Tuesday, 19 January 2016

Juzuu 11 Mtume---Kujenga uongofu katika nyoyo za vijana














Alitoka -rehema za Allah na amani zimshukie- kwenda Shaam pamoja na ami yake Abu Talib ambaye alisimama pamoja naye katika misukosuko iliyompata, alimnusuru na kumgombea bila ya yeye mwenyewe kuingia katika Uislamu juu ya kuwa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- alimtaka afanye hivyo katika kauli yake:

 قل كلمة أحاج بها لك عند الله    maana yake: “Sema neno nitakugombea kwalo mbele ya Allah”. Badili yake wakati alipozidiwa na uangamiaji wake alisema: “Siwezi kuacha dini ya mashekhe(wazee)”. Lakini kwa sababu ya msimamo wake mzuri (wa kumhami Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie-) amepunguziwa adhabu kama ilivyokuja kutokana na Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- kuwa adhabu yake itakuwa katika kina cha chini cha moto wa Jahannam(“Dhahdhah”). Laiti ningejua nini hii “Dhahdhah”. Watu wa Oman husema katika methali: “Hakuna katika moto jinga lililo baridi”. Twajikinga kwa Allah na moto wa Jahannam, ufupi wake wa kina au urefu wake.


Aloposafiri na ami yake umri wake ulikuwa miaka tisa, na alimuowa Bibi Khadija bint Khuwailid wakati umri wake ulipokuwa miaka ishirini na tano na umri wa Bibi Khadija miaka arubaini na watoto wake Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- wote amezaa na Bi Khadija isipokuwa Ibrahim amezaa na Maria Al-Qibtiya. Alipokufa Ibrahim alikuwa mwenye umri wa miaka miwili na alilia Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- kwa huzuni ya kufa kwake, alipoambiwa wewe walia na watukataza sisi kulia akasema:

                                إنما أبكي شفقة ورحمة له ولا أقول ما يسخط الرب

“Hakika mimi nalia kwa kumuonea huruma na sisemi lile linalomghadhibisha Mola wangu.                                                                                                                                                                                                                 


Alisafiri Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie-, kabla ya kumuowa Bibi Khadija, kwenda kufanya biashara huko Shaam pamoja na mfanya kazi wa Bibi Khadija, Maysara, basi aliporudi kutoka Shaam akamuelezea bibi yake juu ya Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie, tabia zake nzuri na ishara zioneshazo Utume wake (hapa kabla ya kupewa Utume) baada ya kusikia  hayo Bibi Khadija alimtaka Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- amuoe na akampelekea posa yeye mwenyewe, akakubali -rehema za Allah na amani zimshukie- kisha akamuoa. Basi akapata hadhi kubwa Duniani na akafuzu huko Akhera kwa kuingizwa Janna kwani amembashiria Jibril A.S kuwa ana Nyumba ya Jawhar huko Peponi yasiyokuwemo makelele humo(ugomvi) wala machofu. Alikufa Bibi Khadija mwaka ule ule aliokufa ammi yake Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie, Abu Talib, kwa hivyo ukaitwa mwaka huo “mwaka wa huzuni” baada ya Utume kwa miaka kumi na mbili.

                                                                                                                                                                         Alipokuwa umri wake miaka thelathini na sita Makureshi waligombana wakati wa kulijenga Al-Kaaba juu ya nani aliweke “Al-Hajar Al-Aswadi”(Jiwe lijulikanalo katika pembe moja ya Al-Kaaba) na kila kabila liliona lina haki ya kuliweka. Hapo wakamchagua Mtume awe hakimu wao na kuwa watakuwa radhi na hukumu atakayoitoa kwani walikuwa wakimwita Al-Amiin(mwaminifu). Basi alileta -rehema za Allah na amani zimshukie- kitambaa na kuliweka hilo jiwe juu yake kisha akaita kila kabila lilete mbele mtu mmoja akamate hicho kitambaa kisha walinyanyue na kuliweka mahali pake maalumu kwenye pembe ya Al-Kaaba.


Alipokuwa umri wake miaka arubaini na moja aliletewa “Wahyi” alipokuwa katika pango lijulikanalo kwa “Ghaar Hiraa”.Wakati huu alikuwa apenda kujitenga na kuwa pekee kwa ajili ya kuabudu katika pango hilo. Akaja Jibriil A.S kumletea Wahyi kutoka kwa Mola wake akamuambia:  اقرأ yaani soma akajibu siwezi kusoma basi akambana huku akimwambia soma akajibu siwezi kusoma akamfanyia hivyo mara tatu kisha akamsomea:

 اقرأ باسم ربك الذي خلق  “Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba”, aya ya kwanza ya sura Al-Alaq. Basi akahofu na akenda kwa Bibi Khadija akamwambia:دثريني دثريني  yaani nifunike nifunike, alifahamu Bi Khadija kuwa ana hofu akamuliza sababu yake   akamwambia aliyoyaona akamwambia: Tumaini Allah Subhanahu Wataala hawezi akakuwacha kwani wewe unawasili Rahimu na unawasaidia wenye kupata misiba.Na ikamteremkia: يأيها المدثر “Ewe uliyejifunika maguo”.


Walipojua tu Maqureshi juu ya jambo hili, na baada ya Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- kuwadhihirishia huu mwito wa kufuata Dini ya Allah Subhanahu Wataala wakamgeukia na kumfanyia maudhi mbali mbali tokea kumtukana mpaka kumpiga na kumkadhibisha na mengineyo yaliotajwa katika vitabu vya sira. Na mwishowe wakamfunga pamoja na ahli ya nyumba yake na kabila lake, Waumini na makafiri wao miongoni mwa kabila la Abdil Muttalib. Wakawafunga katika bonde, baina ya milima miwili, lisilokuwa na uwazi wa kutokeya upande wa pili. Wakawazuilia kupewa chakula, maji, kufanya biashara na hata kutembeleana,  msuso haujatokea bado kama huo na wakaunganika makabila yote ya Qureshi juu ya msuso huo, wakaandikiana mkataba kuwa asitoke Muhammad na watu wa nyumba yake katika bonde hilo mpaka wafe humo. Wakabakia humo miaka mitatu kama ingekuwa si kwa maangalizi ya Allah Subhanahu Wataala  na hifadhi yake kwao hakika wangekufa.


Kinatosha kisa kilichowatokea  kuwa zingatio la kuonesha hali gani ngumu na mashaka iliyowapata. Alisimulia mmoja wao: Niliamka usiku kwenda haja ndogo basi nikakojolea kitu kitoacho sauti chini yangu nikakichukua kumbe ngozi ya ngamia,nikaiosha na kuichoma kisha nikaila. Jee kuna kitu tena zaidi ya hicho?.


Baada ya kupita miaka mitatu Allah Subhanahu Wataala akajaalia watu fulani kwenda kuuharibu huo mkataba wakaukuta wote umeliwa na mchwa isipokuwa    اللهم باسمك      na hiyo ilikuwa ndiyo sababu ya kutolewa kifungoni. Akaelekea Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- kwenda Taaif kwa kudhania labda huko atawapata watakaosikiliza mwito wake lakini ukweli ulikuwa kinyume cha hayo, kwani alipata maudhi makubwa hayana mfano kutoka Thaqiif kama ilivyozungumziwa katika vitabu vya Sira (hakika mukhtasari huu ni kwa ajili ya kuhimiza kutafuta-elimu).


Basi akarejea kutoka Taaif hali ana uzito katika moyo wake kwa mambo yaliyompata huko na hali ikazidi kuwa mbaya kwa kufiwa  na mkewe mtiifu na ammi yake mwenye huruma naye. Akataka Mola wake kumuondolea uzito huo na kumliwaza kwa kumchukua katika mwendo wa usiku wa Israa kutoka Masjid A-Haraam kwenda Masjid Al-Aqsa kisha kumpaza Mbinguni kwenda “Sidrat Al-Muntahaa”. Allah Aliye Karimu                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                 Amempa heshima -rehema za Allah na amani zimshukie- kwa muujiza huu mtukufu hata asifikirie kuwa amemwakilishia mambo yake juu ya mmoja katika viumbe vyake. Akamuamini mwenye kuamini (baada ya kuelezea watu kisa chake hicho) na akamkadhibisha mwenye kukadhibisha  na hakuna aliyetokea katika sura nzuri zaidi kwenye jambo hili kama Abu Bakar Assiddiq,hakuna mwingine aliyewafikiwa kama yeye. Wakati alipoambiwa juu ya madai ya sahibu yake (Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- kuwa amefika Masjid Al-Aqsa kisha akapazwa kwenda Mbinguni katika sehemu ndogo ya usiku huo) alisemaكان قال فقد صدق: إن maana yake “Ikiwa amesema hivyo basi   usemi huo ni  kweli”. Kwa hiyo Allah Subhanahu Wataala akamwita Siddiiq na akapata heshima kubwa kwa sifa hiyo.


Akaendelea Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- pamoja na Waumini wenye kudhalilishwa waliyonae kupata kila maudhi kwa washirikina. Mpaka alipotoa idhini Allah Subhanahu Wataala kwa kila anayetaka katika hao waumini kuhajiri kwenda Uhabeshi ili kuwapunguzia mateso wanayoyapata. Allah Subhanahu Wataala akawatiishia mfalme wa Uhabeshi aitwaye Annajaashiy, akawaangalia vizuri na kuwaonea huruma. Aliingia Uislamu kisirisiri na alipokufa, alisaliwa na Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- huko madina sala ya maiti “ghaiib”(maiti asiyekuwepo). Kisha yakawa matayarisho yanafanywa kwa Hijra kubwa ya kwenda Madina. Ukafanyika muahada wa mwanzo wa kujitolea na Maansari “Beiy’at Al-Aqaba” katika musimu wa Hija.


Muahada wa pili ukafanyika katika mwaka uliofatia na ambao ulifatiwa na hijra ya Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- baada ya kuhajiri wengi katika Masahaba kwenda Madina, pahala penye amani ambapo imepelekwa Da’awa iliyotahirika.


Visa vingi vilitokea vinavyoambatana na tukio hili la Hijra, ama Abubakar Siddiq   alifuzu kuupata Usuhuba wa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- ambaye ndiye pekee aliyehajiri nae kutoka Makka kwenda Madina. Waislamu wote walihajiri kisirisiri isipokuwa Omar bin Khattab Al-Faaruuq alihajiri wazi wazi bila ya kificho, aliwaita Maqureshi baada ya kuiaga Al-Kaaba akasema: Mimi nahajiri basi anaetaka mama yake amkose  anifuate na hakuna aliyejasiri kumfuata. Nguvu ni kitu kisifiwacho kwani kinaweza kufanya mengi.


Alipofika Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- Madina kitu cha kwanza alichokifanya ni kujenga Msikiti wake -rehema za Allah na amani zimshukie. Ikawa ni Sunna kwa kila anaehamia mahala,kitu cha kwanza ajue sehemu atakaposalia, na hata nyumbani kwake  Muislamu inapendelewa aweke mahala maalumu pa kusalia. Kadhalika ukijengwa mji mpya kitu cha kwanza  kinachowekwa katika plani na kujengwa ni Msikiti. Waliafikiana Waislamu waifanye Tarehe yao kutokana na tukio la Hijra na wakaufuta ule mvunjiko ulioko baina ya Muharram na Rabiil-Awal (Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- alihajiri katika Rabiil-Awal lakini Muharram ndio uliojaaliwa mwanzo wa mwaka). Hapo mwanzo tarehe ilikuwa juu ya msingi wa matukio yaliokuwa yakipita. Kama kusema miaka fulani imepita baada ya tukio fulani. Kwa mfano wamesema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- amezaliwa katika mwaka wa Al-Fiil na kadhalika.


Yasikitisha leo kuwa Waislamu wamejisahaulisha tarehe yao ya Hijra baada ya kuijua na kuifuata wakaiwacha na kukamata tarehe ya Miladi (A.D). Nadhani kwa sababu mishahara yao inaambatana nayo. Kuna mithali ya Ki-Omani inayosema ‘Mwezi ambao huna matumizi ndani yake huhisabu siku zake’. Imebakia Serikali ya Suudiya imehifadhi Tarehe ya Hijra, Allah aijazi kheri.


Katika mwaka wa pili wa Hijra imefaridhiwa funga ya mwezi wa Ramadhani na katika mwaka huo huo vilikuwa vita vya Badri vilivyotenganisha baina ya Haki na batili kwa hivyo ikanyanyuka shani ya Uislamu na wakauliwa humo waliouliwa miongoni mwa majabbari wakubwa wa Kiqureshi. Na katika mwaka wa tatu wa Hijra vilikuwa vita vya Uhud ambavyo waliuliwa humo Waislamu wengi kwa sababu ya  kuihalifu amri ya Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- na dhana nzuri waliokuwa nayo  Masahaba (ya matumaini ya kushinda vita) kisha wakashindwa washirikina. Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- aliwaamrisha watupa mishare na upinde wakamate sehemu zao bila ya kuziacha hata wakiona washirikina washindwa, wao wakenda kinyume ya amri yake -rehema za Allah na amani zimshukie- wakaziwacha hizo sehemu kukimbilia ngawira. Hapo ndipo wapiganaji wakishirikina wakazikimbilia hizo sehemu na kusababisha kushindwa kwa Waislamu mara ya pili. Wakauliwa wengi katika Waislamu kisha Allah Subhanahu Wataala akawapa nguvu na kurejea katika mpambano ndipo waliposhindwa washirikina kama alivyosimulia Allah Subhanahu Wataala katika Kitabu chake kitukufu.


Kutokana na vita hivi kuna zingatio muhimu la kuchukuliwa nalo kwa ajili ya kupinga amri moja tu katika amri zake Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- kumesababisha kushindwa Waislamu vipi leo itakuwa hali yao Waislamu na  wamekwenda kinyume cha amri zake zote Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie? Lini kushindwa na maadui zao kutawabanduka? Leo umebainika ukweli wa hadithi ya Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- juu ya hali Waislamu-:

يوشك أن تتداعى عليكم الأمم كما تتداعى الأكلة على قصعتها قالوا : أومن قلة  يومئذ نحن يا رسول الله؟ قال : بل أنتم كثير ولكنكم غثاء كغثاء السيل ولينزعن الله الهيبة من قلوب أعدائكم وليقذفن الوهن في قلوبكم قالوا : وما الوهن يارسول الله ؟ قال : حب الدنيا وكراهية الموت                    

“Uko karibu wakati ambao umma zote zitaitana kuwakusanyikia (Waislamu) kama wanavyoitana walaji kukikusanyikia chakula chao. Wakasema: Je ni kutokana na  uchache wetu siku hiyo ewe Mtume wa Allah? Akasema: Bali nyie wengi lakini  nyie ni takataka kama takataka za (maji ya) mvua, kwa hakika Allah ataondoa katika nyoyo za maadui zenu kuwaogopeni na hakika atawatia katika nyoyo zenu udhaifu wakamuuliza na ni udhaifu gani ewe Mtume wa Allah, akajibu kupenda Dunia na kuchukia mauti.”


Amesema shekhe Abu Muslim Allah Amrehemu katika shairi: “Mtengano katika Uislamu haukusababishwa na upanga wa adui yake zaidi ya ulivyo baina ya watu wake(Waislamu wenyewe kwa wenyewe).”


Katika mwaka wa sita wa Hijra alielekea Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- kwenda kufanya Umra kwa mara ya kwanza tokea kuihajiri Makka lakini washirikina walimzuia kuingia kwa hivyo alirejea kutoka Hudeibiya. Na humo ukafanyika muahada wa 'Arridhwaan' na ikashuka sura ya Al-Fat-h. Ikawa ndio mara ya kwanza Maqureshi kumtambua Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- na Dola yake, kwa hivyo ukawa ndio Ushindi wa mwanzo wa Waislamu na utangulizi wa kuifungua kwao Makka (kuichukua kutoka kwa washirikina) na kudhihirika kwao. Na katika mwaka wa nane ilifunguliwa Makka ihishimiwayo na ndio ikawa mwisho wa nguvu ya washirikina wakadhihirika katika hali ya udhalilifu na utiifu kwa Waislamu wakasema (kumwambia Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie : “Ndugu mheshimiwa na mtoto wa ndugu mheshimiwa umemiliki basi samehe,” akasema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie:اذهبوا فأنتم الطلقاء  “Nendeni kwani mko huru”. Basi akawaachia na kuwakomboa baada kuwa umewamiliki mkono wake wa kuume na hii ndio shaani ya watu wakarimu.


Katika mwaka wa tisa Abu Bakar - Allah amridhie- alikwenda kuwapeleka watu kuhiji na ikateremka sura ya Bara’ah (Tawba). Basi Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- alimtuma Ali bin Abi Talib kwenda kuwasomea watu (hiyo sura) na awafukuze washirikina wasiingie Al-Haram kwa hiyo ikawa mwisho wao kuitufu Kaaba. Walikuwa wanawalazimisha watu kutufu uchi isipokuwa akikodi nguo kwao ili atufu eti wadai haifai mtu kutufu Kaaba na nguo aliyomuasi nayo Allah Subhanahu Wataala wakijisahau nafsi zao kuwa wametopea katika najasa na maasi, methali inasema: “Unaliona vumbi katika jicho la ndugu yako lakini hulioni gogo katika jicho lako”.


Katika mwaka wa kumi alihiji Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- hija ya “Al-Wida’a (Muagano)na akawafundisha watu namna ya kuhiji na akasema:خذوا عني مناسككم  “Chukueni kutoka kwangu Ibada zenu”. Kila alichofanya Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- katika Hija hiyo wanawajibika Waislamu wakifanye na kinyume chake ni kuhalifu Sunna yake. Na katika mwaka wa kumi na moja ilikamatwa roho yake Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- na akajiunga na Rafiki zake waliyotukuka(Watu wa Peponi).


         الزمر: ٣٠

“Kwa yakini wewe  utakufa na wao pia watakufa”


Akasimamia jambo hili (la Uislamu) Abu Bakar Siddiq baada ya kufa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- usimamizi ulio barabara kwa muda wa miaka miwili na miezi kadha. Kisha akasimamia Omar bin Khattab -Al-Farooq- kwa muda wa miaka kumi kisha baada yake Othman bin Affan kwa muda wa miaka kumi na mbili, walimsifu watu mwanzo wa Khilafa yake kisha baada ya hapo wakachukizwa na mambo yake mwishowe akafa kwa kuuliwa. Akasimamia baada yake Ali bin Abi Talib kwa muda wa miaka mitano na miezi kadha akafa hali ya kuwa ameuliwa. Kisha Khilafa (utawala wa Kiislamu) ukabadilika kuwa ufalme wakawa Maumawiy wanapasiana baina yao ufalme kisha baada yao Maabasiy kisha waliokuja baada yao. Na mwenye kutaka kujua zaidi basi arejee kwenye vitabu vya sira na tarehe.


Baada ya mwaka  arubaini wa Hijri haukubakiya tena mwendo (sira)wa kweli wa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- na wa Makhalifa wake wenye kufuata muongozo wa sawasawa (Arraashidiin) isipokuwa baada ya kuuhuisha mwendo huu Waislamu waitwao kwa jina la Maibadhi (Al-Ibaadhiya) katika mwaka wa mia na ishirini na nane Hijri. Katika Oman walimsimamisha Al-Julanda bin Masood ahukumu kwa sheria ya Allah na katika nchi za Magharibi ya Arabuni walimsimamisha Abu Al-Khattab Al-Maafriy na ama katika Hadhramaut na Yemen walimweka Taalib Al-haq Abdallah bin Yahya Al-kindiy. Na hii ni neema kutoka kwa Allah Subhanahu Wataala juu ya Maibadhi kwani Sunna hii haikupatikana isipokuwa kwao tu, hakika hakuna wengine waliyosimamisha Maimamu wakahukumu katika msingi wa Makhalifa waliongoka tokea wakati ule mpaka wakati wa mwisho tuliokuwa nao sasa hivi isipokuwa wao. Tutaelezea akitaka Allah Subhanahu Wataala kisa cha kufa kwake Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- kwa kirefu.




Amemhusisha Mola wake kwa kumtukuza kwani yeye ndiye mbora  wa viumbe vyote. Amemhusisha kuwa mwisho wa Manabii na kumteremshia Qurani ambao ni muujiza wa milele. Kadhalika amehusishwa kwa mambo mengi nayo ni kama yafuatayo:- kuchimbuka maji chini ya vidole vyake, Laylatul- Qadri, siku ya Ijumaa, sala ya Ishaa Al-aakher, sala ya jamaa, Adhana,sala ya Witri, kupiga mswaki, kutofanya mashairi kwani haipendezi kwake kufanya hivyo, kuona kwa nyuma kama anavyoona kwa mbele, ardhi yote kuwa Msikiti na udongo wake   ni tahiri, kuhalalisha ngawira, kuendelea kufunga (siku kadha bila ya kufuturu magharibi), kutokuolewa wake zake baada yake na wao kuwa Mama wa Waumini, hatoi mahari na hahitajii walii kwani yeye ni karibu zaidi kwa Waislamu kuliko nafsi zao, amkubalie mwanamke anayejitoa nafsi yake kwake, ameharamishiwa kuowa wanawake watumwa, hakidhihiriki kitokacho tumboni mwake bali kinamezwa na ardhi,mtu hawezi kuona utupu wake na akiuona hupofuka macho, huogopewa na maadui kutoka mwendo wa miezi miwili, ni mtu wa kwanza inayempasukia ardhi (siku ya Kiyama), ni wake Uombezi mkuu (الشفاعة العظمى) siku ya Kiyama, ni wake Umma mkubwa zaidi kuliko umma nyingine, atatoa ushahidi kuwa Mitume wengine wamefikisha ujumbe ijapokuwa yeye ndie wa mwisho wao, ana Hodhi watakaloingia watu wema katika Umma wake, yeye wa kwanza atakaeingia Peponi, amepelekwa kwa    wote majini na binadamu, wakati alipopelekewa ujumbe zilikuwa mbingu zikilindwa. Amesema Ibn Abbas Allah Subhanahu Wataala amridhie: Hakuumba Allah nafsi bora kwake kuliko Muhammad -rehema za Allah na amani zimshukie- kwani hakuapa kwa uhai wa yoyote isipokuwa wake -rehema za Allah na amani zimshukie- na akaapa juu ya uongofu wake. Amesema:-








Na kaapa juu ya Ujumbe wake:-


يس: ١ - ٣

“Yaa Siyn(1) Naapa kwa (hii) Qur’ani yenye kutengenezwa vizuri(2) Kuwa hakika wewe ni miongoni mwa Mitume (wa Allah)(3)”

 Na kaapa juu ya mapenzi yake:-


الضحى: ١ - ٣

“Naapa kwa mchana(1) Na kwa usiku unapotanda(2) Hakukuacha Mola wako wala hakukasirika (nawe Ewe Nabii Muhammad)”

Na kaapa juu ya utukufu wa tabia yake:-


القلم: ١ - ٤

Nuun(Naapa kwa) Kalamu na yale wayaandikayo (kwa kalamu hizo)(1) Kwa neema ya Mola wako wewe si mwendawazimu. (Makafiri wakimwambia Mtume-kwa ajili ya kumtukana tu-kuwa yeye ni mwendawazimu)(2) Na kwa hakika una malipo yasiyokatika (yataendelea maisha)(3) Na bila shaka una tabia njema kabisa(4)”

Na kaapa juu ya kusalimika kwake na upungufu:-


الحاقة: ٣٨ - ٤٣

“Basi naapa kwa mnavyoviona(38) Na msivyoviona(39) Kwa hakika ni kauli iliyoletwa na Mjumbe(wa Allah ) mwenye heshima (kubwa)(40) Wala si kauli ya mtunga mashairi (kama mnavyosema). Ni machache sana mnayoyaamini(41) Wala si kauli ya mchawi (kama mnavyodai). Ni kidogo kuwaidhika kwenu(42) Ni uteremsho utokao kwa Mola wa viumbe vyote(43)”


Na kaapa kuwa Allah amlipiza kisasi anayemuudhi Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie:-


العلق: ١٥ - ١٦

Sivyo hivyo (anavyofanya!). Kama haachi, Tutamkokota kwa nywele za utosi (wake tumtie motoni)(15) Utosi muongo, wenye madhambi(16)”


Na kaapa kwa Uhai wake -rehema za Allah na amani zimshukie:-


الحجر: ٧٢

“Naapa kwa umri wako! Hakika wao walikuwa katika ulevi wao (wa maovu) wanahangaika ovyo.”


Na kaapa juu ya umbali wa maadui zake kutokana naye:-


المطففين: ١٥

“Sivyo hivyo! Hakika watazuiliwa, siku hiyo na (neema za) Mola wao.”


Na kamhusisha kuwa tofauti na watu wengine:-


النور: ٦٣

“Msifanye wito wa Mtume baina yenu kama wito wa nyinyi kwa nyinyi”

Na kamhusisha kupunguzwa sauti mbele yake na kuwa kunyanyanyua sauti kwabomoa vitendo (thawabu):-

الحجرات: ٢                                  

“Enyi   mlioamini! Msipaze sauti zenu kuliko sauti ya Mtume wala msiseme  naye kwa sauti ya nguvu kama mnavyosemezana nyinyi kwa nyinyi, visije vitendo vyenu vikakosa thawabu, na hali hamtambui”


Na kamhusisha kwa kutajwa jina lake pamoja na jina la Allah kwani kila zinapotolewa shahada mbili ikiwa katika Adhana, Ikama, hotuba au kushahadia hatajwi Allah isipokuwa hutajwa naye Mtume  -rehema za Allah na amani zimshukie.

Kamhusisha kwa kuwaamrisha Malaika wake na waja wake Waumini wamsalie:-


الأحزاب: ٥٦

“Hakika Allah anamteremshia rehema Mtume; na  Malaika wake (wanamuombea dua kwa vile vitendo vizuri alivyovifanya). Basi enyi Waislamu (mliopata neema hii ya kufindishwa haya na Mtume) msalieni (Mtume, muombeeni rehema) na muombeeni amani.”

Na Allah Subhanahu Wataala amemtaja Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- pamoja naye mara nyingi katika Qurani:-


التوبة: ٧٤

“Na hawakuona baya (kwa kuja Uislamu) ila ya kuwa Allah na Mtume wake amewatajirisha kwa fadhila zake”


Na katika kauli yake :-


النساء: ٨٠

“Mwenye kumtii Mtume amemtii Allah (kwani anayoyaamrisha Mtume yametoka kwa Allah”


Na wakati alipomlaumu alimtangulizia msamaha kabla ya lawama :-



التوبة: ٤٣

“Allah amekuwia radhi (amekusamehe). Kwa nini umewapa ruhusa? (Ungengoja) mpaka wanaosema kweli wakupambanukie, na uwajue waongo.”


Na kamhusisha kwa kumghufiria madhambi yake yaliyopita na yajayo:-

 

الفتح: ٢

“Ili Allah akusamehe makosa yako yaliyotangulia na yanayokuja, na kukutimizia neema zake na kukuongoa katika njia iliyonyooka”


Na amemhusisha kuwa hakumwita kwa jina lake kama Manabii wengine bali alimwita kwa kauli yake:-

( يأيها النبي ، يأيها الرسول ، يأيها المزمل ، يأيها المدثر ) Ewe Nabii, ewe Mtume, ewe Uliyejifunika maguo, ewe Uliyejifunika maguo.

Na pia amemhusisha kwa kuwajibishia Waislamu wamsalie na kuifanya  Ibada juu yao. Ziko hadithi nyingi zithibitishazo hayo kama kauli yake Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie:-

( من ذكرت عنده فليصل علي وإن صلاتكم علي إجابة لدعائكم وزكاة لأعمالكم ومرضاة لربكم ) 

“Ninaetajwa mbele yake basi na anisalie kwani kunisalia kwenu ndio kukubaliwa dua zenu na ndio kuvitakasa vitendo vyenu  na ndio kumridhisha Mola wenu”.

Na hii ni amri ambayo tunawajibika kuitekeleza.











Jua kuwa tuna mfano mzuri sana  wa kufuatwa kutoka kwa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- katika uhai wake na mauti yake. Na  mambo yake yote ni mazingatio kwa watazamao kwani hakuna aliyekuwa bora kwa Allah  Subhanahu Wataala  kuliko yeye Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie. Kwani yeye alikuwa rafiki yake, kipenzi chake  na mchaguzi wake basi hebu tizama je alimchelewesha saa moja  ilipofika ajali yake au alimsogezea mbele walau kwa muda mfupi kabisa mauti yake? Hapana hakufanya hivyo bali alimpelekea Malaika wakarimu wakaichukue kwa haraka roho yake iliyosafika iliyo bora ili waihamishe, na kuiaguwa (kwa tabu) ili waitenganishe na mwili wake ulio tahiri kuipeleka kwenye rehema na radhi za Allah Subhanahu Wataala huko kwenye Mahuru Al Ain walio wazuri pasi na mfano kwenye kikao cha ukweli mtupu kabisa, katika ujirani wa Mola mwenye rehema. Na  juu ya hayo yote utowaji wa  roho yake ulikuwa mzito, kukadhihiri kuugua kwake pamoja na kuwa na hali ya wasiwasi ikabadilika rangi yake na kutoka jasho kipaji chake na ikapiga piga mikono yake wa kuume na wa kushoto  huku ikijikunja na kujikunjua hata wakalia walio hudhuria mauti yake na wakapandisha sauti zao katika kilio kwa kuona uzito wa hali yake. Je unaona daraja yake ya unabii ilimkinga na lililokwisha kuandikwa na Allah Subhanahu Wataala?  Je Amemhurumia Allah kwa kuwa ana wake watoto na jamaa  au amemsamehe kwa kuwa yeye anainusuru haki kila wakati na kuwa ameletwa kwa viumbe kutoa habari nzuri kwa wanaomuamini na kufanya vitendo vyema na kuwaonya waliokufuru na kufanya mabaya. Haya yote yako mbali kabisa na yaliyotokea, bali huyo Malaika alitekeleza amri alizopewa na kufuata yale yaliyoandikwa katika “Louh Al Mahfuudh”. Hii ilikuwa hali yake juu ya kuwa yeye ni (Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie-) mbele ya Allah Subhanahu Wataala na ni mwenye msimamo wa kushukuriwa (Maqaam Al-Mahmuud) na mwenye lile Hodhi linaloingiwa kunywiwa na kila aliyekuwa mwema, yaani Muumin, katika Umma wake (Al Houdh Al Mawruud) naye ni wa kwanza itakayempasukia ardhi siku ya Kiama na vile vile ndiye  aliyepewa uombezi siku ya kiama. Ni kitu cha ajabu kuwa hatusomi kutokana na haya yaliyompata Mtume  -rehema za Allah na amani zimshukie- katika kifo chake wala tunayoyaona kila siku katika kuondokewa na wazee, watoto na watu wetu mbali mbali, bali sisi ni mateka wa mapendeleo ya nafsi zetu  na sisi ni marafiki wa maasi na madhambi. Hebu jitizame  nafsi yako  ujilinganishe na sira za watu wema waliopita, walikuwa juu ya kuwafikishwa kwao kufanya vitendo vizuri walikuwa na hofu kuwa hawatakabaliwi na Allah .





حين دخلنا على رسول الله في بيت أمنا عائشة رضي الله عنها حين دنا الفراق فنظر إلينا فدمعت عيناه صلى الله عليه وسلم ثم قال :(مرحبا بكم حياكم الله آواكم الله نصركم الله وأوصيكم بتقوى الله وأوصي بكم الله إني لكم منه نذير مبين ألا تعلوا على الله في عباده وبلاده وقد دنا الأجل والمنقلب إلى الله وإلى سدرة المنتهى وإلى جنة المأوى وإلى الكأس الأوفى فاقرؤا على أنفسكم وعلى من دخل في دينكم بعدي مني السلام ورحمة الله )

“Wakati  tulipoingia kwa Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani zimshukie- katika nyumba ya mama yetu Aisha R.A wakati wa kufariki kwake dunia kumekaribia, basi akatutizama kisha yakamtoka machozi -rehema za Allah na amani zimshukie- akasema: Karibuni Allah awape uhai, Allah awape pa kufikilia (pa kukimbilia) Allah awape ushindi, nawausia  mumche Allah na namuomba Allah awahifadhi na kuwa kanileta mimi kwenu muonyaji wa uwazi kabisa kwa adhabu yake. Basi msifanye dhuluma na ufisadi kwa waja wake na ardhi yake Subhanahu Wataala na kuwa ajali yangu imekurubia na kurudi kwangu ni kwa Allah kwenye Sidratul Muntaha na Jannat Al Maawa. Na kwenye nasibu yangu (malipo) kubwa kabisa, basi jitoleeni juu ya nafsi zenu na wale watakaoingia katika  dini yenu baada yangu, jitoleeni kutoka kwangu salamu na rehema ya Allah Subhanahu Wataala


Inasemekana kuwa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- amemwambia Jibril A.S kwenye mauti yake:

( من لأمتي بعدي )

 “Nani atakaowatizama Umma wangu kwa kuwaongoza baada yangu”, basi Allah  akamteremshia wahyi Jibril kuwa:   

( أن بشر حبيبي أني لا أخذله في أمته وبشره بأنه أسرع الناس خروجا من الأرض إذا بعثوا وسيدهم إذا جمعوا وأن الجنة محرمة على الأمم حتى تدخلها أمته ) فقال( الآن قرت عيني )                                                                                     

Mbashirie Mpenzi wangu kuwa mimi sitamuacha (kumkatisha tamaa) kwa kuwa Umma wake wako chini ya hifadhi yangu na mbashirie kuwa yeye ni wa kwanza kutoka ardhini siku watakaofufuliwa watu na bwana wao siku watapokusanywa watu na kuwa pepo imeharimishwa kwa umma nyingine mpaka uingie umma wake”. Basi hapo akasema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie:  “Sasa limeburudika jicho langu”.


Amesema  Bibi Aisha R.A ametuamrisha Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani zimshukie- tumuoshe kwa makanda ya ngozi saba(ya maji) kutoka visima saba, tukafanya hivyo akahisi raha basi akatoka na akasalisha watu na kuwaombea maghufira watu wa Uhud na kuwaombea dua kisha akawausia Muhaajiriin juu ya Maansaar akawaambia:

 (أما بعد يا معشر المهاجرين فإنكم تزيدون وأصبحت الأنصار لا تزيد على التي هي عليها اليوم وأن الأنصار عيبتني التي آويت عليها فأكرموا كريمهم – يعني محسنهم – وتجاوزوا عن مسيئهم ) ثم قال إن عبدا خير بين الدنيا وبين ما عند الله فاختار ما عند الله ) فبكى أبو بكر رضي الله عنه وظن أنه يريد نفسه فقال النبي صلى الله عليه وسلم : على رسلك يا أبا بكر ( سدوا هذه الأبواب الشوارع في المسجد إلا باب أبي بكر فإني لا أعلم امرءا أفضل عندي في الصحبة من أبي بكر )                                      

“Amma baad, enyi wana wa Muhaajiriin hakika nyie mwaongezeka (yaani yazidi idadi yao kwani wanahajiri kutoka Makka) na Maansaar wao hawaongezeki zaidi ya vile walivyokuwa na hakika Maansaar ni wahifadhi wangu niliofikilia kwao basi mkirimuni aliokuwa mwema wao na msameheni aliokuwa mbaya wao, kisha akasema: Hakika kuna mja aliekhiarishwa baina ya Dunia na baina ya kile kilichokuwa kwa Allah Subhanahu Wataala basi akachagua kilichokuwa kwa Allah.  Hapo akalia Abu  Bakr R.A. kwani alitambua kuwa huyo mja aliekhiyarishwa ni yeye Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie. Basi akasema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie: Pole pole ewe Abu-Bakr! Fungeni hii milango  ya njiani ilioko katika msikiti isipokuwa mlango wa Abu Bakr kwani sijui mtu aliyekuwa bora kwangu katika usuhuba kuliko Abu Bakr. 


Kasema Bibi Aisha R.A. akachukuliwa (akafa) Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- katika nyumba yangu na katika siku yangu na baina ya kifua changu na shingo yangu (yaani katika mikono yangu) na akakutanisha Allah baina ya mate yangu na mate yake katika mauti yake.  Kaingia kwangu ndugu yangu Abdur-Rahman na amekamata katika mkono wake mswaki basi ikawa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- autizama ule mswaki nikajua kuwa autaka nikambwambia jee nikuletee? Akanifanyia ishara kwa kichwa chake kuwa naam basi nikampa akauchukua kisha akautia katika mdomo wake ukawa ule mswaki mgumu kwake nikamwuuliza je nikulainishie? Akanifanyia ishara kwa kichwa chake kuwa naam. Basi nikaulainisha na kulikuwa mbele yake chombo kina maji akawa aingiza mkono wake ndani ya hicho chombo na  huku akisema laa ilaaha illa Allah hakika mauti yana maumivu makubwa. Kisha akausimamisha mkono wake akisema “Ar-Rafiq Al Aalaa” yaani kuwa wakati ule akihiarishwa na yeye anachagua usuhuba wa walioko Peponi basi hapo nikasema Wallahi  hakutuchagua sisi.


Walipoona Maansar kuwa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- azidi kuwa mzito wakauzunguka Msikiti na alipoambiwa hayo Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie, akatoka na huku amewaegemea Al Fadhl na Aliy na mbele yake yuko Al Abbas  na kichwa chake Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- kimefungwa na miguu yake aiburuza mpaka akakaa katika kidato cha chini cha minbari, wakamsimamia watu akamshukuru Allah Subhanahu Wataala na kumsifu akasema:-

 ( أيها الناس إنه بلغني أنكم تخافون عليَ الموت كأنه استنكار منكم للموت وما تنكرون من موت نبيكم ألم أنع إليكم وتنعى إليكم أنفسكم هل خلد نبي قبلي فيمن بعث فأخلد فيكم ألا إني لاحق بربي وإنكم لاحقون به وإني أوصيكم بالمهاجرين الأولين خيرا وأوصي المهاجرين فيما بينهم فإن الله عزَ وجل قال :                                                


وإن الأمور تجري بإذن الله فلا يحملنكم استبطاء أمر على استعجاله فإن الله عزَ وجل لا يعجل بعجلة أحد ومن غالب الله غلبه ومن خادع الله خدعه – فهل عسيتم إن توليتم أن تفسدوا في الأرض وتقطعوا أرحامكم – وأوصيكم بالأنصار خيرا فإنهم الذين تبوءوا الدار والإيمان من قبلكم – أن تحسنوا إليهم ألم يشاطروكم الثمار ، ألم يوسعوا عليكم في الديار ، ألم يؤثروكم على أنفسهم وبهم الخصاصة ألا فمن ولي أن يحكم بين رجلين فليقبل من محسنهم وليتجاوز عن مسيئهم ألا ولا تستأثروا عليهم ألا وأني فرط لكم وأنتم لاحقون بي ألا وأن موعدكم الحوض ألا ومن أحب أن يرد علي الحوض غدا فليكفف لسانه ويده إلا مما ينبغي ) فقال العباس يا نبي الله أوص بقريش فقال ( إنما أوصي بهذا قريشا والناس تبع لقريش برهم لبرهم وفاجرهم لفاجرهم فاستوصوا آل قريش بالناس خيرا يا أيها الناس إن الذنوب تغير النعم وتبدل القسم فإذا بر الناس تبرهم أئمتهم وإذا فجر الناس عقوهم


“Enyi watu imenifikia habari kuwa mwaniogopea kufa kama kwamba kwa hayo mnapinga mauti na ni kitu gani kinachowafanya mpinge mauti ya Mtume  wenu. Jee hamkuarifiwa kifo changu na mkaarifiwa vifo vyenu wenyenu? Je alipata kuisha milele Nabii kabla yangu katika manabii waliotumwa hata mkataka mimi niishi kwenu milele? Basi nawahakikishia kuwa mimi napelekwa kwa Mola wangu nanyi vile vile mwapelekwa kwake na kuwa mimi nawausia juu ya Muhaajiriin wa kwanza kheri  (mkae nao vizuri) na wausia Muhaajirin baina yao wenyewe kwa wenyewe kwani Allah Subhanahu Wataala amesema

 “Naapa kwa zama (zako ewe Nabii Muhammad)(1) Kuwa Binadamu yuko katika hasara (2) Isipokuwa wale walioamini na wakafanya vitendo vizuri, na wakausiana (kufuata) haki na wakausiana (kushikamana) na subira (kustahamiliana)”.

“Na hakika kuwa mambo yanakwenda kwa idhni yake Allah basi isiwapelekee kuharakisha kitu mnachokiona kinakwenda pole pole kwani Allah Subhanahu Wataala haharakishi kitu kwa ajili ya haraka ya mtu fulani na atakaye kushindana na Allah humshinda na anaemkhadaa Allah naye vile vile humkhadaa (hampi hidaya kwenye njia ilionyooka). Pengine huenda mkapotea na mkafisidi katika ardhi na kuwakata jamaa zenu, na nawausieni juu ya Maansaar Kheri kwani wao ndio waliofanya maskani yao hapo Madina kabla yenu na ndio walioutakasa Uislamu wao barabara kabla yenu nawausia muwafanyie wema.Jee, hawakuwagawia nusu ya mazao yao?  Jee, hawakuwafanyieni nafasi katika nyumba zao? Jee, hawakuwapendeleeni nyie juu ya nafsi zao japokuwa wao wenyewe wahitaji sana? Basi mjue kwa hakika aliyepewa wilaya ya kuhukumu baina ya watu wawili (katika wao Maansari) amkubalie mwema wao na amsemehe mbaya wao, basi msije mkapendelea (nafsi zenu) juu yao, hakika mie ndie nitakaowatangulia na nyie mtanifuatilia, hakika miadi yenu ni Hodhi. Hakika anayetaka kungia kwangu katika hodhi langu kesho (siku ya kiyama) basi azuiye ulimi wake na mkono wake isipokuwa kwa kilicho lazima. Akasema Al Abbas ewe Mtume wa Allah toa usia kwa Maqureish. Akasema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie:  Hakika mimi huu usia (wa kuwafanyia mema Maansaar na Muhajiriin)  nawausia Maqureish wao ndio wanaofuatwa na watu, mwema (wa watu) anafuata mwema wao (Maqureish) na mbaya (wa watu) anafuata mbaya wao (Maqureish) (wao ndio viongozi wa kiwa wazuri na raia zao watakuwa  wazuri na wakiwa wabaya raia watakuwa hivyo hivyo).  Basi nawausieni enyi Maqureish kuwafanyia watu kheri.  Enyi watu hakika madhambi yabadilisha mema na mgawanyo wa riziki, wakifanya mazuri watu (kumtii Mola) na viongozi wao watawafanyia mazuri na wakifanya watu maasi basi nao watataabishwa na viongozi wao na kutofanyiwa uadilifu.”

وروى ابن مسعود رضي الله عنه أن النبي صلى الله عليه وسلم قال لأبي بكر رضي الله عنه سل يا أبا بكر فقال يا رسول الله دنا الأجل فقال دنا الأجل وتدلى فقال : ليهنئك يا نبي الله ما عند الله فليت شعري عن منقلبنا فقال " إلى الله وإلى سدرة المنتهى ثم إلى جنة المأوى والفردوس الأعلى والكأس الأوفى والرفيق الأعلى والحظ والعيش المهنا فقال يا نبي الله من يغسلك قال رجل من أهل بيتي الأدنى فالأدنى قال ففيم نكفنك قال في ثيابي هذه وفي حلة يمانية وفي بياض مصر" فقال كيف الصلاة عليك منا وبكينا وبكى ثم قال " مهلا غفر الله لكم وجزاكم عن نبيكم خيرا إذا غسلتموني وكفنتموني فضعوني على سريري وفي بيتي هذا على شفيري قبري ثم اخرجوا عني ساعة فإن أول من يصلي علي الله عزَ وجل ثم يأذن للملائكة في الصلاة علي فأول من يدخل علي من خلق الله ويصلي عليَ جبريل ثم ميكائيل ثم إسرافيل ثم ملك الموت مع جنود كثيرة ثم الملائكة بأجمعها عليهم السلام ثم أنتم فادخلوا علي أفواجا فصلوا علي أفواجا زمرة زمرة وسلموا تسليما ولا تؤذوني بتزكية ولا صيحة ولا رنة وليبدأ منكم الإمام وأهل بيتي الأدنى فالأدنى ثم زمر النساء ثم زمر الصبيان قال فمن يدخلك في قبرك قال " زمر من أهل بيتي الأدنى فالأدنى مع ملائكة كثيرة لا ترونهم وهم يرونكم قوموا فأدوا عني إلى من بعدي ")                                                               

Imetolewa na  Ibn Masood zimshukie Radhi za Allah  kuwa  Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- amesema kumwambia Abu Bakr R.A.: Uliza ewe Abu Bakr. Akasema Ewe Mjumbe wa Allah imekaribia ajali yako? Akasema imekaribia ajali na kuteremka. Akasema (Abu Bakr R.A.) hakika nakupongeza na utafurahishwa kwa kile utakachokipata kwa Allah na  laiti ningejua nini utakuwa mwisho wetu. Akasema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie:  Ni kwenda kwa Allah na Sidratu Al Muntahaa kisha kwenye Pepo ya Maawaa na Firdaws ya Juu kabisa na malipo makubwa sana na rafiki wa Juu kabisa na hadhi na maisha ya raha. Akasema Jee Mjumbe wa Allah nani  atakaekuosha akasema mwanamme katika Ahli Al-Beit (katika familia yangu au jamaa yangu) aliyenikaribia zaidi kisha aliyenikaribia zaidi. Akamuuliza Jee tukuvike sanda (tukufunge sanda) kwa kitu gani? Akasema katika nguo zangu hizi na katika shuka za Kiyamani na weupe wa Masri.  Akamuuliza jee vipi  tukusalie ? Hapo tukalia naye akalia kisha akasema : Polepoleni Allah Subhanahu Wataala awaghufiriye na awajazi kheri kutokana na Mtume wenu.  Mkisha niosha na kunifunga sanda niekeni juu ya kitanda changu katika nyumba yangu hii katika ukingo wa kaburi langu kisha tokeni nje muda mdogo kwani wa kwanza atakaye nisalia ni Allah Subhanahu Wataala kisha atawapa idhini Malaika kunisalia basi wa kwanza katika viumbe vya Allah Subhanahu Wataala atakayeingia kunisalia ni Jibriil A.S kisha Mikaaiil kisha Israafiil kisha Malaika wa Mauti  pamoja na askari wake wengi halafu Malaika wote wengine A.S. kisha nyie ingieni vikundi na munisalie vikundi mkusanyiko mkusanyiko na nisalimieni (niamkieni) mwamkio wala msiniudhi kwa kunisifu au kulia kwa makelele au kuomboleza. Na aanze miongoni wenu Imamu na watu wa nyumba yangu aliekaribu zaidi kisha anaefuatia kisha vikundi vya wanawake kisha vikundi vya watoto. Akauliza nani atakaekuingiza kaburini mwako ? Akajibu  mikusanyiko katika watu wa nyumba yangu aliye karibu zaidi kisha anaefuatia pamoja na malaika wengi hamuwaoni na wao wanawaona fikisheni ujumbe kwa niaba yangu kwa wale watakao kuwa baada yangu.


Kasema Abdullah bin Zamaa :-

جاء بلال في أول شهر ربيع الأول فأذن بالصلاة فقال رسول الله صلى الله عليه وسلم (مروا أبا بكر يصلي بالناس ) فخرجت فلم أر بحضرة الباب إلا عمر في رجال ليس فيهم أبو بكر فقلت قم يا عمر فصل بالناس فقام عمر فلما كبر – وكان رجلا صيتا – سمع رسول الله صلى الله عليه وسلم صوته بالتكبير فقال ( أين أبو بكر يأبى الله ذلك والمسلمون ) قالها ثلاث مرات ( مروا أبا بكر فليصل بالناس)  فقالت عائشة رضي الله عنها  يا رسول الله إن أبا بكر رجل رقيق القلب إذا قام في مقامك غلبه البكاء فقال  (إنكن صويحبات يوسف مروا أبا بكرفليصل بالناس )                                  

 Amekuja Bilal katika mwanzo wa mwezi wa Rabee Al Awwal akaadhini akasema Mtume wa Allah Subhanahu Wataala Muamrishe Abu Bakr awasalishe watu. Basi nikatoka na sikumuona hapo mlangoni miongoni mwa watu ispokuwa Omar, na Abu Bakr alikuwa hayupo pamoja nao nikasema simama Ewe Omar uwasalishe watu akasimama alipopiga takbira ya Ihram – alikuwa mtu mwenye sauti kubwa akamsikia Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie-  katika kupiga takbira akasema – Yuko wapi Abu Bakr, Allah pamoja na Waislamu wakataa hivyo  (kusalisha mwingine ila Abu Bakr) kasema maneno hayo mara tatu  Mwamrisheni Abu Bakr awasalishe watu   akasema Aisha R.A. Ewe Mjumbe wa Allah hakika Abu Bakr moyo wake mwepesi akisimama mahali pako hataweza kujizuia kulia. Akasema : hakika nyie (wanawake) ni masahib wa Yusuf (wale wanawake waliomfanyia Yusuf A.S  kila aina ya vitimbi) muamrisheni Abu Bakr awasalishe watu. Akasema, basi Abu Bakr akawasalisha watu baada ya ile sala aliowasalisha Omar. Alikuwa Omar akimwambia Abdullah bin Zamaa baada ya hapo vipi mambo gani ulionifanyia wallahi kama ningejua kuwa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- amekuamrisha (umwambie Abu Bakr) basi nisingelifanya (kusalisha) akajibu Abdullah bin Zamaa hakika sikumpata mtu aliyekuwa wa mbele kufanya hivyo kuliko wewe. Kasema Aisha R.A sikusema hayo (niliomwambia  Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie) wala sikumuepushia nalo jambo hilo Abu Bakr isipokuwa kumtakia ajiweke mbali  na dunia na vile vile nimefanya hivyo kwa kuona hatari na hilaki iliokuwepo katika uongozi wa nchi (ukubwa) isipokuwa aliesalimishwa na Allah Subhanahu Wataala, vile vile nimeogopa kuwa watu wasije kuwa hawatampenda milele mtu atakaesimama kusalisha mahali pa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- naye bado yuko hai isipokuwa akitaka Allah, kwa hivyo watamhusudu na kumfanyia ubaya na wakipata mkosi itakuwa yeye ndiye sababu na hali jambo hilo ni jambo la Allah na lilipitishwa kwa Kadhaa yake. Juu ya hivyo Allah akamuepusha na kila nilichomuogopea kuwa kitampata katika mambo ya Dunia na Dini. Akasema Aisha – Ile siku aliokufa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- walipoona watu amepata nafuu katika maradhi yake mwanzo wa mchana wakamuaga kwenda majumbani mwao na kufanya haja zao huku wana matumaini wakawa pamoja na wake zao. Basi tulivyokuwa sisi tuko katika hali hiyo ambayo hatujawahi kabla ya hapo kuwa katika hali kama hiyo ya matarajio na furaha  hapo  akasema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- tokeni (kuwambia wake zake) huyu Malaika aomba idhini ya kuingia kwangu wakatoka wote waliokuwa nyumbani  isipokuwa mimi (Aisha R.A.) na kichwa chake kiko juu ya kipakatio changu akakaa na mimi nikajitenga kwenye upande mwingine wa nyumba akawa anazungumza (kwa sauti ndogo) na Malaika muda mrefu kisha akanita na kurudisha kichwa chake kwenye sehemu yangu mahali pa kupakatia akasema kuwaambia wake zake na watoto wake ingieni. Nikasema hii sio sauti ya Jibriil A.S. akajibu Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie: Kweli ewe Aisha, huyu ni Malaika wa mauti (wa kutoa roho za watu )  amenijia akaniambia kuwa Allah SWT amenileta na ameniamrisha kuwa nisingie kwako isipokuwa kwa idhini na ikiwa hukunipa idhini nirudi na ukinipa idhini niingie na akaniamrisha nisikamate roho yako mpaka uniamrishe basi nini amri yako ? Nikamjibu nisubirie mpaka anijie Jibriil A.S. kwani hii ni saa yake Jibriil. Akasema Aisha R.A. tukawa tumekabiliwa na jambo hatuna jawabu lake wala rai juu yake.  Basi  tukapigwa na mshangao (mduwao) kama tumepigwa na umeme hatujui nini la kufanya wala hakuna anaezungumza katika watu wa nyumba ya Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- kwa kulitukuza kulioje hilo jambo na vipi haiba ilivyojaa katika nyoyo zetu akasema (Aisha R.A) akaja Jibriil (A.S) katika saa yake akaamkia nikaitambua sauti yake na hapo wakatoka watu wa nyumba yake (-rehema za Allah na amani zimshukie-) naye akaingia akasema hakika Allah aliyekuwa na nguvu na kutukuka akupa salamu na akwambia wajihisi vipi ? Naye ni Mjuzi zaidi wa hali yako kuliko yoyote mwingine lakini ametaka kukuzidishia heshima na sharafu na atimize heshima yako  na sharafu juu ya viumbe vyote vingine na uwe sunna katika Umma wako (yaani mfano). Akamwambia nahisi  maumivu akamjibu jibashirie kwani Allah Subhanahu Wataala ametaka akufikishe kule alipokuahidi (yaani daraja kubwa kwani mtu hupewa mtihani na Allah Subhanahu Wataala akasubiri ikawa sababu ya kupandishwa daraja yake). Akamwambia Ewe Jibril Malaika wa mauti ametaka idhini yangu kisha akamuelezea ile habari yote. Akasema Jibriil wewe Muhammad hakika Mola wako ana shauku na wewe kwani hakukujulisha kitu gani amekutakia? (amekutakia daraja Kubwa). Akamjibu kumwabia usiondoke sasa mpaka atakapokuja (Malaika wa mauti) hapo ndipo alipowaruhusu wake zake na watoto wake kuingia nyumbani. Akasema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie-  « Ewe Fatima nisogelee karibu yangu » akaja akamuinamia, akamnong’oneza,  akanyanyua kichwa chake (Fatma) huku machozi yamtoka na hawezi kuzungumza kisha akamwambia “sogeza kichwa chako karibu yangu” akamuinamia na (Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie-) akamnong’oneza akanyanyua kichwa chake huku hawezi kuzungumza kwa kucheka na hakika tuliyoyaona (mzungumzaji ni Aisha) kwake (Fatma R.A) yalikuwa maajabu nikamuuliza baada ya hapo akanijibu kuwa mara ya kwanza alinambia (Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie-) kuwa mimi nitakufa leo basi hapo nikalia kisha akasema nimemuomba Allah SWT uwe wewe wa kwanza katika watu wangu watakaonifatia na tuwe pamoja na ndipo nilipocheka,halafu akamsogezea watoto wake wawili (Hassan Na Hussein R.A.) akawanusa.  Akasema (Aisha R.A.) halafu akaja malaika wa mauti  akaomba idhini ya kungia akapewa idhini akasema watuamrisha nini ewe Muhammad akasema “ Nifikishe kwa Mola wangu hivi sasa”  akasema (Malaika wa mauti ) ‘Ndio katika siku yako hii, ama hakika Mola wako ana shauku ya kukutana na wewe na hakusita kwa mtu yeyote mwingine kama alivyosita (kuchukua roho yako) kwako wewe na hakunikataza kuingia kwa mtu yoyote mwingine  bila ya idhini isipokuwa kwako wewe lakini saa yako iko mbele yako’ kisha akatoka (Nasema kauli yake   « Hakusita kwa mtu yoyote kama alivyosita kwako”  maneno haya sivyo yanavyoonekana katika udhahiri wake kwani Allah Subhanahu Wataala halibadiliki neno kwake lakini yametokea hayo kwa kuonewa huruma na kuzidishwa heshima yake -rehema za Allah na amani zimshukie- » maneno ya mtungaji).


Akasema Bibi Aisha R.A. akaja Jibril akasema  ‘Amani iwe juu yako Ewe Mtume  wa Allah  hii ni mara yangu ya mwisho kuteremka ardhini umekwisha fungwa wahyi na imekwisha fungwa Dunia na sikuwa na haja yoyote ardhini isipokuwa wewe na wala sikuwa na haja ardhini isipokuwa kuweko kwako ( yaani Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie-) kisha baada ya kufa kwako nikae huko niliko bila ya kuteremka tena ardhini’.  Hapana naapa  kwa yule aliyemleta Muhammad kwa haki hakuna mtu nyumbani alieweza kumrudishia neno lolote kwa hayo aliyoyasema wala kumtumia mtu katika watu wake ( kumueleza juu ya hali ya Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie-) kwa utukufu wa yale yanayosikika katika mazungumzo yake (Jibril A.S.) na kwa kumuonea kwetu huzuni  na huruma ( Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie).  Akasema basi nikasimama kwenda kwa Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie- ili nikieke kichwa chake katika kifua changu na nikamkamata kifuani na akawa azimia mpaka apoteza fahamu na huku kipaji chake chatoka jasho sijawahi kuliona (jasho) kama hilo katu kabla kwa mtu yeyote basi nikiwa nalipangusa hilo jasho na sikupata kunusa harufu ya kitu cho chote nzuri kuliko hilo jasho na nilikuwa namwambia anaporudisha fahamu “Wewe niliyejitolea mhanga kwa baba yangu na  mama yangu na nafsi yangu na watu wangu aina gani hii ya jasho linalotolewa na kipaji chako?  Akasema ewe Aisha hakika Muumin yatoka roho yake na jasho zuri lamtoka na kafiri yatoka roho yake baina ya tama zake mbili kama roho ya punda (inavyotoka).

Nilivyosikia hayo nikaogopa tukawatumia jamaa zetu waje. Na mwanamme wa mwanzo aliefika ni ndugu yangu tukamtuma kwenda kumwita baba – Abu Bakr akaja lakini alipoona hali ya Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie- imekuwa ya nafuu akamuomba ruhusa ili ende nyumbani kwake huko As-Sanh nje ya Madina akamwambia Ewe Mtume wa Allah nakuona hujambo na usiku huu ni usiku wa fulani (mmoja katika wake zake) basi nipe ruhusa nimweendee hapo akampa ruhusa Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie- kwa hivyo akafa wakati Abu Bakr hayupo akenda mjumbe wake Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie- kwenda kumwita akaja ( Abu Bakr R.A.) na huku amsalia Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie- na macho yake yapukutika machozi na huku duku duku limemshika kwa huzuni yake ilivyokuwa kubwa naye juu ya yote hayo ni mshupavu katika vitendo vyake na maneno yake Akamwinamia kisha akamfunua uso wake na kumbusu kipajini na mafundani na akampangusa usoni, akawa analia na huku asema “wewe ninayejitolea muhanga kwa baba yangu na mama yangu na nafsi yangu na watu wangu umependeza (umzuri) katika uhai na mauti, kimekatika katika kufa kwako kile kilicho kuwa hakikukatika kwa mauti ya Nabii ye yote mwingine wala kukatika kwa Unabii wo wote mwingine, sifa yako ni juu zaidi kuliko vile tunavyoweza kuisifu, msiba wako ni mkubwa zaidi kuliko vilio vyetu na majonzi yetu. Umekhusiwa (kufanywa mambo yako tafauti na watu wengine) mpaka ikawa hafi mtu isipokuwa ukawa msiba wa kufa kwako  sababu ya nafuu ya huo msiba ikiwa Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie- amekufa basi msiba wangu ni nafuu,na ukafanywa kama watu wengine mpaka tukawa sisi na wewe sawasawa. Kama ingekuwa mauti yako sio kwa khiari yako mwenyewe basi nafsi zetu zingekuhuzunikia huzuni kubwa kabisa na kama usingetukataza kulia basi tungelikulilia mpaka machozi yetu yakakauka. Ama kile tulichokuwa hatuwezi kujizuia nacho ni majonzi juu yako na kukukumbuka  vitu viwili  hivi  viko pamoja (havibandukani) na wala haviondoki. Ewe Mola wetu tufikishie hisia zetu kwake (Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie-).  Tutaje Ewe Muhammed –rehema za Allah na amani zimshukie- kwa Mola wako na iwe katika moyo wako basi kama ingekuwa sio kwa ule utulivu uliotuachia asingeweza mmoja katika sisi kusimama kwa sababau ya upweke tulioupata kwa kifo chako.  Ewe Mola tufikishie kwa Mtume wako haya tuliyo yapata kwa ajili yake (kifo chake)  na umhifadhi katika nyoyo zetu (tuwe twamkumbuka wakati wote na kufuata aliyotufundisha)


Akasema Aisha R.A. akawa kila akizimia (na kufufuka) asema “Bali Rafiki alie wa Juu” kama kwamba arudishiwa kuhiarishwa naye achagua hicho alicho kitaja.  Akiweza kusema husema “Salaa Salaa kwani nyie mtaendelea kukamatana ikiwa mtasali pamoja Salaa, Salaa”  Akawa aendelea kuusia hivyo mpaka kufa kwake –rehema za Allah na amani zimshukie- katika wakati baina ya kupanda kwa dhuhaa na katikati ya mchana siku ya jumatatu. Baada ya kufa wakaja watu (kwa wingi kuingia nyumba yake Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie-) baada ya kusikia vilio na maombolezi ya kumsikitikia Mtume wa Allah Subhanahu Wataala wakahitilifiana watu katika mauti yake wengine hawakusadiki (wakaifanya hii habari uongo) wengine wakaduwaa (wakawa hawasemi kama mabubu) na wengine wakachanganyikiwa na wakasema maneno yaliyokuwa hayaeleweki, wakabakia wengine na akili zao timamu na wengine wakawa kama viwete (hawawezi haraka yoyote)  basi akawa Omar bin Al Khattab miongoni mwa waliofanya uongo habari ya kufa kwake –rehema za Allah na amani zimshukie- na Aliy miongoni mwa walioshindwa kufanya haraka yoyote wakawa wamekaa tu. Na Othman miongoni mwa waliokuwa wamenyamaza hawawezi kusema kitu) na akatoka Omar kwa watu akasema kuwa Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie- hakufa na Mwenyezi Mungu SWT atamrudisha kama alivyomuahidi Musa naye atawajia Wallahi nisimsikie Mtu ataja kuwa Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie- amekufa isipokuwa nitamrukia na upanga wangu huu. Na hakuwa katika Waislamu mtu kama Abu Bakr na Al Abbas kwani Allah SWT amewapa tawfiiq yake na muongozo wake na alipo watokea watu Abu bakr baada ya kupata yakini ya kifo cha Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie- akasema “Enyi watu yule aliekuwa amuabudu Muhammad basi Muhammad amekwisha kufa na aliekuwa amuabudu Mola wake Muhammad  basi yeye Mola ni Hai hafi.  Amesema Allah SWT:


آل عمران: ١٤٤

« Na hakuwa Muhammad ila ni Mtume tu. Wamepita kabla yake Mitume (wengi kabisa). Akifa au akiuwawa ndiyo mtarudi nyuma (kwa visigino vyenu muwe makafiri kama zamani?) Na atakayerudi nyuma kwa visigino vyake hatamdhuru Allah cho chote. Na Allah atawalipa wanaomshukuru.”


Basi ikawa kama watu hawakuisikia Aya hii isipokuwa siku  hiyo. Hapo wakalia kwa makelele ahliya yake Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie- pamoja na wale wote waliohudhuria.  Hayakusita makelele haya ya vilio isipokuwa kwa mwamkio wa mtu kwa sauti kubwa hapo mlangoni akasema Assalaam Alayku enyi watu wa nyumba ya Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie- ( كل نفس ذائقة الموت )                

“Kila nafsi haina budi kuonja mauti”.  Hakika kwa Allah kuna mabakio kwa kila anaendoka (ukipatikana msiba huwalipa Allah SWT wale wenye msiba badala yake kitu kinachowapumbazisha ukawa nafuu) na kwake yeye hupata mtu kila anachokitaka na kwake yeye SWT huokoka mwanadamu kutokana na kila anachokiogopa basi Allah ndio mumuombe na yeye mumtumainie, wakawa wamsikiliza bila ya kumuona na wakanyamaza kulia, waliponyamaza ikakatika sauti yake akatoka mmoja wao kumchungulia bila ya kumuona yeyote. Kisha wakarudia tena kulia na hapo tena akaita muitaji mwingine wasiyeitambua sauti yake, Enyi watu wa nyumba ya Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie- mdhukuruni Allah SWT na mshukuruni katika kila hali mtakuwa wenye Ikhlasi.  Hakika kwa Allah kuna nafuu kwa kila msiba na malipo kwa kila kinachotakiwa basi mtiini yeye Allah SWT na kwa mujibu  wa  amri yake mutende.  Akasema Abu Bakr hawa ni Al Khadr AS na Al Yasaa A.S wamehudhuria kifo  cha Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie.











Na asiwashughulishe sheitani kwa kufa kwa Mtume wenu wala asiwapoteze kutokana na dini yenu kwa kuwafanya msiweze kufanya kheri au kuchelewa kufanya kheri.  Msipofanya kheri na kuchelewa kuifanya ndipo atakapowajia na kuwapoteza (huyo sheitani)


Alipomaliza kutoa hotuba yake akasema “Ewe Omar ndio juu yako wewe imenifikia habari kuwa unasema Mtume wa Allah SWT hakufa kwani hujuwi  kuwa Mtume wa Allah SWT amesema siku kadha kadha wa kadha na siku kadha kadha wa kadha na amesema Mola katika kitabu chake:


الزمر: ٣٠

“Kwa yakini wewe utakufa na wao pia watakufa”


Akasema (yaani Omar R.A) Wallahi kama kwamba sijaisikia aya hii katika kitabu cha Allah SWT kabla ya sasa kwa yale yaliyotupata. Nashuhudia kuwa kitabu cha Mola kama kilivyoteremshwa na kuwa hadithi za Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie- kama zulivyozungumzwa na kuwa Allah  SWT yuhai nae hafi.


البقرة: ١٥٦

“Hakika sisi ni wa Allah na hakika kwake yeye tutarejea (atatupa jaza yake)”


Na sala za Allah (Rehema zake) zimfikie Mtume wake na twatarajia ujira wetu kwa Allah SWT kwa msiba huu wa kuondokewa na Mtume wake –rehema za Allah na amani zimshukie.


Kisha Abu Bakr akakaa, akasema Aisha R.A. walipokusanyika kumuosha wakasema wallahi hatujui vipi tumuoshe Mtume wa Allah  –rehema za Allah na amani zimshukie, tumvue nguo zake kama tunavyowafanyia  maiti zetu, au tumuoshe na nguo zake, akasema basi Allah akawapelekea usingizi hata hakubakia miogoni mwao mtu isipokuwa kidevu chake kiko kifuani kwake kwa usingizi kisha akasema msemaji - hajulikani nani- muosheni Mtume wa Allah –rehema za Allah na amani zimshukie- na nguo zake (yaani bila ya kumvua nguo) basi ndipo walipotanabahi na wakafanya hivyo mpaka walivyo maliza kumuosha akavishwa sanda.  Akasema Aliy tumetaka kumvua kanzu yake tukaitwa kuambiwa msimvue Mtume wa Allah nguo zake basi tukaitikia na tukamuosha na kanzu yake na tukamlaza kama tunavyoosha maiti zetu na hatukutaka tugeuziwe kiungo cho chote katika viungo vyake tupate kukiosha isipokuwa twageuziwa na twakiosha mpaka twamaliza na kukawa na harufu nyumbani kama twapuliziwa upepo wenye harufu nzuri sana na huku twaisikia sauti yatwambia muwe wapole (katika kumuosha) na Mtume wa Allah –rehema za Allah na amani zimshukie- kwani mtatoshelezwa ( yaani mtasaidiwa kumuosha).


Likatandikwa kaburi lake –rehema za Allah na amani zimshukie- kwa kitandikio chake (shuka lake) na kitambaa cha makhmeli (قطيفته) na zikatandikwa nguo zake juu yake (kaburi lake ) zile alizokuwa kazivaa. Kisha akatiwa kaburini baada ya kuvishwa sanda.  Kwani hakuacha baada ya kufa kwake mali wala hakujenga  katika uhai wake tofali juu ya tofali yaani hakujenga nyumba ya udongo wala hakuweka boriti  (قصبة )  juu ya boriti yaani hakujenga nyumba ya makuti na  katika kifo chake –rehema za Allah na amani zimshukie- kuna zingatio kamilifu naye ni mfano mzuri kwa Waislamu.




Yeye ni mbora wa makarimu wote, halali na hali ya kuwa ana dinari au dirham na kama kimembakilia cho chote hakupata wa kumpa na umemjia usiku basi harudi nyumbani kwake mpaka ajisafishe nacho kwa kumpa yule anayekihitajia. Hachukui kile alichopewa na Allah SWT isipokuwa chakula chake cha mwaka tu katika vile vilivyokuwa rahisi kupatikana kama tende na ngano. Haombwi kitu isipokuwa atoa. Katika waliokuwa wakijizuia nafsi zao  kufanya  haramu  yeye ni wa mwanzo. Mkono wake haukugusa mwanamke aliokuwa haukumiliki mkono wake wa kuume wala aliekuwa sio mke wake wala si katika maharim wake. Alikuwa akishona viatu vyake na kutia kiraka nguo yake na akifanya kazi za nyumbani (yaani akiwasaidia wake zake kufanya kazi zao) na akikata nyama pamoja na wake zake na alikuwa na haya sana kupita watu wote, hawezi kumtizama mtu usoni moja kwa moja.  Alikuwa apokea zawadi ijapokuwa chubuo moja la maziwa au paja la sungura (kwa udogo wake hiyo zawadi) na amlipa huyo aliotoa zawadi kwa kumpa kitu kingine na anakula zawadi lakini hali sadaka alikuwa aghadhibika kwa ajili ya Allah SWT na haghadhibiki kwa ajili ya nafsi yake na atekeleza haki hata ikiwa marejeo yake ni madhara kwake yeye au kwa masahaba zake.  Alikuwa afunga jiwe katika tumbo lake kwa njaa na alikuwa anakula kilichokuepo na wala hakirejeshi alichokipata na alikuwa anakula halali bila ya kuizuia nafsi yake nayo. Alikuwa hali na huku ameegemea. Alikuwa hakupata kushiba mkate wa ngano kwa muda wa siku tatu mfululizo hadi akakutana na Mola wake. Alikuwa akifanya hivyo kuizuia nafsi ( asiiendekeze nafsi yake inachotaka) yake sio kutokana na umasikini au ubakhili. Alikuwa aitikia mwito wa karamu na awatizama wagonjwa na aenda kuzika na anakwenda peke yake baina ya maadui zake bila ya mlinzi.  Alikuwa mnyenyekevu kushinda watu wote na mtulivu kuliko wote bila ya kibri na mwenye maneno yenye kufahamika kuliko watu wote bila ya kurefusha hadithi yake. Na alikuwa mtu mwenye uso mkunjufu wenye bashasha kuliko wote.  Alikuwa hashituliwi na kitu cho chote katika mambo ya dunia. Na avaa anachokipata, mara avaa jokho mara avaa kunzu yenye mistari ya Kiyemen mara kilemba cha sufi na hivyo kila anachokipata kinachoruhusiwa hukivaa na pete yake ni ya fedha huivaa katika kidole kidogo cha mkono wa kulia na wa kushoto. Alikuwa akipanda mnyama humpandisha nyuma yake mtumwa wake au mwenginewe na hupanda  anachokipata mara farasi mara ngamia mara ‘baghla’ (mnyama kama punda lakini mwenye umbo kubwa zaidi na mdogo kuliko farasi, mwenye rangi nyeupe iliyozidi weusi) na mara hupanda punda. Mara hutembea kwa miguu bila ya viatu, bila ya shuka ya juu (ridaa) wala bila kuvaa kilemba wala kuvaa kofia. Na alikuwa apenda mafuta mazuri na achukia harufu mbaya. Akaa pamoja na mafakiri na awalisha maskini na awakirimu watu wa fadhila kwa kuwatendea muamala mzuri wenye tabia nzuri na ashikamana na watu wenye sharafu kwa kuwatendea mema. Alikuwa akiwasiliana (awatembelea na kuwasaidia wanaohitaji msaada ) na arhamu (anaohusiana nao kwa damu kama ndugu wa baba au ndugu wa mama n.k) bila ya kuwapendelea wao juu ya wale waliokuwa bora kuliko wao.  Alikuwa hamfanyii mtu ubaya. Akubali udhuru wa yule anayemtolea huo udhuru. Akifanya mzaha  hasemi isipokuwa ukweli mtupu.  Acheka bila ya kutoa sauti ( inayotoka kooni). Akiona mchezo unaoruhusiwa  hasemi kitu kuupinga. Ashindana mbio na wake zake.  Apigiwa makelele na asubiri.  Alikuwa ana mbuzi na ngombe, akinywa maziwa yao yeye na watoto wake nyumbani.  Alikuwa ana watumwa na vijakazi, haipendelei nafsi yake juu yao kwa chakula na mavazi. Hapitishi wakati bila ya kufanya amali kwa ajili ya Allah SW.T au kufanya kile kilichokuwa hakina budi  kuitengeza nafsi yake.  Amekulia –rehema za Allah na amani zimshukie- katika nchi yenye ujinga na ya jangwa katika hali ya ufakiri na kuchunga wanyama. Na hali ya kuwa yatima hana baba wala mama akamfundisha Mola wake tabia zote njema na njia nzuri zinazopendeza na habari ya watu wa mwanzo na wa mwisho na akamfundisha yale yanayoleta uokozi na kufuzu katika akhera na kuwa katika hali nzuri duniani na kuikiuka mitihani yake kwa usalama. Allah SWT atuwafikishe katika taa yake na hiyo hupatikana katika kufuata amri za Mtume wetu –rehema za Allah na amani zimshukie- na kumuiga katika vitendo vyake.  Amin ewe Mola wa Ulimwengu.













Maneno yake yalikuwa kidogo (hazungumzi isipokuwa kwenye haja) na mepesi kufahamika. Na hazungumzi mambo ya kipuuzi na ayapangilia maneno yake kwa mpango mzuri hayagongani katika maana yake.  Amesema Aisha R.A. alikuwa asoma Qur’ani upesi upesi lakini bila ya kukosea au kuacha kitu sio kama kusoma kwenu huku kwa haraka (Alikuwa husoma Qur’ani kwa mfuatilio wa maneno mzuri sana sio kama kusoma kwenu huku). Alikuwa mbora wa wafupishaji wa maneno na kwa hivyo alivyokuwa anakuja Jibriil A.S. alikuwa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- pamoja na kufupisha kwake maneno  akusanya maana ya yote aliyokuja nayo Jibriil A.S. Alikuwa asema maneno kidogo yaliyochukua maana kubwa haongezi maneno bila ya haja wala hapunguzi kusema kitu ambacho kitaleta kasoro katika maana kama kwamba maneno yake yafuatiya baadhi yake baadhi. Na baina ya maneno yake kuna kusimama hata kwa yule anayemsikiliza ahifadhi anayoyasema na kuyasikia vizuri. Alikuwa mwenye sauti kubwa na nzuri kuliko sauti za watu wote. Hunyamaza muda mrefu na hazungumzi palipokuwa hapana haja, hasemi isipokuwa haki katika hali zote mbili za kuridhika na kughadhibika.  Hamsikilizi  yule anayezungumza maneno yaliyokuwa si mazuri.Ikiwa kalazimika kusema kitu ambacho sio cha kusemwa basi husema kwa “kinaya” yaani dhahiri yake hufahamika vingine na vile kinavyokusudiwa.  Alikuwa asema

( لا تضربوا القرآن بعضه ببعض فإنه نزل على وجوه )                                 

“Msiipiganishe Qur’ani baadhi yake na baadhi kwani imeteremka katika mielekeo mingi (rai nyingi)"

Alikuwa akitabasamu sana kwa masahaba zake hana mfano wake. Siku moja alikuja mbeduwi akamkuta Mtume –rehema za Allah na amani zimshukie- amebadilika rangi yake hali ambayo haikuwaridhisha masahaba zake, akataka yule mbedui kumuuliza wakamwambia usifanye hivyo ewe mbeduwi kwani sisi hatupendezewi na hali ya rangi yake. Akawajibu niachieni kwani naapa kwa yule aliemleta kwa haki Mtume sitamwacha mpaka atabasamu. Akasema Ewe Mtume wa Allah imetufikia kuwa Masiih Dajjaal atawajia watu na mkate hali ya kuwa wafa njaa jee unaona wewe nawatoa mhanga kwako baba yangu na mama yangu nijizuie nisiule ule mkate wake kwa ajili ya kujikataza kula haramu na kuitakasa nafsi yangu hadi nife njaa au niupige mkate wake (niule) mpaka nikashiba (mbavu zangu zikajaa kwa shibe) hapo nimwaamini Allah SWT na nitamkufuru yeye (Masiih Dajjaal). Wakasema (Masahaba) basi hapo akacheka Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani zimshukie- mpaka meno yake magego yakaonekana kisha akasema! “Hapana bali Allah Subhanahu Wataala atakutosheleza kwa kile atakachowatosheleza Waumini.” Alikuwa mwenye kutabasamu zaidi na mwenye nafsi safi kuliko watu wote isipokuwa wakati wa kuteremka Qur’ani au akikumbuka kiyama au akihutubu hutuba kubwa. Alikuwa akipatwa na jambo hujivua nafsi yake na uwezo na nguvu (kuwa hana uwezo wala nguvu na hivyo ni vya Allah) na humtegemea Allah SWT na kutawakali kwake katika jambo hilo. Vile vile humuomba Allah SWT amuongoze katika njia iliyonyooka:

( اللهم أرني الحق حقا فأتبعه وأرني الباطل باطلا وارزقني اجتنابه وأعذني من أن يشتبه علي فأتبع هواي بغير هدى منك واجعل هواي تبعا لطاعتك وخذ رضا نفسك من نفسي في عافية واهدني لما اختلف فيه من الحق بإذنك إنك تهدي من تشاء إلى صراط مستقيم )                                                                                         

“Ewe Mola wangu nioneshe haki niione kuwa ni haki ili niifuate na nioneshi upotofu na niuone kuwa upotofu na nijaalie niepukane nao. Na niepushe na kuchanganyikiwa nisije nikafata mapendekezo ya nafsi yangu bila ya muongozo wako nijaalie mapendekezo yangu yende sambamba na amri zako (taa yako). Niridhie hata unilinde kutokana na kila lililokuwa baya na uniongoze katika yale yaliokhtalifiwa katika haki kwa idhini yako hakika wewe unamuongoza umtakaye katika njia iliyonyooka.”











Mara nyingi wakati anapokula hukusanya magoti yake mawili na miguu yake miwili kama anavyokaa anaesali (kikao cha Attahiyatu) na husema:

( إنما أنا عبد آكل كما يأكل العبد وأجلس كما يجلس العبد )

 “ Hakika mimi ni mja nala kama anavyokula mja na nakaa kama anavyokaa mja”.

Na alikuwa ala kile kilicho mbele yake (katika sahani). Akamjia Othman na ‘ faaludhaj’ ( aina ya chakula) akaila na akasema:

( إن هذا الطعام طيب )

"Hakika chakula hichi kizuri."

 Na katika matunda ya majimaji aliyokuwa ayapenda kuliko yote ni tikiti (Batteekh) na zabibu na siku moja alikula tende mbichi (rattab) kwa mkono wake wa kulia na akashika kokwa kwa mkono wake wa kushoto akapita mbuzi akamuashiria akawa (yule mbuzi) anakula katika mkono wake wa kushoto na yeye anakula kwa mkono wake wa kulia mpaka alipomaliza na akaondoka yule mbuzi. Na alikuwa pengine anakula zabibu kwa kukamata mkole wake (mkole wa zabibu) halafu hula hizo  zabibu moja moja kutoka mkoleni  hata vipunje vyake huanguka na kuonekana katika ndevu zake. Alikuwa -rehema za Allah na amani zimshukie- apenda maboga na alikuwa akisema hakika huu ni mti wa ndugu yangu Yunus A.S.Na alikuwa asema:

( يا عائشة إذا طبختم قدرا فأكثروا فيها من الدبأ فإنه يشد قلب الحزين )              

 "Ewe Aisha mkipika chungu (cha mchuzi) kithirisheni mboga (mabamia, mabilingani upate kuwa  mwingi) kwani huko kunatia nguvu moyo wa mwenye huzuni (akipelekewa katika huo mchuzi)".

Alikuwa apenda katika nyama ya mbuzi miguu ya mbele na mabega na katika viungo apenda siki na katika tende apenda aina fulani inayoitwa « al-Ajwa » na alikuwa achukia mafigo kwa mahala pake karibu na mkojo. Alikuwa hali thomu na vitunguu maji wala kiraathi (aina fulani ya vitunguu ambayo vile vile yatoa harufu). Hakuwa kabisa akitia kasoro chakula lakini kikimpendeza akila na ikiwa hakukipenda akiwacha hasemi cho chote cha kufanya hicho chakula kichukiwe na wengine watakaosikia kasoro hiyo. Alikuwa aramba vidole vyake baada ya kumaliza kula mpaka vyageuka vyekundu aramba kimoja kimoja na huku akisema :( إنه لا يدري في أي الطعام البركة )                       « Hakika mtu hajui katika chakula gani kilichokuwa na baraka. » Na akimaliza husema:

( الحمد لله اللهم لك الحمد أطعمت فأشبعت وسقيت فأرويت لك الحمد غير مكفور ولا مودع ولا مستغنى عنه )                                                                     

«  Sifa zote njema ni za Allah.  Ewe Mola shukrani ni zako umelisha mpaka ukashibisha na ukanywisha mpaka ukaitoa kiu.  Shukrani ni yako isiyokufuriwa wala isiokatika wala isiowezekana kuachwa bila kushukuriwa ». Alikuwa akishakula mkate na nyama khasa huosha mikono yake miwili vizuri kisha hupangusa yale maji yaliobakia mikononi katika uso wake na alikuwa anywa katika michubuo mitatu kabla ya kila chubuo asema ‘Bismillahi’ na mwisho wake asema ‘Al Hamdulillah’ (Yaani husoma Bismillah mara tatu na Al-Hamdulillah mara Tatu). Alikuwa akinywa maji huyafyonza hayabugii na alikuwa hahemi mbele ya kile chombo anachonywea bali ahema kando yake na alikuwa nyumbani kwake ana haya zaidi kuliko mwana mwali. Hawaulizi juu ya chakula (wampe chakula) au kuwahimiza wampe chakula wakimpa chakula ala na cho chote wanachompa akikubali na wanachomnywesha anywa na pengine husimama mwenyewe na kuchukua  kile anachotaka kula au knywa(ajitumikia).










Alikuwa Mtume  -rehema za Allah na amani zimshukie- avaa pete na pengine hutoka na katika pete yake kuna uzi umefungwa ili akiuona  akumbuke kitu fulani na alikuwa avaa kofia chini ya kilemba (amama), na alikuwa ana kilemba chaitwa “Assahaab” (wingu) akamgaia Aliy bin Abi Talib  na Ali wakati mwengine hutokea kakivaa na Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- husema:

( أتاكم علي في السحاب )

“Amewajia Aliy katika wingu.”

Nasema labda hadithi hii ndio iliyowafanya wale katika mashia wanaosema kuwa Aliy bin Abi Talib yuko katika mawingu. Basi wakisikia radi wamwamkia Aliy.  Alikuwa -rehema za Allah na amani zimshukie- akivaa nguo huanza upande wa kulia na asema:

( الحمد لله الذي كساني ما أواري به عورتي وأتجمل به في الناس )      

 ‘Namshukuru Allah aliyenivalisha ninachojistiria utupu wangu na ninachojipambia kwa watu.’ Na akivua nguo huanza kwanza upande wa kushoto.  Alikuwa akivaa nguo mpya humpa nguo yake ya zamani maskini kisha husema :-

( ما من مسلم يكسو مسلما من سمل ثيابه لا يكسوه إلا لله إلا كان في ضمان الله وحرزه وخيره ما واراه حيا وميتا )                                                           

“Hampi Muislamu nguo yake ya zamani Muislamu mwenzake na hamvalishi ila kwa ajili ya Allah (kutaka radhi yake) isipokuwa huwa katika dhamana ya Allah Subhanahu Wataala  na kinga yake na kheri yake madamu ameivaa hiyo nguo wakati yu hai au amekwishakufa.”  Ilikuwa katika tabia yake -rehema za Allah na amani zimshukie- kuwapa majina wanyama wake, silaha zake na vitu vyake na lilikuwa jina la bendera yake “Al-uqaab” yaani “mwewe”. Na jina la upanga wake anaokwenda nao vitani “Dhul-Faqaar” yaani “Wenye misingi”  na anao upanga unaoitwa “Al-Mikhdham”  (mkali) na upanga mwingine waitwa “Ar-Rasuub” (unaozama) na mwingine waitwa “Al-Qadhiib” (unaopendeza) mshikio wake  umepakwa kwa fedha na lilikuwa jina la upinde wake “Al-Katuum” (usiovuma) na jina la podo lake (mfoko wa mishale) “Kaafuur” na jina la ngamia wake “Al-Qaswaa” na mwingine “Al-Adhbaa”  na jina la baghla wake (mnyama baina farasi na punda kwa kimo) aitwa “Addaldal” na jina la punda wake “Yaafuur” na jina la mbuzi wake aliekuwa akinywa maziwa yake “iyna” ( عينة ) .












Na alipokwisha ondoka akasema -:

( ردوه علي رويدا )                                            

“mrudisheni kwangu polepole”


Alikuwa -rehema za Allah na amani zimshukie- katika vita basi maadui wakawaona waislamu wako katika ghafla, akaja mtu (katika washirikina) mpaka akasimama mbele ya Mtume wa Allah huku ameshika upanga akamwambia nani anayekukinga na mie? Akamwambia (-rehema za Allah na amani zimshukie-) "Allah". Na hapo ukaanguka ule upanga kutoka mkononi mwake akauchukua Mtume wa Allah akamwabia yule mtu  “nani anaekukinga na mimi?” Akamwabia kuwa wewe bora kuliko mimi ( katika kusamehe). Akamwambia Sema Ash-hadu an laa ilaah Illa Allah wa Anniy Rasool Allah. Akasema hapana (yaani sisemi hivyo) isipokuwa natoa ahadi kuwa sipigani vita na wewe wala siwi pamoja na watu wanaopigana na wewe. Hapo akamwachia kwenda zake akenda kwa watu wake akawaambia nimewajia kutoka kwa mbora wa watu.


Anazo -rehema za Allah na amani zimshukie- habari nyingi namna kama hii alikuwa asema:- Asiniletee mmoja wenu habari  juu ya mmoja katika masahibu zangu kwani napenda kuwajia na moyo wangu uko safi juu yenu. Akasema Aliy bin Abi Taalib amenipeleka Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani zimshukie-  mimi, Zubair na Al-Miqdaad akasema “ Nendeni kwenye bustani ya “Khaakh” ndani yake kuna mwanamke (yumo ndani ya kihema kidogo kinachoekwa juu ya ngamia yaani ‘Khaudaj’) ana barua ichukueni kutoka kwake. Tukenda kisha tukamwambia yule mwanamke itoe hiyo barua au tutakuvua nguo akaitoa katika mikia ya nywele zake tukaileta kwa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie-. Ikajulikana kuwa inatoka kwa Haatib bin Abi Balta’a (katika Masahaba) na inakwenda kwa washirikina wa Makka anawapasha habari juu ya jambo katika mambo ya Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- ambayo  hakutaka jambo hilo alijue mtu yo yote nalo nafikiria ni juu ya kuiteka Makka wakati aliposema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie:- “Ewe Mola tuzibie macho (tusionekane ulisitiri jambo letu hili la kuteka Makka) mpaka tuwachukue Quraish kwa ghafla” au kama ilivyokuwa katika maana ya hadithi. Akasema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- kitu gani Ewe Haatib kilichokusababisha ufanye hivyo? Akasema Ewe Mtume  usiniharakishiye, mimi ni mtu niliokuwa nimeshikana sana na watu wangu na katika Muhaajiriin uliokuwa nao wanao jamaa zao Makka wanaohami watoto wao (hao Muhaajirin), kwa hiyo mimi nikataka msaada kwa watu wengine (Mushrikiin) wawahami watoto wangu kwa sababu sina watu wangu wa karibu kwa damu wa kunifanyia hivyo, si kufanya hivyo kukufuru au kuridhika na ukafiri baada ya Uislamu au kurtadi kutokana na dini yangu.  Akasema Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie:- Hakika aliyowaambia ni ukweli. Akasema Omar R.A niwache niikate shingo ya munafiq huyu. Akajibu Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie, hakika yeye amepigana vita vya Bader na kitu gani kitakacho kujulisha pengine Allah Subhanahu Wataala amewatazama waliopigana vita vya Bader akasema “Fanyeni mnayotaka kufanya mimi nimekwisha waghufiria madhambi yenu.”












Alikuwa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- mnyenyekevu zaidi kuliko watu wote juu ya cheo chake kikubwa kabisa. Amesema Ibn Aamer: Nimemuona anapiga mawe Jamara Al Aqaba kutoka juu ya ngamia mweupe mwenye weusi kidogo alikuwa akipiga mawe pamoja na watu wa kawaida sio kuwapiga na kuwafukuza watu ili apite yeye Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- (kama wanavyofanyiwa wafalme). Alikuwa akipanda punda alietandikwa kwa kitambaa cha makhameli na pamoja na hayo alikuwa akimpandisha mtu mwingine pamoja naye. Aliletwa mtu kwa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- alivyomuona  akatetemeka kwa haiba yake (sura yenye kumfanya mtu amuogope akimuona mara ya kwanza). Basi hapo Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- akamwambia: "Pole pole kwani mimi si mfalme isipokuwa ni mtoto wa mwanamke wa Kiqureish aliekuwa akila nyama ilyokaushwa kwa jua". Alikuwa akikaa pamoja na masahaba zake huchanganyika nao akawa kama mmoja katika wao hata akija mtu mwengine asiweze kumtambua Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- baina yao mpaka aulize.


Nasema (maneno ni ya mtungaji) wamechukua mfano wake Maimamu wa Kibaadhi radhi ya Allah SWT ziwe juu yao (wakitawala kwa sharia ya Allah Subhanahu Wataala). Alikuwa mgeni aingiapo katika mjumuiko wa watu hamjui nani kati yao Imam mpaka aambiwe huyu ndiye Imam. Tizama kisa kilichokuwemo katika “Allulu Arratb” (kitabu cha mtungaji) cha Imam Azzan bin Qais  alipoingia mtu aliemkusudia yeye akenda kumuamkia mtu mwingine badala ya kumwamkia  Imam kwa jinsi anavyo changanyika na masahibu zake.


Alikuwa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- haitwi na mmoja katika masahaba zake isipokuwa kuitikia kwake huwa ni “Labbeik”, na alikuwa atabasamu nao wakati wanapozungumza na wanapocheka  na hawakatazi isipokuwa kutokana na haramu.











Kughadhibika na kuridhika kwake kulikuwa mara kwajulikana katika uso wake kwa usafi wa rangi yake ya uso (mabadiliko yo yote katika uso wake mara yaonekana). Mmoja katika waliomsifu kamshabihisha kama mwezi unavyoonekana usiku wa bader (usiku unaokamilika mwezi).  Amemsifu sahibu wake Abu Bakr R.A:- Mwaminifu Al Mustafa anaita kwenye kheri kama kwamba ni mwanga wa mwezi uliokamilika umebainika kizani, kilikuwa kipaji chake Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- kipana na nyusi zake nyembamba na zimekamilika (za kifungo) na baina ya nyusi zake kwametameta kama fedha iliyosafi na yalikuwa macho yake mapana (makubwa) na  vile vile yalikuwa meusi sana na yemchanganyika na wekundu, kope za macho yake zilikuwa nyingi na pua yake imenyanyuka na imenyooka na meno yake yana mwanya, na akifungua mdomo wake kucheka kama kwamba amefungua mwanga wa umeme unavyometameta, midomo yake miwili katika bora ya viumbe vya Allah Subhanahu Wataala, akiufunga mdomo wake honekana kuwa mdogo, mafunda yake yameingia ndani na magumu. Ana ndevu nyingi aziwachia, achukua (apunguza au anyoa) masharubu, na ile sehemu ya shingo yake inayopigwa na jua na upepo rangi yake ni kama birika la fedha lililochanganyika na dhahabu inametameta katika weupe wa fedha na wekundu wa dhahabu. Ni mwenye kifua kipana na nyama ya mwili wake imeshikana vizuri (haikutebwereka) kama kiyoo katika kusimama kwake na kama mwezi kwa weupe wake.  Amewasilishiwa baina ya mwanzo wa kifua chake (chini ya roho yake) mpaka kwenye kitovu chake kwa nywele zilizotengezwa kama namna ya bomba (la maji), hapakuwa katika kifua chake wala katika tumbo lake nywele isipokuwa hizo na vile vile alikuwa na mikunjo ya tumbo mitatu aifunika na kikoi katika hiyo mitatu mmoja na miwili yaonekana. Ana mabega makubwa yenye nywele nyingi na mwenye vifundo vya vidole vya mikono vikubwa. Ni mwenye mgongo ulio mpana, baina ya mabega ya mawili kuna mhuri wa unabii (khaatam Annubuwa) umefuatia (huo mhuri) bega lake la kulia ndani yake kuna doa jeusi (ndugu) limepiga manjano, kando yake kuna nywele zimelizunguka hilo doa kwa mfatilio kama ile alama iliyoko juu ya uso wa farasi. Mikono yake mikubwa imejaza (tokea mabegani kwenda vifundoni mpaka mwanzo wa viganja) na viganja  vyake virefu (sehemu ya kushikia ya mkono  upande wa nje) na vile vile mikubwa yenye wasaa (sehemu ya kushikia upande wa tumboni yaani ndani) vidole vyake virefu na kama kwamba mabomba ya fedha. Kiganja chake kilaini kuliko aina fulani ya kitambaa (hariri). Anukia ikiwa kajitia mafuta mazuri au hakujitia, akimwamkia mtu hubakiliwa na harufu nzuri siku nzima. Huweka mkono wake juu ya kichwa cha mtoto akawa hujulikana miongoni mwa watoto wengine kuwa ameshikwa na Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- kwa jinsi anavyonukia. Ilikuwa miguu na mapaja yake mikubwa na huonekana kuvimba kwake chini ya kikoi chake. Alikuwa wastani katika umbo lake alinenepa kidogo katika siku zake za mwisho na ilikuwa nyama ya mwili wake imekamatana. Alikuwa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- katika kutembea kwake kama vile ang’oka katika ardhi na khatua zake zakikaribiana na hutembea polepole (kwa taratibu) bila ya maringo.  Alikuwa asema nina majina kumi kwa Mola wangu, mimi Muhammad na mimi Ahmad na mimi Al-Maahiy na mimi Al Aaqib na mimi Al Haashir na mimi Rasool ar- Rahma na  mimi Rasool at- Tawbah na Rasool- Al Malaahim an Al Maqfiy na mimi Quthum (Aliye kamilisha, aliyejumuisha) Allah Amteremshie Rahma na Amani nyingi sana. Twamuomba Mwenyezi Mungu Subhanahu Wataala aturuzuku tumfuate na wala tusipotee njia yake. Ukoo wake Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- (Nasab Yake)  Muhammad bin Abdillah bin Abdel Al Muttalib bin Haashim bin Abd Manaaf bin Qusey bin Kinanah bin Murrah bin Kaab bi Luay bin Ghaalib bin Fihr bin Maalik bin Annadhr bin Kanaanat bin Khuzaymah bin Mudrikah bin Ilyaas bin Mudhar bin Nizaar bin Maaddi bin Adnaan na mpaka hapa umehifadhiwa ukoo wake wenye sharafu kwa mujibu wa kauli yake Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- kwani  akiutaja ukoo wake na akafika Adnaan husema “wamesema uwongo wanaoandika juu ya ukoo” kasema mara mbili au mara tatu kwa sababu baada ya Adnaan kuna mpingamano mkubwa.


Amekufa baba yake Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- naye bado yuko katika tumbo la mama yake na amekufa mama yake Aminah bint Wahb na umri wake –rehema za Allah na amani zimshukie- miaka sita, na amekufa babu yake Abdul Muttalib na Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani zimshukie- ana umri wa miaka minane. Akamchukua kumlea baada yake mtoto wake huyo Abdul Muttalib naye ni Abu Taalib ammi yake Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie. Amemuowa Bi Khadija R.A. na umri wake miaka ishirini na tano na ukoo wake wakutana na ukoo wa Mtume -rehema za Allah na amani zimshukie- katika Qusey.  Amefanya sulhu baina ya Maquraish katika ugomvi wao wa kulinyanyua Jiwe jeusi (حجر الأسود) wakati ana umri wa miaka thelathini na tano.  Amepewa Utume wakati  umri wake miaka  arubaini (40) na alificha Mtume wa Allah  kuteremshiwa kwake wahyi kwa muda wa miaka mitatu mpaka ilipoteremka:


الحجر: ٩٤

“Basi (wewe) yatangaze ulioamrishwa  (wala usijali upinzani wao) na ujitenge mbali na (vitendo vya ) washirikina”


Amepelekwa katika safari ya Israa kwenda Bait Al-Maqdis kisha akapazwa kwenda mbinguni katika safari ya Miiraji kabla ya Al Hijra kwa mwaka na huko ikafaridhishwa sala.Akafa ammi yake Abu Taalib na mkewe Bi Khadija R.A. katika mwaka mmoja kabla ya Al Hijra kwa miaka mitatu na ukaitwa mwaka huo mwaka wa huzuni.


Hijra ya Mtume wa Allah -rehema za Allah na amani zimshukie- kwenda Madina ilikuwa baada ya miaka kumi na tatu baada ya kupewa Utume.

Kubadilishwa Kibla kutoka Beit Al Maqdis kwenda Al-Kaaba kulikuwa  mwanzo wa miezi kumi na nane kutoka A-Hijra.

No comments:

Post a Comment

Note: only a member of this blog may post a comment.