah muombe Allah aniruzuku
mali akasema:-
( يا ثعلبة قليل تؤدي شكره خير من كثير لا تطيقه )
Ewe Thaalaba kidogo unachoweza kutoa shukrani
yake bora kuliko kingi (mali nyingi) ambacho hukiwezi. Akasema: Ewe Mtume wa
Allah niombee kwa Allah Aniruzuku mali, akasema:-
( يا ثعلبة أما ترضى أن تكون
مثل نبي الله تعالى أما والذي نفسي بيده لو شئت أن تسير معي الجبال ذهباً وفضة
لسارت )
“Ewe Thaalabah huridhiki
kuwa mfano wa Mtume wa Allah Mtukufu, kwa kweli naapa kwa Aliye nafsi yangu
katika mikono yake kama ningelitaka majabali (milima) kuwa dhahabu na fedha
yangelikuwa”.
Akamwambia:- Naapa kwa Aliye kuleta kwa haki
Mtume kama ukimuomba Allah aniruzuku mali hakika nitampa kila mwenye haki, haki
yake na nitafanya na nitafanya....
akasema Mtume wa Allah Salallahu Alayhi
Wasalam:-
“Allah mruzuku Thaalabah mali اللهم ارزق ثعلبة مالا Akafuga mbuzi wakazaana kama wanavyozaana wadudu
mpaka Madina ikawa ndogo kwao (jinsi walivyokuwa wengi) basi akahama katika bonde
katika mabonde yake mpaka ikawa asali ِAdhuhuri na Alasiri jamaa tu na sala nyingine
akawacha kusali jamaa na wakazidi kuongezeka hao mbuzi mpaka ikabidi ahame
mbali zaidi hadi akaacha kusali sala ya jamaa isipokuwa sala ya Ijumaa nao bado
wangali wakaongezeka kama wanavyoongezeka wadudu mpaka hatimaye akaacha kusali
Ijumaa mpaka ikawa habari za Madina awauliza wanaokwenda huko siku ya Ijumaa.
Hapa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam akauliza juu yake:
ما فعل ثعلبة
بن حاطب
Je nini amefanya Thaalabah bin Haatib.
Akaambiwa Ewe Mtume wa Allah amefuga mbuzi wakawa wengi mpaka ukadhikika mji wa
Madina nao, na wakamuelezea habari yake yote akasema:-
( يا ويح ثعلبة بن حاطب يا ويح
ثعلبة يا ويح ثعلبة )
“Ewe Thaalaba bin Haatib ole
wako, ewe Thaalaba ole wako, ewe Thaalaba ole wako”.
Allah akateremsha Aya hii:-
ﭽ
ﮚ ﮛ
ﮜ ﮝ ﮞ
ﮟ ﮠ ﮡ
ﮢﮣ ﮤ ﮥ
ﮦ ﮧ ﭼ التوبة:
١٠٣
“Chukua sadaka katika; mali zao, uwasafishe kwa ajili ya hizo (sadaka
zao) na kuwataja kwa vizuri (mbele yangu) na uwaombee dua. Hakika kuwaombea
kwako kutawapa utulivu (watengenekewe)”
Baada ya kuteremka Aya hii ya kufaridhisha Zakaa Mtume Salallahu Alayhi
Wasalam akawatuma watu wawili na akawaandikia barua ili kwenda kwa Waislamu
kukusanya sadaka mmoja wao katika kabila la Juhainah na wapili kabila yake ni
Bani Saliim, akawaambia Salallahu Alayhi Wasalam:-
( مر بثعلبة بن حاطب وفلان رجل
من بني سليم )
Mpitieni Thaalabah bin Haatib na fulani, mtu mmoja katika Bani Saliim.
Akawaambia wachukue kutoka kwao Sadaka iliyo haki kwao kuitoa. Wakenda mpaka
wakafika kwa Thaalabah wakamwambia atoe Sadaka na wakamsomea barua ya Mtume
Salallahu Alayhi Wasalam akasema hiki si kingine isipokuwa kodi (twatozwa) hii
si kingine isipokuwa mwenzake kodi nendeni mpaka mkishamaliza rudini kwangu.
Wakenda zao kwa yule Assalimiy akawakaribisha na akenda kuwatolea bora wa
ngamia aliekuwa nao akawatenga kisha akaja nao kuwakabidhi hao wajumbe (hakika
hii ni taufiki kutoka kwa Mola Subhanahu Wataala). Walipowaona wale ngamia na
hali yao
ilivyokuwa nzuri kabisa wakamwambia Assalimiy haina haja ya kutupa katika bora
ya ngamia uliokuwa nao inatosha utupe walio hali ya wastani lakini akawaambia
hapana chukueni hawa. Walipomaliza kuchukua sadaka kwa Assalimiy wakarejea kwa
Thaalabah bin Haatib wakamtaka awape sadaka akawambia hebu nionesheni barua
yenu (iliyotoka kwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam) akaitazama kisha akasema
hii ni mwenzake (mfano wa) kodi nendeni zenuni mpaka nitazame nini rai yangu
juu ya jambo hili wakaondoka mpaka wakamjia Mtume Salallahu Alayhi Wasalam na
alipowaona akasema Salallahu Alayhi Wasalam:-
يا ويح ثعلبة
“Ole wako Thaalabah” kabla wao hawajamwambia kitu na akamuombea
Assalimiy halafu wakamwambia alivyowafanyia Thaalabah na alivyowafanyia
Assalimiy.
Akateremsha Allah Subhanahu Wataala juu ya Thaalabah Aya ifuatayo:
ﭽ ﮓ ﮔ ﮕ
ﮖ ﮗ ﮘ ﮙ ﮚ ﮛ
ﮜ ﮝ ﮞ
ﮟ ﮠ ﮡ
ﮢ ﮣ ﮤ
ﮥ ﮦ ﮧ
ﮨ ﮩ ﮪ
ﮫ ﮬ ﮭ
ﮮ ﮯ ﮰ
ﮱ ﯓ ﯔ
ﯕ ﯖ ﯗ
ﯘ ﯙ ﯚ ﭼ
التوبة: ٧٥ - ٧٧
“Na miongoni mwao (hao wanafiki) wako waliomuahidi Allah kuwa: Akitupa
katika fadhila zake tutatoa sadaka na tutakuwa miongoni mwa wanaotenda mema
(75) Lakini alipowapa hizo fadhila zake walizifanyia ubakhili na wakakengeuka,
nao (mpaka hivi sasa) wanakengeuka (76) Kwa hiyo akawalipa unafiki (kutia)
nyoyoni mwao mpaka siku ya kukutana naye (Allah), kwa sababu ya kukhalifu kwao
waliomuahidi Allah na kwa sababu ya kusema kwao uwongo”(77).
Wakati ilipoteremka Aya hii kwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam alikuwepo
hapo mtu miongoni mwa jamaa zake Thaalaba akasikia kitu gani Allah Subhanahu
Wataala ameteremsha juu yake (Thaalaba) akatoka kumuendea Thaalaba alipofika
kwake akamuambia:- Huna mama ewe Thaalaba Allah Ameteremsha juu yako kadha wa
kadha. Akatoka (Thaalaba) mpaka akafika kwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam
akamuomba amkubalie sadaka yake akasema Salallahu Alayhi Wasalam:-
إن
الله منعني أن أقبل منك صدقتك
“Hakika Allah amenikataza kuipokea sadaka yako”. Hapo akawa ajimwagia
udongo juu ya kichwa chake basi Mtume Salallahu Alayhi Wasalam akamwambia:-
هذا عملك أمرتك فلم تطعني
“Hii ni kazi yako (malipo ya kitendo chako) nimekuamrisha nawe hukunitii
(hukunifuata maneno yangu)” Basi alipoona amekataa (Salallahu Alayhi Wasalam)
kupokea kitu cho chote kutoka kwake akarudi nyumbani kwake na alipofariki Mtume
wa Allah Salallahu Alayhi Wasalam akaja na sadaka yake kwa Abu Bakar Siddiq RA
na vile vile akakataa kuipokea kisha akaja nayo kwa Omar RA naye kadhalika
hakuipokea na akafa Thaalabah katika khilafah ya Othman bin Affan. Kama
ilivyotolewa kutokana na Nabii wa Allah Subhanahu Wataala Isa AS kuwa alikuwa apita njiani akamfuata
mtu na huku akimwambia napenda kuwa katika usuhuba wako basi ndio hivyo wakawa
pamoja na wakaondoka katika safari yao na wakaishia katika ukingo wa mto na
wakakaa hapo kula chakula cha mchana na wao wana vipande vitatu vya mkate
wakavila vipande viwili kikabakia kipande kimoja halafu akasimama Nabii Isa AS
kwenda kunywa maji mtoni kisha akarudi. Aliporudi hakukikuta kile kipande
kilichobakia cha mkate akamuuliza yule mtu: Nani aliechukua kipande cha mkate?
Akamjibu: Sijui. Kisha akaendelea na safari yake pamoja na sahibu yake akaona
paa na watoto wake wawili akamwita mmoja wao akamchinja kisha akamchoma halafu
akamla pamoja na sahibu yake baadaye akamsemesha yule mtoto wa paa (aliekwisha
chinjwa na kupikwa na kuliwa) simama kwa idhini ya Allah Subhanahu Wataala hapo
akasimama na kumuendea mama yake. Akamwambia yule mtu nakuuliza kwa jina la
yule aliekuonesha Aya hii nani aliechukua kile kipande cha mkate akajibu : “Sijui”
kisha akaishia katika bonde la maji akauchukua Nabii Isa AS mkono wa yule mtu
kisha akatembea nae juu ya yale maji alipovuka upande wa pili akamwambia:-
Nakuuliza kwa jina la Yule aliekuonesha Aya hii nani aliekula kile kipande cha
mkate akamjibu: Sijui kisha wakenda mpaka wakafika mahala penye amani. Hapo
akakaa Isa AS na akawa akusanya mchanga mpaka ukawa kichuguu halafu akakiambia
kuwa dhahabu kwa Idhini ya Allah Subhanahu Wataala kikawa dhahabu. Na akakigawa
vifungu vitatu kisha akasema theluthi moja yangu na moja yako na moja ya
aliekula kipande cha mkate. Basi hapo upesi akasema mimi ndio niliekula kile
kipande cha mkate. Na baada ya kusikia haya Mtume wa Allah AS akasema chukua
wewe mafungu yote matatu. Kisha akamwacha hapo naye akenda zake akabakia
kainamia ile dhahabu ajaribu kuibeba lakini hawezi kwa uzito wake mkubwa na
huku hawezi kwenda zake akaiwacha. Hatimaye wakaja watu wawili wakataka kumuuwa
ili wapate kuichukua hiyo dhahabu, akafikiria ujanja kisha akawambia tuigawe sawasawa
baina yetu na mmoja wenu ende mjini akatuchukulie chakula tupate kula. Akenda
mmoja katika wao na huku afikiria katika nafsi yake kuwa awatilie wale wenzake
sumu ili wafe halafu ile dhahabu yote aichukue yeye. Na kweli akafanya hivyo na
huku wale waliobakia kuilinda ile dhahabu wakashauriana kumuua yule aliekwenda
kuchukua chakula baadaye wagawane mali . Aliporudi wakamuua na wakakila
kile chakula chenye sumu wakafa wote wawili na ikabakia ile mali na wenyewe
wote wamekufa kando yake. Akapita Mtume wa Allah Isa AS nao wako katika hali
hiyo akawaambia masahibu zake hii ndio Dunia na jinsi inavyowafanyia wale
wanayoipenda basi tahadharini nayo. Hakuna kitu kibaya kama kuhadaika
(kudanganyika) na Dunia kwani matokeo yake ni mabaya sana kwa mwenye kudanganyika nayo na
kufikiria kuwa yuko katika maisha ya raha na wasaa Allah Subhanahu Wataala
ametutolea mfano katika kitabu chake kitukufu:-
ﭽ
ﭶ ﭷ
ﭸ ﭹ ﭺ ﭻ
ﭼ ﭽ ﭾ
ﭿ ﮀ ﮁ
ﮂ ﮃ ﮄ
ﮅ ﮆ ﮇ
ﮈﮉ ﮊ ﮋ
ﮌ ﮍ ﮎ
ﮏ ﮐ ﮑ
ﮒ ﮓ ﮔ
ﮕ ﮖ ﮗ
ﮘ ﮙ ﮚﮛ
ﮜ ﮝ ﮞ
ﮟ ﮠ ﮡ
ﮢ ﮣ ﮤ
ﮥﮦ ﮧ ﮨ
ﮩ ﮪ ﮫ
ﮬ ﮭ ﮮ
ﮯ ﮰ ﮱ ﭼ النور: ٣٩ - ٤٠
“Na wale waliokufuru, vitendo vyao (wanavyoviona
vizuri) ni kama mazigazi, (mangati - sura ya
maji) jangwani, mwenye kiu huyadhani ni maji, akiyaendea hayaoni chochote (na
wao watakapoziendea amali zao Siku ya Kiyama. Hawatapata chochote kwani
waliupinga Uislamu, na hali ya kuwa wanajua kuwa ndio Dini ya haki); Wamkute
Allah hapo, awalipe hisabu yao
sawa sawa; na Allah ni Mwepesi wa kuhisabu. (39) Au (amali zao zile mbaya) ni
kama giza katika bahari yenye maji mengi;
inayofunikwa na mawimbi juu ya mawimbi; na juu yake kuna mawingu, giza hili juu ya hili;
anapoutoa mkono wake anakaribia asiuone (kwa kiza kilivyoshtadi); na ambaye
Allah Hakumjaalia nuru hawi na nuru”.
Basi hivyo hakika kuhadaika na Dunia kunapoteza. Na sawasawa ikiwa
kuhadaika huko ni kwa elimu au cheo au mali au heshima au ushujaa au
ukarimu au mengineyo yanayomfanya mwanadamu ajione nafsi yake bora kuliko
wengine.
Allah Subhanahu Wataala Ametuhadhirisha katika Qurani wakati Aliposema:-
ﭽ ﯢ ﯣ ﯤ
ﯥ ﯦ ﯧ ﯨ ﯩ ﭼ
لقمان: ٣٣
“Basi yasikudanganyeni maisha ya (hii) Dunia, wala asikudanganyeni yule
mdanganyi mkubwa, (Ibliis) katika (mambo ya) Allah”.
Na amesema Allah Subhanahu Wataala :-
ﭽ ﮌ ﮍ ﮎ
ﮏ ﮐ ﮑ
ﮒ ﭼ
الحديد: ١٤
“Walakini nyinyi mlijitia wenyewe katika ukafiri (baada ya kuwa
Waislamu) na mkangojea (mabaya yawafike Waislamu), mkajitia shaka (zisizokuwa
na sababu), na matamanio ya nafsi (zenu) yakakudanganyeni”.
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam amesema[1]:-
(حبذا نوم الأكياس وفطرهم كيف
يغبنون سهر الحمقى واجتهادهم ولمثقال ذرة من صاحب تقوى ويقين أفضل من ملئى الأرض
من المغترين)
“Ni bora usingizi (kulala) wa wenye akili na kula kwao (bila ya kuwa
wamefunga kuliko ibada ya wajinga) na vipi (hao wenye akili) wanatamani kukesha
kwa wajinga na jitihada yao (katika kufanya ibada) na hakika uzito wa punje
(uzito mdogo sana wa kitendo) wa mwenye kumcha Mungu na mwenye yakini ni bora
kuliko (vitendo) vya wanaojivuna waliojaa katika Dunia (kwa wingi wao)” Ameitoa
hadithi hii Abu Addardaa.
Amesema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
( الكيس من دان نفسه وعمل لما بعد الموت والأحمق من أتبع نفسه
هواها وتمنى على الله الأماني )
“Mwenye akili ni yule
anayeifanyia hisabu nafsi yake (akafanya mema) na akatenda kwa ajili ya
(usalama wake) baada ya mauti na mjinga ni mwenye kufuata matamanio ya nafsi
yake (akafanya maasi na akatarajia kwa Allah malipo mazuri”. Ameitoa Shaddaad
bin Aws.
Baadhi ya wanavyuoni wamefasiri maana ya “ghuruur” ni “kuipa mtu nafsi
yake mambo yanayowafiki matamanio”. Huyu haipingi nafsi yake na anaifuata moja
kwa moja (nafsi mara nyingi inaamrisha mabaya) na inavyotaka kuifanyia jihadi
(kupigana nayo jihadi). Na mfano wa watu hawa kama
wale wanaosema kulipwa keshi (tasliimu) ni bora kuliko kuakhirishwa yaani
kulipwa baadaye. Na Dunia ni keshi na Akhera ni kuakhirishwa. Yakini ni bora
kuliko shaka na ladha za Dunia ni yakini ama ladha za Akhera ni shaka na kipimo
kama hichi kibovu kinafanana na kipimo cha
Ibliis katika kauli yake Allah Subhanahu Wataala Akizungumzia habari yake (Ibliis):
ﭽ ﭙ ﭚ ﭛ
ﭜ ﭝ ﭞ ﭟ ﭠ
ﭡ ﭢ ﭼ الأعراف:
١٢
“Akasema: Mimi ni bora kuliko yeye. (mimi) umeniumba kwa Moto, naye
umemuumba kwa udongo”.
Na anasema huyu mwenye kughurika na Dunia kama
ingekuwa mimi sie bora na mpendwa kwa Allah Subhanahu Wataala asingenipa neema
zote hizi na ihsani zote hizi kwa hivyo amekosea wakati anapofikiria kuwa kila
aliejaziwa ihsani amependwa anapofikiria kuwa kila neema za Dunia zafuatia
baadaye neema za Akhera:
ﭽ ﭢ ﭣ ﭤ
ﭥ ﭦ ﭧ ﭨ ﭩ ﭼ
الكهف: ٣٦
“Na kama (kitatokea hicho kiama)
nikarudishwa kwa Mola wangu, bila shaka nitakuta kikao chema kuliko hiki.”
Watu wema wakikabiliwa na Dunia huogopa na hufikiria kuwa hii ni fitina
(mtihani) imewajia kinyume ya walioghurika (na Dunia) ikiwakabilia hufikiria
kuwa ni heshima kutoka kwa Allah na ikiondoka Dunia kutoka kwao huona kuwa
wamepuuzwa, kama Alivyosema Allah Subhanahu
Wataala :
ﭽ ﮓ ﮔ ﮕ
ﮖ ﮗ ﮘ ﮙ ﮚ
ﮛ ﮜ ﮝ
ﮞ ﮟ ﮠ
ﮡ ﮢ ﮣ
ﮤ ﮥ ﮦ
ﮧ ﮨ ﭼ الفجر:
١٥ - ١٦
“Lakini mwanadamu, Mola wake Anapomfanyia mtihani Akamtukuza na
kumneemesha, basi husema: Mola Wangu Amenitukuza (wala hashughuliki kufanya
mema ili kutengeneza Akhera yake) (15) Na Anapomfanyia mtihani Akampunguzia
riziki yake husema: Mola wangu Amenidhalilisha (nikifanya mema au mabaya ni sawa
sawa, hatayashughulikia basi naendelea kufanya mabaya)(16)”.
Akamjibu Allah Subhanahu Wataala kumwambia huyo mtu sivyo hivyo (كلا) bali nyinyi hamuwatizami mayatima wala hamuwalishi masikini.
Wakati mtu anapofanya maasi na
akiambiwa awache kufanya hayo maasi husema:- Hakika Allah Karimu
(Atanisamehe madhambi). Amesema Al-Ghazaliy:- Ukisema kuwa makosa wanayo wale waasi
wanaosema kuwa Allah Karimu na sisi twatarajia rehema zake na maghufira kwani
Yeye Amesema Mimi niko katika dhana ya mja wangu kwangu basi anidhanie mja
wangu anavyotaka. Basi jua kuwa sheitani hampotezi binadamu isipokuwa kwa
maneno yanayokubalika katika dhahiri yake na yakatalika katika undani wake
kwani ingekuwa sio kwa uzuri wa dhahiri yake zisingehadaika nyoyo kwao, lakini
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam ametufunulia hayo akasema:-
( الكيس من دان نفسه وعمل لما بعد الموت و الأحمق
من أتبع نفسه هواها ويتمنى على الله )
“Mwenye akili ni yule
anayeifanyia hisabu nafsi yake (akafanya mema na kuacha mabaya) na akatenda kwa
ajili ya (usalama wake) baada ya mauti. Na mjinga ni mwenye kufuata matamanio
ya nafsi yake (akafanya maasi) na akatarajia kwa Allah malipo mazuri.”
Akasema (Al-Ghazaliy) na hii ndio kutamani (bila ya kufanya vitendo) ambako
shaitani amekuita kutaraji (رجاء) (huku ni kutumai na kutaraji rehema ya Allah baada ya kutekeleza
amri zake) ambako amewahadaa wajinga wakafikiria kuwa inawezekana kupata rehema
na maghufira bila ya kumtii Allah Subhanahu Wataala.
Allah Subhanahu
Wataala ametoa sherehe ya kutaraji (رجاء)
Akasema:-
ﭽ
ﮯ ﮰ
ﮱ ﯓ ﯔ
ﯕ ﯖ ﯗ
ﯘ ﯙ ﯚ
ﯛ ﯜ ﭼ البقرة:
٢١٨
“Hakika wale walioamini na
wale waliohajiri (wakahama kwenda Madina) na wakapigania njia ya Allah, hao
ndio wanaotumai rehema za Allah”.
Basi hao ndio hakika watumai rehema ya Allah Subhanahu Wataala baada ya
kuamini na kutenda wanayowajibika kuyafanya. Kuna tofauti kubwa baina ya
Aliyesema Allah juu yao :-
ﭽ
ﭒ ﭓ
ﭔ ﭕ ﭖ
ﭗ ﭘ ﭙ
ﭚ ﭼ المؤمنون: ٦٠
“Na hao ambao watoa (Zaka na sadaka katika mali ) waliyopewa, na hali nyoyo zao
zinaogopa kwa kuwa watarejea kwa Mola wao.”
Wajiangusha katika kumuabudu Mola wao nao wanalia kwa kumuogopa (Mola
wao).
ﭽ ﮓ ﮔ
ﮕ ﭼ الذاريات: ١٨
“Na wakiomba maghufira (msamaha) nyakati za kabla ya alfajiri.”
Kuna tofauti kubwa sana baina ya hawa na
baina ya waliojizamisha katika matamanio yao
na juu ya hivyo wacheka wasema Allah Karimu basi nani mwenye akili asema hawa
wawili mbele ya Allah ni sawa. Au kauli yake Allah Karimu inamtosha yaani hana
haja tena ya toba na kurejea kwa Mola wake.
Basi mbona yule wa mwanzo vile vile kasema Allah Karimu, mwenye rehema
na mwenye kughufuru lakini hakutosheka bali akafatilia na vitendo vizuri.
ﭽ ﯬ ﯭ
ﯮ ﭼ القلم: ٣٥
“Je!
Tuwafanye wanaotii sawa na waasi?”
ﭽ
ﯠ ﯡ
ﯢ ﯣ ﯤ
ﯥ ﯦ ﯧ
ﯨ ﯩ ﯪ
ﯫ ﯬ ﯭﯮ
ﯯ ﯰ ﯱ ﭼ الجاثية:
٢١
“Je! Wanafikiri wale waliofanya maovu kuwa tutawafanya kama wale
walioamini na kutenda mema kwamba maisha yao na
mauti yao yawe sawa?
Ni hukumu mbaya wanayoihukumu (ya kuwa wote watakuwa sawa).”
Na ghururi (kuhadaika na kudanganyika kwa kujiona kuwa neema alizokuwa
nazo ni kwa uhodari wake mwenyewe kama elimu, mali, uzuri, cheo n.k) iliokuwa
mbaya sana ni ile inayowapata wenye elimu (wanavyuoni) kujiona na kujivunia na
elimu yao na kufikiria kuwa wao ni bora kuliko wengine na kuwa Allah Subhanahu
Wataala Hakuwapa elimu isipokuwa Kawachagua na kuwapenda na wamesahau nini
Allah Amesema juu yao:-
ﭽ
ﮛ ﮜ
ﮝ ﮞ ﮟ
ﮠ ﮡ ﮢ
ﮣ ﮤ ﮥ ﮦ ﮧ ﭼ
الأعراف: ١٧٥
“Na wasomee habari za wale tuliowapa Aya zetu (kuzijua), kisha wakajivua
nazo (wasizifuate). Na shetani akawaandama, wakawa miongoni mwa waliopotea
(wasomee habari za wabaya pia wazijue wajiepushe nazo)”.
Na wengineo wengi aina kama hii na hasa
wenye kutoa mawaidha wakati wanaposimama juu ya majukwaa wafikiria katika nafsi
zao kuwa kipaji hichi hawakupewa isipokuwa wao tu na Allah Subhanahu Wataala na
kuwa wao tu ndio wanaoinusuru Dini ya Allah na wanao waongoza Waislamu. Na
ikiwa wao wanajiona kama hivyo basi wao sio isipokuwa kama taa yamulika kwa
ajili ya watu nayo yenyewe (hio taa) yaungua na vile vile kama mfano wa nyumba
iliyo giza na
taa ipo lakini imewekwa juu ya sakafu yake. Wao katika dhahiri yao wawaita watu ili kumuabudu Allah na hali
wao wenyewe wamkimbia na kadhalika watia katika nyoyo za watu hofu ya Allah Subhanahu
Wataala na hali wao wenyewe nyoyo zao ziko katika amani na adhabu yake Subhanahu
Wataala.
Allah ameshabihisha mfano wa hao ni kama
mbwa na punda basi kudhalilishwa na kupuuzwa gani kukubwa zaidi kuliko huko. Na
hao wako vikundi viwili kikundi kimoja kimejiepusha na maasi ya dhahiri na
waonekana kuwa watu wema lakini undani wao umeingiliwa na kujiona nafsi zao
bora kuliko wengine na wawaona watu wengine ni mzigo juu yao na kuwa
wawategemea wao katika mambo yao na kuwa wana fadhila kubwa kwa sababu ya uwezo
wa kuzungumza waliopewa. Na kikundi cha pili vile vile waonekana watu wazuri
kwa mujibu wa madh-hari yao (udhahiri) lakini hawaoni mambo ya matamanio
isipokuwa huyafanya, wala tamaa isipokuwa huigeuza ndio mungu wao basi unawaona
kama simba juu ya majukwaa lakini huwa kama nzi (hawawezi kujizuia kwa udhaifu
wao) mbele ya tamaa ama katika upweke wao wanakuwa majahili hawafanyi yale
wanayowahimiza watu kuyafanya (katika amri za Allah Subhanahu Wataala) na
husema mambo yahukumiwa kwa mwisho wake, na mengineyo katika mielekeo
inayowadhuru.
Anasema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
)من ازداد علما ولم يزدد هدى لم يزدد من الله إلا بعدا(
“Mwenye kuzidi elimu bila ya
kuzidi uongofu hazidi isipokuwa kuwa mbali zaidi na Allah Subhanahu Wataala”.
Na amesema Salallahu Alayhi Wasalam:
( يلقى العالم في النار فتندلق أقتابه فيدور بها في النار كما يدور الحمار في الرحى )
“Hutupwa Mwanachuoni Motoni
mpaka yatoka matumbo yake na huzunguka nayo Motoni (hayo matumbo) kama
anavyokizunguka punda kinu (cha kusagia nafaka kama
ngano n.k)”.
Na anasema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
( ويل لمن لم يعلم مرة وويل
لمن يعلم ولم يعمل مرتين )
“Ole wake aliekuwa hajui
(mjinga) mara moja na ole wake aliekuwa anajua na hakutenda (kwa mujibu wa
elimu yake) mara mbili”. Yaani elimu yake inakuwa hoja juu yake Siku ya Kiyama.
Na anasema Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
( أشد الناس عذابا يوم القيامة عالم لم ينفعه
الله بعلمه )
“Watu watakaoadhibiwa zaidi
Siku ya Kiyama ni Mwanachuoni ambaye Allah hakumjaalia kufaliwa na elimu yake”.
Amesema Ibn Masood RA:-
( كفى بخشية الله علما وكفى بالاغترار بالله جهلا )
“Kumuogopa Allah kunatosha kuwa elimu na kuhadaika na Allah
kunatosha kuwa ujinga’.
Omar bin Al-Khattab RA alimuona mmoja katika Masahaba azunguka Al-Kaaba
(afanya tawaf) na nyuma yake wanafunzi wake akampiga (Omar RA yule Sahaba)
fimbo yule sahaba akamuuliza ubaya gani ulioniona nimeufanya? Akamjibu sikuona
ubaya wowote lakini ni kumbusho kwani watu kidogo tu ambao hayaingii katika
nyoyo zao majivuno vikipigapiga viatu nyuma yao watembeapo. Tizama hadhari yao iko namna
gani watu walioridhiwa na Allah Subhanahu Wataala na wamechaguliwa basi
walinganishe hao na watu wa siku zetu hizi utamuona mmoja wao anajigamba
(anasema) nani kama mimi kwa uhodari na ufasaha na ndie mimi nilioihami Dini
hii ya Allah Subhanahu Wataala na nikiwafundisha waja wake hii Dini na nikapata
radhi ya Allah Subhanahu Wataala kwa kufanya hivyo. Hajui maskini huyu kuwa
amepata ghadhabu ya Allah Subhanahu Wataala na amejiweka mbali nae wakati
anapojifikiria kuwa anajikaribisha nae.
Ewe unaemtaka Allah (radhi yake) muendee katika njia yake ama sivyo
kunyimwa (radhi ya Allah Subhanahu Wataala ) ndio matokeo yake.
Kwa ujumla Muislamu yuko katika hatari ambayo imemzunguka kutoka kila
upande lakini iwapo ataichunga nafsi yake kwa makini sana na kuifanyia hisabu basi matokeo yake ni
kupewa tawfiiq na Allah Subhanahu Wataala ya kufikia radhi yake.
ﭽ ﮧ ﮨ
ﮩ ﮪ ﭼ التغابن:
١٦
“Mcheni
Allah muwezavyo (mwisho wa jitihada yenu).”
Kinazungumziwa
kisa katika kuihisabu nafsi hisabu iliyo ngumu:-
Kuwa kuna mtu alikuja kwa Bishr bin Al-Haarith kumuaga akamuambia
nimeazimia kutoka kwenda kuhiji je kuna utumwa wowote? Akamuuliza kiasi gani
ulichotayarisha kwa matumizi yako? Akamjibu dirham elfu mbili. Akasema Bishr
wakusudia kwa hija yako hii nini? Kwa ajili ya kuabudu (kufuata amri zake Allah
Subhanahu Wataala) au kwa kutamani kuiona Al-Kaaba au kwa ajili ya kutaka ridha
ya Allah Subhanahu Wataala? Akajibu ni kwa ajili ya ridha ya Allah Subhanahu
Wataala. Akamwambia jee ukipata ridha ya Allah Subhanahu Wataala nawe uko
nyumbani kwako kwa kuzitumia hizo dirham elfu mbili utakaa nyumbani kwako?
Akamuambia ndio nitakaa. Akamuambia nenda ukawape hizo pesa watu kumi walio na
madeni wapate kulipa madeni yao na umpe fakiri umuondolee mashaka yake na umpe
mwenye watoto masikini awatosheleze watoto wake na umpe anaelea mayatima
umfurahishe na moyo wako ukiwa una nguvu ya kuweza kumpa mtu mmoja (pesa zote
hizo) basi mpe kwani kuingiza kwako furaha katika moyo wa Muislamu na kumwokoa
alie na shida na kumuondolea mtu madhara na kumsaidia aliye dhaifu ni bora
kuliko hija mia baada ya hija ya faridha (ya Uislamu) basi simama nenda kazitoe
kama nilivyokuamrisha na kama sivyo basi nambie kitu gani kilichokuwa katika
moyo wako. Akasema Ewe Aba Nasr safari yangu kwenda kuhiji ndio yenye nguvu
zaidi moyoni mwangu. Akacheka Bishr na akamwambia:- mali ikikusanywa mnamo
uchafu wa biashara na shubuha inalazimika nafsi itumie (hiyo mali) katika haja
yoyote ile na hapo inajidhihirisha kuwa inafanya vitendo vizuri (kama kwenda
kuhiji “tatawuu”(sunna) na hali ziko njia nyingine ambazo ukiitumia humo
unapata ridhaa yake Subhanahu Wataala na ujira mkubwa) na Allah Subhanahu
Wataala Ameapa kwa Nafsi yake kuwa hakubali vitendo isipokuwa kutoka kwa wacha
Mungu.
Katika miongoni mwa adabu za waliotangulia ni walikuwa wapole kwa ndugu
zao (wa Kiislamu) na kuamkiana kwa kupeana mikono na katika hayo kuna hadithi
nyingi zilizokuja moja wapo kauli yake Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
)قبلة المسلم أخاه المصافحة(
“Kumuamkia Muislamu ndugu yake ni kumpa mkono”.
Na imetolewa na Anas bin Malik kuwa amesema: Aliambiwa Mtume Salallahu
Alayhi Wasalam kuwa mtu akutana na ndugu yake na rafiki yake amuinamie?
Akasema: Hapana. Akaambiwa amkumbatie na ambusu akasema: Hapana. Akaulizwa ampe
mkono Akasema : Ndio.
Vile vile katika adabu zao kumsimamia anaekuja nayo ni sunna yake
Salallahu Alayhi Wasalam imetolewa habari kuwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam
alimsimamia Jaafar bin Abi Taalib wakati alipomjia na akasema Salallahu Alayhi
Wasalam:-
( ما أنا بفتح خيبر أسر مني بقدوم
جعفر )
“Furaha
yangu ya kufunguliwa (kushinda vita vya) Kheiybar si zaidi kuliko ya kuja kwa
Jaafar.”
Akawaambia
Salallahu Alayhi Wasalam Ansari wakati alipokuja Saad bin Muadh RA:
( قوموا لسيدكم )
“Msimamieni bwana wenu”
Basi ada ya
watu wa Oman
ya kumsimamia anaekuja kwao iko katika msingi wa sunna ya Mtume Salallahu
Alayhi Wasalam.
Katika
sunna kumletea chakula mgeni wake (anaemtembelea) kama alivyotoa kisa Laqiit
bin Sabrah akasema tumekwenda kwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam lakini
hatukumkuta nyumbani kwake tukamkuta Aisha RA akaamrisha tufanyiwe harisa
(chakula chatengezwa kwa unga na maziwa) tukafanyiwa na vile vile tukaletewa
sahani ya tende tukala kisha akaja Mtume Salallahu Alayhi Wasalam akasema: Je
mmepata chochote (chakula) هل أصبتم شيئا Tukajibu ndio ewe Mtume wa Allah.
Vile vile
katika sunna kwa mtu anaerudi safarini awaletee chakula wanaokuja kumwamkia kama ilivyokuja kuwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam
alirudi kutoka safari akachinja ngamia.
Haitakiwi
kurudi mtu nyumbani kwake usiku kutoka safarini kwa makatazo ya Mtume Salallahu
Alayhi Wasalam kuwagongea watu wa nyumbani kwako usiku akasema Salallahu Alayhi
Wasalam:-
)إذا قدم أحدكم من سفر فلا يطرقن أهله ليلا(
“Akija mtu
kutoka safarini asiwagongee watu wa nyumbani kwake usiku”.
Nasema
katika wakati huu ambao mtu hana hiari katika kufika nyumbani kwake (kwa sababu
taratibu za nyakati za misafara imekwisha pangwa na makampuni ya ndege, train
na mabasi n.k. haiko katika mikono ya mtu binafsi kuchagua wakati anaotaka
kusafiri na kurudi nyumbani kwake pengine wakati wa kurudi kwake usiku basi
ikiwa hapana budi isipokuwa hivyo na awapigie simu nyumbani kwake awajulishe
kuwa anarejea wakati huo wa usiku na akifanya amekuwa kama kwamba amerejea
mchana kwani inakuwa imeondoka ile sababu ambayo kwa ajili yake amekatazwa na
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam. Amesema Kaab bin Maalik kuwa Mtume Salallahu
Alayhi Wasalam harudi kutoka safarini isipokuwa mchana katika wakati wa dhuhaa.
Vile vile
katika adabu za anaerudi safarini asali rakaa mbili katika msikiti ulio jirani
na nyumba yake na hichi kitu kimependelewa na wanavyuoni kwa fadhila kubwa kwa
mwenye kuweza kukifanya.
Katika
wasiya wa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam uliojumuisha mengi ni wasiya wake kwa
Muadh bin Jabal wakati alipomwambia:
( يا معاذ أوصيك بتقوى الله
وصدق الحديث والوفاء بالعهد وأداء الأمانة وترك الخيانة وحفظ الجوار ورحمة اليتيم
ولين الكلام وبذل السلام وحسن العمل وقصر الأمل ولزوم الإيمان والتفقه في القرآن
وحب الآخرة والجزع من الحساب وخفض الجناح وإياك أن تسب حليما أو تكذب صادقا أو
تطيع آثما أو تعصي إماما عادلا أو تفسد أرضا . أوصيك باتقاء الله عند كل حجر وشجر
ومدر وأن تحدث لكل ذنب توبة السر بالسر والعلانية بالعلانية بذلك أدب الله عباده
ودعاهم إلى مكارم الأخلاق ومحاسن الأدب )
“Ewe Muaadh
nakuusia katika kumcha Allah Subhanahu Wataala na ukweli katika kuzungumza, na
kutimiza ahadi na kutekeleza amana na kuacha khiyana na kuhifadhi ujirani na
kurehemu yatima na kuzungumza kwa upole na kutoa Salamu (kuamkiana kwa
Kiislamu) na kufanya vitendo vyema na kufupisha mategemeo (ya kuishi) na
kujifungamanisha na Imani na kusoma (na kuielewa) fiqhi ya Qur’ani na kupenda
Akhera na kuiogopa hesabu na kuwa mpole na usije ukamtukana mtu mwenye subira
(subira kubwa na mpole) na usimkadhibishe mkweli na usimtii mfisadi na usimuasi
Imamu (kiongozi) muadilifu au usiharibu ardhi. Nakuusia umche Allah panapo kila
mawe na miti na kijiji. Na utubu kwa
kila dhambi (unalolifanya) siri kwa siri na uwazi kwa uwazi (dhambi la siri
ulifanyie toba kisirisiri na la uwazi vile vile toba yake iwe uwazi) hivyo
ndivyo Allah alivyowafunza adabu waja wake na akawaita kufanya tabia njema na
adabu nzuri”.
Ametoa
Muadh vile vile kutokana na Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
( خذ الإسلام بمكارم الأخلاق ومحاسن الأدب )
“Uchukue
Uislamu kwa tabia njema na adabu nzuri”.
Inasemekana
kuwa hakuvaa mja vazi lililo bora kuliko unyenyekevu na anaeruzukiwa
unyenyekevu basi amepumzika na amepumzisha (watu wengine).
Na ametoa
(hadithi) Anas RA kuwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam amesema:-
( إن الله أوحى إلي أن تواضعوا
ولا يتباهى بعضكم على بعض )
“Hakika
Allah ameniletea wahyi kuwa Muwe wanyenyekevu na msiringiane baadhi yenu kwa
baadhi”.
Na amesema
Salallahu Alayhi Wasalam kuwa katika kauli ya Allah Subhanahu Wataala :-
ﭽ ﭮ ﭯ
ﭰ ﭱ ﭲ
ﭳ ﭼ
آل عمران: ٣١
“Sema (ewe Muhammad)ikiwa mnadai
mnampenda Allah basi nifuateni mimi”
Kasema:
)على البر والتقوى والرهبة وذل النفس(
“Kuwa
kumfuata katika mambo mazuri (ukiyafanya wapata thawabu na radhi ya Allah) na
kumcha Mungu na kumuogopa (kumuabudu Allah) na kujidhalilisha nafsi”.
Na alikuwa
Salallahu Alayhi Wasalam kwa unyenyekevu wake anakubali mwito wa aliye huru na
mtumwa na akubali zawadi ijapokuwa ni chubuo moja la maziwa (kwa udogo wake) au
paja la sungura na alikuwa akiilipa (hiyo zawadi kwa kutowa kitu kingine kwa
yule aliempa zawadi) na akiila (hiyo zawadi) na hatakabari katika kuitikia
mwito wa kijakazi (mtumwa mwanamke) na wa masikini na husema:
( إن من رأس
التواضع أن تبدأ بالسلام من لقيت وترد على من سلم عليك وأن ترضى بالدون من المجلس
وأن لا تحب المدحة والتزكية والبر )
“Hakika miongoni mwa kiini cha unyenyekevu ni kuanza
kumsalimia (kuamkiana kwa Kiislamu) unaemkuta na kumjibu Salamu anaekuamkia na
kuridhika na kikao cha duni(chini kabisa) katika majlisi na usipende kusifiwa
na kuonekana kuwa wewe ni bora kuliko wengine kwa imani na vitendo.”
Na anasema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
)طوبى لمن تواضع من غير منقصة وذل في نفسه من غير مسكنة(
“Malipo
makubwa (mazuri na inasemekana kuwa طوبي ni jina la mti katika Al-Jannah) kwa mtu
aliye mnyenyekevu bila ya kuwa ana upungufu wowote (yaani hana upungufu wa mali
au cheo au ukoo mzuri) na aliyejidhalilisha nafsi yake bila ya haja (hahitajii
kwa mtu kitu chochote).”
Na
aliulizwa mmoja katika watu wema juu ya unyenyekevu akasema kuikubali haki na
kuifuata na kuikubali kwa alieisema na umsikilize na vile vile kasema anaeiona
nafsi yake ina thamani basi huyo hana sehemu katika unyenyekevu. Inasemekana
kuwa imeandikwa katika vitabu vya Allah: “Hakika Nimetoa vizazi (vya binaadamu)
kutoka mgongo wa Adam (AS) na sikupata moyo ulio na unyenyekevu zaidi kwangu
kuliko moyo wa Musa (AS) ndio kwa hivyo Nimemchagua na Nimezungumza nae”. Na
yasemekana anaetambua yaliyofichika katika nafsi yake basi hafanyi tamaa ya
kupata makubwa na heshima na huenda njia ya unyenyekevu wala hagombani
(hamkasirikii) na anaemtukana. Na humshukuru Allah Subhanahu Wataala kwa yule
atakaemsema yeye kwa vizuri. Na amesema Luqman
AS : “Kila kitu kina kipando na
kipando cha elimu ni unyenyekevu”. Hakuna kitu kinachomletea mtu unyenyekevu kama kusuhubiana na watu wema. Mmoja wao aliulizwa nini
kikomo cha unyenyekevu akasema:- Uwe unapotoka nyumbani kwako humkuti mtu
isipokuwa unamuona bora kuliko wewe.
Aliulizwa
mmoja katika watu wenye hekima: Je unajua neema ambayo hahusudiwi mwenye kuwa
nayo wala balaa ambayo hahurumiwi mwenye kuwa nayo. Akasema ndio. Akasema amma
neema ambayo hahusudiwi aliye nayo hiyo ni unyenyekevu na balaa ambayo hahurumiwi
mwenye kuwa nayo ni kiburi. Na unyenyekevu ni sifa yenye nguvu inakuwa katikati
baina ya kiburi na kujiteremsha mtu kadari yake (kupindukia kiasi) amma kiburi
ni kujipandisha mtu nafsi yake zaidi ya kadari yake amma sifa inayokabili hii
ni kujiteremsha mtu nafsi yake kufika daraja ya kujipuuza na kujidharau na
inafikisha kupoteza haki yake. Na katika sifa ya waumini kuwa baina ya sifa
mbili hizi (daraja mbili hizi) mbaya (ovu) kwani kiburi bila ya shaka chanzo
chake ni ujinga kama ilivyosemwa na mmoja wa walioghurika:-
“Nimemvisha (farasi wangu tandiko lake) na nimejifunika uso wangu nikazunguka
sehemu zote za ardhi na nikasema je yuko aliye tayari kutoka kupigana na mie
basi hakutoka mtu kunijia”. Kiburi kinamtia mtu ukubwa aliekuwa hakuufikia.
Allah Subhanahu
Wataala amewatoa maanani wenye kiburi Amesema Subhanahu Wataala:-
ﭽ ﮪ ﮫ
ﮬ ﮭ ﭼ النحل:
٢٣
“Kwa hakika Yeye hawapendi
wanaotakabari”
Na
akasema:-
ﭽ ﭽ ﭾ
ﭿ ﮀ ﮁ ﭼ
الزمر: ٦٠
“Je, si katika Jahannamu
makazi ya wale wanaotakabari”
Amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam katika hadithi Qudusiy:
( الكبرياء ردائي والعظمة إزاري فمن نازعني
واحدا منها قذفته في نار جهنم )
“Kiburi
ni shati langu na ukubwa ni kikoi changu atakaenyan’ganyiana nami moja katika
hayo basi nitamtumbukiza Motoni.”
Na Allah
ametuonesha dawa kwa aliyepata maradhi hayo Akasema Subhanahu Wataala:-
ﭽ ﭣ ﭤ ﭥ
ﭦ ﭧ ﭨ ﭩ ﭪ
ﭫ ﭬ ﭼ الطارق:
٥ - ٦
“Hebu
naajitizame mtu, ameumbwa kwa kitu gani (5) Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa
kuchupa(manii)”(6).
Na kauli
yake:
ﭽ ﮐ ﮑ ﮒ
ﮓ ﮔ ﮕ
ﮖ ﮗ ﮘ
ﮙ ﮚ ﮛ
ﮜ ﮝ ﮞ ﭼ
عبس: ١٧ - ١٩
“Ameangamia
binaadamu namna gani ulivyo kwendelea mno ukafiri wake (17) Kwa kitu gani
Amemuumba (18) Kwa tone la manii; Amemuumba Akamuwezesha (Akampa uweza)”(19).
Amesema
mwana hekima:
( كيف يزهو من رجيعه أبد الدهر ضجيعه )
“Vipi ajiona
bora ambaye kwenye tumbo lake
kumejaa uchafu na kila
anapolala haumbanduki uchafu huo.”
Vipi
anatakabari mtu hali ameumbwa kwa udongo. Milele yeye huwa mwenye kufanya
makosa.
Mukabili
wake ni kujiteremsha mtu chini ya kadiri yake kwani haitakiwi Muislamu
kujiteremsha nafsi yake mahala pa kujidharaulisha na kufanyiwa masikhara na
hasa waliosoma na wavaao vilemba vyeupe (amama) wanaojishabihisha na watu wema
hao ndio wachukiza zaidi wakifanya hivyo. Basi na wawe katika msimamo wa mtu
mwenye nguvu katika elimu yake na Dini yake na sio kusimama msimamo wa alie
shindwa na kuwa dhalili na ajijue kuwa yeye yuko katika nguvu kubwa mazali
ameshikamana na kumtii Allah Subhanahu Wataala kwani Asema:-
ﭽ ﮔ ﮕ
ﮖ ﮗ ﭼ
المنافقون: ٨
“Na utukufu hasa ni wa Allah
na Mtume wake na wa Waumini”.
Hakuwaambia
maneno haya matajiri na wanaojikaribisha na viongozi basi ijue kadiri yako ewe
uliesoma na uiweke pale alipoiweka Allah. Wala usijidhili kwa kuwafuata wanaopenda
Dunia na kujifanya una haja mbele yao
kwani wewe ni bora zaidi kuliko wao. Kisha baada ya hivyo muweke kila mtu
katika daraja yake bila kumdharau. Ameitwa Al-Hassan bin Aliy “mdhalilishaji wa
Waumini” wakati alipojiteremsha (daraja) na kumpa Muawiya haki bila ya kuwa na
haki nayo. Hakika katika mambo yanaosikitisha sana kuwa baadhi ya waliosoma au
wanaojifananisha na watu wema wajitenga na kujidhalilisha mbele ya wenye vyeo
au matajiri basi kwa hivyo waliharibu jina la haki na watu wake (wa haki) kwani
wawafanyia sababu watu wajeuri kurefusha ndimi zao juu ya watu wa fadhila (wa
Dini, wema).
Mara nyingi
wasikia watu wajeuri (wahuni) wakiwasema watawaa (walioshika Dini) kwa
kujitakia na kujiharibia wenyewe watawaa hata wakawapa fursa hao wahuni kuwaudhi.
Yasemekana hapo zamani kulikuwa na kadhi ambaye ameimbiwa na muimbaji mpaka
akastarehe kisha akajivalisha kamba shingoni akasema nivuteni nipate kuwa
zawadi (hadyi) ya Al-Kaaba kwani mie n’gombe, kwani kajidharaulisha mwenyewe na
huu ni mfano kwa wengine vile vile.
Omar bin
Khattaab RA alimuona mtu anakwenda kajiinamia akamwambia nyanyua kichwa chako
usituharibie Dini yetu. Sheikh Saleh bin Aliy Al-Haarthy alimuona mtu
amejitenga naye kajiinamia akamwambia una nini? Akamjibu nimevaa amama (kilemba
cheupe ambacho ukikivaa umefuata sunna ya Mtume Salallahu Alayhi Wasalam)
nimekuwa mutawaa. Akamwambia kazana kwani wafikiria anaekuwa mutawaa anapooza
na kuwa mnyonge. Akamvua amama yake na kuitupa chini. Mtu anaekamata Dini
lazima awe mfano mzuri kwa wengine kwa tabia nzuri na ushujaa na kukazana.
Amesema Abu Nasr Al-Maghribiy katika shairi lake kwa
maana yake:-
Nampenda
kijana anaetafuta maendeleo (elimu na kazi na mengineyo) na amekazana kwa ajili
ya Dunia na Akhera. Amma ndugu yake usingizi hakaribishwi kwangu wala alielegea
na kupooza asiependa maendeleo.
Kuingiliana
na watu pamoja na kushika amri za sheria ya Dini (zinazohusiana na haki za
watu) ni bora kuliko kujitenga ijapokuwa imekuja katika hadithi ya Mtume
Salallahu Alayhi Wasalam ishara ya kupendelea kujitenga na mtu kukimbia na Dini
yake. Basi hivyo ni wakati hawezi muumini kusimamisha Dini yake na aogopa kuwa
atawacha kufanya yaliyomuwajibikia kuyafanya au kufanya maasi (ikiwa
atachanganyika na watu) kama ilivyokuja
(hadithi) kutokana na Abdullah ibn Masood RA amesema:-
Amesema
Mtume Salallahu Alayhi Wasalam :-
( ليأتين على الناس زمان لا
يسلم لذي دين دينه إلا من فر بدينه من قرية إلى قرية ومن شاهق إلى شاهق ومن جحر
إلى جحر كالثعلب الذي يروغ قالوا ومتى ذلك
يا رسول الله قال إذا لم تنل المعيشة إلا بمعاصي الله فإذا كان ذلك الزمان
حلت العزوبة) . قالوا وكيف ذلك يا رسول الله
وقد أمرتنا بالتزويج قال (إنه إذا كان ذلك الزمان كان هلاك الرجل على يد أبويه فإن
لم يكن له أبوان فعلى يد زوجته وولده فإن لم يكن له زوجة ولا ولد فعلى يد قرابته)
قالوا وكيف يا رسول الله قال (يعيرونه بضيق المعيشة فيتكلف ما لا يطيق حتى يوردوه
موارد الهلكة)
“Utawajia
watu wakati hasalimiki mwenye Dini na Dini yake isipokuwa ataekimbia na Dini
yake kutoka mji kwenda mji mwingine na kutoka mlima (mrefu) kwenda mlima
mwingine na kutoka shimo kwenda shimo jingine kama
mbweha anayechenga. Wakasema na lini yatakuwa hayo ewe Mtume wa Allah, Akasema:
wakati maisha yatakuwa hayapatikani isipokuwa kwa maasi ya Allah. Basi ukifika
wakati huo unahalalika ujane. Wakasema na vipi hivyo ewe Mtume wa Allah na hali
wewe umetuamrisha kuoa. Akasema : Hakika unapokuja wakati huo kunakuwa
kuangamia kwa mtu katika mikono ya wazazi wake na akiwa hana wazazi basi katika
mikono ya mkewe na watoto wake na akiwa hana mke wala watoto basi katika mikono
ya jamaa zake. Wakasema vipi hivyo ewe Mtume wa Allah. Akasema wanamnyanyasa
kwa ajili ya udhiki wa maisha yake basi hapo ndipo anapojikalifisha zaidi ya
uwezo wake mpaka wanamwingiza katika mambo ya kuangamiza”.
Basi kama
hivyo amebainisha Mtume Salallahu Alayhi Wasalam wakati gani kujitenga (na
watu) kwapendelewa bali ni wajibu ikiwa kuchanganyika na watu kutamharibia mtu
Dini yake.
Ama ikiwa
aweza kusema haki hata ikiwa hasikilizwi na ikiwa aweza kumuongoza anaetaka
kuongozwa na kumuelekeza aliepotea basi kama huyu kukaa kwake katika jamii ni
bora kuliko kuondoka kama ilivyotolewa kuwa Allah Subhanahu Wataala
amemteremshia wahyi Dawud AS : Ewe Dawud vipi Nakuona umejitenga uko
peke yako. Akajibu: Mola wangu nimewaacha watu kwa ajili Yako. Basi Allah
Akamletea wahyi; Ewe Dawud kuwa mwenye kuzinduka ujichukulie marafiki na kila
rafiki aliyekuwa haniridhishi Mimi usifuatane nae kwani huyo moyo wako utaingia
ugumu kwake na atakupeleka mbali na mimi. Imekuja katika habari: Hakika aliye
na daraja bora miongoni mwenu mbele ya Allah ni wale wanaozoea na kuzoewa (na
watu) kwani muumini anazoea na anazoewa (azoeleka). Amesema Ubadat bin Assaamit
RA kuwa Mtume Salallahu Alayhi Wasalam amesema:-
( يقول الله عز وجل حقت محبتي للمتحابين في
والمتزاورين في والمتباذلين في والمتصادقين في )
“Asema
Allah Mwenye nguvu Aliyetukuka yamewajibika mapenzi yangu kwa wanaopendana kwa
ajili Yangu na wanaotembeleana kwa ajili Yangu na wanaopeana kwa ajili Yangu na
wanaofanyiana ukweli kwa ajili Yangu.”
Vile vile
imetokana na Mtume wa Allah:
( المؤمن كثير بأخيه )
“Muumini ni
mwingi kwa ndugu yake”.
Kuyafanyia
umuhimu mambo ya Wailamu ni wajibu na asiyeyafanyia umuhimu mambo ya Waislamu
basi sio miongoni mwao na aliekuwa hana rafiki hana maisha (mazuri) na amesema
Allah azungumzia hali ya makafiri katika Akhera:-
ﭽ ﮮ ﮯ ﮰ
ﮱ ﯓ ﯔ ﯕ ﯖ
ﯗ ﭼ
الشعراء: ١٠٠ - ١٠١
“Basi hatuna
waombezi (100) Wala rafiki khalisi (101)”
الحميم katika asili yake ni الهميم ikabadilishwa harufu هـ ikawekwa badala
yake ح na الهميم imechukuliwa kutokana na الاهتمام yaani kufanya umuhimu mambo ya ndugu yake
(rafiki yake awe naye).
Amesema Omar RA:- Akiona mmoja wenu mapenzi kutoka kwa ndugu yake
(rafiki yake) basi amkamate (huyo rafiki awe naye).
Tunamuomba
Allah Subhanahu Wataala Atupe taufiki (ya kushika Dini yake) na mwisho mwema na
kufa katika uongofu na tufanye kwa mujibu wa elimu yetu na hakuna uwezo wala
nguvu isipokuwa kwa Allah na rehema na Salamu ziwe juu ya mbora wa viumbe vya
Allah Muhammad bin Abdullah na juu ya watu wake na Masahaba wake na kila
aliyemfuata.
[1] Inavoonesha, mtungaji amechukua hadithi hii kutoka
kitabu cha Imam Al-Ghazali kiitwacho (Ihyaau Uluumi 'Diin),
nayo ni miongoni mwa hadithi za humo ambazo Maulama wa Hadithi wamesema
hazikuthibiti kutoka kwa Mtume – rehma za Allah na amani zimshukie. Bali
imesemwa kuwa ni maneno ya Abu Addardaa
mwenyewe, kama alivoitoa Imam Ahmad katika kitabu chake (A'zuhd) na
Alhaafidh Al-Iraaqiy katika (Takhriiju Ahaadithi Al-Ihya).
No comments:
Post a Comment
Note: only a member of this blog may post a comment.